Nicholaus Kilunga
JF-Expert Member
- Feb 15, 2014
- 1,188
- 570
Wana Jf wasalaam!
Mmoja kati ya watu walio kuwa wanautaka Urais na walitegemea sana ndio wataongoza kijiti cha UKAWA ni Dr.W.Slaa ambaye kwa sasa amesusa kabisa baada ya kupatikana mbadala wake..!
WanaJf kama mtakumbuka siku ya mkutano wa CHADEMA pale mwanza Dr Slaa alipokelewa na wananchi kwenye gari la wazi huku akiwapungia mkono, kwakweli Dr alidhani kabisa ameshakuwa Rais na kwa kuonesha furaha alianza kuruka ruka kwa furaha,kama Mungu angemuonesha kuwa mbeleni atakatwa basi asingeliruka kabisa na angesusa kwenda kwenye mkutano kama alivyofanya sasa!
WanaJf tatizo la Dr Slaa sio Lowassa bali ni Urais, na laiti Lowassa asingegombea Urais wala Slaa asingesusa na kujifungia nyumbani kwake!
WanaJf, Slaa ana sifa zote za wanafiki waliotukuka maana asiye mnafiki husema wazi wala hakai kimya na kususa.Nilitegemea Slaa kama kweli anapinga suala la Lowassa ajitokeze hadharani na kusema sio kususa kama watoto
Watanzania hadi sasa hawajui msimamo wake na isitoshe wenzie wamesema na yeye alibariki Lowassa kushika kijiti cha UKAWA!
Kama kuna mwanaCHADEMA bado anafikiri Dr. Slaa bado ni mwana chadema basi mtu huyo atakuwa amechanganyikiwa!
Dr. Slaa sio mwana chadema tangu Lowassa alipokabidhiwa kijiti lakini kwa kuwa Slaa ni mnafiki sana basi hataki kuwambia ukweli anajifanya amesusa!
CHADEMA wanapoteza muda kumbembeleza Slaa lakini hawatofanikiwa kwa kuwa Slaa alishahamua kuachana na CHADEMA baada ya kukosa nafasi ya kugombea Urais..!
Sasa hivi anachofanya Dr. Slaa ni mbinu ya kuhakikisha kura za Lowassa hazitoshi kwa kuwagawa wana UKAWA na bila shaka atafanikiwa katika hili na hatoshiriki campaign za kumnadi fisadi!
Dr. Slaa aliizoea nafasi ya kuwa Rais kimvuli sasa anaona ndoto yake imepotea na hayuko tayari kuendelea na CHADEMA lakini kwa kuwa ni mnafiki basi hataki kuwambia ukweli CHADEMA!
Jambo ambalo wanaweza jaribu CHADEMA ili kumshawishi Slaa kumnadi Lowassa basi ni kumhaidi mshahara mnono kuanzia Million 20 kwa mwezi maana ili ndio tatizo lake na kamwe hawatofanikiwa kumshawishi kama hawatokwenda na wazo la Pesa!
Karibuni wanajamvi!
Ni upumbavu wa kiwango cha PHD kumponda na kumdis kwa namna yeyote Dr Slaa,nawachukia sana watu wa aina hyo