watu gani wapate criminal case? nyie mnao msapot lowassa? kwa nini hujiulizi takukuru lini imetoa matamko ya uchunguzi wa watu wote wanao tuhumiwa na ufisadi? zaidi ya propaganda za akina mramba na yona na liyumba? epa wako wapi? kagoda wapo wapi, richmond? meremeta etc!! ungekuwa ww au mie tusingefungwa? double standards!, je wezi wengine wapewe muda warudishe pesa?
lowassa ni fisadi papa kiasi kwamba hata system nzima inamuogopa. kwangu mwakyembe TU!! alidhubutu, au unataka tukupe data za mkewe akihaha kwa mwakyembe nyumbani kuokoa hiyo skendo? acheni nyie jamani. LOWASSA HAFAI NI FISADI
Mwingine huyu hajui tofauti ya kum support Lowassa na ku support due process.
The woe of african politics, people steeped in personalities rather than policies.
Wewe unachosema data za mkewe akihaha nyumbani kwa Mwakyembe kuokoa hiyo scandal Lowassa anaweza kukuambia ilikuwa ni attempt yake Lowassa kupata audience na kamati ya Mwakyembe ili na yeye aweze kueleza side yake ya story, kwa nini Mwakyembe hakutaka kumhoji Lowassa.
The fact kwamba TAKUKURU haijafanya kazi vizuri ilitakiwa kumfanya Mwakyembe afanye kazi vizuri zaidi, kwa kumhoji Lowassa na kutupa wananchi nafasi ya kujua utetezi wa Lowassa fully, hata kwa a criminal case. Sasa hivi wananchi hatujui utetezi wa Lowassa fully, tunapata snippets za story anazotaka yeye kutupa, mie nataka aulizwe kila swali ambalo Watanzania wanalo, what's wrong with that? Huko ni kumtetea Lowassa?
Kati yangu mie ninaetaka Lowassa kushurutishwa kuulizwa maswali yote na hata kufunguliwa criminal charges ikibidi na wewe unayeridhika na Lowassa kujiuzulu bila kushurutishwa kujibu maswali, nani anamtetea Lowassa hapa?
Kama Lowassa ni fisadi papa na system nzima inamuogopa, mie ninaetaka ashurutishwe kuulizwa maswali yote na hata kufunguliwa criminal charges na Mwakyembe aliyeogopa kumhoji, nani anaendeleza kumuogopa huku? Mwakyembe kathubutu nini kwa kutomshurutisha Lowassa kujibu maswali na kumpa msemo kwa technicalities za "natural justice" ? Kama tunafikiri huku ndio kuthubutu no wonder CCM inatupeleka resi kila siku Tanzania.
Watu hawako curious, low standards is the order of the day, wanapenda majibu rahisi kwa maswali magumu, hawaoni cover up right in front of their eyes, indeed hawawezi kui recognise cover up kama samaki aliyeyazoea maji kiasi hayajui.
Mediocrity inashangiliwa kwamba ni ushujaa. This explains our poverty.