zimmerman
JF-Expert Member
- Feb 17, 2011
- 1,683
- 3,226
Kumbe watu tunatofautiana sana katika kuona na kutafsiri mambo na kwa kuisoma hii makala ya Kitila (japo anasema itaendelea wiki ijayo), basi leo nimepata uhakika kabisa kwamba nchi hii inarudishwa nyuma na wasomi waliojijengea taswira ya kuwa kwa vile ni wasomi walioelimika katika jambo moja wanadhani hiyo inawapa freepass ya kuwa sahihi kwa mambo mengine.
Kitila ni mfano mmojawapo. Makala imeanza vizuri ila ilipofika katikati ikaonyesha mambo fulani wazi. Kumbe makala imelenga kujipoza machungu kwa kufukuzwa uanachama wa Chadema, imelenga kuficha udhaifu wake kuuhamishia kwa wengine, imelenga kufurahisha saikoljia yake kwamba upande wake uko sahihi, upande wa wengine uko hovyo.
Na hii ndo saikolojia ya wakosaji katika asili ya binadamu, hatuwezagi kukaa kimya tukikosea. Sasa tukirudi kwenye article yake kuna vitu vichache vinavyoonyesha wazi kabisa malengo ya Dr. Kitila ni nini. Hebu mcheki hapa:
Kwa haraka haraka tayari umeshajua Kitila anaelekea wapi. Tayari keshataka kuwaamninsha watu kwamba kwa vile yeye kafukuzwa hii ni sawa na mgogoro uliosababisha NCCR ikaffifia, na Chadema haina jipya inaelekea huko huko.
Watu wa dizaini hizi huwa hawawezi kuondoka sehemu halafu wakapatakia mema sehemu waliyotoka. Ni ubinafsi tu wa mwafrika, na pengine binadamu tulio wengi. Leo hii nikifukuzwa kazini kwangu kwa utovu wa nidhamu fulani, deep inside nitapaombea sehemu yangu hiyo ya kazi pafilisike -- kwa style ile ile ya 'adui mwombee njaa'. No, Dr. Kitila, you can do better than this.
Kitila ni mfano mmojawapo. Makala imeanza vizuri ila ilipofika katikati ikaonyesha mambo fulani wazi. Kumbe makala imelenga kujipoza machungu kwa kufukuzwa uanachama wa Chadema, imelenga kuficha udhaifu wake kuuhamishia kwa wengine, imelenga kufurahisha saikoljia yake kwamba upande wake uko sahihi, upande wa wengine uko hovyo.
Na hii ndo saikolojia ya wakosaji katika asili ya binadamu, hatuwezagi kukaa kimya tukikosea. Sasa tukirudi kwenye article yake kuna vitu vichache vinavyoonyesha wazi kabisa malengo ya Dr. Kitila ni nini. Hebu mcheki hapa:
Makosa yaliyofanywa na uongozi na wanachama wa CHADEMA unafanana sana na makosa yaliyofanywa na viongozi na wanachama wa NCCR Mageuzi miaka ya tisini. Kama inavyotokea kwa CHADEMA leo, wanachama wa NCCR Mageuzi waligeuka kuwa mashabiki wa viongozi, kundi moja likimshabikia Mrema na kundi jingine likiwashabikia akina Marando. Kwa kudhani kwamba chama kilikuwa imara sana, kundi la akina Marando likaamua kumfukuza Mrema likiamini kwamba alikuwa hana madhara yoyote kwa sababu chama kilishaimarika mno, wakisahau kwamba msingi wa ufuasi ulijengwa kwa viongozi na sio kwa chama.
Kwa haraka haraka tayari umeshajua Kitila anaelekea wapi. Tayari keshataka kuwaamninsha watu kwamba kwa vile yeye kafukuzwa hii ni sawa na mgogoro uliosababisha NCCR ikaffifia, na Chadema haina jipya inaelekea huko huko.
Watu wa dizaini hizi huwa hawawezi kuondoka sehemu halafu wakapatakia mema sehemu waliyotoka. Ni ubinafsi tu wa mwafrika, na pengine binadamu tulio wengi. Leo hii nikifukuzwa kazini kwangu kwa utovu wa nidhamu fulani, deep inside nitapaombea sehemu yangu hiyo ya kazi pafilisike -- kwa style ile ile ya 'adui mwombee njaa'. No, Dr. Kitila, you can do better than this.