Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani Kigamboni

Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani Kigamboni

CfxBWfdXEAAmTkA.jpg


2016%2B-%2B1


Hizi picha nimezipenda kuna watu watazikimbia muda si mrefu.
Prof Ngongo.

Naona sasa hivi umeachana na ile ripoti ya CAG umeamua kujikita kwenye maswala ya picha na utabiri.
 
Jamani maneno yamipasho hayasaidii hili taifa huru na kila kazi inautekelezaji wake in short sio yeye alie leta mpango mkakati wa daraja yeye alikuwa pale kama mtumishi kutekeleza matakwa ya watu wake in short kuna maswali watanzania wanataka kujuwa ikiwa daraja lietafuna 200B na huyo bwana mkubwa anasemekana anaukwasi wahatari unaofikia 100B atueleze alizipataje watanznia tunataka ukweli kuhusu hili full stop

Inasemekana, inasemekana, inasemekana...
 
MBUNGE mkongwe wa Jimbo la Rombo mkoani Kilimanjaro, Basil Mramba, ameibuka na kaulimbiu ya kutetea kiti chake hicho, akijifananisha na panga la zamani, lakini
likiwa na makali mapya.
Mbali na hilo, mwanasiasa huyo amewaeleza wapiga kura wake kwamba wasiache mbachao kwa msala upitao na mcheza kwao hutuzwa.
Mramba aliyewahi kushika madaraka ya uwaziri katika serikali za awamu zote nchini, amejitetea pia kutokana na umbile lake fupi, akiwaeleza wananchi kwamba wanapaswa kuwachagua watu wafupi ili wakawasimamie warefu.
Waziri huyo wa zamani aliyasema hayo leo kwa nyakati tofauti alipotambulishwa kwa wananchi katika mikutano ya kampeni jimboni kwake, na Mgombea Urais wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
“Nyie mnanifahamu, kazi zangu mnazifahamu. Nia ninayo, nguvu ninazo na uwezo ninao. Panga la zamani, lakini makali yale yale…msiache mbachao kwa msala upitao na mcheza kwao hutuzwa,” alisema Mramba.
Akimnadi Mramba, Rais Kikwete alisema mwanasiasa huyo ni mbunge wao wa miaka mingi, lakini akammiminia sifa kuwa ni mzee kijana, ambaye amekuwa na mawazo mapya wakati wote.
“Huyu kwa maneno ya mjini, ni Mzee Kijana, kwani ni mwenye mawazo mapya yenye manufaa wakati wote…siyo wale wazee ambao wakichoka la mbele linawekwa nyuma, la nyuma linawekwa mbele. Huyu ubongo wake unajadidika (renewal), ni chimbuko la maarifa mapya,” alisema Kikwete.
Awali, akielezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005-2010, Mramba alieleza mafanikio makubwa katika sekta mbalimbali, na kumshukuru Rais Kikwete kwa kuipatia barabara za lami Rombo; maji ya uhakika; kuipatia vocha za ruzuku za pembejeo na umeme vijijini.
Alisema katika miaka mitano ijayo, kazi kubwa ya Rombo ni kupambana na umasikini
wa watu katika kaya, na nia yao ni kuwawezesha wananchi ili kuondokana na umasikini na kujipatia kipato.

jakaya2010kikwete at 12:11 PM
 
Magori umeona?Dau siyo level yako Magorii...

Aibu kwako sasaa...na Ukurugenz pia umekosaa...

Kaa utulie na tunguri zako
 
Magori umeona?Dau siyo level yako Magorii...

Aibu kwako sasaa...na Ukurugenz pia umekosaa...

Kaa utulie na tunguri zako

The big show umeona ya kilango,ukiona ya mramba,kama huna taarifa basi hyo ndo system Leo mnacheka kesho lupango
 
2016%2B-%2B1


2016%2B-%2B1



‘’Wastara haumbuki,
Wa mbili havai moja…’’

Haya ni baadhi ya maneno kwenye nyimbo niliyokuwa nikiisikia katika gramaphone nyumbani kwetu wakati nikiwa na umri mdogo sana. Mama yangu akipenda kuuimba mwimbo huu kila afanyapo kazi iwe kupika au kufua. Kuna beti za mwisho nazikumbuka na nikizpenda sana. Zilikuwa na maneno haya:

''Kwetu Congo natumaini,
Kwetu Kongo natumaini.''

Beti hizo nilizipenda kwa kuwa akifurahi alikuwa akiniadhimisha kwa kuniambia kuwa mimi nimetoka Congo.

Wakati huo Bi. Hawa biti Maftah mwanamke wa Kimanyema akimuimbia Nyerere mwimbo
maarufu katika mikutano ya TANU Mnazi Mmoja: ''Hongera mwanangu hongera...''

Wakati ule Dar es Salaam ilikuwa ndogo na jamii ya Kimanyema mjini ilikuwa na hadhi ya kipekee.

Kuanzia wanawake wao hadi wanaume.

Kubwa ni yale maumbo makubwa ukimouna mwanamke wa Kimanyema kapanda ana futi
sita na mwanamme halikadhalika.

Basi nilikuwa nizkizisikia beti hizo mama akiziimba nikawa nasisimkwa na mwili.

Nilipopata umri na kila nilipokutana na shida za dunia khasa katika mambo ya hasad na mengine kazini na kwengineko, vikwazo na nini... mama yangu akinambia: ''Wa mbili havai moja.''

Maana yake ni kuwa ikiwa Allah kakuandikia kupata ndivyo itakavyokuwa hivyo hivyo hata zije fitna kiasi gani.

Ndipo hapo inaingia, ''Wastara haumbuki.''
Yaani hutoweza kumfedhehesha aliyenyanyuliwa.

Fuatilia ukurasa huu...

2016%2B-%2B1

Posted 2 hours ago by Mohamed Said
Nyerere Bridge ndio imeshakamilika, Watanzania wote bila ya kujali dini, rangi au itikadi za Vyama hatuna budi kujivunia mambo yetu.
 
Walimuanza January...waka shindwa..sasa wamehamishia fitina zao kwa Dau.
 
tatizo sio dau tatizo uislam wake mungu akupe kila lakheri kwakuipenda dini yako na mola wako
 
Prof Ngongo.

Naona sasa hivi umeachana na ile ripoti ya CAG umeamua kujikita kwenye maswala ya picha na utabiri.
Kwanza kwenye ripoti ya CAG hakuna swala LA daraja ufujaji ktk ripoti upo kwenye majengo na viwanja,sasa huko kachomeka atachomoaje?
 
Kwanza kwenye ripoti ya CAG hakuna swala LA daraja ufujaji ktk ripoti upo kwenye majengo na viwanja,sasa huko kachomeka atachomoaje?
Mkuu hiyo ripoti unayo tuwekee basi tuitadavue.
 
Swali lili kusudiwa liwe jinsi lilivyo kuwa na hapana shaka yoyote, na wala si haja yangu kumjua huyo mhisani wako zaidi ya anavyo julikana na alivyo jidhihirisha.
Franco Zetta,
Huwezi kujua Dau ana hisani na watu wangapi katika mji huu
mimi nikiwa mmojawapo na ni rafiki na ndugu yangu wa miaka
mingi.

Sasa nakupa nyingine.
Dr. Dau ni bingwa wa kuzungumza Kiingereza.

Rudi tena nikupe nyingine.
 
  • Julius Nyerere International Airport
  • Mwalimu Nyerere University
  • Mwalimu Nyerere Foundation
  • Kigoda cha Mwalimu Nyerere
  • Uwanja wa Kambarage Shinyanga
  • Mwenye Heri Nyerere
  • Daraja la Nyerere
sasa hivi vitu vinamsaidia nini nyerere mwenyewe huko aliko au hata familia yake.
tumia hata akili yako ndogo ya kulia mikate.
 
ACHENI KUMPA TU SIFA ZA KIJINGA. HIZO FEDHA ZILIZOJENGA DARAJA ZIMETOKA MFUKONI MWAKE AU NI FEDHA ZA WANACHAMA WA NSSF WANAOKOSA MAFAO PINDI WAKISTAAFU?
 
Matusi ya nini mkuu kwani kila mtu si atabeba mzigo wake mwenyewe? Saaana dau mtamuwekea dhamana tusigombane kwa mambo ya kipuuzi Lisa mtu mmoja tena mjinga anatetewa na wajinga wengine,tuwe na maono kuhusu mustakabali wa taifa letu,
Vyombo vya kiuchunguzi vikimuona DAU Hana Shida ataishia raha mustarehe

"New castle ya Mtanzania mwenzetu Dau" leo inacheza na Man City!!!
 
Hili swala la Dau kwanini mnaligeuza kama vita ya kidini?

Dau ni mtanzania mwenzetu na ameitumikia nchi yake vema...

Acheni kuchochea udini...
AMEITUMIKIA NCHI YAKE VIZURI KWA KUFISIDI MICHANGO YA WANACHAMA WA NSSF KWA KUANZISHA MIRADI HEWA?
 
Back
Top Bottom