Dr. Slaa aomba ukimbizi Canada

Dr. Slaa aomba ukimbizi Canada

Dr. Slaa Mungu akupe moyo Wa ujasiri. Kwa kweli mwanadamu ni kiumbe mbaya kuliko mnyama. Hivi kweli yote uliyoyafanya Chadema yametupwa Leo unaambulia matusi mazito hivi kwa vijana Wa Chadema??

Kama wameufanyia hivi mti mbichi??, itakuwaje kwa mti mkavu?? Kweli vita ya madaraka hasa urais ni mbaya mno.

Ushauri wangu kwasababu wewe ni mtu wa dini basi mtwike Bwana fadhaa zako zote maana yeye hujishughulisha na maisha yako. Wale wanaofahamu ulipoitoa Chadema wataendelea kukuheshimu bila hata KUJALI vyama vyao. Wale wenye moyo mgumu, moyo Wa lucifer wataendelea kukukejeli, hilo lisikusumbue yote ni maisha.

Jitahidi kuishinda vita yako kwa maombi BINAFSI na neno la Mungu kwa wingi. ZABURI 121

Queen Esther
Mnatabia mbaya ya kumsingizia Mungu ili awaonee huruma!

Dr. Slaa ni mwanadamu kama wewe, Mimi na yule, anamapungufu yake, ikiwa ni pamoja ya kukengeuka na kuwa na tamaa kama binadamu yeyote yule.

Dr. Hapa hatukanywi. Wanaelezea tabia zake na role ya mpenzi wake ilivyo affects career yake. Hii huruma unayoinesha hapa ndiyo hiyo hiyo bi mshumbushi alitumia kumshughulikia Dr. Hivyo si vema kutumia neno la Mungu kuhalalisha madhaifu yenu/yako.
 
Si unajua binti Nshomire hajazoea shida.......
 
Kwa kweli mimi iyo Taharifa inanisikitisha sana pamoja na usaliti alioufanya akiongozwa na Mwakyembe..kuishi maisha ya kikimbizi ni aibu sana kwake na kwa familia na Taifa kwa ujumla vijana South Africa,UK,Canada wanaishi kwa Refugee Permit wao huziita Mpango..hayo sio maisha kabisa..aje Bongo aanze upya tuu arudishe mpira kwa Kipa aanze upya Maisha yataendelea tuu kuriko huko....
 
Habari za kutoka magazetini leo asubuhi itv zimesema kuwa Dr. Slaa ameomba ukimbizi huko Canada kwa madai kuwa maisha yake yamo hatarini Tanzania!

Swali: Ni nani huyo anayetishia uhai wa Dr.Slaa?
Nina mashaka huenda huyu mtu hakupewa alichohaidiwa na huenda kaambiwa SHUT UP! ukiinua mdogo kujifanya kuongea kinyume nyume ndio itakua tiketi ya kutangulia mbele za haki, kumbukeni mtu ukitumika kwa mabaya baada ya kazi wale waliokutuma wanapanda mkakati wa kukutokomeza kabisa ili usije kuwa kigeu geu
 
Chadema laana ya Dr Slaa ita watesa milele..
 
Naye hatakuwa na kikao katika nchi ya uzao wake
Nakumbuka uzi wako mmoja ulikua ukichambua hali ya Dr katika ulimwengu wa roho, ulisema ataendelea kua mtu wa ahangaiko mpaka mwisho wake, kweli nimekukubali!!
 
Swala la lipumba...na dr slaa ni tofauti..

Mahangaiko yanayomsumbua dr ni mengi.... usaliti wa chama na kanisa... ni vitu hatari sana...

Lipumba anaweza kuomba msamaha akasamehewa ikumbukwe wakati anajiengua kwenye kiti chake bado hajakaa mbali na siasa...

Huyu dr makando ni mengi mara familia...mara chama...mara kanisa...mara bango la nyumba...
Kama zito
 
Kwani idara ya usalama wa viongozi wa ccm na vibaraka wao wameshindwa kumhakikishia usalama wake?! Dhambi ya usaliti inamtafuna, atajikuta kaomba hifadhi burundi kwa interahamwe Pierre!
Zitto vipi?
 
Habari za kutoka magazetini leo asubuhi itv zimesema kuwa Dr. Slaa ameomba ukimbizi huko Canada kwa madai kuwa maisha yake yamo hatarini Tanzania!

Swali: Ni nani huyo anayetishia uhai wa Dr.Slaa?
Bila shaka MZEE wa sumu za kunyonyoa ngozi ndo anamtisha Dr slaa kimbia kabla hajakufanya ya mwakyembe
 
Me nashindwa kuthibitisha moja kwa moja kwa sababu ni vigumu kuthibitisha usaliti. Me naona kila mmoja anatenda kulingana na mtazamo wake juu ya jambo fulani wakati fulani.
 
Chadema laana ya Dr Slaa ita watesa milele..
Kati ya CHADEMA na CCM ni yupi aliyeharibu future ya huyu Mzee? Jitahidi kufikiri kwa kina na utumie ubongo wako vizuri sio kufikiri kwa kutumia viungo vya kutolea haja kubwa.
 
Back
Top Bottom