Nimeshaanza kuwa na wasiwasi na uelewa wa hawa wasomi wetu ambao ndio tunaowategemea,ndugu umeeleza vizuri sana ,huyu Dr Kitila kaonyesha umbumbumbu wa hali ya juu,na nakubaliana na mdau kuwa kuingiza hilo kwenye mambo binafsi huo ni ufinyu wa akili,hasa kwa mtu msomi kama Kitila(?)nafikiri pia huyu Dr wakati alitaka tu kujionyesha kuwa anamjua Mbeki ndani nje na mwishowe kaharibu wakati ambao wengine wangetumia kuuliza maswali,unapomuuliza mtu kwa kurejea mambo yake binafsi ana haki ya kuhamaki ,na sawa hata yeye Kitila umuulize swali na kwa kufuata mambo yake binafsi tena yanayohisi kifo sijui kama angefurahi.Kwa mila mambo ya vifo yanayomhusu mlengwa hayaletwi kwenye mijadala,huo ni kukosa heshima na adabu