Dr. Slaa anastahili kuheshimiwa

Dr. Slaa anastahili kuheshimiwa

Leo ni aibu kuona comment za kejeli na matusi ambazo wanachama wamekua wakimkosea heshima Dr Slaa.

Kwa namna mzee huyu alivyopambana kwa jasho na damu shukrani aliopatiwa haikumstahili, Hivi kama mti mbichi mmeutenda hivi je mti mkavu mtaufanyaje?

Hii ndio inayoitwa shukrani ya punda, Kwa namna chama hiki kinavyoongozwa kibabe ni wazi wengine wanaofikiri wamesimama basi na wajiandae.

L'su,mny'ka,na wengineo mjiandae siku yenu inakuja.
 
Leo ni aibu kuona comment za kejeli na matusi ambayo wanachama wamekua wakimkosea heshima Dr Slaa.
Kwa namna mzee huyu alivyopambana kwa jasho na damu shukrani aliopatiwa haikustahili,
Hivi kama mti mbichi mmeutenda hivi je mti mkavu utaufanyaje?
Hii ndio inayoitwa shukrani ya punda,
Kwa namna chama hiki kinavyoongozwa kibabe ni wazi wengine wanaofikiri wamesimama basi na wajiandae.
L'su,mny'ka,na wengineo mjiandae siku yenu inakuja

Time will tell
 
Hatupuuz wala hatuwez kupuuza mchango wa dk slaa lakin hatukubalian nae kutuacha ktk wakat kama huu wa mabadiliko, nenda tu dk tulikupenda ila tunapenda mabadiliko zaid
 
Mkuu ungekuwa rafiki, ndugu au mshauri wa Dr Slaa mimi binafsi ningekutuma kwake kumwambia ilikuwa busara kubwa kwake kuendelea kubakia kimya kama alivyofanya awali. Kimya kile kilimpa heshima na sote tuliopenda Dr Slaa tuliona ilikuwa busara kubwa ili aweze kupisha huu upepo wa madiliko hata kama yeye binafsi hakuafikiana na wenzie.

Lakini tazama waliomuhonga na hata kumpa ushauri wa kilaghai kuibuka kwa lengo la kuichana CHADEMA na UKAWA na mgombea wake katika kipindi hiki kigumu cha mapambano ya kufa kupona wamemponza sana. Heshima yake yote aliyojijengea miaka yote ya kuimarisha na kujenga Chama leo ni kama mchango wake umekuwa ni zero kabisa. Kauli zake zimegusa na kukwaza watu wengiiii mno maarufu katika jamii pasipo na sababu ya maana.

Umma wote leo unafahamu kuwa nyuma ya Dr Slaa kuna nguvu kubwa (iliyo mnunua). Hata ajitape vipi kuwa ati yeye hana bei lakini ukweli ni kuwa Dr Slaa ana bei na ameshanunuliwa na ndio maana ameamua kufanya aliyofanya jana pale Serena. Kwa kifupi ame disappoint watu wengi na pia kujijengea uadui mkubwa na watu wa kada mbalimbali wakiwemo wapiga kura na watu waliokuwa na mapenzi mema na yeye.

Na madhara haya yatamfuata kwa miaka mingi sana ya watu kumuona mtu wa hovyo. Watu 'walimwamini kwa makubwa' (na wakampa mapenzi makubwa) mno lakini tazama 'alivyojiangusha kwa madogo' bila kujali kazi njema aliyoijenga kwa miaka tele.
 
CCM walitoa rushwa kwa Lipumba ili kuvuruga upinzani lakini mbinu hiyo haikulipa! Wananchi wakamdharau na Ukawa ikasonga mbele. Sasa CCM wameibuka na mbinu ya Penati ambapo Dr Slaa amehongwa ili apige bao la kuifunga timu yake mwenyewe.

Lakini inaonakana kapiga bao hafifu na wananchi wamezuia goli! Wamemwambia amechelewa! Sasa Dr Slaa ajihadhari. CCM wanaweza kumfanyia chochote kibaya na hata kumuua na kisha kuwasingizia Wapinzani kama mbinu yao ya mwisho iliyobaki..
 
Leo ni aibu kuona comment za kejeli na matusi ambayo wanachama wamekua wakimkosea heshima Dr Slaa.
Kwa namna mzee huyu alivyopambana kwa jasho na damu shukrani aliopatiwa haikustahili,
Hivi kama mti mbichi mmeutenda hivi je mti mkavu utaufanyaje?
Hii ndio inayoitwa shukrani ya punda,
Kwa namna chama hiki kinavyoongozwa kibabe ni wazi wengine wanaofikiri wamesimama basi na wajiandae.
L'su,mny'ka,na wengineo mjiandae siku yenu inakuja
Kuna CHADEMA ASILI na kuna CHADEMA LOWASSA. Hawa CHADEMA LOWASSA hawawezi kumuelewa Dr. Slaa alichosema, watamtukana na kumkashifu sababu hawa ni wahamiaji tu, hawajui uchungu wa CHADEMA. Hawajui mchango wa Dr. Slaa kwa CHADEMA.Hawa ni "friends of Lowassa" 4U MOVEMENTS; ni wahamiaji tu, hawa ndio kila siku wanaandika "ulipo tupo". Lowassa alipokuwepo CCM walikuwa nae. sasa hivi yupo CHADEMA wako nae. Lakini kuna kundi la wanachama, hawa ni CHADEMA asili. CHADEMA asili wanajua uchungu wa CHADEMA, wanamuheshimu Dr. Slaa kama CCM wanavyomuheshimu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere! Hawa CHADEMA asili wanaujua mchango wa Dr. Slaa kwa CHADEMA. Wanafahamu wazi kuwa Dr Slaa ndio aliyekijenga CHADEMA na kufikia hapo kilipo. Kamwe maisha yao yote hawawezi kumpuuza na kumdharau Dr. Slaa. CHADEMA asili ndio wanajua walipotoka na CHADEMA mpaka leo hii. Hawa ni vijana ambao kwao Dr. Slaa ni "hero". Hawa vijana ndio watakao washa moto usiozimika CHADEMA! ....."friends of Lowassa" ni wahamiaji tu, na hawana uchungu na CHADEMA. Kilicho wapeleka pale ni Lowassa tu. Hawa ni watu wasiomjua Dr. Slaa na kwao hana dhamani yoyote ile, hawa ndio watu tunao waona hapa JF wakimtukana Dr. Slaa kwa kila aina ya matusi. Viongozi wa CHADEMA dhambi hii itawatafuna siku zote za maisha yenu. Dhambi ya kuuza chama kwa "fisadi Lowassa" kamwe haitawaacha mkae kwa amani.
 
umuhumu wake umepotea kwan angekuwa na ghamira ya kweli ya hicho anacho kisimamia basi ange wasaidia wenzake ndipo aje baadae na hoja zake ila sasa kawa msaliti pia ajue hata bila mboye chadema kitakwepo na mabadiliko ni lazima
 
Leo ni aibu kuona comment za kejeli na matusi ambayo wanachama wamekua wakimkosea heshima Dr Slaa.
Kwa namna mzee huyu alivyopambana kwa jasho na damu shukrani aliopatiwa haikustahili,
Hivi kama mti mbichi mmeutenda hivi je mti mkavu utaufanyaje?
Hii ndio inayoitwa shukrani ya punda,
Kwa namna chama hiki kinavyoongozwa kibabe ni wazi wengine wanaofikiri wamesimama basi na wajiandae.
L'su,mny'ka,na wengineo mjiandae siku yenu inakuja

Hata shetani alikua ni Malaika kabla hajaasi...! Sasa huwezi kuendelea kumsifu shetani kwa kofia ya malaika, Unaweza ukajijengea heshma kwa miaka mingi na ukaibomoa ndani ya nusu saa...! Ndicho kilimpata Dr Slaa, ajilaumu mwenyewe kwa kuelemewa na mapenzi kuliko chama chake alichokipigania kwa nguvu zake zote.
 
Kitendo alichokifanya lipumba na Dr ni vya kutuumiza wa tz walishiriki mwanzo mwisho kumkaribisha Lowassa, wamenunuliwa na ccm ili kuivuruga UKAWA,wamejivunjia heshima wao wenyewe.
 
Kwa kuwa amekuwa mzalendo na mwanaharakati kwa muda mrefu,na kwa kuwa amekuwa mstari wa mbele katika kukuza na kuendeleza chama,na kwa kuwa aliwekeza rasilimali akili na moyo wa dhati na kwamba aliweka maisha yake shakani na kupata misuko suko mingi kufanikisha haya heshima yake itakuwa active hadi 01/09/2015. Kwa umri atakaojaaliwa na mwenyezi Mungu kuishi ajue database ya heshima yake haitokuwa updated!Amewaudhi sana waliomwamini!
 
Slaa lazima apuuzwe kwa sababu amesaliti vuguvugu la mabadiliko ambalo yeye mwenyewe alikuwa sehemu yake kwa miaka 20. Alichoongea 90% ni upotoshaji (biased interpretation) kwa kutumia nyaraka ambazo tayari ziko kwenye public domain (hakuna jipya) kwa lengo la kumshambulia kibinafsi Lowassa na kudhoofisha upinzani. Kwa taarifa: kuhusika kwa Lowassa katika Richmond (uwajibikaji wa kisiasa) ni sawa na kuhusika kwa Pinda katika Tegeta Escrow; mtakumbuka kutokujiuzulu kwa Pinda ilikuwa ni compromise tu ya iliyofikiwa bungeni. Eti hamwezi kutafakari hili? Richmond ilibadilishwa jina na kuitwa Dowans; na sasa inaitwa Symbion. Wamiliki ni walewale! Mwaka 2013 Rais Obama alialikwa na akaizindua upya hiyo mitambo kwa mbwembwe nyingi. Lowassa anahusikaje hapo? Kwa hesabu za haraka, 'mkutano wa Slaa' uligharimu zaidi ya Sh 200 milioni. Nawapa changamoto mfuatilie aliyeratibu na kulipa hizo gharama kwa kuzingatia usemi huu: "He who pays the piper chooses the tune" ("Mlipa mpuliza zumari huchagua wimbo").
 
Hata shetani alikua ni Malaika kabla hajaasi...! Sasa huwezi kuendelea kumsifu shetani kwa kofia ya malaika, Unaweza ukajijengea heshma kwa miaka mingi na ukaibomoa ndani ya nusu saa...! Ndicho kilimpata Dr Slaa, ajilaumu mwenyewe kwa kuelemewa na mapenzi kuliko chama chake alichokipigania kwa nguvu zake zote.

Hii ni miongoni mwa comment za kejeli,leo kumfananisha mzee yule na malaika muasi yaani shetani si sawa,Mzee yule lazima aheshimiwe kwani maamuzi yake na alichoongea ni mawazo na mtizamo binafasi,hata kama atajibiwa lakini si busara kumkejeli na kumtukana,tunahitaji tuwe waungwana
 
Dr.WILBROAD SLAA ALINUNULIKA,HILO LIKO WAZI,ILA SISI WATANZANIA:-

-TUTAMPIGIA KURA EDWARD LOWASSA NA SIO MAGUFULI. Hakika!
 
Kwa kuwa amekuwa mzalendo na mwanaharakati kwa muda mrefu,na kwa kuwa amekuwa mstari wa mbele katika kukuza na kuendeleza chama,na kwa kuwa aliwekeza rasilimali akili na moyo wa dhati na kwamba aliweka maisha yake shakani na kupata misuko suko mingi kufanikisha haya heshima yake itakuwa active hadi 01/09/2015. Kwa umri atakaojaaliwa na mwenyezi Mungu kuishi ajue database ya heshima yake haitokuwa updated!Amewaudhi sana waliomwamini!

Amewaudhi wahamiaji haramu, yale makundi yanayo ambaa ambaa na Lowassa kokote aendako. Kwa wale wazawa wa CHADEMA, raia halisi wa CHADEMA, wazalendo halisi, CHADEMA ilikoma pale tu miiko yake ilipokiukwa na interest za watu binafsi kutamalaki. Historia itaongea
 
Leo ni aibu kuona comment za kejeli na matusi ambazo wanachama wamekua wakimkosea heshima Dr Slaa.
Kwa namna mzee huyu alivyopambana kwa jasho na damu shukrani aliopatiwa haikumstahili,
Hivi kama mti mbichi mmeutenda hivi je mti mkavu mtaufanyaje?
Hii ndio inayoitwa shukrani ya punda,
Kwa namna chama hiki kinavyoongozwa kibabe ni wazi wengine wanaofikiri wamesimama basi na wajiandae.
L'su,mny'ka,na wengineo mjiandae siku yenu inakuja

Baada ya ziara ya PAPA nchini Dr Slaa alikubaliwa na makao makuu kustaafu na kuagwa na kanisa kwa sherehe kubwa. Baada ya kustaafu Dr. Slaa alirudi kwao Karatu na kuanzisha miradi ya jamii, aliweza kupata wafadhiri mbalimbali hivyo kufanikiwa kuleta maendeleao Karatu. Baada ya wananchi kuona mafanikio yake, walimwomba agombee ubunge, na kweli akagombea kupitia CCM, CCM waliona kama ni mgeni katika siasa wakakata jina lake na kumpa mshindi wa tatu aliyekuwa mbunge wakati huo. Hivyo basi wananchi wakamshawishi kuhamia chama cha upinzani na kuwa wangempa kura, Dr Slaa akahamia CHADEMA wakati huo CHADEMA hakina umaarufu kama sasa, chama kilichikuwa maarufu kilikuwa ni NCCR mageuzi. Dr Slaa akashinda kwa kishindo na kuwa mbunge wa kwanza kutoka CHADEMA na Dr Warid Kabour kutoka jimbo la Kigoma mjini. Tangu mwaka huo Dr Slaa alikifanya CDM kuwa chama chenye nguvu kwa kupambana na CCM iliyokuwa na wabunge zaidi ya 80% kwa kusimamia alichoamini bila kuyumba, baade alipata support baada ya Mbunge kijana Zitto Kabwe kuingia bungeni hivyo CDM ikapata nguvu kwa kuwa ilijonyesha ndiyo CHAMA cha kutetea wanyonge. Dr Slaa hajapewa heshima stahili. tuache kumbeza.

Kwa wasio jua Dr Slaa ndiye aliyeanziasha taasisi ya tiba ya CCBRT na ni mkurugenzi wa board. Nafikiri ni taasisi peke hapa nchini inayotoa tiba ya ulemavu wa viungo na macho kwa gharama nafuu.


In 1994: With the support of CBM, Dr. Willbrod Slaa, (still on the CCBRT Board) and Geert Vanneste founded CCBRT. Their mission was to contribute towards poverty alleviation by making rehabilitative services accessible and affordable to people with disabilities. In 1994, CCBRT was registered as a private Non-Governmental Tanzanian Society (NGO), under the Tanzanian Societies Act, No SO8261.
 
Back
Top Bottom