Mmmh! Kazi ipo! Hivi Slaa na Lowassa nani anamatatizo makubwa. Lowassa wengi tumejua habari zake, hebu mnisaidie wanajamii katika kutafakari kwangu huku. Slaa alikuwa padrii, akatofautiana na wenzake, akaacha utumishi huo, akaoa, akatofautiana na mkewe, akamwacha hadi leo, akaingia kwenye siasa ccm, akaona sivyo kwa nmna ajuavyo yeye, kaachana nao, kaingia chadema, ametofautiana na uongozi kwa jambo moja la kumkaribisha Lowassa, ameachana nao. Kwa kifupi akitofautina tu na wenzake anakuwa wa kwanza kukimbia, je, hizo ni sifa za kiongozi mzuri? Na je, kila sehemu hizo alizozikimbia zote yeye tu ndiye yuko perfect by 100%? Nina mkanganyiko hapo, tusaidiane wanajamii forum.