Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 85,763
- 145,546
Nyongeza ni kuwa Lowassa amekuwa mbunge kwa muda mrefu na alikuwa ni Waziri Mkuu; kama angetaka Bunge likae kama kamati maalum tena katika "closed session" angeweza kutoa hoja na kueleza sababu. Lowassa hakutaka kujitetea Bungeni kwa sababu alijua ni mahali pekee ambapo wenzake nao wanaweza kutumia haki hizo hizo. Watu wengi wanajifanya wamesahau alipotoa hoja ya "magazeti ya mitaani" alipojibiwa na Lucas Selelii mle mle Bungeni!
Lowassa hakuonewa na issue ya natural justice haipo. Alijiuzulu pasipo kuhukumiwa baada ya kujipima yeye mwenyewe na kuamua kuwa ni bora kujiuzulu kuliko kujitetea mbele ya Bunge ambako alituhumiwa na ambacho ndiyo chombo pekee ambacho kingeweza kumcondemn!
Justice delayed is justice denied. Kama kulikuwa na uwezekano wa kupata input ya Lowassa kabla ya ripoti ya Mwakyembe haikukamilishwa kwa nini hilo halikufanyika?
Msiongelee kama nafasi ya utetezi inaweza kuwa postponed tu, akaandikiwa ripoti inayo mu implicate bila kupewa nafasi ya kutoa input yake kwa wanakamati, kama kujieleza ajieleze bungeni, kitendo cha kukosa nafasi ya kutoa input kwa kamati kinaweza kuwa na implications kubwa katika proces nzima kiasi issue inakuwa so convoluted, mtu anaona bora ajiuzulu.
Hilo moja,
Pili siwezi kufagilia ripoti imeandikwa, muandishi kasema mengine hajayaweka kwenye ripoti na hajasema ambayo hayapo kwenye ripoti ni yapi. Kashampa Lowassa msemo kwamba ripoti imekaa kisiasa zaidi.
Kwamba Lowassa ni corrupt is known. Lakini issue ya kwamba hakupewa nafasi ya kujieleza kwa kamati inampa msemo kwamba kaonewa, hususan kwa sababu moja ya objective ya kamati ni kuchunguza mchakato mzima kwa mamkini.
Kwa nini hawakumuhoji Lowassa? Mtu ambaye it turns out amekuwa implicated?
Halafu naona watu bado wana confuse watu tunaoongelea "due process" na kutuona "watetezi wa Lowassa". Mi natetea "due process" ambayo Mwakyembe ameiharibu, simtetei Lowassa.