Dr. Bilal and the Future of COSTECH

Dr. Bilal and the Future of COSTECH

sasa turudi kwenye swali, future ya COSTECH itakuwa mikononi mwa nani maana naona wote tunataka a perfect candidate..
 
...future ya COSTECH itakuwa mikononi mwa nani maana naona wote tunataka a perfect candidate.
Salamu mkuu. Nadhani hata tungempata Einstein au Newton bado hatoweza kufanya la maana COSTECH. Najua umuhimu wa kuwa na figure yenye CV nzuri ktk organization kama COSTECH, lakini nachelea kuamini kama msukumo uliopo, toka Serikalini hadi mashirika binafsi, unaweza kusaidi huyo mtarajiwa kuibadili COSTECH (kama kweli ndio lengo la kumtoa aliyekuwepo).

Kimtazamo (unaweza kuwa finyu pia) ni bora tujadili namna ambayo atakayekabidhiwa ataweza kuibadili; tukichambua namna ya kupata 'research funds', mchango wa $erikali na mashirika mengine ya ndani, kuimalisha ukaribu kati ya COSTECH na hao wenye CV hata kama hawatachaguliwa, mchango wa wanasayansi wa nje, mchango wa mashirika ya teknolojia ya nje, na mbinu nyingine za kuifanya iwe World Class S&T Commission (kama kweli tunaihiitaji wakati huu).

Nina hakika wapo wengi wanaofahamu haya mambo, hapa JF, zaidi yangu
==================
 
sasa turudi kwenye swali, future ya COSTECH itakuwa mikononi mwa nani maana naona wote tunataka a perfect candidate..

Mwanakijiji,

Hivi kwani lazima huyo kingozi wa Costech awe Dr? Hivi nini malengo ya COSTECH? Nijuavyo mimi hawako pale kufanya researches na badala yake wana manage technology transfer.

Kwa maana hiyo kinachotakiwa zaidi ni manager mwenye ujuzi kwenye mambo ya technology na wala sio lazima awe researcher.

Technology management ni nyanja tofauti kabisa na inahitaji vision, innovative mindsets and a person who is ready to embrace changes.

Labda ndio maana COSTECH wanashindwa kazi zao, tumeng'ang'ania kuweka pale madokta na maprofesa wakati skills zinazotakiwa pale huwezi kuzipata kwa kusomea Ph.D.

Dunia imebadilika na technology inabadilika haraka sana kiasi kwamba isipokuwa managed ni rahisi mno kupoteza mwelekeo maana kila ukigusa hiki kile kinatokea, kinachotakiwa sasa ni cordinated efforts on how to manage technologies.

Kwa mawazo yangu sio lazima profesa au Ph.D holder kwa hiyo kazi. Tukipata mmoja ambaye ni Ph.D holder lakini pia anajua mambo ya management ni nzuri vinginevyo ni bora tuchague mtu
mwingine hata kama sio reseacher.
 
johnshaaban

Mtanzania

You're damn right buddies! COSTECH inahitaji managerial skills mpya na endelevu. Suala la kuangalia wenye PhD tu (tena wengine almost wamechizi) ni tatizo. Akipatikana Prof ama PhD holder mwenye managerial skills nzuri na mjasiriamali shupavu basi COSTECH itakuwa ile inayotamaniwa na kila mzalendo mwenye uchungu na nchi hii!
 
Mimi nadhani kuwa COSTECH ndicho chombo chenye jukumu la kuratibu tafiti za kisayansi ili kuzaa teknolojia mpya za kuwaendeleza watanzania kama ilivyo kwa chombo kama National Science Foundation huko Marekani. Kama kweli ni hivyo, basi kinahitaji kuongozwa na mtu anayejua kufanya utafiti wa kisayansi na wala siyo mwanasiasa au mjasiliamali. National Science foundation imekuwa inaongozwa na maprofessor mbalimbali wanaokuwa seconded kwa muda wa miaka mitatu mitatu. Labda COSTECH nayo ingetumia utaratibu wa namna hiyo wa kuwa-second maprofessor wanaojua utafiti wa kisayansi. Tatizo kubwa hapa ni kwa vile malipo ya director wa COSTECH ni makubwa sana kuliko yale ya professor.
 
Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) is a parastatal organisation with the responsibility of co-ordinating and promoting research and technology development activities in the country. It is the chief advisor to the Government on all matters pertaining to science and technology and their application to the socio-economic development of the country.


Mission Statement
COSTECH's mission is to seek appropriate means of utilising selected research results; to promote technology development; to co-ordinate research endeavours; and to mobilise financial and academic support in favour of research; in order to implement/advise the Government on most efficient methods of achieving sustainable socio-economic development in Tanzania.
 
lakini, vipi kuhusu suala la Administration? Je yawezekana kutengenesha "administration" na daily duties za wanaofanya kazi pale, kama ilivyo kwenye vyuo vikuu vingi ambapo Administration is not part of the faculty?
 
Kichuguu,

Ukiangalia mission statement ya COSTECH bado naamini wanahitaji
watu wenye skills zaidi kwenye Technology management, watu hao pia wakiwa na Ph.D ni nzuri zaidi ingawaje binafsi sioni kama ni lazima.

COSTECH hawahitaji kujua hizo researches mbalimbali in details na badala yake naona wao wako zaidi upande wa implementation or exploitation of the technology concerned.

Pia hao Technology Managers wana ujuzi wa reseach ingawaje sio lazima wabobee.
 
Mtanzania, kama your take is correct, basi naona ipo haja kabisa ya kuibadili na kuwa a research pioneer na kama nilivyosema hapo nyuma iunganishwe na mojawapo ya Chuo Kikuuu kama Los Alamos inavyofanya kazi na UCLA or something of that sort. Sidhani kama ilivyosasa itakuwa ni msaada mkubwa kwa eneo la Teknolojia hadi pale itakapoweza kuanzisha, kuendesha, na kusimamia tafiti mbalimbali and dare go where no Tanzanian has ever gone before!
 
The COSTECH ni useless body. Kazi ya kuuza na kutumika kwa technolojia nia jukumu la wajasiliamali siyo kazi ya serikali. Mimi nilitegemea COSTECH iwe kama NSF kutafuta taknoljia mpya na kuziweka hadharani kwa wananchi ili wajasiliamali wanaotaka wazitumie kuleta maendeleo.


COSTECH yetu kwa sasa hivi huwezi kuifananisha na National Labs za Marekani zilzo chini ya serikali lakini ziongongzwa na vyo kwa mfano Los Alamos ambayo iko chini ya Departement of Energy na University of New Mexico au JPL iliyo chini ya NASA na CALTEC.
 
The COSTECH ni useless body. Kazi ya kuuza na kutumika kwa technolojia nia jukumu la wajasiliamali siyo kazi ya serikali. Mimi nilitegemea COSTECH iwe kama NSF kutafuta taknoljia mpya na kuziweka hadharani kwa wananchi ili wajasiliamali wanaotaka wazitumie kuleta maendeleo.


COSTECH yetu kwa sasa hivi huwezi kuifananisha na National Labs za Marekani zilzo chini ya serikali lakini ziongongzwa na vyo kwa mfano Los Alamos ambayo iko chini ya Departement of Energy na University of New Mexico au JPL iliyo chini ya NASA na CALTEC.

Prof. Kichuguu,

Kwi kwi kwi!!!! Uko right kabisa, pitia website yao na ukiangalia hakuna cha maana wanachofanya. Labda wabadilishwe kabisa ili walenge zaidi kwenye research, watimue watu wengi walioko pale ambao hawafit kwenye new structure.

Lakini anayetaka kufanya hayo mambo inatakiwa awe na nguvu, vinginevyo yatampata yale ya Dr. Bamwenda kule Arusha.
 
Nadhani huu mjadala tangu uanze ulikuwa unafanyika ukiwa na wrong assumptions.. sasa naona mambo yanaanza kukaa sawasawa..
 
...Nijuavyo mimi hawako pale kufanya researches na badala yake wana manage technology transfer.
...ningekubaliana nawe kama COSTECH ingekuwa na ukaribu na vyuo vya elimu ya juu nchini maana ni vigumu kutenganisha 'technology transfer' na 'researches' labda kama unataka ubabaishaji (kama ilivyo COSTECH ya sasa). Huwezi kuhamisha teknoloji toka 'area x' itumike 'area y' bila kufanya 'customization, which needs research' kujua kama teknolojia husika itafaa kwa mazingira ya 'area y' (...just among many examples).

...na kama nilivyosema hapo nyuma iunganishwe na mojawapo ya Chuo Kikuuu kama Los Alamos inavyofanya kazi na UCLA or something of that sort.
Linaweza kuwa suluhisho lakini Tz chuo kipi sasa, maana kila Dept./Faculty/College inataka kuwa Chuo kinachojitegemea kisa uVC na vyeo vingine (wakati wenzetu wanaunganisha vyuo vyao kuwa na nguvu ya pamoja ktk tafiti zao).

Tatizo nadhani ni kwamba COSTECH ya sasa imekuwa institute isiyothamini ushiriki/mchango toka vyuo vya elimu ya juu. 'Sometimes' wamefikia mpaka kuwa na 'conflict' na vitengo fulani vya vyuo, utadhani wana malengo tofauti. Ukifatilia kwa undani unashangaa kisa cha 'conflict' ni wote kubid for same research fund. Pengine ibadilike na kuwa karibu na vitengo vyenye tafiti za kisayansi ktk vyuo vikuu.

Mfano, wanaweza kutoa baadhi ya vyumba ktk jumba lao kwa vitengo husika vya vyuo vikuu na kuruhusu waanzishe R&D-Cs kisha kusupport upatikanaji wa fund pale inapoonekana utafiti ni muhimu kwa maslahi ya Taifa. Au wanaweza kuanzisha State-key R&D-Cs zitazoendeshwa na vitengo vyenye taaruma husika toka vyuo vikuu na wao kuwa 'monitor' wa tafiti hizo.

Haya ni mawazo tu, nina hakika wapo JFs' wenye mazuri zaidi!
===================
 
Kuna Chuo Kikuu cha Mbeya (zamani nadhani ilijulikana kama Mbeya Tech). Nadhani kitafaa sana... kuwa mahali ambapo wataalamu wetu wanajichimbia..
 
...ningekubaliana nawe kama COSTECH ingekuwa na ukaribu na vyuo vya elimu ya juu nchini maana ni vigumu kutenganisha 'technology transfer' na 'researches' labda kama unataka ubabaishaji (kama ilivyo COSTECH ya sasa). Huwezi kuhamisha teknoloji toka 'area x' itumike 'area y' bila kufanya 'customization, which needs research' kujua kama teknolojia husika itafaa kwa mazingira ya 'area y' (...just among many examples).

Johnshaban,

Technology management ni pana zaidi ya researches kwa maana ya kwamba reseach inakuwa subset kwenye technology management.

Kikawaida technology management inaongelea mambo makuu matano (Gregory Model)ambayo ni :
1. Identification - Unaamua technologies zipi kama nchi
tunataka kuzipa kipaumbele
2. Selection - Unachagua technologies unazotaka ziwe developed
3. Acquisition - Hapa ndipo reseaches zinaweza kutakiwa kwa
ajili ya technologies ambazo hazipo na sio
lazima hizi reseaches wafanye wenyewe,
wanaweza ku outsource kwenye vyuo vikuu
mbalimbali, au kufanya wao kwa kushirikiana na
wengine na pia hata kununua ikibidi.

4. Exploitation - How too exploit existing and future
technological capabilities
5 - Protection - Mwisho lazima uwe na njia za kulinda wajanja
wasiibe.

Kama unavyoona malengo ya COSTECH yanaweza kuwa mapana zaidi ya malengo ya vyuo vikuu. COSTECH inaweza kuwa kiungo pia kati ya
vyuo vikuu na viwanda au watumiaji wengine. Ujuzi unaotakiwa kwenye hizo kazi zote ni zaidi ya ule wa kufanya reseaches..

Hii model ndio ambayo hata makampuni sasa yanatumia kwenye developments za technologies mbalimbali. Lakini pia model hiyo hiyo inaweza kutumiwa na serikali.

Kwa maoni yangu COSTECH kama wako makini na wana watu makini wanaweza kabisa kufanya technology transfer bila hata ya wao wenyewe kujihusisha na reseaches moja kwa moja. Nafikiri umenielewa.
 
Bottom line Nuclear Physics bongo kakosea njia.

Hapo umepatia. Nuclear Physics inaambatana na matumizi ya pesa na labs.

Bongo hakuna labs, na hakuna pesa zinazotengwa na bado watu wanataka scientists andike papers.

Na zaidi ya hapo, UDSM sio research institution. Ni 4 years college, na maprofesa wanakuwa na kazi kubwa ya kufundisha kuliko kufanya research.

Hivyo kwa Dr. Bilal kurudi bongo ni kuBugi steps.
 
Mzalendohalisi, je outside Tanzania, do we have any scientists working for some of world class research institutions ukiondoa wanaofundisha vyuoni? Ambao serikali yao ikiwa ofa ya kurudi nyumbani kuunda upya research industry watakubali? Nakumbuka jinsi Nigeria ilivyoweza kutengeneza wataalamu wake...
Kwa mazingira ya sasa Costech, Tirdo etc si sehemu za kutegemea kitu chochote cha maana interms of reaserch. Mazingira ya institutions hizi bado hayavutii na sidhani kama kuna lolote la maana linaendelea zaidi ya watu kwenda kuripoti asubuhi na kupiga mishemishe zao wakisubiri siku nyingine ionekane. Kuna hitajika mabadiliko makubwa ili tuweze kupata Tofauti
 
Kuna Chuo Kikuu cha Mbeya (zamani nadhani ilijulikana kama Mbeya Tech). Nadhani kitafaa sana... kuwa mahali ambapo wataalamu wetu wanajichimbia..

Kwanini unafikiri mwanaSayansi anaweza kujichimbia Mbeya wakati nyie mnajirusha DSM?
 
Kwa mazingira ya sasa Costech, Tirdo etc si sehemu za kutegemea kitu chochote cha maana interms of reaserch. Mazingira ya institutions hizi bado hayavutii na sidhani kama kuna lolote la maana linaendelea zaidi ya watu kwenda kuripoti asubuhi na kupiga mishemishe zao wakisubiri siku nyingine ionekane. Kuna hitajika mabadiliko makubwa ili tuweze kupata Tofauti


What is the future for COSTECH maana nasikia kuna kitu mpya inaitwa National Economic Empowerment Council ambayo ndio itacoordinate research zote nchini

Costech kwisha?


 
Back
Top Bottom