DR. Mwakyembe na Natural Justice

Kiranga, unachosema ni kujaribu kumuweka Lowassa kuwa ni object ya investigation wakati hakuwa. Uchunguzi ulihusu Richmond na ndio maana ukisoma mahitimisho kuhusu Richmond were swift and precise. Sasa watu waliokuwa implicated kimsingi walihitaji hatua zaidi dhidi yao kuchukuliwa na kuchunguzwa zaidi na vyombo husika.

Lowassa alikuwa implicated and that is it. He was not accused or even condemned of any wrong doing. Ukisoma maelezo niliyoyaweka ya Kamati ni kuwa hatua zozote zaidi dhidi ya Waziri Mkuu zilikuwa zichukuliwe na Bunge na yeye mwenyewe. Kamati isingeweza kwenda zaidi ya mandate iliyopewa kwani hata kumuita Waziri Mkuu kumhoji ingekuwa ni kujipa ajenda wasiokuwa nayo. Wao waliangalia nyaraka wakaona zina muimplicate WM kwa kiasi kikubwa. Sasa kwenda the next level - ya kuanzisha uchunguzi dhidi ya Waziri Mkuu - Bunge lilitakiwa kukubali kwani ndicho chombo cha nidhamu ya juu ya Waziri Mkuu ukiondoa Rais.

Lakini pia implication ya Waziri Mkuu ilikuwa na jambo jingine ambalo watu tayari wameliona - ilikuwa ina muimplicate Rais vile vile. Fikiria hivi - kama aliyoyasema Lowassa kuhusika Kikwete na Richmond yaliripotiwa kwa usahihi na kuwa ndivyo ilivyokuwa ina maana kuwa ushahidi ambao kina Mwakyembe waliuona kumhusu Waziri Mkuu ulimhusu Rais vile vile. Sasa je, kamati ingeenda na kumuita RAis? Watu wanachosahau ni kuwa hata Kikwete hakuhojiwa na Kamati! Kikwete ndiye aliyesimama na kutuambia kuwa Richmond haitolipwa n.k na alikuwa anajua kilichokuwa kinaendelea lakini hakuitwa na Kamati.

Hapa ndipo unaona ni kwanini kutomhoji Lowassa na kuachilia Bunge ilikuwa ni kamba yenye vifungo viwili - kwa upande wa Rais na upande wa Waziri Mkuu. Kina Mwakyembe walijua - kwa usahihi na kwa uhakika wa kisheria - wasingeweza kumhoji Waziri Mkuu bila kumuita RAis vile vile.

Fikiria - Lowassa anaitwa na kusema "Nilimuambia Rais..", "Rais alinielekeza"... "Niliandika barua kwa Rais" n.k n.k Je kwa kumtaja Rais si kunalazimisha Rais naaye kuhojiwa maana asipohojiwa naye yeye angesema "Miye Rais lakini hamkuniita". Hivyo, walimpa Lowassa kitanzi cha kumnyoshea kidole Rais. Lowassa leo anaweza kumnyoshea Rais kidole kwenye vikao vya vyama lakini alishindwa kufanya hivyo mbele ya wabunge? Leo anaweza kunyosha kidole hadharani lakini alishindwa kufanya hivyo Bungeni? Hakuna fact iliyobadilika kuhusu Richmond. Lolote analolijua Lowassa leo, alikuwa analijua 2008.

Kina Mwakyembe walimuambia "yeye mwenyewe ajipime". Well, alitumia masaa akajipima, akafikiria na kushauriana na Regina na alipomaliza aliona hana njia isipokuwa kuruka. Alitambua asingeweza kuilaumu ripoti ya Mwakyembe bila kujibiwa. Alijaribu kudai kuwa ripoti iliokoteza toka magazetini na Selelii alisimama akamjibu Bungeni aoneshe ni wapi kwenye hiyo ripoti vilitoka magazetini au afute kauli yake - akafuta! Lowassa, alipewa nafasi ya kupinga yote yaliyosemwa na Kamati Teule na hata kuweka ushahidi kuwa yeye ndiye alijitahidi kuvunja mkataba wa Richmond hakufanya hivyo. Hakufanya hivyo Bungeni isipokuwa aliamua kufanya hivyo siku chache kwenye TVT na ever since amejaribu sana.


Lazima watu waseme ukweli kuwa Lowassa alijiuzulu kwa makosa yake mwenyewe. Alijiuzulu bila kuombwa kujiuzulu na Bunge wala Rais hakumuambia ajiuzulu. Kamati ya Mwakyembe haikumuambia ajiuzulu. Yeye mwenyewe alijipima. Alijigundua hafai kuwa Waziri Mkuu, aligundua hakuwa na hoja ambayo isingeweza kujibiwa Bungeni. Ndio maana yeye mwenyewe aliamua kujiuzulu. Lowassa hakuonewa, Lowassa hakunyimwa haki ya asili, Lowassa aliogopa kujitetea na aliogopa kusimama kuonesha upande wake. Hili ni kosa la Lowassa peke yake na wale waliomshauri kujiuzulu. Siyo kosa la Kikwete wala Mwakyembe wala wabunge waliozungumza kwa ukali Bungeni. Hili ni kosa la Lowassa na tuanze kuliita hivyo.





kuongezea yeye kapewa nafasi aongee mi nilitegemea aongee huo ukweli anaousema kwenye vikao vya ccm na tv yeye analalama utafikiri hafikiri oh nimeonewa sana, nimesikitishwa sana, sikusikilizwa, tatizo uwaziri mkuu lol!!

kamati haikumsikiliza yeye sio wa level yake, kamati ni ndogo sana kwa waziri mkuu jamani, yeye ni level ya bunge!! hivyo siku aliyopewa nafasi alitakiwa ajitetee sio kujiuzuru na ndipo angepimana na bunge zima na ndipo amtaje na jk na serikali kifo kiwe pale! na kujipima huko na bunge alijua angeshindwa maana wangempigia kura ya kutokuwa na imani nae!

kumchukia mwakyembe ni kumuonea, makosa ni yako mwenyewe na huyo rafiki ako mnajua fika mlichokuwa na mnachokifanya.
 
unataja majina ya akina mwanakiji yanakusaidia nini? huyo kiranga naye aliuliza kwa nini mwakyembe hakumhoji Lowasa naona naye unasema hoja yake ina mashiko!

uko bize? leo hii , hii ni post yako ya pili kwa siku nzima ya leo! jana umepost post tatu tu, yet uko bize mno na unasema nakupotezea muda!!! unafiki huu na kugawa watu makundi hakukufikishi popote pale na kunakuabisha tu

kama ni slow learner bear with me, kama ni low thinker nibebe tu, kama nina logic jibu, na ukishindwa potezea.. thread nyingi sana humu!

huyo malecela anatapatapa tu na CCM yake, wanataka kutuaminisha mwizi ni Lowassa wakati na mwakyembe ni hero! wote ni wezi tu , sikuwa na divert mjadala..umewaza hivyo...kutaka kukomaza unafiki wake anasema the powerfull PM?? this doesnot make sense at all?? tabia za kinafiki mbaya..sisi wengine tunawawasha tu na HUNA UWEZO WALA MAMLAKA YA KUNINYAMAZISHA labda uje unipokonye L/top yangu, ofisi yangu na ufunge cafe zote...niache kwa sababu umesema haiwezekani...na kwa haraka nimeishajua wewe unajikomba watu wenyewe hauwajui..tunashindana na hoja, wewe kaa pembeni kajadili tunda alilokula adamu na eva..that is your limit!

Nitakujibu ...
Yes niko bussy, lakini huwezi kupima namna gani niko bussy kwa kuhesabu posts zangu hapa JF...you are wrong kama ilivyo kawaida yako! Si kila mtu lazima apost bandiko hapa, kuna wengine wanasoma tu na kubonyeza "Like" ama kuwacha hivyo hivyo..

Sijikombi kwa hao watu uliowataja, lakini ninawasoma na kuelewa hoja zao...their contributions have less contradictions and flow well, na siyo kama zile za kwako... Pia naomba ujuwe kuwa, mimi si mwanasheria, lakini ninao uwezo wa kufuatilia logic za mtu/watu vizuri ..that is why nimefuatilia logic zao na kuzielewa. Wewe unashindwa ku-cope na mtiririko mzuri wa hoja kwa kutaka kutuletea vitu vipya katika mada inayoendelea. Ndiyo maana nikakukemea kama siyo msikivu baki ulivyo ni tatizo lako na utabaki nalo...

Umesema ninagawa watu makundi siyo kweli...bali ninagawa hoja. Hoja za kujifunza na zile zinazoonesha bayana shina la matatizo katika siasa za nchi yetu. Wewe ni mtanzanaia kama mimi, siwezi kukugawa au kukutenga kwa sababu yoyote isipokuwa katika hoja za mijadala makini kama huu, ili watu waweze kufuatilia vizuri na kujifunza.

Wewe kwanza siyo slow learner, wewe una tatizo la much know na u haraka haraka katika conclusions zako. Ungekuwa unajitahidi kufuatilia kwanza wenziyo wanasema nini ili uone gap liko wapi na kisha unaunganisha, siyo kuleta frequence ya kwako inayovuruga mtiririko wa maelezo... halafu unakuwa king'ang'anizi tu...

Kuhusu Mwakyembe kuwa mwizi sijuwi! Mada iliyopo hapa ni Ripoti ya Kamati ya Mwakyembe na E. Lowasa na Natural Justice. Kama kosa la Mwakyembe ni kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge, kuibuwa udhaifu wa serikali ndiyo iwe sababu ya kumwona na yeye ni mwizi tu, basi tutokapo na tunapokwenda hapajulikani... Kwakuwa sisi wote ni wachafu naomba tufunge mjadala huu, kwa sababu hakuna mtu wa kumsema mtu mwingine. Tuagize malaika kutoka mbinguni waje waunde kamati za kufanya uchunguzi wa matatizo ya nchini kwetu...

Context ya the powerful PM imeelezwa vizuri na watu ninaojikomba kwao, kama hujaelewa rudi ukaisome tena huko nyuma, taratibu utaelewa, mimi nimeelewa. Kama bado unashindwa kuelewa omba msaada.

Mwisho, sikufungi mdomo wako. Mdomo ni wako, ongea unavyotaka. Mimi nilikuonya usiharibu mtiririko wa mada kwa kung'ang'ana na hoja iliyokuwa imevunjwa. Ama kumbe wewe ni mgumu kuelewa, kukiri kushindwa katika hoja, na kusalimu amri? Kama uko hivyo, uwanja ni mkubwa jimwage utakavyo...

Mimi nitajadili tunda la adam na eva, lakini hiyo siyo limit yangu. Hunijuwi na hivyo limit yangu pia huijuwi ...ila kwakuwa hujambo kwa kujiaminisha kanyaga twende shujaa wangu...
 
Kiranga, hili la Lowassa nimejaribu lakini alinichomolea na kila nikimpigia hataki kupokea tena kwa sababu maswali yangu kwake yanajulikana - maswali ambayo Waandishi nyumbani hawataki kumuuliza kwani yana implication kubwa sana ya uwezo wake kuongoza. Binafsi napenda kusikia hoja nyingine kuhusu Lowassa lakini hii ya "kutotendewa haki" au "kuonewa" haina msingi. Niliikataa siku ya kwanza anajiuzulu, nimeikataa siku alipohojiwa na TVT na nimeendelea kuikataa kwa sababu haiingii akilini. NImeandika mara nyingi kuwa Lowassa hakuonewa.

Sasa tuambiwe tu vitu vingine lakini hili la watu kumlaumu Mwakyembe kwa Lowassa kujiuzulu nalo halina msingi. Lowassa alijiu zulu baada ya kujipima na kujiona hatoshi. Hakujiuzulu kwa sababu Kamati ilimtaka ajiuzulu; hakujiuzulu kwa sababu Bunge lilimtaka ajiuzulu na hakujiuzulu kwa sababu Rais alimtaka ajiuzulu. Alijiuzulu kwa sababu aliamini asingeweza kujitetea mbele ya hostile environment (hata Clinton alijitetea mbele ya hostile Congress!). Lowassa hata leo akitaka anaweza kuleta hoja Bungeni ya kutaka uamuzi wa Bunge upitiwe lakini akileta hoja hiyo anajua kuwa kina Mwakyembe na wabunge wengine watatakiwa wajibu. Watasema na kumuuliza. Tena hivi ni mbunge anaweza hata kuleta hoja iundwe kamati teule ya kuchunguza ushiriki wake kwenye Richmond; yes he can. But, he won't.

Ataenda kwenye vyombo vya habari, atalalamika kwenye vikao vya chama n.k lakini Bungeni hawezi. Itakuwa mwisho wake.
 
Mwanakijiji,

..yale madai yake kwamba maisha yake yapo hatarini yameishia wapi?

..na madai kwamba amelishwa sumu nayo yamefikia wapi?
 
Mwanakijiji,

..yale madai yake kwamba maisha yake yapo hatarini yameishia wapi?

..na madai kwamba amelishwa sumu nayo yamefikia wapi?


Kwa kweli sijui kwani sijawahi kuyafanya hayo kuwa mambo ya miye kufuatilia. Nadhani anapaswa kuulizwa yeye au Polisi - maana polisi walisema wanafuatilia yote mawili.
 
Kiranga, hili la Lowassa nimejaribu lakini alinichomolea na kila nikimpigia hataki kupokea tena kwa sababu maswali yangu kwake yanajulikana - maswali ambayo Waandishi nyumbani hawataki kumuuliza kwani yana implication kubwa sana ya uwezo wake kuongoza. Binafsi napenda kusikia hoja nyingine kuhusu Lowassa lakini hii ya "kutotendewa haki" au "kuonewa" haina msingi. Niliikataa siku ya kwanza anajiuzulu, nimeikataa siku alipohojiwa na TVT na nimeendelea kuikataa kwa sababu haiingii akilini. NImeandika mara nyingi kuwa Lowassa hakuonewa.

Sasa tuambiwe tu vitu vingine lakini hili la watu kumlaumu Mwakyembe kwa Lowassa kujiuzulu nalo halina msingi. Lowassa alijiu zulu baada ya kujipima na kujiona hatoshi. Hakujiuzulu kwa sababu Kamati ilimtaka ajiuzulu; hakujiuzulu kwa sababu Bunge lilimtaka ajiuzulu na hakujiuzulu kwa sababu Rais alimtaka ajiuzulu. Alijiuzulu kwa sababu aliamini asingeweza kujitetea mbele ya hostile environment (hata Clinton alijitetea mbele ya hostile Congress!). Lowassa hata leo akitaka anaweza kuleta hoja Bungeni ya kutaka uamuzi wa Bunge upitiwe lakini akileta hoja hiyo anajua kuwa kina Mwakyembe na wabunge wengine watatakiwa wajibu. Watasema na kumuuliza. Tena hivi ni mbunge anaweza hata kuleta hoja iundwe kamati teule ya kuchunguza ushiriki wake kwenye Richmond; yes he can. But, he won't.

Ataenda kwenye vyombo vya habari, atalalamika kwenye vikao vya chama n.k lakini Bungeni hawezi. Itakuwa mwisho wake.

Again,

Lowassa ni corrupt tunamjua, lakini first principles ni first principles tu. Huwezi ku conclude na kuandika report pasi na hata kumuhoji mtu.
 
‘’Silence reigned in the House as the PM read his speech and accused the committee of violating principles of natural justice by condemning him unheard, despite the fact that the allegations leveled against him were serious. ‘I would like to thank Dr. Harrison Mwakyembe for his presentation. Mwakyembe, a university lecturer in the department of law is aware of the law of natural justice, yet he refused to seek my response over the allegations`` Lowassa said.
(OPEN HEART, OPEN MIND: JK avunja Baraza la Mawaziri)

SITALIPIZA KISASI

Katika mazungumzo yake na waandishi wa habari wa IPP, aliweka mbele nguvu za Mungu, ambapo alisema kama kuna watu walitaka kumuangamiza anawasamehe na hana sababu ya kulipiza kisasi.“Sitalipiza kisasi hiyo sio kazi yangu bali Mungu anajua cha kufanya na watu wenye kulipiza visasi maisha yao sio marefu,”

What are the rules of natural justice?

The principles of natural justice concern procedural fairness and ensure a fair decision is reached by objective decision maker. Maintaining procedural fairness protects the rights of individuals and enhances public confidence in the process. A word used to refer to situations where audi alteram partem (the right to be heard) and nemo judex in parte sua (no person may judge their own case) apply.

Kutokana na matukio ya hivi karibuni mpaka sasa nampa Lowasa ‘the benefit of the doubt’’, kwasababu inawezekana kweli kamati ya Mwakyembe haiku exercise natural justice. Kama Mwakyembe yeye mwenyewe ameshindwa kujipa natural justice je ataweza kumpa mtu mwingine?. Watu wameongea kuhusu ugonjwa wake, , watu wamenusurika kuuwawa na kupoteza kazi kwa ajili yake, watu wamefunga na kuomba kwa ajili yake ili tu Mungu ampe uzima na aseme kuhusu sababu ya ugonjwa wake.

Lakini cha ajabu yeye anarudi anasema sitalipiza kisasi! Kwa maana nyingine tayari kisha jenga visasi na watu. Maana yake nini? Je Mwakyembe anaweza kulipa kisasi? Ana nguvu gani za kumlipa kisasi mtu aliyetaka kumuua?. Je kisasi cha mtu anayetaka kukutoa roho ni nini?. Kwa utaratibu wa natural justice mtu hawezi kuwa hakimu wa kesi yake mwenyewe. Inatkiwa aseme anayoyajua kuhusu ugonjwa wake, kisha sisi wananchi (natural court) ndo tutoe maamuzi. Kwanini hataki kuwa muwazi kama hajalishwa sumu mambo ya visasi yanatoka wapi? Na kama ni sumu kwanini hataki kusema ukweli?. Mtu mwenye PHD ya sheria ni mtu ambaye anatakiwa kuwa sio muoga na kikubwa asimamie ukweli daima. Sasa hizi kauli za ‘’kiswahili’’ kuwa sitalipiza kisasi maana yake nini?

Amesema ameiachia serikali; hakuna mtu anaweza kujali uhai wa mtu mweingine. JB katueleza humu kuwa LTK’s ndo wanaohusika, halafu leo yeye anatuambia ameiachia serikali sisi tumueleweje?. Toka nimezaliwa sijawahi kusikia serikali au bunge likitangaza ripoti ya ugonjwa wa mtumishi wake, kwanini iwe kwa Mwakyembe tu? Ingekuwa bora asingetoa kauli ya kusema hatalipiza visasi, angewashukuru watz basi ingetosha. Kama anaficha mambo ya kuhusu uhai wake mwenyewe, angeshindwa vipi kuficha mambo mengine ya Richmond kama alivyosema mwenyewe bungeni?

Nashauri Dr . Mwakyembe atoe ultimatum kwa serikali kuwa isipotoa tamko kuhusu ugonjwa wake kufika muda fulani i.e 5[SUP]th[/SUP] January 2011, basi yeye ataitangaza ripoti ya ugonjwa wake. Hebu awasikilize hata wanafamilia na rafiki zake, na ndugu ambao wanataka aweke wazi ripoti ya ugonjwa wake kama alivyofanya kuhusu ajali na ‘’Alshababy”

kinakuuna nini mwakyembe kukaa kimya? Au ndo nyie wahucka? Maamuz anayo yeye, atangaze au akae kmy.
 
Again,

Lowassa ni corrupt tunamjua, lakini first principles ni first principles tu. Huwezi ku conclude na kuandika report pasi na hata kumuhoji mtu.

Waliotakiwa kuhojiwa walihojiwa na wale ambao hawakutakiwa kuhojiwa hawakuhojiwa. Ushahidi ulikusanywa kwa ajili ya uchunguzi uliotakiwa kufanyika. Unafikiri Lowassa alifanya makosa kushindwa kuelezea upande wake Bungeni au kutaka ahojiwe kabla ripoti haijakubaliwa na Bunge?
 
Nitakujibu ...
Yes niko bussy, lakini huwezi kupima namna gani niko bussy kwa kuhesabu posts zangu hapa JF...you are wrong kama ilivyo kawaida yako! Si kila mtu lazima apost bandiko hapa, kuna wengine wanasoma tu na kubonyeza "Like" ama kuwacha hivyo hivyo..

Sijikombi kwa hao watu uliowataja, lakini ninawasoma na kuelewa hoja zao...their contributions have less contradictions and flow well, na siyo kama zile za kwako... Pia naomba ujuwe kuwa, mimi si mwanasheria, lakini ninao uwezo wa kufuatilia logic za mtu/watu vizuri ..that is why nimefuatilia logic zao na kuzielewa. Wewe unashindwa ku-cope na mtiririko mzuri wa hoja kwa kutaka kutuletea vitu vipya katika mada inayoendelea. Ndiyo maana nikakukemea kama siyo msikivu baki ulivyo ni tatizo lako na utabaki nalo...

Umesema ninagawa watu makundi siyo kweli...bali ninagawa hoja. Hoja za kujifunza na zile zinazoonesha bayana shina la matatizo katika siasa za nchi yetu. Wewe ni mtanzanaia kama mimi, siwezi kukugawa au kukutenga kwa sababu yoyote isipokuwa katika hoja za mijadala makini kama huu, ili watu waweze kufuatilia vizuri na kujifunza.

Wewe kwanza siyo slow learner, wewe una tatizo la much know na u haraka haraka katika conclusions zako. Ungekuwa unajitahidi kufuatilia kwanza wenziyo wanasema nini ili uone gap liko wapi na kisha unaunganisha, siyo kuleta frequence ya kwako inayovuruga mtiririko wa maelezo... halafu unakuwa king'ang'anizi tu...

Kuhusu Mwakyembe kuwa mwizi sijuwi! Mada iliyopo hapa ni Ripoti ya Kamati ya Mwakyembe na E. Lowasa na Natural Justice. Kama kosa la Mwakyembe ni kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge, kuibuwa udhaifu wa serikali ndiyo iwe sababu ya kumwona na yeye ni mwizi tu, basi tutokapo na tunapokwenda hapajulikani... Kwakuwa sisi wote ni wachafu naomba tufunge mjadala huu, kwa sababu hakuna mtu wa kumsema mtu mwingine. Tuagize malaika kutoka mbinguni waje waunde kamati za kufanya uchunguzi wa matatizo ya nchini kwetu...

Context ya the powerful PM imeelezwa vizuri na watu ninaojikomba kwao, kama hujaelewa rudi ukaisome tena huko nyuma, taratibu utaelewa, mimi nimeelewa. Kama bado unashindwa kuelewa omba msaada.

Mwisho, sikufungi mdomo wako. Mdomo ni wako, ongea unavyotaka. Mimi nilikuonya usiharibu mtiririko wa mada kwa kung'ang'ana na hoja iliyokuwa imevunjwa. Ama kumbe wewe ni mgumu kuelewa, kukiri kushindwa katika hoja, na kusalimu amri? Kama uko hivyo, uwanja ni mkubwa jimwage utakavyo...

Mimi nitajadili tunda la adam na eva, lakini hiyo siyo limit yangu. Hunijuwi na hivyo limit yangu pia huijuwi ...ila kwakuwa hujambo kwa kujiaminisha kanyaga twende shujaa wangu...
Sasa wewe unataka kumlazimisha mwenzako achangie kama unavyotaka, unachotakiwa wewe ni kuchangia si kukemea wanaochangia.
 
Sasa tuambiwe tu vitu vingine lakini hili la watu kumlaumu Mwakyembe kwa Lowassa kujiuzulu nalo halina msingi. Lowassa alijiu zulu baada ya kujipima na kujiona hatoshi. Hakujiuzulu kwa sababu Kamati ilimtaka ajiuzulu; hakujiuzulu kwa sababu Bunge lilimtaka ajiuzulu na hakujiuzulu kwa sababu Rais alimtaka ajiuzulu. Alijiuzulu kwa sababu aliamini asingeweza kujitetea mbele ya hostile environment (hata Clinton alijitetea mbele ya hostile Congress!). Lowassa hata leo akitaka anaweza kuleta hoja Bungeni ya kutaka uamuzi wa Bunge upitiwe lakini akileta hoja hiyo anajua kuwa kina Mwakyembe na wabunge wengine watatakiwa wajibu. Watasema na kumuuliza. Tena hivi ni mbunge anaweza hata kuleta hoja iundwe kamati teule ya kuchunguza ushiriki wake kwenye Richmond; yes he can. But, he won't.

Ataenda kwenye vyombo vya habari, atalalamika kwenye vikao vya chama n.k lakini Bungeni hawezi. Itakuwa mwisho wake.
MKJJ sidhani kama kuna watu wanamlaumu Mwakyembe kwa kujiuzulu kwa Lowassa ila wanahoji masuala kama mawili ya msingi kabisa naona wengi mnayazunguka,

1) Kwa nini kamati haikumhoji Lowassa wakati kama ni kesi anaonekana ni suspect mkubwa, (suala ya u-PM hali-justify hapa).
2) Kwa nini au kuna mtu anaweza kutueleza sababu zilizomfanya Mwakyembe asisome ripoti yote.

Majibu ya maswali haya ndiyo yanayomsumbua Mwakyembe na ndiyo yanayompa Lowassa nguvu ya kusema.
 
kuwa mwakyembe hakumuhoji Lowassa kwenye ile kamati...yet watu wanaisifia ile kamati ..imetuacha uchi wa mnyama!!


Webby,

Hivi Lowassa alinyimwa nafasi ya kujieleza?.............hakujua kama kuna kamati?..........aliwahi nini kujiuzulu pale bungeni?...........na maswali aliyomuuliza mukulu JK yanamaanisha nini.?.........

Webby hivi unamfahamu Lowassa au?........

Nashangaa sana kuona watu wanampigia kifua Lowassa huyu tunayemfahamu.........duhh!!
 
Webby,

Hivi Lowassa alinyimwa nafasi ya kujieleza?.............hakujua kama kuna kamati?..........aliwahi nini kujiuzulu pale bungeni?...........na maswali aliyomuuliza mukulu JK yanamaanisha nini.?.........

Webby hivi unamfahamu Lowassa au?........

Nashangaa sana kuona watu wanampigia kifua Lowassa huyu tunayemfahamu.........duhh!!

We nawe na hiyo midoti yako aaaarrggghhh
 
MKJJ sidhani kama kuna watu wanamlaumu Mwakyembe kwa kujiuzulu kwa Lowassa ila wanahoji masuala kama mawili ya msingi kabisa naona wengi mnayazunguka,

1) Kwa nini kamati haikumhoji Lowassa wakati kama ni kesi anaonekana ni suspect mkubwa, (suala ya u-PM hali-justify hapa).


Jamani, kama hii mada haijaeleweka siwezi kuelezea zaidi. Chombo ambacho kingeweza kumhoji Waziri Mkuu na hata kupendekeza kuwajibishwa kwake ni Bunge. Soma Katiba vizuri utaona ni utaratibu gani unaweza kumfanya Waziri Mkuu apigiwe kura ya kuwa na imani. Kamati ilionesha kuhusika kwa Waziri Mkuu lakini haikuwa na ajenga ya kumchunguza Waziri Mkuu. Hii si kwa ajili ya Lowassa tu bali kwa ajili ya Waziri Mkuu yeyote yule. Hata leo hii ikiundwa kamati usitarajie itaenda kumhoji Waziri Mkuu kama haijaundwa kufanya hivyo. Nimelieleza hili vya kutosha na Kamati ililiweka wazi. Lowassa hakutaka kuhojiwa maana kama angetaka asingejiuzulu.

2) Kwa nini au kuna mtu anaweza kutueleza sababu zilizomfanya Mwakyembe asisome ripoti yote.

Ripoti yote ilisomwa Bungeni na iko hadharani.

Majibu ya maswali haya ndiyo yanayomsumbua Mwakyembe na ndiyo yanayompa Lowassa nguvu ya kusema.

Majibu ya maswali hayo yameshatolewa watu hawaamini au hawayakubali kwa sababu wanaamini Lowassa alionewa licha ya facts zote kuwa wazi kuwa hakuonewa. Sasa watu wanaamini kwa sababu ya hisia tu of a perceived denial of "natural justice". Hakukuwa na issue ya natural justice kwa Lowassa; none whatsoever. Hili watu hawaamini.
 
Webby,

Hivi Lowassa alinyimwa nafasi ya kujieleza?.............hakujua kama kuna kamati?..........aliwahi nini kujiuzulu pale bungeni?...........na maswali aliyomuuliza mukulu JK yanamaanisha nini.?.........

Webby hivi unamfahamu Lowassa au?........

Nashangaa sana kuona watu wanampigia kifua Lowassa huyu tunayemfahamu.........duhh!!


Kaka mnakosea kusema anapigiwa kifua! for what?

tunachokisema ni kuwa tulikubali report ya mwakyembe kijuu juu tu! mwakyembe angemuuliza lowassa, mwakyembe angesema ukweli....Hata kikwete tusingekua naye!

Lowassa kuondoka na akabaki Kikwete hatujafanya kitu...nadhani unajua Kikwete chini ya ridhwani ameishmpita lowassa kwa mbali mno...kila dili lake hata la kuuza toothpicks!

halafu mkuu tusiishi kwa kufahamu is not civilisation..tuishi kwa vithibitisho mkuu!

read my signature
 
Waliotakiwa kuhojiwa walihojiwa na wale ambao hawakutakiwa kuhojiwa hawakuhojiwa. Ushahidi ulikusanywa kwa ajili ya uchunguzi uliotakiwa kufanyika. Unafikiri Lowassa alifanya makosa kushindwa kuelezea upande wake Bungeni au kutaka ahojiwe kabla ripoti haijakubaliwa na Bunge?

At the very least due diligence (on the part of Mwakyembe) kwa mujibu wa objectives za kamati haikufuatishwa kama nilivyonukuu objectives za kamati ulizoleta mwenyewe kwenye thread hii.

Kama issue ni Richmond na PM yuko implicated that gravely, PM anaitwa na kuhojiwa ili watu wajue. Mwakyembe mwenyewe kasema "There are some ghetto secrets I can't rhyme in this song", bado unataka kumpitisha tu na secrecy hii? Bila flack?

At the near-worst case scenario the whole thing is so convoluted in political machinations kiasi kwamba, those who know don't talk, those who talk don't know a thing.

I can't even imagine imagining the worst case scenario.
 
.............halafu mkuu tusiishi kwa kufahamu is not civilisation..tuishi kwa vithibitisho mkuu!

read my signature
...Mkuu Webby....trust me!....na ibakie hivyo hivyo kama ilivyo kwenye signature yako.......you don't wanna see vithibitisho vya huyu EL..........
 
...Mkuu Webby....trust me!....na ibakie hivyo hivyo kama ilivyo kwenye signature yako.......you don't wanna see vithibitisho vya huyu EL..........

ha ha ha! umenifurahisha

Nadhani tumefika hii level ya kuamini, kuaminishwa na kujiaminisha...ndio maana tukifuata principles report ya mwakyembe ni nullified..ila tuamini iko sahihi na maisha yanaendelea

asante kuikubali signature yangu mkuu!
 
Mwakyembe is my hero, Mbunge wa kwanza Tanzania kuongoza kamati iliyofanya kazi kwa haki na kutupa wananchi na Taifa ukweli wa nani Mwizi na kumkimbiza a powerfull sitting PM in our history. Mwakyembe ni binadam mpungufu kama sisi wote lakini the end of the report justifies the means.
Ni kweli Dr Mwakyembe alifanya kazi nzuri but there some doubts
  • Kwanini hawa kumhoji PM EL, Mzee Mwanakijiji ameeleza lakini amezunguka tu hajahit point. Kwenye ripoti yake alisema Rostam alimkwepa hivyo wakaamua kuachana naye na RA ni rafiki wa mkuu kama hoja ni urafiki Tatizo langu Mwakyembe hasemi sababu za kutomhoji direct EL ili hali alipewa rungu kwa nini Je, ni chuki binafsi ? ni zipi ? if no why ??
  • Dr Mwakyembe bado anasema yapo mengine mengi ambayo hawakuyasema, Kwa nini hakuyasema by then kama kweli aliamua kuufichua uoovu wa serikali/viongozi wazi ninachokiona naye anaelement za kulindana Angesema tu hata kama ni mabaya kiasi gani kwani ndiyo wanayo yatenda Sasa anawapa watu stress za bure kwa kutishia kwake unaweza ona akilazimishwa aseme hatasema lolote la maana
 
Back
Top Bottom