Dr. Slaa anastahili kuheshimiwa

Dr. Slaa anastahili kuheshimiwa

Amani iwe nanyi wanaJF!
Ndugu zangu wanaJF na wapenzi wa mabadiliko nchini kwa ujumla....!
Hivi kama Dr Slaa amehudhuria vikao vyote vya kamati kuu ya chama na waliafiki na kuridhia kumpokea ndugu EDWARD LOWASA,Wakaweka msharti ya kumpokea ikiwemo ni pamoja na kukuueleza umma ukweli juu ya kampuni hewa ya Richmondi na sababu ya kujiuzulu kwake uwaziri mkuu mwaka 2008.
Lowassa alikubaliana na masharti hayo na akatekeleza! Je, Dr Slaa kama mtu mwenye akili timamu na uelewa wake tunavyoujua alikua na sababu ipi ya msingi kususia wenzake! Kama ingekua ni kweli si angeiangikia kamati kuu barua juu ya kutokukubaliana na suala hilo?
Ninyi msiokua wanachadema nani kawapa mamlaka kujua na kumfuatilia Dr Slaa anafanya nini na yuko wapi? Anawahusu nini? Je, kama mwenyekiti anawaambieni anawasiliana naye mnataka nini zaidi? Mnajua wanawasiliana nini viongozi hao wakuu wa CHADEMA!
Mimi sio msemaji wa CHADEMA lakini sioni sababu ya msingi ya Dr Slaa kususa.
Kama sio msemaji wa Chadema unahusika vipi hili kaa kimya.
 
Hao wanao kuja na swaga za Dr kasusa hawanipagi shida maana wamejiapiza kuzimu na mauti pia huishi kwa maneno ya uongo. Tuwapuuze maana asiri yao nikuzimu ambako baba wa uongo ibilisi shetani ndiko yaliko makao yake. Tuwapuuze milele
 
Hakika wanaomtukana DR.#Slaa wataalaniwa na #Mungu kwani ni mjinga na mpuuzi pekee yake ambaye hawezi kuona mchango mkubwa na kazi kubwa aliyoifanya Dr.Slaa kwa faida ya chama pamoja na taifa kwa ujumla.
Lengo letu ni kuiondoa ccm madarakani bila mchango wa Dr.#Slaa hatofanikiwa kabisa .Dr.#Slaa watu wengi tuna imani kubwa na wewe tunakusubiri tumeambiwa kwenye utashiriki kwenye vikao vya kamati kuu ya chama tunakusubiri kwa hamu kwa hamu kubwa tunakuombea kwa #Mungu afya njema ,ulinzi wa #Mungu siku zote tunakuhijitaji sana tuna imani kubwa na wewe .dada Tetty umepitia huku?

Nimepita
 
Siku hazigandi nimeamua kusubiri adi atakapo ongea niweze kumhukumu kwa mandishi au kwa kumpa jiba zuri kunzia leo sitasoma neno lolote lililoandikwa dr slaa kama siyo la kujitokeza kwake na kuongea ninaweza mhukum kabla ya wakati maana ninajuwa kama akisusa hukumu kwa wananchi haijapata tokea kwa kiongozi yeyote Tanzania
 
Dr slaa yupo lakini Kwa sasa yupo na Nape na Membe wamemficha kwao wanamhesabia Dola nyingi toka kwenye yale mapesa lundo ya Marehemu Gadafi kisha watamsaidia namna ya kutorokea italy mafichoni au hata marekani , ccm wapo busy wanabuni mbinu za kuwafarakanisha Ukawa huu ni Mgodi mkubwa wengi watavuna pesa nyingi kupitia huu Mladi waliobuni yaani bajeti ya mabilioni ya kuwachakaza wapinzani hizo pesa zitakuwa zinapitia mikononi mwa Nape anapiga cha juu kabla ya kwenda Kwa waliyemkusudia, Nape anasali usiku na mchani Dili litiki Apate pesa Kwa mgongo huo wa kuwavuruga Upinzani

Duh...kwa hiyo Slaa amekubali kuhongwa na Nape?
 
WanaJF na hasa wana CHADEMA wenzangu tuwe makini sana na maandishi yetu hapa jukwaani kuhusu huu ukimya wa DR SLAA, tafadhalini sana, DR ni kiongozi mkubwa sana anastahili kuheshimiwa, wale wenye uchungu na CHADEMA na tunaofahamu tulipotoka hatuwezi kumkashifu huyu mtu, kwa lipi hasa ? Acheni kabisa jambo hilo, sikupenda kuandika jambo hili maana linaweza kuendeleza malumbano zaidi lakini nimelazimika kuliweka kama angalizo.
Ni ngumu kwa wakati uliopo. Usisahau mmeambiwa lowasa kaja na mamilioni ya wanachama, mamilioni hao wanachojua ni lowasa. Ndiyo maana wote kama makondoo sasa mnaimbishwa tuna imani na lowasa.

Mtaufahamu umuhimu wa Dr baada ya fisadi lenu kuangukia pua Novemba.
 
Kama ana ruhusa ya kuwapo nje ya ofisi je pia achukuliwe hatua? Hakuna watu wanaokwenda likizo? Kwani yeye chama ndio ametembea nacho kwa hiyo hawawezi kufanya jambo lolote bila yeye?
 
naunga mkono,huyu hafai hata kushika nchi maana atatuletea yaleyale ya mke toka mtwara na watoto ake wa msoga kujimilikisha chama na kumzidi mume na baba yao katika maamuzi yenye tija na nchi. Slaa kaonyesha udhaifu mkubwa sana maana unapo milikiwa na mwana mke wewe hufai katika jamii.
Mwenzake lowassa anamsimamo hata marafiki zake na mkewe walipo jaribu kumshauri abakie ccm na awe mnafiki akaliona hilo na kukataa. saa mfumbuzi bin slaa ana mremote contol slaa wake

Mzee Slaa apumzike sasa, kama amefikia hatua ya kufichwa na Mchumba wake, hafai huyo!
 
Vipi mkuu ile biashara yako ya unga inaendeleaje?

Kwa sasa anaombea ccm ishinde ili aendelee nayo maana ikiingia ukawa ndio basi tena kwani mikataba yoote itabidi ipitiwe upya
 
Mkuu upo sahihi, binafsi sion haja ya dr.slaa kususa na mbaya zaidi kuna kipeperushi kinaitwa RAI kimekuwa mstari wa mbele kuandika habar za dr. as if wana wasiliana., ushauri wangu naomba dr. ajitokeze atoe maelezo kama n kweli kajitoa chadema tujue, .
 
Teh teh teh!!

Laki si Pesa, anatoa tamko kuwa Dr.Slaa awapishe kwenye chama chao Chadema.

Siasa hizi tutasikia mengi.

Mwenzio kasoma alama za nyakati,bado wewe bado hujachelewa njoo tuunganishe nguvu kuiondoa ccm madarakani ili tufaidi asali na maziwa
 
wana jf.
Kesho vikao vya kamati kuu ya chadema vinaendelea ili kupanga mikakati ya kuhakikisha ukawa inapata ushindi wa kishindo october .
Ili mikakati ya ushindi kwenye uchaguzi mkuu october iende vizuri, wajumbe wote wanatakiwa wawepo akiwemo katibu mkuu wa chama dr. Wilbroad slaa ambae mpaka sasa hivi hajulikani alipo, endapo dr. Slaa hatahudhuria kikao kesho naomba kamati ya maadili imchukulie hatua kali za kinidhamu ili kulinda kanuni na maadili ya chama.
chadema sio mali ya mtu binafsi ,ni mali ya watanzania wote, na hakuna mtu mkubwa kupita chama.
Asietaka ukombozi wa nchi october atupishe.

hapo kwenye red: Chadema nako kuna kamati ya maadili? Sio kamati kama hiyo ilitumika kumuangamiza fisadi lowasa? Na huko itafanya kazi ya kuchuja majina ?na kama ndivyo lowasa atapenya? Akipenya kwenye kamati hiyo ntaamini wenye chama na kamati yenu wote hamna maadili.

Lakini maadili yenu ya kupambana na ufisadi hata hivyo yashakufa baada ya kununuliwa na fisadi lowassa kwa pesa za kifisadi alizofisadi watanzania,si ajabu mafisadi mkampitisha fisadi mwenzenu lowassa kugombea urahisi wa kufanya ufisadi tanzania.
 
asante sana Dr. onesha msimamo wako. walioamua kodhoofisha upinzani kwa kutengeneza ccm B achana nao.
 
naunga mkono,huyu hafai hata kushika nchi maana atatuletea yaleyale ya mke toka mtwara na watoto ake wa msoga kujimilikisha chama na kumzidi mume na baba yao katika maamuzi yenye tija na nchi. Slaa kaonyesha udhaifu mkubwa sana maana unapo milikiwa na mwana mke wewe hufai katika jamii.
Mwenzake lowassa anamsimamo hata marafiki zake na mkewe walipo jaribu kumshauri abakie ccm na awe mnafiki akaliona hilo na kukataa. saa mfumbuzi bin slaa ana mremote contol slaa wake
Mkuu mimi nilikuwa shabiki wa huyu babu lakini baada ya kujua kwamba mshumbushi ndio mwenye remote ya huyu padri nimemdharau sana
 
Jamani mm mgeni hivi umu ndani kuna mshiko au?au watu mnakazi zenu tusiwaingilie?maana ni zaidi ushabiki! Mnatisha wana jf
 
Kweli CCM mmeishiwa sera! Hivi Magufuli mtamnadi lini?

Walivyo stukiwa kutumia ndege ya serikali kumnadi makomeo mikoani ndio basi tena wamemtupa kuleeeeee ameambiwa ajitegemeee
 
Back
Top Bottom