Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani Kigamboni

Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani Kigamboni

Humu ndani watu wana mihemuko, watu wanaweka busara mfukoni wanaendekeza mihemuko kwasababu zozote zile si sawa namuunga mkono raisi kutambua mchango wa Dr.Dau raisi amefanya kizuri kabisa aibu ni kuanza kukashifiana humu ndani kwa jambo jema kama hilo eti kwasababu tu ya dini, Ritz siko huko kabisa na sitaki kuwa sehemu ya mijadala ya kukashifiana haina tija.
Kuna watu hawana cha kufanya zaidi ya dini na sifa za kijinga. Rais kumpongeza Dau haijamfanya kuwa mwanzilishi wa Taifa hili na hata haiondoi wasiwasi wa watu juu ya tabia yake yoyote mbaya anayoweza kuwa nayo. Hata wale wanaofahamika kwa upuuzi wao ktk dunia hii walifanya makubwa kuliko hata ya Dau!

Hitler anasifika hadi leo kwa upuuzi wake lakini huwezi kumuondoa kwenye historia ya maendeleo ya ujerumani kama nchi. Sasa huyu Dau kuongoza taasisi moja tunamzungumzia utadhani kaokoa roho za watu wanaoangamia!
 
Dau yupo vzur sana hata hotuba yake alyoongea uutaona ni level nyingne kabisaaa,pigen kelele hazsaidii mpewa hapokonyek
Dau, Dau! Hotuba, Hotuba ipi hiyo? Kucheka ndo hotuba? Dak. 4 kuna hotuba ya kusifia kitu gani? Kama una elimu kidogo na kama lengo ni kuwasifia walio na dini kama yako, hebu sikiliza hotuba na mihadhara ya marehemu Ali Mazrui.
 
Umenikumbusha mbali sna sheikh Mohamed Said marehemu Baba yngu alikuwa na Rafiki kipenzi mzee wa Dar es salaam akiitwa Saad juma Mzee huyo saad Baba yke akiitwa Juma Mzee alikuwa anaishi kariakoo mtaa wa PEMBA alikuwa na mabasi yke alikuwa ameyaandika ilo jina au ni sema huo wimbo WASTARA HAUMBUKI WASTARA MJA WA MUNGU sasa sijui wanajisikiaje waliokuwa wanamuombe mabaya DK DAU bila Sababu ya msingi watanzania tuache chuki za kijinga na udini sio kuwa na sababu Ongera Dk Ramadhani Kitwana Dau
 
2016%2B-%2B1


2016%2B-%2B1



‘’Wastara haumbuki,
Wa mbili havai moja…’’

Haya ni baadhi ya maneno kwenye nyimbo niliyokuwa nikiisikia katika gramaphone nyumbani kwetu wakati nikiwa na umri mdogo sana. Mama yangu akipenda kuuimba mwimbo huu kila afanyapo kazi iwe kupika au kufua. Kuna beti za mwisho nazikumbuka na nikizpenda sana. Zilikuwa na maneno haya:

''Kwetu Congo natumaini,
Kwetu Kongo natumaini.''

Beti hizo nilizipenda kwa kuwa akifurahi alikuwa akiniadhimisha kwa kuniambia kuwa mimi nimetoka Congo.

Wakati huo Bi. Hawa biti Maftah mwanamke wa Kimanyema akimuimbia Nyerere mwimbo
maarufu katika mikutano ya TANU Mnazi Mmoja: ''Hongera mwanangu hongera...''

Wakati ule Dar es Salaam ilikuwa ndogo na jamii ya Kimanyema mjini ilikuwa na hadhi ya kipekee.

Kuanzia wanawake wao hadi wanaume.

Kubwa ni yale maumbo makubwa ukimouna mwanamke wa Kimanyema kapanda ana futi
sita na mwanamme halikadhalika.

Basi nilikuwa nizkizisikia beti hizo mama akiziimba nikawa nasisimkwa na mwili.

Nilipopata umri na kila nilipokutana na shida za dunia khasa katika mambo ya hasad na mengine kazini na kwengineko, vikwazo na nini... mama yangu akinambia: ''Wa mbili havai moja.''

Maana yake ni kuwa ikiwa Allah kakuandikia kupata ndivyo itakavyokuwa hivyo hivyo hata zije fitna kiasi gani.

Ndipo hapo inaingia, ''Wastara haumbuki.''
Yaani hutoweza kumfedhehesha aliyenyanyuliwa.

Fuatilia ukurasa huu...

Nimeshindwa kuhusianisha Title na contents.
 
Franco Zetta,
Unajaribu kunifedhehesha kwa lugha ya kebehi na dharau.
Waswahili tuna msemo: Asiyekujua hakuthamini.

Hayo usemayo mengine wala hayapo katika mjadala wetu,
Hunifahamu kwa hiyo unaweza kusema lolote likujialo akilini.

Wala hoja hii kwangu mimi toka nakujibu mwanzo haijapatapo
kuwa ni kwa kuwa Dr. Dau kaondolewa NSSF na kupewa ubalozi.

Mimi nimetembea dunia lakini siwezi kufikia hata theluthi ya nchi
ambazo Dr. Dau katia mguu wake.

Hii ni moja katika maajabu yake.
Rejea tena nikupe mengine ya Dr. Dau.
Wala hayuko anaye kufedhehesha umea amua mwenyewe kuji fedhehesha kwa radhi yako,na ije siku uka baini fadhila ulizo kuwa unapata zilitokana na ufisadi ni haramu nawe umesema ni mtu wa ibada sipima hata utajisikiaje,haya nikutakie kila la kheri na Uwakili ulio jivika.
 
Wala hayuko anaye kufedhehesha umea amua mwenyewe kuji fedhehesha kwa radhi yako,na ije siku uka baini fadhila ulizo kuwa unapata zilitokana na ufisadi ni haramu nawe umesema ni mtu wa ibada sipima hata utajisikiaje,haya nikutakie kila la kheri na Uwakili ulio jivika.
Franco Zetta,
Unanitukana kisha unanambia nataka kutukanwa.

Hapa tulipofika panatosha hapana haja ya matusi
zaidi.
 
Diniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Mohammed Said niliingia wikipedia jana. Sikuliona kabisa jina la huyu daktari nguli wa masoko.
 
Kabla sijaanza kuongea ngoja nimkaribishe mtu mwenye mchango mkuubwa kabisa katika Daraja hiliii...

Na yeye si mwingine nae ni Dr Dauuu...

Hebu Dr Dau Njoo Hapa mara moja uongee kidogoo...

Makofiii Makofiiii...

Teh teh teh...

Mfikishie Salaaam Magoriii...

Mwambie aendelee na Tunguri...

Hayo ya kilango sijui mramba mm yananihusu nin...

Kilango si nimemuona juz kanisani?sijui alienda kuuungama?

Teh teh teh Magufuli noma sana
The big show utapotea humu jamvini siku si nyingi usidhani jpm kumsafisha dau kwa kashfa zingine zooote maana viwanja alivyonunua na ubia na azimio bado majibu zero,zile bilioni 179 bado majibu,nyumba anazomiliki nazo bado majibu na hayo majibu hana magufuli,kwenye kujua ya dau ni TAKUKURU na TISS,muda ukifika jipu litatumbuliwa tu,
 
Umenikumbusha mbali sna sheikh Mohamed Said marehemu Baba yngu alikuwa na Rafiki kipenzi mzee wa Dar es salaam akiitwa Saad juma Mzee huyo saad Baba yke akiitwa Juma Mzee alikuwa anaishi kariakoo mtaa wa PEMBA alikuwa na mabasi yke alikuwa ameyaandika ilo jina au ni sema huo wimbo WASTARA HAUMBUKI WASTARA MJA WA MUNGU sasa sijui wanajisikiaje waliokuwa wanamuombe mabaya DK DAU bila Sababu ya msingi watanzania tuache chuki za kijinga na udini sio kuwa na sababu Ongera Dk Ramadhani Kitwana Dau
Rubawa,
Hizi chuki zimeletwa kwa watu kutoijua historia ya wazee wetu.

Laiti ingesomeshwa historia ya kweli na watu wakajua mapenzi
yalikuwapo enzi zile za kupigania uhuru vipi Nyerere Mkristo kaja
kapokelewa na Waislam na wakamweka madarakani hii ingeleta
kujua tulipotoka.

Tungejua mizizi yetu ilikochimbukia.

Hii khiyana ya kutaka kubadili historia na kufanya kama vile Nyerere
alikuwa peke yake na kuleta uhuru peke yake ndiyo iliyotufikisha
hapa.

Miaka ya 1950 dini ya mtu haikuwa tatizo kwa wazee wetu hata kidogo.
Angalia mfano huu.

Wakati wazee wetu wanataka kubadilisha uongozi wa TAA baada ya Vita
Vya Pili Vya Dunia aliyekuwa mbele kutaka Dr. Kyaruzi na Abdul Sykes
wachukue uongozi kama rais na katibu alikuwa Schneider Abdillah Plantan.

Huyu Schneider ndiye akaja kuwa katibu wa Daawat Islamiyya (Wito kwa
Waislam) chini ya Sheikh Hassan bin Amir.

Na huyu Sheikh Hassan bin Amir ndiye aliyemjenga Nyerere kwa umma wa
Waislam kama kiongozi wa harakati za kudai uhuru.

Hawa Waislam wote niliowataja hapa wapi historia yao imeandikwa?
Hili ndilo tatizo kubwa.
 
Alwayz...,
Watu wengi wamefurahishwa na aya hii iliyokuwa munasab
na tukio.
Kabisa Shekhe wangu Kwenye ukweli uongo hujitenga wanamsingiza sana Dr Dau lkn wanamsingizia kwa chuki zao tu lkn mola atadhihirisha ufalme wke na uongo utajulikana tu Inshaallah
 
Dream Boy,
Abdulwahid Sykes
hakualikwa sherehe za uhuru.
Alizisikiliza sherehe za uhuru akiwa nyumbani kwake.

Wazee wa TANU waliompeleka Nyerere UNO 1955
walikuja Uwanja wa Uhuru wakakaa majanini.

Mzee Haidari Mwinyimvua anasema tulimuona Nyerere
amekaa jukwaa kuu na wale ambao wakati tunajenga TANU
wao walikuwa bega kwa bega na mkoloni wakitucheka.

Masikini hawa wazee walioijenga TANU, hivi walimkosea nini Nyerere?
 
Franco Zetta,
Unanitukana kisha unanambia nataka kutukanwa.

Hapa tulipofika panatosha hapana haja ya matusi
zaidi.
Umedai awali kuwa nina kufedhehesha nime kuambia unaji fedhehesha mwenyewe,kuna tusi wapi? lugha ya matusi huipati kwangu mimi ni Mtanga kaka Kiswahili nime kishiba, maneno unayotoa mwenyewe yana kuwia Mwiba,Pumzika muungwana punguza mawazo.
 
Swali lako kalijibu Rais katika hotuba yake. Kasema gharama ziliongezeka kutokana na kutitia kwa kitanda cha bahari na kutokea kwa korongo la karibu mara mbili ya urefu walioukadiria hivyo gharama lazima iongezeke.
Kama ni kweli, basi kwa hoja yako hii naungana na wale wanaosema kuwa Tanzania hakuna haja ya feasibility study ambayo nasikia ilichukua billions kadhaa pia kwenye huu mradi.
 
Dau, Dau! Hotuba, Hotuba ipi hiyo? Kucheka ndo hotuba? Dak. 4 kuna hotuba ya kusifia kitu gani? Kama una elimu kidogo na kama lengo ni kuwasifia walio na dini kama yako, hebu sikiliza hotuba na mihadhara ya marehemu Ali Mazrui.
MuchunguZI,
Unafananisha mambo mawili yasiyo na uhusiano hata kidogo.

Lakini si kitu ikhtilafu baiana ya binadamu ndiyo inafanya dunia
izunguke.

Umemtaja Prof. Ali Mazrui.
Mimi nimejuana na Prof. Mazrui kupitia Dr. Dau.

Yeye ndiye alikuwa rafiki yake na nilipotoa kitabu changu cha
kwa ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924- 1968)
The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism
in Tanganyika,'' London 998 alimpa kitabu hiki mkononi Marekani.

Niliandika maneno haya katika kitabu: ''Kwa mwalimu wa wa
masafa marefu Prof. Ali Mazrui.''

Prof. Mazrui aliniletea barua na katika maneno aliyosema alisema
kafurshishwa na kitabu changu kwa kueleza nini Waswahili wamefanya
kupinga ukoloni.

Huu ndiyo ukawa mwanzo wetu wa kujuana.

Lakini usuhuba huu ukanoga zaidi pale Dr. Harith Ghassany
alipomweleza Prof. Mazrui kuwa mimi ni rafiki yake.

DSCN0096.JPG

Kushoto Tamim Faraj ( Muslim University of Morogoro),
Prof. Ali Mazrui na Mwandishi Nile Hilton Kampala

Ukipenda habari zaidi ingia hapa:
Mohamed Said: TAAZIA YA PROF. ALI MAZRUI 1933 - 2014
 
Kabisa Shekhe wangu Kwenye ukweli uongo hujitenga wanamsingiza sana Dr Dau lkn wanamsingizia kwa chuki zao tu lkn mola atadhihirisha ufalme wke na uongo utajulikana tu Inshaallah
Alwayz,
Allahuma Amin.
 
Back
Top Bottom