Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,305
- 33,765
Mkuu Chama,
Nimekusoma katika nadiko lako hapo juu. Nadhani hukusoma bandiko langu kwa kina. Nafafanua nilichoandika
1. Mleta mada amepotosha umma na kumweka Dr Katila katika position isiyo yake. Ukweli wa upotoshaji unaonekana katika swali la msingi hapo juu kutoka kwa Dr mwenyewe. Hakuna mahali alimtaja mtoto wa Mbeki. Cha kushangaza watu walimshambulia kwa ''kumuongezea machungu bwana mbeki''.
Ukweli unabaki kuwa swali halikuwa na uhusiano na mtoto wa Mbeki na mashambulizi yote yalikuwa ni kundahlililisha.
2. Nimesema kuwa swali la Kitila halina tatizo ukiliangalia leneyewe, mada iliyokuwepo na mtu aliyepsawa kulijibu.
Katika jamii zetu na duniani kwa ujumla ni ngumu sana mtu kutofautisha kati ya HIV na AIDS.
Mtu anapotoa kauli kama za Mbeki ni wazi kuwa jamii inaweza kufuata maneno yake kwa namna tofauti
Ukiangalia video utaona kuwa ilibidi Mbeki atoe ufafanuzi baada ya kuleta sintofahamu miongoni mwa jamii tena ya wasomi. Hii ni dhahiri kuwa maneno yake yaliathiri sana jamii.
Ni kwa mtazamo huo swali la Kitila linabaki kuwa na uzito. Mkuu Kichuguu kagusia vema sana hapo juu kuhusu hili.
3. Katika bandiko langu nimeweka wazi kuwa bila kujali maudhui ya hoja ya Mbeki kuhusu kauli yake(nikiamaanisha iwe kweli au si kweli) hoja kubwa niliyoiona imeleta sintofahamu ni upotoshaji wa maneno ya Dr Kitila, kumwekea maneno ambayo hakuyasema na kuongezea chumvi katika jibu la mbeki.
Tuna ushahidi kuwa Mbeki alijibu na wala hakusema ''pinch.......'' kama ilivyosemwa.
Hii maana yake nini! kwamba kuna watu pengine hawaelewi mada na wanachagua maneno mawili matatu na kuleta usumbufu usio wa lazima kwa baadhi ya watu kama ilivyo kwa Kitila na Mbeki kama angetusoma.
Hitimisho
Mleta mada amepotosha jamii. Ukweli wa kilichotokea upo hapo juu kutoka kwa mhusika. Usumbufu alioupata Dr Kitila hata kushambuliwa kwa mambo nje ya mada ilikuwa ni personal attack na wanaofanya hivyo ima hawakujua ukweli au waliujua lakini hawakutumia ''fair play''.
Pili, Mbeki aliongea maneno kama kiongozi wa taifa kubwa bila kujua madhara yake. Maana yake kama anavyoitetea sasa ina mantiki na ukweli kuhusu HIV na AIDS na yatokanayo na hayo.
Kwasababu hiyo Mbeki anabeba dhamana ya vifo kwa kundi lililoshindwa kumwelea kutokana na maelezo ya kisayansi yaliyoshindikana kutafsiriwa vema na jamii. Kiongozi asiyeelewa ni hatari kwa jamii, wenzetu wana kauli isemayo '' Don't worry if you don't understand people, worry if they don't understand you''
Inategemea uono wa kila mmoja wetu, kwangu mimi swali la Dr Kitila lilikuwa na mantiki sana.
Wale wanaosema halina mantiki, tumie kipande cha swali lake kutetea hoja zenu kwa kuonyesha udhaifu wa hoja zake na si kulitazama swali kwa jina la Dr Kitila.
Nimekusoma katika nadiko lako hapo juu. Nadhani hukusoma bandiko langu kwa kina. Nafafanua nilichoandika
1. Mleta mada amepotosha umma na kumweka Dr Katila katika position isiyo yake. Ukweli wa upotoshaji unaonekana katika swali la msingi hapo juu kutoka kwa Dr mwenyewe. Hakuna mahali alimtaja mtoto wa Mbeki. Cha kushangaza watu walimshambulia kwa ''kumuongezea machungu bwana mbeki''.
Ukweli unabaki kuwa swali halikuwa na uhusiano na mtoto wa Mbeki na mashambulizi yote yalikuwa ni kundahlililisha.
2. Nimesema kuwa swali la Kitila halina tatizo ukiliangalia leneyewe, mada iliyokuwepo na mtu aliyepsawa kulijibu.
Katika jamii zetu na duniani kwa ujumla ni ngumu sana mtu kutofautisha kati ya HIV na AIDS.
Mtu anapotoa kauli kama za Mbeki ni wazi kuwa jamii inaweza kufuata maneno yake kwa namna tofauti
Ukiangalia video utaona kuwa ilibidi Mbeki atoe ufafanuzi baada ya kuleta sintofahamu miongoni mwa jamii tena ya wasomi. Hii ni dhahiri kuwa maneno yake yaliathiri sana jamii.
Ni kwa mtazamo huo swali la Kitila linabaki kuwa na uzito. Mkuu Kichuguu kagusia vema sana hapo juu kuhusu hili.
3. Katika bandiko langu nimeweka wazi kuwa bila kujali maudhui ya hoja ya Mbeki kuhusu kauli yake(nikiamaanisha iwe kweli au si kweli) hoja kubwa niliyoiona imeleta sintofahamu ni upotoshaji wa maneno ya Dr Kitila, kumwekea maneno ambayo hakuyasema na kuongezea chumvi katika jibu la mbeki.
Tuna ushahidi kuwa Mbeki alijibu na wala hakusema ''pinch.......'' kama ilivyosemwa.
Hii maana yake nini! kwamba kuna watu pengine hawaelewi mada na wanachagua maneno mawili matatu na kuleta usumbufu usio wa lazima kwa baadhi ya watu kama ilivyo kwa Kitila na Mbeki kama angetusoma.
Hitimisho
Mleta mada amepotosha jamii. Ukweli wa kilichotokea upo hapo juu kutoka kwa mhusika. Usumbufu alioupata Dr Kitila hata kushambuliwa kwa mambo nje ya mada ilikuwa ni personal attack na wanaofanya hivyo ima hawakujua ukweli au waliujua lakini hawakutumia ''fair play''.
Pili, Mbeki aliongea maneno kama kiongozi wa taifa kubwa bila kujua madhara yake. Maana yake kama anavyoitetea sasa ina mantiki na ukweli kuhusu HIV na AIDS na yatokanayo na hayo.
Kwasababu hiyo Mbeki anabeba dhamana ya vifo kwa kundi lililoshindwa kumwelea kutokana na maelezo ya kisayansi yaliyoshindikana kutafsiriwa vema na jamii. Kiongozi asiyeelewa ni hatari kwa jamii, wenzetu wana kauli isemayo '' Don't worry if you don't understand people, worry if they don't understand you''
Inategemea uono wa kila mmoja wetu, kwangu mimi swali la Dr Kitila lilikuwa na mantiki sana.
Wale wanaosema halina mantiki, tumie kipande cha swali lake kutetea hoja zenu kwa kuonyesha udhaifu wa hoja zake na si kulitazama swali kwa jina la Dr Kitila.