Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani Kigamboni

Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani Kigamboni

The big show umeona ya kilango,ukiona ya mramba,kama huna taarifa basi hyo ndo system Leo mnacheka kesho lupango

Kabla sijaanza kuongea ngoja nimkaribishe mtu mwenye mchango mkuubwa kabisa katika Daraja hiliii...

Na yeye si mwingine nae ni Dr Dauuu...

Hebu Dr Dau Njoo Hapa mara moja uongee kidogoo...

Makofiii Makofiiii...

Teh teh teh...

Mfikishie Salaaam Magoriii...

Mwambie aendelee na Tunguri...

Hayo ya kilango sijui mramba mm yananihusu nin...

Kilango si nimemuona juz kanisani?sijui alienda kuuungama?

Teh teh teh Magufuli noma sana
 
1461125085471.jpg
zaidi sana kwa unafaika huu .lazima utetee
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Acheni mambo ya udini, serikali ya Tanzania haina dini, hiyo hakuna sababu ya kujadili dini ya mtu kwenye masuala ya serikali kwa sababu ni suala binafsi. Baada ya kubaguana kwenye dini mtaanza kubaguana kwenye makabila kisha rangi, mkifika huko hakuna atakayekuwa na ujasiri wa kusema sisi ni wamoja.
 
Nenda shule kasome sio kuhorojoka na maneno ya mtaani.kabisa na akili zako wazee zako unaambiwa eti alimaliza units zote akawa anasubiri kumaliza tu...sio mnakuja Jf na habari za kutunga..

Hiyo habari kwako ni ngeni kwa kuwa umesoma vyuo vya Matopeni. Hapa JF ukifungua baadhi ya thread lazima ujue upo darasani hivyo uwe na peni na karatasi kwa kuwa kuwa kuna elimu mpya utakuwa unafunzwa. unaposoma Vyuo vyote vikubwa ikiwemo UDSM miaka hiyo (sijui siku hizi) unaruhusiwa kuchukua hata units za watu wa miaka ya mbele kama ratiba haziingiliani, uwezo huo unao na ikifika class yako huta attend class wala ku sit mitihani uliyokwisha ifanya. Usijifedheheshe kwa kudhani ni jambo geni kwa kuwa tu ulihudhuria chuo (kama kweli) lakin hukuwahi kulijua hilo
 
Jadi,
Kuna mwandishi alifika NSSF kutaka kumhoji Dr. Dau kuhusu
shutuma kuwa NSSF ina ajiri Waislam.

Afisa Uhusiano wa NSSF akamwabia angependa maswali yake
kwa Dr. Dau.

Afisa uhusiano alipoona kuwa moja ya maswali ni hilo la kuajiri
Waislam akamuuliza kwani hairuhusiwi kuajiri Waislam?

Mwandishi hapo akaanza kubabaika kwa kuwa hakutegemea swali
kama lile.

Afisa Uhusiano akamwambia naweza nikakuunganisha na Dr. Dau
lakini mimi nitaka nikuonye.

Akamwambia kuna shirika la serikali limefanya mahojiano hivi majuzi
na walioajiriwa ni Wakristo watupu.

Una nini la kusema kuhusu hili?
Mwandishi akasema hana taarifa hizo.

Akampa jina la shirika hilo na akamshauri kwanza aende huko kuuliza
akimaliza ndiyo arejee NSSF.

Mwandishi akakusanya mizigo yake akaondoka mnyonge.

Mzee wangu Mohamed Said napata ukakasi na maneno yako sana....inaonyesha kuna kitu kimekukaa rohoni baada ya huyo bwana kutolewa Nssf..kuna sehemu hapo nyuma ulisema moja ya maajabu yake kutembea nchi nyingi duniani sijajua umeweka kwenye maajabu kwa misingi ipi...hila yote kwa yote punguza mahaba ya ukereketwa maana yakizid sana yanakuwa ugonjwa
 
Ukimuandama mtu kwa dini yake jua atatetewa kwa dini yake!
Ushawahi kusikia Rostam,Karamagi, Said lugumi katetewa kwa dini yake?
Chuki yenu dhidi ya Dr.Dau imeanza tangu kateuliwa January 2001 kabla hajaanza lolote NSSF mlishaanza Chuki na husda zenu.

Kama ni tuhuma za ufisadi wanazo wengi what is so special kwa Dau mpaka mnafikia kumtoa kwny vigazeti vyenu anasulubiwa?
"...Kama mnashindana shindanen kwa yaliyo bora..."

Fanyeni kazi bora kuliko aliyofanya badala ya kuishia kufoji Auditors report na kusambaza na kutumia nguvu kubwa kumuandama wakati alikuwa ni Mkurugenzi tu Mfuko wa hifadhi ya Jamii!
sasa kama kapiga hela za wanachama wa NSSF watu tukae kimya kwa 7bu alikuwa mkurugenzi wakati kaiba fedha za umma?
 
dr dau haandamwi kwa DINI bali anaandamwa kwa UFISADI. wale waliokosa hoja ndio wanahusishaj suala hili na dini. wapuuzi wakubwa!
 
Franco Zetta,
Unajaribu kunifedhehesha kwa lugha ya kebehi na dharau.
Waswahili tuna msemo: Asiyekujua hakuthamini.

Hayo usemayo mengine wala hayapo katika mjadala wetu,
Hunifahamu kwa hiyo unaweza kusema lolote likujialo akilini.

Wala hoja hii kwangu mimi toka nakujibu mwanzo haijapatapo
kuwa ni kwa kuwa Dr. Dau kaondolewa NSSF na kupewa ubalozi.

Mimi nimetembea dunia lakini siwezi kufikia hata theluthi ya nchi
ambazo Dr. Dau katia mguu wake.

Hii ni moja katika maajabu yake.
Rejea tena nikupe mengine ya Dr. Dau.
wewe mzee mbona unazeeka vibaya? tetea hoja, acha kurukaruka. kutembea dunia kwa dr dau hakuwezi kumuondolea tuhuma za UFISADI zinazomkabili. subiri siku akifikishwa mahakamani uende ukamtetee.
 
wewe mzee mbona unazeeka vibaya? tetea hoja, acha kurukaruka. kutembea dunia kwa dr dau hakuwezi kumuondolea tuhuma za UFISADI zinazomkabili. subiri siku akifikishwa mahakamani uende ukamtetee.




Mzee wangu MS ananipa mashaka kuamini kwamba anazeeka vibaya
 
Mzee wangu Mohamed Said napata ukakasi na maneno yako sana....inaonyesha kuna kitu kimekukaa rohoni baada ya huyo bwana kutolewa Nssf..kuna sehemu hapo nyuma ulisema moja ya maajabu yake kutembea nchi nyingi duniani sijajua umeweka kwenye maajabu kwa misingi ipi...hila yote kwa yote punguza mahaba ya ukereketwa maana yakizid sana yanakuwa ugonjwa
Makodinda,
Bahati mbaya sana kuwa kauli zangu zinakutia ''ukakasi.''
Kuwa kuna jambo limenikaa rohoni hilo umesema kweli.

Sipendezwi na hizi chuki dhidi ya Dr. Dau na ndiyo maana
niko hapa tunajadili lakini sijachukia yeye kutolewa NSSF
na kufanywa balozi.

Kuna aya katika Qur'an Allah anasema unaweza kulichukia
jambo nalo lina kheri na wewe na ukalipenda jambo lina
shari nawe.

Hili la ''globe trotter,'' hakika ni katika maajabu yake na mimi
si mtu wa kushangazwa na hilo kwani Alhamdulilah nimesafiri
kiasi changu.

Nilipata kuzuiwa siku za nyuma Heathrow Airport London kisa
pasi yangu imeingia nchi nyingi sana wakataka kujua vipi na
siku hizo ni kijana katika miaka ya kati.

Miezi mitatu baada ya mkasa ule nikaja tena London.

Mtu wa Uhamiaji kashangaa akaniuliza, ''Wewe si juzi juzi tu
ulikuwa hapa?''

Haukupita mwaka nikaingia tena London lakini nikitokea Paris.
Hawa jamaa wanapenda sana kuweka taarifa.

Akaniuliza nimekuja kufanya nini?

Nikamwambia nenda Cardiff nina shida kidogo na nitaondoka
hata juma simalizi.

Juu ya hilo ilikuwa wakati wa Hija na nilitaka nipite Uingereza ili
niswali Eid Kubwa Regents Park Mosque London.

R6C8a7km-YmWQVzxU-s5fsYEyvGilxIvLOjU60FQ36Ucjvu9zGKnuBGO_W6hSSZtn4lzn17T0vag8UKIx0VTKN2UI9XmfEg30tEk_EG2U-h7neEH_BFA-uuEubgpKDQIsgumcR9AyDVBqVfYyUeXRDGg_7e5No87Ohb_l9bO74r4YQQ5jsr6h28MP1xj7VlEW1fs5XLksAaYWXX6JohoxwUzPsiKQuBbBln_jeQIeQhMgMhm1Ve9SzoRWZx_fLdiJs_zyB5z3BEXmTxpgZWVGhnRuS1J6PiqhO4J6MyUGhCC3FuDsvUXomHK3DwF877AT-wyQ1p_h8_peWeARoXzuQhkKLQI8ehkM_05hMHYCWdpyAvSLnGoUlPziWKjJrpkIApXmqBasjOpGS3gk-uwjUawGMfCRhoYub1XWqILxAI3FWc6MLegmoGDhlKs5cj1GJBULjwi1T_llsFh7vssp3gvx10XunS_qdOUvBIbzXqYORfLW0IYLQEf2LqbBomOj9jl4FK4c8ZQyDOez9hdgVbY7j4Dr3RTxZtQw30nSPfd1JCQdOIZzcWZW4OxMQx1Lkf11g=w435-h643-no

Niko Paris Central Mosque

Kwa hiyo labda kwa kuwa wewe hujui ukubwa wa hilo ukaona
si kitu kukuambia kuwa Dr. Dau kaitembea dunia.

Ama kuhusu mahaba na ukereketwa vyote hivyo ni sifa zangu
wala hukukosea.

Katika mafunzo yetu hizi ni sifa njema sana kwani zinampamba
mtu katika jamii.

Sifa hizi ajabu yake hujidhihirisha siku unapokwenda kuzikwa.

Baba yake Dr. Dau alipokufa alipata maziko hayapata kuonekana
Dar es Salaam.
 
Ila kiukweli wahusika wakuu wengine wa sherehe ukitoa rais na mwingine, walikuwa wakitaja wageni waalikwa ila Dr. Dau hawakuwa wanamtaja. Hata katibu wa shughuli hakumtaja.
Na lazima utumie akili kujiuliza, kwa nini rais alimuita Dr. Dau?? Ni baada ya kuona hamna aliyemtaja kama ambavyo 'alistahili'!
Ki-ukweli kuna mushkeri, hata TBC wakati wa prime time (saa mbili usiku), clip ya Dr. Dau ilikuwa na urefu wa sekude takribani 0.25!!!
 
dr dau haandamwi kwa DINI bali anaandamwa kwa UFISADI. wale waliokosa hoja ndio wanahusishaj suala hili na dini. wapuuzi wakubwa!
Ufisadi upi km nyir sio wanafiki?

Leta Ushahidi wa mahakama iliomhukumu kwa kosa la Ufisadi.

We unajifanya kipofu sio?
Huoni nyie wote mnaompakazia huyu DR kesi ambazo HAJASHTAKIWA nazo ni nyie ni Makatonta wa Vatican?
 
Hata mm nashindwa kuelewa
ina maana Dr Dau angebakia basi Daraja la Dar - Zanzibar lingewekwa?
hivi mnajua hizo pesa zas Wanachama wa NSSF hawaambulii lolote
hakuna cha riba
hakuna kupewa kwa wakati
wengi wanafariki na kuziacha nyuma
km ningekuwa na uwezo mifuko yote ningeifunga ukabaki mmoja tu
toka Mzazi wangu alipokosa na akafariki tukaambiwa yameisha siiamini tena mifuko hii ya ujanja ujanja
Mkuu kuna manunda hayajui hili na badala yake yanashangilia UJINGA tu eti kwa kuwa ni 'MWENZAO'
 
Back
Top Bottom