DR. Mwakyembe na Natural Justice

DR. Mwakyembe na Natural Justice

Wengine tunaweza kusema hii ndiyo sababu hasa iliyomfanya Mwakyembe asimhoji Lowassa, kwa sababu angemhoji Lowassa, Lowassa angemwambia mambo yote yamepita katika cabinet na PM si kiongozi wa cabinet, nenda kamuhoji mukulu mwenyewe akupe kipande kamili.

Tukisema hivi, na kwamba Lowassa kashindwa kusema hili katika utetezi bungeni out of loyalty and concern for a national crisis, kaambiwa "take this bullet for the team tutakupa ulaji juu kwa juu" akasema poa, yapishie mbali, Mwakyembe atasemaje?

Hivi inaingia akilini katika system ya bongo PM afanye mambo bila rais ku approve? Especially PM mshikaji wake rais kama EL na JK? Kwa mambo makubwa yanayozungumzwa katika cabinet level?

JK na EL wanacheza mchezo wa kuigiza ila soon utawagharimu .Kama Gadaffi aliigiza na akawapa watu wake neema lakini bado watu wakashikilia mabaya yake wakasahau mazuri ,Itashindikanaje kwa hawa wanaodhulumu na kufanaya mabaya kila kukicha kwa manufaa ya familia zao.Hawana zuri la kusifiwa.
 
Kiranga je Lowassa alinyimwa au alikosa nafasi ya kutumia haki ya kujitetea na kujieleza mbele ya Bunge ambalo ndiyo lilimpitisha kuwa Waziri Mkuu? I'm granting you kwamba nafasi hiyo hakupewa kwenye Kamati Teule.

Issue sio kwamba kapewa nafasi bungeni, hilo tushali establish. Katika kutafuta justice, objective sio tu vitu vifanyike, bali pia vifanyike timely. Ndio maana wanasema justice delayed is justice denied, kwa sababu, umeme ukikatika, TANESCO wakichelewa kurudisha umeme unaweza kukuta barafu kwenye friji imeharibika na nyama ishaoza. Kwa hiyo kurudisha umeme ni muhimu, lakini kurudisha umeme timely ni muhimu zaidi.

Hizi processes nyingine ni irreversible, kama kutoa the proverbial genie out of the bottle. Ukishazifanya hurudi nyuma, kwa hiyo nilitegemea Mwakyembe ajue hili na kuhakikisha anakuwa thorough kuhakikisha hakuna mess itakayosababisha integrity ya ripoti yake itiliwe shaka. Hakufanya hivyo.

Sasa wewe mtu kakatiwa umeme, hakurudishiwa timely, by the time karudishiwa nyama ishaharibika. Analalmika "Sikurudishiwa umeme timely, nimeshindwa ku preserve nyama yangu". Wewe unamwambia "Ulirudishiwa umeme, huwezi kulalamika". Tatizo ni timeline.

Kwa wale wanaojua principle ya uongozi ya "Caesar's wife cannot afford even suspicion of infidelity, let alone actual infidelity", kwamba kiongozi bora hatakiwi hata kuwa implicated na madoa ya scandal, wataelewa kwamba suala zima la Lowassa kuwa implicated katika Ripoti ya Mwakyembe lilimtia mawaa tayari. Yaani hata kama angeweza kusimama bungeni, na kujitetea vizuri, kuna wengine tungebaki na shaka, tungesema Lowassa katumia ukubwa wake tu ku force utetezi.

Kwa hiyo utaona katika situation kama hii, kwa nchi ambayo ina revere viongozi wake kama Tanzania, Waziri Mkuu kuwa implicated tu ni mawaa tosha. Na kwa sababu Waziri Mkuu kuwa implicated tu, hata kama atajitetea vizuri au vibaya, ni mawaa, basi ilitakiwa sana kwa kamati ya Mwakyembe kuhakikisha kwamba haimtii mawaa Waziri Mkuu bila kutafuta habari zote kwa ukamilifu.

Na kutafuta habari zote kwa ukamilifu hakukuwezekana bila kumhoji Waziri Mkuu mwenyewe.

Mwakyembe alichofanya, kaona Caesar's wife yuko implicated katika infidelity, Caesar wife anatembea na bodyguard saa mbaya bustanini, Mwakyembe kaenda moja kwa moja kwenye Senate kapeleka ripoti inayo mu implicate Caesar's wife bila kumuuliza Caesar's wife kwamba alikuwa anafanya nini na bodyguard bustanini. Hatujui pengine Caesar's wife anapanga mipango ya kuficha ugonjwa wa Caesar, na Caesar anajua.

Sasa Caesar's wife kaitwa kwenye Senate ajitetee kwamba hakufanya infidelity, anaona kitendo cha kujitetea kitafichua ugonjwa wa Caesar. Anaamua kukubali kujitoa katika kasri ya Caesar.

Kunyimwa au kupata haki ya kujitetea katika bunge sio material hapa. Kitu material ni kwamba due process haikufuatwa, justice ilikuwa delayed na kwa hiyo justice ilikuwa denied.

Isitoshe Mwakyembe haku act professionally kwa kutomshurutisha Lowassa atupe side yake ya story. Zaidi ya hapo, Mwakyembe kwa kusema "kuna mengine nimeyaacha" ame undermine credibility ya report yake. Wengine tunaona inawezekana Mwakyembe anaujua ugonjwa wa Caesar na ndio alioacha kuuandika ripotini.
 
Naomba nikujibu kifupi tu. Sifahamu uwezo wako wa kufikiri au ufahamu ila jibu ni FUPI.

NEC ya CCM ni CLOSED meeting, taarifa zake hazirushwi na vyombo vya habari.

Bunge ni OPEN meeting.

KIongozi hawezi kuanika mambo ya ndani hadharani kama unavyofikiri.

fairplay ndo Lowasa au Richmond?
 
Kiranga, kuna uhusiano gani kati ya Kamati Teule ya Bunge na Bunge? Maana nina hofu kuwa unaangalia Kamati Teule kama kikosi cha Polisi au Wapelelezi fulani na katika kufanya hivyo unaweka Kamati Teule upande mmoja na Bunge upande mwingine. Labda, tuanzie upande huu mwingine yawezekana ukaona ni kwanini alichofanya Mwakyembe kilikuwa ndani ya majukumu ya Kamati yake. Na vile vile inaonekana unaweka mzigo kwa Mwakyembe binafsi as if alikuwa na madaraka ya kuamua lolote na kufanya lolote kwa vile tu alikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati Teule. Labda pia uangalia Mwenyekiti wa Kamati Teule ana nguvu gani kulinganisha na wajumbe wengine wa Kamati hiyo.
 
Kiranga, kuna uhusiano gani kati ya Kamati Teule ya Bunge na Bunge?

Kamati teule ya bunge ni kamati teule ya bunge, inafanya kazi kwa niaba ya bunge, badala ya wabunge wote kufanya kazi fulani, wanateuliwa wachache kufanya kazi hiyo.

Maana nina hofu kuwa unaangalia Kamati Teule kama kikosi cha Polisi au Wapelelezi fulani na katika kufanya hivyo unaweka Kamati Teule upande mmoja na Bunge upande mwingine.

Kwa mujibu wa objectives ulizotuletea hapa wewe mwenyewe, kazi yakuchunguza na kupata ukweli wote kuhusu sakata zima la Richmond lilikuwa ni moja ya objectives za kamati teule. Kamati teule imewakilisha bunge lakini imepewa jukumu la kufanya due diligence kwa niaba ya bunge ili kama kuna vitu irrelevant havifai kufikishwa bungeni kuhukua muda wa wabunge wote, kamati teule imaliz kuvichunguza na kuvimaliza bila kuchukua muda wa wabunge wote. Let's say Lowasa angekuwa na a perfect explanation iliyo reasonable kwa implications zote ambayo angeweza kuitoa kwa kamati ya Mwakyembe, Mwakyembe angeweza kumuhoji na kuandika conclusions tu bila embarassment ya kumburuza PM bungeni kwa sakata a rushwa. Hakufanya hivyo.

Labda, tuanzie upande huu mwingine yawezekana ukaona ni kwanini alichofanya Mwakyembe kilikuwa ndani ya majukumu ya Kamati yake.

Labda hujanielewa. Ukiondoa hizo kauli zilizoprove kuwa unprofessional za "kuna mengine nimeacha" sina matatizo na alichofanya Mwakyembe. Mwakyembe amefanya kilichokuwa ndani ya majukumu yake. Sijasema kwamba Mwakyembe amefanya kilichokuwa nje ya majukumu yake. Nina tatizo na yale ambayo Mwakyembe hakufanya.Ninachosema ni kwamba Mwakyembe hakutimiza majukumu yake, hususan yaliyohusu kupata ufumbuzi wa maswali kuhusu Richmond. Alipewa mandate iliyomuwezesha kumuhoji Lowassa, lakini hakumuhoji. Alipewa haki ya kumshurutisha Lowassa kujibu maswali. Hakumshurutisha.Kwa nini? Hatimaye Lowassa kapewa nafasi ajitetee anavyotaka yeye, au akatae kujitetea, bila kushurutishwa kujibu maswali. Kwa nini Mwakyembe hakufuatisha wajibu wa kupata majibu yote kutoka kwa mtu key kama PM? Kwa nini unamuachia Lowassa apate nafasi ya kuamua terms za utetezi wake? Kwa nini kampa mwanya wa kupiga kelele zote hizi za natural justice wakati angeweza kuzimaliza zote kwa kumuhoji kabla ya kuwasilisha ripoti bungeni?

Na vile vile inaonekana unaweka mzigo kwa Mwakyembe binafsi as if alikuwa na madaraka ya kuamua lolote na kufanya lolote kwa vile tu alikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati Teule. Labda pia uangalia Mwenyekiti wa Kamati Teule ana nguvu gani kulinganisha na wajumbe wengine wa Kamati hiyo.

Nikisema "Mwakyembe" naongelea kamati nzima collectively. Mwakyembe anatajwa kwa kuwa yeye ndiye kinara wao. Obviously simaanishi kumpa lawama personally, lakini yeye kama mwanasheria aliyebobea na mwenyekiti wa kamati anachukua sehemu kubwa sana ya lawama personally apart lawama ambayo kamati inachukua collectively.
 
Kwa upeo wangu usio wa kisheria, Kiranga una hoja nzito zaidi ya ile ya M/Kijiji. Ingawaje hoja ya M/Kijiji ina mashiko...

Ni kweli Dr Mwakyembe alimpa mh EL fursa ya kulipiga chenga Bunge la JMT.

Inawezekana Dr Mwakyembe alitarajia kumbana zaidi mh EL pindi atakapojijitetea ndani ya Bunge ... lakini Mh EL akaruka mtego huo. Kulikuwepo na natural justices mbili, ya kwanza kwenye kamati na ya pili ndani ya bunge. Mh Lowasa alitaka ile ya kwanza, Dr Mwakyembe alimpa ile ya pili. Huo ukawa mwanya wa EL kutorokea... ama kweli huo ni kama mchezo wa draft game... ha ha ha! wajinga ndio waliwao...

Mimi nimeelewa na ninawashukuru sana wale muliojitolea kujadili mada hii sincerely, objectively, dedicatively, na elaboratively. Naamini Tanzania/Tanganyika itasalimika...

Suali dogo la nyongeza: Je inawezekana Kamati ya Bunge ilikuwa upande wa Rais Kikwete ili kumfanya Mh EL kuwa kondoo wa kafara?
Asanteni sana
 
Nadhani ipo haja ya kuelezea nguvu, mamlaka, na haki za bunge. Nimeweza kugundua kuwa hoja hii ya "natural justice" inatolewa bila kuelewa kwa usahihi kamati teule ya bunge ni nini hasa na kazi yake inahusiana vipi na bunge zima. Kamati teule inachukuliwa kama chombo independent cha law enforcement cha bunge. Na wengine waweza kuchukulia KT kama chombo fulani cha mahakama. Hivyo, kwa makosa wanaona ripoti ilipotekewa bungeni basi KT ilimaliza kazi yake na bunge likapokea ripoti basi vyombo hivyi "viwili" vikatimiza wajibu wake. Hapa ndipo watu wanakosea na ndugu yangu Kiranga amekosea kwa kuona kuwa KT inafanya kazi kwa "niaba ya Bunge".
 
Mwanakijiji,

Kiranga ameshasema:

"Kwa wale wanaojua principle ya uongozi ya "Caesar's wife cannot afford even suspicion of infidelity, let alone actual infidelity", kwamba kiongozi bora hatakiwi hata kuwa implicated na madoa ya scandal, wataelewa kwamba suala zima la Lowassa kuwa implicated katika Ripoti ya Mwakyembe lilimtia mawaa tayari. Yaani hata kama angeweza kusimama bungeni, na kujitetea vizuri, kuna wengine tungebaki na shaka, tungesema Lowassa katumia ukubwa wake tu ku force utetezi."

Sasa tayari kamati ilishamtia DOA. Kujitetea ilikua ni kiini macho. Lowassa aliligundua hilo.
 
Natural justice inatakiwa iwepo katika kila stage inayowezekana. Polisi hawezi kuja kukukamata uzembe na uzururaji bila ya kukuuliza "unafanya nini hapa? Unatoka wapi na kwenda wapi? etc" eti kwa kusema "Utaenda kujieleza mahakamani" Unaweza kwenda mahakamani ukakutwa huna kosa polisi akawa kapoteza muda wako.

Leo tumesoma polisi wa Oslo Norway wamemuomba msamaha researcher wa Uganda aliyekuwa kaenda Norway kwenye a climate summit, katoka nje ya mkutano a stretch legs, polisi wa Norway kamshika. Mtaa huo una historia ya watu weusi kuuza madawa ya kulevya, na huyu bwana mweusi, tena ana mikono mfukoni inaonekana kama kaficha kitu. Kabla polisi kumuuliza vizuri kamu arrest, hataki kusikia kitu.

Baadaye ikaja kugundulika jamaa ni researcher, alikuwa kwenye mkutano, na sababu iliyofanya aweke mikono mfukoni ni kwamba alikuwa anasikia baridi na kwao Uganda hajazoea baridi.

Sasa polisi angefuata natural justice katika kila stage, angempa nafasi ya kujieleza, kusingekuwa na embarassment.

Alichofanya Mwakyembe ni kama huyu polisi, kamu implicate Lowassa bila kumpa nafasi ya kujieleza, zaidi ya hapo Lowassa alipofikishwa bungeni hakutaka kujitetea. Wengine tunaweza kusema labda Lowassa hakutaka kujitetea kwa sababu anajua ana makosa, kataka mambo yaishe. Lakini hata kama huo ndio ukweli, hili haliondoi ukweli kwamba Mwakyembe alitakiwa kumuhoji.

Mwakyembe katunyima haki ya kujua side ya story ya Lowassa, kwa sababu, Lowassa kupewa haki ya kujitetea bungeni hakukumshurutisha kutoa side yake kikamilifu, kasema tu mimi nimeonewa, kisa hapa uwaziri mkuu, basi mie namwaga manyanga.

Mwakyembe alikuwa na nafasi ya kumshurutisha Lowassa atupe side yake ya hii story, lakini hakuitumia.

Mnajua kwa nini?

Kiranga, mtu mwongo mbabaishaji na mla rushwa kama Lowassa ukimpa nafasi ya kujitetea anakushinda. Mwakyembe ni Lawyer, alilijua hili na akaamua kulileta jukwaani kwa kumshtukiza.
 
Nimejifunza mengi ambayo sikutarajia, na nimeona jinsi upepo wa kisiasa ulivyo hapa Tz, na nimeelewa viwango vya watz, ni nimeelewa misimamo ya watu wengi
 
Kiranga, mtu mwongo mbabaishaji na mla rushwa kama Lowassa ukimpa nafasi ya kujitetea anakushinda. Mwakyembe ni Lawyer, alilijua hili na akaamua kulileta jukwaani kwa kumshtukiza.

Strictly from your above post.

Utajuaje mwongo mbabaishaji na mla rushwa kabla ya kusikia upande wake wa habari?

Au ndiyo tuna pre-judge in that old Wild West style kama alivyoisema Rod Blagojevich hapo chini? Unahukumu kwanza, halafu unamtry baadaye, au in your case hakuna hata haja ya trial Lowassa anajulikana mla rushwa?

I like old movies and I like old cowboy movies, and I want to explain how these rules work in a more understandable way.
There was an old saying in the Old West, there was a cowboy who was charged with stealing a horse in town. And some of the other cowboys, especially the guy whose horse was stolen, were very unhappy with that guy.
One of the cowboy's said, "Let's hang him!"
And the other cowboy said, "Hold on! Before we hang him, lets first give him a fair trial. Then we'll hang him."
Under these rules, I'm not even getting a fair trial. They're just hangin' me. - Rod Blagojevich

Lowassa, corrupt or not, has a right to due process.
 
Nadhani ipo haja ya kuelezea nguvu, mamlaka, na haki za bunge. Nimeweza kugundua kuwa hoja hii ya "natural justice" inatolewa bila kuelewa kwa usahihi kamati teule ya bunge ni nini hasa na kazi yake inahusiana vipi na bunge zima. Kamati teule inachukuliwa kama chombo independent cha law enforcement cha bunge. Na wengine waweza kuchukulia KT kama chombo fulani cha mahakama. Hivyo, kwa makosa wanaona ripoti ilipotekewa bungeni basi KT ilimaliza kazi yake na bunge likapokea ripoti basi vyombo hivyi "viwili" vikatimiza wajibu wake. Hapa ndipo watu wanakosea na ndugu yangu Kiranga amekosea kwa kuona kuwa KT inafanya kazi kwa "niaba ya Bunge".

Sikusema kwamba kamati ilimaliza kazi yake ilipopeleka ripoti bungeni, kama una quote unaweza kunipa.

Halafu sijaona wewe ku address swala la kwamba Kamati haija exhaust mandate yake kwa kutomhoji Lowassa.

Hebu tushushie vipande mkuu. I am always eager to learn something from you, if anything. Mimi nimeenda na objectives za kamati ulizotuletea hapa wewe mwenyewe.
 
Kiranga said:
Isitoshe Mwakyembe haku act professionally kwa kutomshurutisha Lowassa atupe side yake ya story. Zaidi ya hapo, Mwakyembe kwa kusema "kuna mengine nimeyaacha" ame undermine credibility ya report yake. Wengine tunaona inawezekana Mwakyembe anaujua ugonjwa wa Caesar na ndio alioacha kuuandika ripotini.

Kiranga,

..hata mimi nilikuwa disturbed sana na statement ya Dr.Mwakyembe aliposema, "kuna mengine nimeyaacha..."


 
sio rahisi kuenda pale front na kutapika kila kitu hata hiyo serikali ya slaa haiwezi operate hivo na wala CDM mpaka wakati huu haiendi hivo. Kama ni weredi unaousema nawasiwasi kama kweli unautumia impartially.
Issue ya uwaziri mkuu kuwa waliutaka au la nadhani speaker , na Dr wanaweza tusaidia kama wakipenda, si Porojo za JF humu kama mlivoziita.
Nadhani struggle ya wanasiasa kupata madaraka makubwa zaidi wakati wote ndiyo hasaa page yenyewe fungua soma.
 
Jamani eehh......rules za procurement ziko straight forward, strict and widely expensive...........ukipindisha tu wewe ni culprit..........Lowassa ni culprit wa hili jambo from the day one.........PERIOD

Edo analitambua/alilitambua hilo.......mbali na kulitambua akamshawishi JK kuwa ni sahihi kupindisha taratibu.......huyu ndiye alikuwa Chief advisor wa JK.......

Lowassa amechangia kuwanyima wananchi Natural Justice........kwenye mambo ya nishati......na mpaka sasa wananchi tunateseka na ma-cost ya ajabu ajabu.........
 
Jamani eehh......rules za procurement ziko straight forward, strict and widely expensive...........ukipindisha tu wewe ni culprit..........Lowassa ni culprit wa hili jambo from the day one.........PERIOD

Edo analitambua/alilitambua hilo.......mbali na kulitambua akamshawishi JK kuwa ni sahihi kupindisha taratibu.......huyu ndiye alikuwa Chief advisor wa JK.......

Lowassa amechangia kuwanyima wananchi Natural Justice........kwenye mambo ya nishati......na mpaka sasa wananchi tunateseka na ma-cost ya ajabu ajabu.........

Dr. Mwakyembe, kwa kuacha kumuhoji Lowassa na kumruhusu Lowassa kujiuzulu kwa terms zake, ameacha opportunity ya kum-nail culprit number one hapa, at least in the court of public opinion. Kikwete.

Tunajua Lowassa ni corrupt.Kikwete kama rais wa nchi, kwa nini kamchagua kuwa PM in the first place? In the second place, kwa nini karuhusu kukubali kupindishwa kwa procurement?

Hapa ndipo tunarudi kwenye ile notion ya pale juu.

Sababu iliyomfanya Mwakyembe asimhoji Lowassa ni kum protect Kikwete. Hili inawezekana ndilo Mwakyembe analomaanisha anaposema "kuna mengine sikuandika kwenye hii ripoti".

Angemuhoji Lowassa, Lowassa angemwambia issue imepitishwa kwenye cabinet, imejadiliwa, rais kaijua, mawaziri wake wameitekeleza, kwa hiyo kama kuna mtu wa kumuwajibisha muwajibishe rais.

Mwakyembe na machinery yake wakaona badala ya kumuuliza katika kamati, wamsulubishe bungeni ambapo political dynamics hazikuruhusu Lowassa kusema hayo live.

Matokeo yake Lowassa kajiuzulu kwa terms zake na Kikwete anadunda mpaka leo. Mwakyembe hakuwa na kifua cha kutetea Watanzania ilivyotakiwa.
 
Dr. Mwakyembe, kwa kuacha kumuhoji Lowassa na kumruhusu Lowassa kujiuzulu kwa terms zake, ameacha opportunity ya kum-nail culprit number one hapa, at least in the court of public opinion. Kikwete.

Tunajua Lowassa ni corrupt.Kikwete kama rais wa nchi, kwa nini kamchagua kuwa PM in the first place? In the second place, kwa nini karuhusu kukubali kupindishwa kwa procurement?

Hapa ndipo tunarudi kwenye ile notion ya pale juu.

Sababu iliyomfanya Mwakyembe asimhoji Lowassa ni kum protect Kikwete. Hili inawezekana ndilo Mwakyembe analomaanisha anaposema "kuna mengine sikuandika kwenye hii ripoti".

Angemuhoji Lowassa, Lowassa angemwambia issue imepitishwa kwenye cabinet, imejadiliwa, rais kaijua, mawaziri wake wameitekeleza, kwa hiyo kama kuna mtu wa kumuwajibisha muwajibishe rais.

Mwakyembe na machinery yake wakaona badala ya kumuuliza katika kamati, wamsulubishe bungeni ambapo political dynamics hazikuruhusu Lowassa kusema hayo live.

Matokeo yake Lowassa kajiuzulu kwa terms zake na Kikwete anadunda mpaka leo. Mwakyembe hakuwa na kifua cha kutetea Watanzania ilivyotakiwa.

kwa line of argument yako hapo juu, inaonekana dhahiri kuwa kumbe lowassa na mwakyembe lao lilikuwa moja - kumlinda JK!
kamati ya mwakyembe haikumhoji lowassa ili kumlinda JK; na lowassa hakutaka kujitetea mbele ya bunge ili kumlinda JK. status-quo maintained, huh?
i don’t need to repeat here the consequences our blessed nation has painfully suffered after this mess.

so, watu wanapoibuka sasa kumtetea yeyote kati ya hawa wawili, is beyond me!
na nikisema hivi sijipambanui kuwa mimi niko neutral katika debate ya hawa watu wawili - far from it.....so mwanakijiji spare me your (in)famous "weak" tag please.

my choice is practically simple - let's screw all the rhetoric and instead nail these two bastards fast.
if we are not smart and intelligent enough to find a way (legal or otherwise) to put these two to sword, then all the debate in this thread is nothing but a political "cyber-pub" and i humbly ask the moderators to cast it out of that window!
 
Back
Top Bottom