Dr.Kitila Mkumbo: Tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA

Dr.Kitila Mkumbo: Tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA

Uyu msaliti analilia uongozi ndani ya chama wakati jimboni kwake ameshinda kama mpaka leo kwenye alimashauri yake anaongozwa na magamba Awezi pia kuongoza taasisi kubwa kama chadema.
 
Nilimkubali Dr K, nikadhani anafa kuwa ktb wa cdm kumbe ata yy hajikubali!!!!!!! goooo gooooooooooooooo lete chama mbadala
 
Tunatambua viongozi walioko ndani ya chama Achana na wasaliti walioko mahakamani Uwezi kuishi namwana mke alie kupueleka makamani.

kwa hiyo zito akadai haki yake wapi? hivi unategemea hiyo kamati kuu ya chadema iliyojaa wachaga imtendee haki zito badala ya mbowe mtu wao?
mbowe amehongwa na mkono asifanye kampeni musoma vijijini huo sio usaliti?
 
Inahitaji Weledi wa hali ya juu kumuelewa Nguli Kitila Mkumbo, Pale tutakapoacha kushabikia Viongozi na badala yake kupenda CHAMA, tutaweza kuchambua hoja za msingi na kasoro zilizopo katika uongozi.

hawa walitumwa kuharibu chama na wamelipwa kwa ajili hiyo , hakuna haja ya kuwahurumia .
 
- Kaka huwezi kushirikiana na wahuni mnafanya wote uhuni halafu one day unasema hawafai kwa sababu wamekufukuza, Zitto amekuwa muwazi always kwamba hakubaliani na mawazo ya wahuni huko, kila wakigomea Serikali Zitto hakujiunga nao hata siku moja, Zitto amesimama kuwataka waoe ,mahesabu mpaka leo wanajikanyaga kanyaga yuel ndio mwanasiasa, sio huyu Kitila hebu tuambie amewahi kufanya nini tofauti na Lema kabla hawajmfukuza?

Le Mutuz

Tatizo mwenzangu hapa umeegemea kwenye facts ambazo hutaki kuziacha! nimeishakwambia kuwa siasa ni dynamic! Leo unaweza shirikiana na shetan kesho ukashirikiana na malaika! Hata Zitto mwenyewe unayemtolea mfano before aliwahi kushirikiana na hao wahafidhina katika kumuangamiza kisiasa Chacha Wangwe but leo Zitto hayupo pamoja nao!
 
we mjinga soma kwanza makala yote ndio ucomment!! Nyie ndo wale wale mnaoifanya cdm kionekane ni chama cha vilaza
Mbadala wa CDM? Kwa hiyo mabadiliko 2013 ilikuwa ni kuleta mbadala wa CDM? Kama nitakuwa nimekuelewa vizuri nia ni kuleta chama kingine cha siasa ili kiwe mbadala ! Kama ni hivyo viongozi na wanachama wote wa CDM wanahaki zote kuwaita wasali, wahaini kwani nia yenu ilikuwa kuuwa CDM na kuanzisha mbadala. Je huoni mlikuwa hamuwatendei haki wale waliokubaliana na CDM, sera, taratibu , katiba, nk. Ni vyema mkaanzisha mbadala mkaendesha kwa vile mnavyoona inafaa ndio maana ZZK anatakiwa atoke mwenyewe kama anafikiri kama unavyofikiri asisubiri tsunami kwani lazima imbebe.
 
anakataza watu waache kushabikia chama afu anasema zzk kama akiondoka basi ataondoka na mashabiki wake
 
So Kitila Mkumbo you need mbadala wa CDM na CCM, kwa hiyo mlitaka muangamize CDM ili muelekee kwa huyo mbala. Acheni uhuni bhana.

Wakati wa uchaguzi 2010 kampeni zinaendelea. Zitto alikuwa busy kutangaza atagombea Urais 2015. Was it right timing? Acheni uhuni na kuaminisha wananchi ujinga.

Ndio Zitto alitaka kugombea Uenyekiti wa CDM, Kitila nakwambia kwamba, huyo Zitto wako angepata Uenyekiti leo CDM isingekuwepo.

Endelea kutuletea porojo zako unadhani wote ni mabwege.......

Naona wapiga Lamri wanaongezeka kwa ari mpya zaidi, kasi mpya zaidi na nguvu mpya zaidi. Viva wapiga LAMRI
 
Dr. Usikwepe hoja je mkakati mliouandaa unarusiwa kikatiba kama sheria mama ya Taasisi husika yaani CDM?
Tunausubiria sana kwa hamu hicho chama chenu Cha ATC mnaojidanganya kuwa ni mbadala wa CDM na CCM hamfiki popote kwa tamaa mlizonazo tena na huyo kibaraka wa ccm.
unazidi kujidhalilisha komaa na taaluma yako zzk ameshakulambisha mavi zako mwenyewe.
 
Kitila Mkumbo!!!, mtu ambaye nilikuheshimu na kukuamini sana, umenishangaza na ninakuomba uache kupotosha umma!!
Ninajiuliza, wewe si ni Dr, kwa maana una PHD!!!??, Inakuwaje unarubuniwa kirahisi na mtu kama Zitto!?

Dr. Kitila, ninaomba uuambie umma, Hivi kuwarubuni wadiwani wa CHADEMA Arusha na kuwafanya wagomee maamuzi halali ya chama hatimae wakafukuzwa na mahakamani wakashindwa kesi, ndio njia halali za kutaka uongozi ndani ya chama?

Hivi kutembea majukwaani ukitukana chama na viongozi wakuu wa chama ndio demokrasia?

Swahiba wako uliekuwa unampigania bwana Zitto, alikuambia kuwa kuhujumu chama kwa kuengua wagombea wa chama chake ili CCM ipite bila kupingwa ndio demokrasia muliokuwa mukiihitaji ndani ya CHADEMA?

Kwenda kinyume na maazimio ya kambi rasmi ya upinzani kama vile;

1)kususia hotuba ya kikwete,
2)kutoshiriki na wenzie kwenye tukio la bomu mkutano wa CHADEMA Arusha,
3)kutotimiza majukumu ya naibu katibu mkuu na kutofika makuu makuu ya chama kwa zaidi ya mwaka, ndio unachohalalisha kuwa ni mbinu za ushindi?

Kitila, watanzania sio wajinga, ni bora tu ukakaa kimya kuliko kuendelea kujivunjia hiyo heshima kidogo uliyobakiza.
 
Tumeikataa CCM kwasababu inakumbatia makosa kwa kuogopa watu eti watayumbisha nchi. Lazima tujifunze kutoa adhabu na kupokea adhabu lazima tuanze na ZZK ili kutengeneza std zinazokubalika. NCCR haikuwa taasisi ilikuwa ni viongozi wenye uchu mkubwa sana wa madaraka na fedha, usalama wa taifa nk. Mazingira yamebadilika sana hatuwezi kuacha kuadhibiana kwa kuogopa kivuli cha NCCR. Dr ingebidi kwanza useme wazi je kwenye sakata lenu kwa vyovyote vile mlivunja katiba ya chama na kama mlivunja adhabu yake ilikuwa nini kwa mujibu wa katiba?

Lazima tuzifuate sheria zetu tulizokubaliana nazo. Sioni upofu wa wanachama ila naona tamaa ya tuliowaamini.

Mkwawa

Kama ni adhabu ilifaa aanze kupewa Slaa, kwa kubadili matumizi ya fedha za chama kujinufaisha binafsi

Ilifaa aadhibiwe mbowe kwa kukosa uadilifu na matumizi mabaya ya madaraka

Kama kweli chama kinauthubutu kwa viongozi wake basi mjadala uwepo juu ya Mbowe na Slaa

Sio kwa zzk na dr kitila pekee
 
Nawe pia Kitila Mkumbo ni mfuata Zitto, ina maana na mapungufu yote ya huyu dogo we ndo uliona anafaa? Kama uliona anafaa una matatizo! Unatuaibisha wasomi
 
Last edited by a moderator:
Mwigamba aliongea ukweli sana ! kwamba lengo lao lilikuwa kuupindua uongozi na kwamba kama wangeshindwa na ikajulikana basi Wangefukuzwa wao , na wala hakuwa shocked na kutimuliwa kwao maana anaamini walistahili ! Sasa hizi ngonjera za kitila hazina mashiko maana walikuwa pamoja na mwigamba .
 
Ugonjwa wa Dr.Kitila Mkumbo wa kumshabikia Zitto baadala ya itikadi ya chama na sera zake asione kuwa watanzania wote wapo hivyo. Hili ni kosa kubwa ambalo wanalo wasomi wengi hapa nchini wa kudharau wananchi wa kawaida kwa kujiaminisha kuwa wapo sahihi. Si dhambi hata kidogo mtu kushabikia chama au mtu katika siasa,dhambi ni mtu kujiaminisha kuwa bila yeye hakuna chama kwa sababu tu ya kushabikiwa na watu. Dr. Kitila unatakiwa kuwaambia watanzania kama mlifukuzwa nje ya utaratibu wa kikatiba wa chama. Binafsi kama mwananchi wa kawaida naona ni afadhali Zitto aondoke na hao wafuasi wake kuliko kuendekeza migogoro na viongozi wake. Ushindi wa jeshi dogo ni nidhamu na umoja.
 
Labda kwa wajinga tu itachukua muda lakini kwa wenye uelewa walishajua kuwa na wewe uliingia mkenge wa kuimaliza chama tu. Watu walijitolea kujenga vyama ndiyo wakakuza demokrasia na siyo kiherehere kama mnazoonyesha nyiye. Mandela fought for long time and nobody said it was enough for him, until he decided to quit. Nyerere did the same. Sasa nyiye wa kuleta mnafikiri mna wafuasi sana. ZZK Kigoma kashindwa kushawishi. Wewe kwenu hata jimbo liko kwa watu. CHarity begins at home my friends.

Halafu hii conclusion, siyo ya mtu wa PhD.
Tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA

ITACHUKUA muda kuelewa nini hasa kilichokikumba Chama Kikuu cha Upinzani nchini (CHADEMA) hadi kikashindwa kutatua mgogoro wa uongozi na hatimaye kuingiza nchi katika kizungumkuti cha kisiasa tunachokishuhudia leo. Binafsi, kama mmoja ya wahusika wakubwa katika mgogoro huu nimepokea pole, lawama, na kwa kiasi fulani hongera kwa kumudu kuhimili mikikimikiki iliyonikumba. Nimepokea pole kutokana na misukosuko niliyokumbana nayo katika sakata hili hadi kufikia kufukuzwa uanachama.

Hili si jambo dogo katika maisha ya binadamu. Kufukuzwa katika ushirika wowote ni jambo linalosababisha mfadhaiko na ninazipokea pole nilizopewa kwa unyenyekevu. Ninashukuru pia kwa wale walionitia moyo kwamba hii ni ajali katika safari na nisikate tamaa katika kutoa mchango wangu katika harakati za mabadiliko ya kisiasa nchini. Nami nawaahidi kwamba bado nipo imara na nitaendelea kushiriki kikamilifu katika harakati za kuleta mabadiliko ya kisiasa hapa nchini, ndani na nje ya vyama vya siasa.

Walionipa lawama ni wale waliokubaliana mia kwa mia na viongozi wa CHADEMA waliotujengea taswira ya usaliti na uhaini kwa chama kwa uamuzi wetu wa kuandaa mkakati wa kushinda uchaguzi ndani ya CHADEMA; mkakati ambao ulikuja kutafsiriwa kama mkakati wa mapinduzi ya uongozi halali ndani ya chama. Na kwa kuwa viongozi waliongea sana na kulirudia jambo hili mara kwa mara, na kwa kuwa jamii yetu imejengwa katika kuamini uongozi zaidi kuliko mtu mwingine yeyote, wapo watu wengi ambao wameafikiana na tafsiri ya uongozi kwamba waraka ule ulikuwa ni mkakati wa mapinduzi na haukuwa na nia njema.

Wapo pia wananchi walionilaumu kama sehemu ya uongozi wa chama kwa kushindwa kuyamaliza mambo yetu ndani ya chama. Na wengine wamenilaumu kwa kutokuwa na moyo wa kubali yaishe, kwamba ningekubali kosa, hata kama siamini kwamba ni kosa, ili niombe msamaha yaishe, tusonge mbele. Natamani ingekuwa rahisi hivi na kwamba kungekuwa na nia njema kwa pande zote mbili, pengine neno samahani lingetosha kumaliza mgogoro huu.

Kwa sababu hii nazipokea lawama zote kwa unyenyekevu pia na ninakubali kwamba nimeshiriki, bila kutarajia, kusababisha usumbufu na kutatiza tamanio na tumaini la mamilioni ya Watanzania katika kuitoa CCM madarakani. Hata hivyo, taswira ya mgogoro huu ni pana kuliko inavyoonekana na pengine tutapata nafasi nzuri zaidi mbele kueleza vizuri kilichotokea katika maandishi ili watu waelewe na waielewe CHADEMA na viongozi wake vizuri, na kuweka kumbukumbu kwa vizazi vijavyo.

Sitarajii katika makala haya kukidhi kiu ya watu wengi wanaotamani kujua ukweli wa mgogoro ndani ya CHADEMA na pengine mimi siye mtu sahihi kueleza jambo hili kwa kuwa nina maslahi ya moja kwa moja. Ninatoa changamoto kwa watafiti wa sayansi ya siasa kulifanyia utafiti jambo hili na kuliweka bayana, ili watu wapate kujifunza na kulijua vizuri.

Nieleze tu kwamba mgogoro huu unatukumbusha kuwa, pamoja na kwamba tupo katika mfumo wa vyama vingi, bado tumeendelea kuukumbatia utamaduni wa chama kimoja. Kwa hiyo tuna vyama vingi vya siasa, lakini vyama hivi bado vinakumbatia utamaduni wa chama kimoja. Utamaduni wa chama kimoja ni utamaduni hodhi na wa kiimla. Uongozi katika utamaduni wa chama kimoja unapatikana kwa njia za uteule, ukiwahusisha watu wachache wateule. Utamaduni wa chama kimoja unakataa ushindani wa wazi. Katika utamaduni wa chama kimoja kutamani cheo fulani ndani ya chama na katika serikali ni ulafi na uroho wa madaraka. Ndio maana vyama vyetu vyote vikubwa hapa nchini vinakataza na kukemea wanachama wao kutamani na kutangaza nia ya kuwania madaraka makubwa kama vile urais au uenyeviti wa vyama.

Kutamani madaraka peke yake kunakatazwa, achilia mbali kuandaa mkakati wa kushinda nafasi unayoitamani. Na hili ndilo kosa tulilolifanya. Tulikuwa wajinga sana kudhani kwamba tupo katika mfumo na utamaduni wa vyama vingi ambapo mtu yupo huru kutamani cheo chochote katika chama chake cha siasa, na kutengeneza mikakati ya kushinda cheo hicho katika uchaguzi huru ndani ya chama. Tulikuwa wajinga kwa kujaribu kuachana na utamaduni wa kuvizia cheo na kujifanya hutaki wakati unataka.

‘Msaliti’ mwenzetu Zitto Kabwe alianza siku nyingi mwaka 2009 kwa uamuzi wake wa kugombea uenyekiti wa chama bila kupata ridhaa ya wazee wa chama. Alikuwa mjinga kudhani kwamba uongozi katika mfumo wa chama kimoja unapatikana kwa kujaza fomu na kuomba kura. Nami nilikuwa mjinga nisiyeelewa kwa kumuunga mkono na kumtaka asonge mbele katika nia yake hiyo. Hakuishia hapo, Zitto Kabwe akafanya ujinga mwingine kwa kutamani na hatimaye kutangaza kugombea urais kupitia chama chake. Huu nao ulikuwa ni usaliti kwa utamaduni wetu wa chama kimoja, kwa sababu katika utamaduni huu nafasi kama hii ni ya kiteule na wateule na wateuaji wapo.

Ninapokubali kupokea lawama katika kushiriki kusababisha mgogoro unaoendelea ndani ya CHADEMA, naomba nami niwarushie lawama tele wanachama na mashabiki wa chama hiki, na wapenda mabadiliko kwa ujumla. Nawarushia lawama wanachama na washabiki wa CHADEMA kwa kuwashabikia viongozi wa chama chao katika kukinyonga chama. Viongozi wa chama hiki wamefanya makosa mengi na makubwa hadi kusababisha mgogoro ufike ulipofika, lakini wanachama na mashabiki wa chama wamekuwa wakishwashangilia katika kila hatua walioifanya. Kwa hiyo lawama ya kwanza kwa wanachama na mashabiki ni pale walipokubali kugeuzwa kuwa mashabiki wa viongozi ndani ya chama badala ya kuwa mashabiki wa chama. Na kwa kuwa ushabiki hupofusha macho na akili, mashabiki wa viongozi hawatofautishi kati ya uongozi na chama. Ni kama vile wamedanganywa na viongozi waliopo na wakakubali kudanganyika, kwamba uongozi wa chama ndio chama, na chama ndio uongozi!

Ni kwa sababu ya ushabiki kwa viongozi, ndio maana ilifika mahala wanachama na mashabiki wa CHADEMA wakagawanyika katika makundi ya washabikia viongozi, na chama kikakosa watu wa kukishabikia na hapo kikajikuta hakina mlinzi.

Makosa yaliyofanywa na uongozi na wanachama wa CHADEMA unafanana sana na makosa yaliyofanywa na viongozi na wanachama wa NCCR Mageuzi miaka ya tisini. Kama inavyotokea kwa CHADEMA leo, wanachama wa NCCR Mageuzi waligeuka kuwa mashabiki wa viongozi, kundi moja likimshabikia Mrema na kundi jingine likiwashabikia akina Marando. Kwa kudhani kwamba chama kilikuwa imara sana, kundi la akina Marando likaamua kumfukuza Mrema likiamini kwamba alikuwa hana madhara yoyote kwa sababu chama kilishaimarika mno, wakisahau kwamba msingi wa ufuasi ulijengwa kwa viongozi na sio kwa chama.

Mrema alipotimka, akatimka na mashabiki wake. Hicho ndicho kinachoendelea ndani ya CHADEMA. Kuna watu wenye mtazamo finyu wanaamini kwamba chama hiki ni imara sana kwa sasa kiasi kwamba hata wakimfukuza Zitto kitaendelea kubaki imara. Wamesahau kwamba wamejenga ufuasi kwa viongozi, na hivyo watakapomfukuza Zitto atatimka na wafuasi wake na chama kitayumba. Wangekuwa na mtazamo mpana wa kimantiki, na kama wangekuwa ni watu wa kujifunza, viongozi wa CHADEMA wangelimaliza sakata la Zitto ambalo sasa lipo mahakamani kwa njia ya usuluhishi kimya kimya kama walivyofanya NCCR kwa Kafulila. Lakini kwa sababu ya upofu unaoendelea unaotokana na kugubikwa na ulevi wa utamaduni wa chama kimoja kwa upande mmoja, na ulevi wa umaarufu kwa upande mwingine, hawatakubali yaishe nje ya Mahakama, na hatimaye watamfukuza Zitto. Wakishakumfukuza Zitto atatimka na mashabiki wake, chama kitayumba na kutoa unafuu kwa CCM. Katika mazingira haya tunahitaji sana mbadala wa CCM na CHADEMA.


Source:
Raia Mwema
 
Dr. Katika hali ya kawaida,y MKAKATI UWE SIRI YA WACHACHE? KAMA NIA NI NJEMA KAMA UNAVYO DAI NA WENZAKO? JE UTATAFSIRI VIPI IWAPO MWANAO AU NDUGU YAKO ANAJIPANGA KUCHUKUA MAMLAKA YAKO KATIKA FAMILIA YAKO KWA NJIA NA HARAKATI ZA SIRI AMBAZO LABDA KWA BAHATI MBAYA UKAJA GUNDUA? JUST BE REAL.....
 
sikiliza kitila, mi nikisoma ule waraka sioni tatizo sana, tatizo kubwa kabisa hata wenzenu wakawatimua walibaini nyuma yenu kuna watu wanaowatuma mfanye hayo. we unajua sana dhumun lenu lilikua nini kama we ujui mulize zito atakwambia.
 
Ama kwa hakika akili nywele kila mtu anazake, bora uwe kimya ataonekana mwenye hekima na pengine itakusaidia kuliko kuongea tu pumba utaonekana -------- na huna busara mwisho wa siku watanzania hawatakuamini kwasababu ya dhambi ya usaliti..
 
Back
Top Bottom