Unanipangia sehemu ya kuomba kazi? Mengi akatafete gesi huko Moshi Kilimanjaro. Mtwara hatumtaki. Mengi ni tapeli, mbinafsi
Kama wamasai anavo watetea ardhi yao ya asili nae mengi huko mtwara hakumuhusu.
Hata iweje haiwezekani serikali ije itowe kitalu cha kuvuna gas kwa mengi...haitowezekana kila mtu mtanzania ana haki hio wala serikali isijaribu kuleta futina hio...ndio mwanzo wa fujo na majaribu.
Kama anayo fedha aingie katika mchakato kama wengine wanapo omba alipie na aoneshe kuwa ana uwezo wa ku explore gas katika muda ulopangwa.
Kupewa bure bila ya masharti ni wizi na dhuluma kubwa kwa watanzania.
Kila mmoja tuna haki ya kupewa ..kwanini mengi peke yake ?
Huko wanako dundana na ambako hakuna utulivu ni kwa sababu ya kugaiana vitalu kwa watu wa tabaka fulani ili kama njia ya kuwanyamazisha kelele zao.
Lakini leo huko Nugeria kuna boko haram kwasababu tu watu wachache wamegawana vitalu na kufaidi peke yao.
Huko gabon ni familia ya Bongo na marafiki na wafanya biashara wachache ..hatima yake Gabon hakuna cha maana na serikali inalindwa na Ufaranza.
Huko Congo ya Brazaville pia waligawa vitalu kwa wana familia na wafanya biashara wachache wanao jiita wazawa hatimae mpaka leo hakuja tulia vuta ya wao kwa wao.
Hata Angola tuna ina mtoto wa Do Santos ndio tajiri kuliko wanawake wote wa Afrika.yote ni 10% kutoka wazawa wachache walopewa vitalu peke yao kutajirika.
Utajiri wa gas ni wetu sote na serikali pekee iwe ndio share holder kwa niaba yetu.
Inachotakiwa ni kwa mengi kupigania uwazi na ubora wa mikataba hii na sio ubinafsi wa kutaka apewe yeye...hilo halitowezekana