Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 10,703
- 11,813
Naona wapiga Lamri wanaongezeka kwa ari mpya zaidi, kasi mpya zaidi na nguvu mpya zaidi. Viva wapiga LAMRI
Whatever, its just a matter of time.
Naona wapiga Lamri wanaongezeka kwa ari mpya zaidi, kasi mpya zaidi na nguvu mpya zaidi. Viva wapiga LAMRI
Acha ujjinga wewe,yaani sababu kipenzi chenu kimaenasa mtegoni ndio iwe kawaida!!!!!
Jingazzz saaaaanaaa
Nani kakwambia ukiwa na kidegree cha SOCIOLOGY ndio unakuwa bweg? Unatakwa kuwaambia wote wenye SOCIOLOGY ni mabwege?
Uzuri ni kuwa ukiwa bweg unaweza usijitambue kuwa wewe ni bweg, na akina Kitila watawadanganya Mabwege kama ninyi. Kwa akili yako Kitila na Zitto ndio unadhani watakuletea hicho chama mbadala. KEEP WAITING, utakuja kudawazwa na ndipo utakapotambua kuwa wewe kweli ni mmoja wa Mabwege.
I can not urge with a fool.
Ili chama kitulie labda mbowe ajiuzuru au afe japo si vema kumwombea kifo
Zitto kakutuma uje umtetee? too late!! Kosa la USALITI huwa halina msamaha!! Matokeo ya Staa wa Kitila 2010 Ubunge haya hapa, hata 50% ya kura zote hakupataKuna watu wenye mtazamo finyu wanaamini kwamba chama hiki ni imara sana kwa sasa kiasi kwamba hata wakimfukuza Zitto kitaendelea kubaki imara.
Wamesahau kwamba wamejenga ufuasi kwa viongozi, na hivyo watakapomfukuza Zitto atatimka na wafuasi wake na chama kitayumba.
Wangekuwa na mtazamo mpana wa kimantiki, na kama wangekuwa ni watu wa kujifunza, viongozi wa CHADEMA wangelimaliza sakata la Zitto ambalo sasa lipo mahakamani kwa njia ya usuluhishi kimya kimya kama walivyofanya NCCR kwa Kafulila.
Wakishakumfukuza Zitto atatimka na mashabiki wake, chama kitayumba na kutoa unafuu kwa CCM. Katika mazingira haya tunahitaji sana mbadala wa CCM na CHADEMA.
Source: Raia Mwema
Mmmh sidhani na kama he is basi alikuwa obsessed na siasa na kama alikuwa obsessed alipoteza objectivity!!!!!!!
Ndio maana mtu smart and objective kuwa siasani tena hizi????!!!!!
yap he is smart at all.
Zitto mwenyewe anajitambua nje ya CDM hana wafuasi zaidi ya wale aliokuwa anawatumia kubomoa CDM!
aanzishe chama chao, maana walikuwa na mkakati mzuri sana, nafikiri ndio itakuwa mbadala wa ccm na cdm. kila la kheri Dr uliyedanganyika.
Kumbe watu tunatofautiana sana katika kuona na kutafsiri mambo na kwa kuisoma hii makala ya Kitila (japo anasema itaendelea wiki ijayo), basi leo nimepata uhakika kabisa kwamba nchi hii inarudishwa nyuma na wasomi waliojijengea taswira ya kuwa kwa vile ni wasomi walioelimika katika jambo moja wanadhani hiyo inawapa freepass ya kuwa sahihi kwa mambo mengine.
Kitila ni mfano mmojawapo. Makala imeanza vizuri ila ilipofika katikati ikaonyesha mambo fulani wazi. Kumbe makala imelenga kujipoza machungu kwa kufukuzwa uanachama wa Chadema, imelenga kuficha udhaifu wake kuuhamishia kwa wengine, imelenga kufurahisha saikoljia yake kwamba upande wake uko sahihi, upande wa wengine uko hovyo.
Na hii ndo saikolojia ya wakosaji katika asili ya binadamu, hatuwezagi kukaa kimya tukikosea. Sasa tukirudi kwenye article yake kuna vitu vichache vinavyoonyesha wazi kabisa malengo ya Dr. Kitila ni nini. Hebu mcheki hapa:
Kwa haraka haraka tayari umeshajua Kitila anaelekea wapi. Tayari keshataka kuwaamninsha watu kwamba kwa vile yeye kafukuzwa hii ni sawa na mgogoro uliosababisha NCCR ikaffifia, na Chadema haina jipya inaelekea huko huko.
Watu wa dizaini hizi huwa hawawezi kuondoka sehemu halafu wakapatakia mema sehemu waliyotoka. Ni ubinafsi tu wa mwafrika, na pengine binadamu tulio wengi. Leo hii nikifukuzwa kazini kwangu kwa utovu wa nidhamu fulani, deep inside nitapaombea sehemu yangu hiyo ya kazi pafilisike -- kwa style ile ile ya 'adui mwombee njaa'. No, Dr. Kitila, you can do better than this.