Mkuu sidhani penginemimi sielewi taratibu lakini navyojua mimi kazi ya Mwakyembe ilikuwa kutafuta ukweli kuhusiana na mkataba wa Richmond not who is involved maana kabla ya kuchaguliwa kamati hii hawakuwa wakiamini ama wakidai wao Lowassa ni mtuhumiwa isipokuwa madai yaliletwa..
Kama ume notice mimi naongea process, siongei personalities. Naongea due process na timely dispensation of opportunity for natural justice, na kuzuia mianya ya malalmiko hata kabla hayajatokea na "justice must not only be done, it must also seem to be done". Kwa hiyo kati yangu mie na hao wanaosema "Lowassa was corrupt, served him right" wao ndio wanaoongea mtuhumiwa badala ya process.
Hivyo kazi ya Mwakyembe ilikuwa kutafuta ukweli kuhusu mkataba wa Richmond
Ambayo wangeweza kuifanya kwa ukamilifu zaidi na kuziba mianya ya ulalamishi kama wangemhoji mmoja wa wahusika wakuu, Lowassa. Kwa nini hawakumhoji, nimeuliza several times hapa, sijapata jibu.
Unachunguza Richmond, deal linamu implicate PM in a big way, unaandika ripoti bila kumhoji? Kwa nini?
na wakadhihirisha kweli ulikuwa feki na kuwataja wahusika ambao bunge lilitakiwa kuwaita na kuwahoji ndivyo utaratibu
Huwezi kukamilisha process ya discovery kabla ya kuwahoji watuhumiwa. Kama kuna figures nyingine nyingi ambazo Lowassa kutokana na security clearance ya Uwaziri Mkuu alizijua, na wengine wa chini yake kwa kuwa hawakuwa na security clearance hawakuzijua Mwakyembe haoni kwamba kwa kutomhoji Lowassa anakuwa kaandika ripoti isiyo kamilisha jukumu lake moja la fact finding ?
unavyofanyika huku kwetu yaani sasa inachaguliwa kamati ya nidhamu ambayo ndio inatazama ushahidi uliopatikana.
Mahojiano na Lowassa nayo yalitakiwa kuwa ushahidi, lakini Mwakyembe kwa kutomhoji Lowassa katunyima ushahidi huu. Kamwachia Lowassa aseme hataki kujitetea, Watanzania tumekosa kujua mambo mengine ya ndani ya sakata hili.
Sema ktk kukusanya ushahidi huo mchunguzi anaweza kuchukua report yako ama asichukue na akachukua ya mwingine
Sawa, lakini kuacha kuchukua story ya Lowassa kama kamati ni udhaifu, kwa sababu Lowassa alikuwa mtu key katika deal hili.
inategemea na ushahidi uliopo una nguvu gani.
Ushahidi ulionyesha kwamba Lowassa alikuwa implicated sana, mpaka vimemo kawaandikia kina bangusilo Msabaha. Sasa kwa nini Mwakyembe hakumuhoji Lowassa ili kumshurutisha ajibu maswali ya msingi na kujenga a watertight case pamoja na kuhakikisha Watanzania wanapata habari yote na sahihi?
Kama vile sisi tunapokwenda andika statement Polisi pale unaweza sema na kujibu maswali lakini wao Polisi wana weza kutowahoji baadhi ya watu wengine kwa sababu ushahidi wako unatosha kufungulia kesi dhidi ya mshtakiwa.
Sawa, hili lingewezekana kama Lowassa angekuwa ni some peripheral person. Lowassa alikuwa PM, mtu mkubwa sana katika deal hili, utamuachaje huyu?
Hivyo Target haikuwa Lowassa bali Richmond
Ambayo Lowassa alihusika sana.
na ushahidi ulitosha kwa kamati ya Mwakyembe kuwakilisha kazi waliyopewa kwamba Mkataba wa Richmond haukuwa halali,
Jukumu lao halikuwa kutafuta the minimum amount of ushahidi utakaotosha kufungua mashauri, kazi yao ilikuwa kupata habari zote kadiri walivyoweza, kumhoji Lowassa kungewawezesha kupata habari nyingine ambazo labda hawakuzipata kabla, kama vile deal lilikuwa na baraka zote za rais. Mwakyembe aliogopa kum implicate Kikwete? Aliliona hili na ndiyo maana alikwepa kumhoji Lowassa katika kamati?
kuhusika kwa Lowassa ama watu wengine haikuwa kazi yao kuwafungulia mashtaka..Ndivyo nilivyo elewa mimi..
Katika objectives za kamati, moja ilikuwa ni kupata habari kamili za hili sakata. Kwa kutomhoji Lowassa kamati imejinyima na kutunyima watanzania nafasi ya kupata habari kamili, instead imemuachia Lowassa atupe habari kwa terms zake, Lowassa kakataa kujitetea, kajiuzulu.
Watanzania tumekosa kujua ukweli kwa sababu ya uzembe/ uoga wa kamati ya Mwakyembe.