DPP Mwakitalu: Uhalifu haulipi, Ukikamatwa na TAKUKURU tunakupa adhabu na Mali zako zinataifishwa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
MKURUGENZI wa Mashitaka nchini ( DPP), Sylvester Mwakitalu, amesema kwa sasa hakuna mwalifu atakayenufaika na mapato ambayo ameyapata kwa njia ya rushwa au uharifu, kwa maana hiyo fedha na mali zitataifishwa.

Amesema Rushwa ni janga kubwa na athari zake zinaonekana katika ngazi ya taifa na Kimataifa.

DPP Mwakitalu, ameyasema leo Mkoani Dar es Salaam, wakati wa kongamano Maalumu kuhusu mapambano dhidi ya Rushwa iliyowahusisha Jeshi la polisi, Takukuru na Taasisi nyingine 11


Amesema kati ya mambo ambayo yanafanyiwa msisistizo kuhakikisha kwamba rushwa na makosa yoyote ya kupangwa yanakabiliwa kikamilifu na si kwa waalifu wanapewa adhabu tu làkini wanakwenda zaidi kutafuta mali na fedha zilizopatikana kwa njia ya uharifu .

," Natoa meseji kwamba uhalifu haulipi bali unapewa adhabu na pia mali ambazo zimepatikana kwa njia ya rushwa zitataifishwa," amesema

Ameongeza kwamba lengo kubwa la kongamano hilo ni kuimalisha mapambano dhidi ya Rushwa na kuhakikisha hakuna mwalifu atakayenufaika na uhalifu.

Akizungumza kuhusu hatua kadhaa zilizochukuliwa kisheria ni pamoja makosa yote ya Rushwa yalikuwa lazima kufika Makao Makuu na DPP mwenyewe lazima kuyaona kisha kusaini vibali làkini.

DPP alisema baada ya kuona umuhimu wa jambo hilo kwa sasa wametatua kwa kutoa sheria ndogo ambayo imewezesha wakuu wa mashitaka wa mikoa na Wilaya kupewa vibali isipokuwa kwa makosa machache yale ambayo yanafedha nyingi au yanayogusa viongozi wa Serikali.

"Kuna makosa machache ambayo natakiwa kuyaona ili niweze kutoa maagizo làkini kwa sasa kesi nyingi zinaishia mkoani mkuu wa mashitaka wa mikoa wanakaa na vyombo vya uchunguzi wanapitia majalada kwani kwa sasa hakuna ucheleweshwaji tena kesi zinasikilozwa," amesema

DPP Mwakitalu, amezungumzia mafanikio ambayo yanapatikana baada ya kuwa na kongamano ni pamoja na kuwajengea uwezo na kisha uchunguzi unafanyika kwa weledi na mashitaka kwa weledi kwani kesi ikichukuwa muda mrefu bila kuisha yako mambo yanajitokeza,

"Kesi ikichukuwa muda mrefu haijafika mwisho yapo mambo yanajitokeza hapa Kati ya mashahidi kwani ni binadamu wanafariki wanahama, wanapotea, hivyo kuna kuwepo na athari nyingi zinaweza kusababisha kesi nyingi zisifike mwisho

" Sio kwa sababj hakukuwa na kosa au ushaidi làkini pengine mashahidi hawapo tena na ushahidi wake haupo tena, hivyo kusikiliza kesi kwa haraka na kufika mwisho inatupa matokeo mazuri," amesema.

Nae mgeni rasmi katika kongamano hilo Naibu Waziri wa nchi, ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora, Deogratius Ndejembi, amesema mapambano dhidi ya rushwa yanahitaji ushiriki mpana wa wananchi, wadau mbalimbali na mbinu imara na endelevu.

Ndejembi ambaye ndiye mgeni rasmi katika kongamano ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa kongamano maalumu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa.

Amesema kutokana na umuhimu wa kupambana na Rushwa Serikali imetunga sheria kanuni na miongozo mbalimbali na kwa sasa mapambano dhidi ya rushwa yanaratibiwa na kusimamiwa na ofisi ya Rais Ikulu kupitia mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa .

Ameongeza kuwa Serikali inatambua uwepo wa changamoto nyingi katika kupambana na rushwa kama ambavyo imekuwa ni changamoto ya maendeleo nchi nyingi duniani.

"Hata hivyo juhudi za Serikali kupambana na Rushwa zimeonesha mafanikio makubwa licha ya changamoto tunazozipata ambazo nina Imani kuwa nazo zitatatuliwa kupitia mikakati ya Serikali," amesema.

Kwa upande wa mwakilishi wa Takukuru, Dk. Emmanuel Kiyabo, alitaja changamoto wanazokabiliana nazo kiwa ni wananchi wanakuwa wagumu kutoa ushirikiano wa kutoa ushahidi

Pia Takukuru wanakabiliwa na changamoto ya kifedha kwa ajili ya kufanya kongamano mbalimbali

Katika kesi 100 mwaka 1995 tulikuwa tunafikia asilimia 40! kwa sasa ni asilimia 60 na tunatarajia kufikia asilimia 80 hadi 90 kwa malengo yajayo
 
Katika watu serious na wasioyumba misimamo ni Wanyakyusa si wanawake si wanaume

DPP Mnyakyusa hatanii nawajua.Take care
 
Aache story, amshughulikie kwanza DPP aliyekuwepo enzi za Magu ambaye ni Jaji kwa sasa Biswalo Kwa mali nyingi alizozulumu vikiwemo viwanja na majumba kwa kigezo cha Plea bargain kisha anajimilimisha kwa kutumia majina ya nduguze.

Hili swala limeumiza wengi na kuliacha kimya ni uhalifu mkubwa sana
 
Halafu atambue ni mahakama ndio itakayoamua kufilisi Mali zilizopatikana kutokana na rushwa
 
MKURUGENZI wa Mashitaka nchini ( DPP), Sylvester Mwakitalu, amesema

DPP amesema baada ya kuona umuhimu wa jambo hilo kwa sasa wametatua kwa kutoa sheria ndogo ambayo imewezesha wakuu wa mashitaka wa mikoa na Wilaya kupewa vibali isipokuwa kwa makosa machache yale ambayo yanafedha nyingi au yanayogusa viongozi wa Serikali..... ...........kutokana na umuhimu wa kupambana na Rushwa Serikali imetunga sheria kanuni na miongozo mbalimbali na kwa sasa mapambano dhidi ya rushwa yanaratibiwa na kusimamiwa na ofisi ya Rais Ikulu kupitia mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa .
TOTAL NONSENSE

Eti viongozi wa serikali na wapiga hela kubwa kushitakiwa itakuwa lazima DPP yeye binafsi apitie faili au atoe kibali maalum. Lakini vidagaa na wezi wa vi per diem vya hapa na pale watashtakiwa ovyo ovyo kwenye ma wilaya kata vijiji huko huko bila kujiuliza mara mbili!

Yani jizi la kitaifa, mhujumu uchumi wa mabilioni, waziri, CEO wa parastatal za umma, RPC, Jaji, Hakimu, ndio anapata robust due process! Kuhakikisha kwamba haonewi, habambikwi kesi, hakai rumande bila sababu. Mmesoma sheria ya wapi nyinyi vilaza wakubwa ?

Na ni kwa nini mapambano ya rushwa yaratibiwe na Ikulu ??

Ili kusudi DPP awe beholden to statehouse crooks???? Katibu Mkuu Kiongozi na Rais na PM ndio waamue nani ashitakiwe nani apeteshwe nani afutiwe kesi? Vipi kama wao wenyewe ndio prime suspects kama alivyokuwa PM Lowassa?

Eti sababu rushwa ni suala muhimu, basi wekeni na KILIMO, MADINI, UTALII, BANDARI chini ya Ikulu kwa sababu hayo ndio vastly more important, ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi hii.

Professional rubbish za Tundu Lissu ndio hizi alizosisema. Incompetent dumbbells ndio wanapewa kuendesha nchi, hatuwezi kupiga hatua.
 
TOTAL NONSENSE

Eti watumishi wa serikali na wapiga hela kubwa wao kushitakiwa itakuwa lazima DPP yeye binafsi apitie faili au atoe kibali maalum. Lakini vidagaa na wezi wadogo wadogo wanaweza kushitakiwa ovyo ovyo kwenye ma wilaya kata vijiji huko huko!

Yani mpiga dili kubwa ndio anapata more robust due process! Kuhakikisha kwamba haonewi, habambikwi kesi, hakai rumande bila sababu. Mmesoma sheria wapi nyinyi vilaza wakubwa ?

Na kwa nini mapambano ya rushwa yaratibiwe na Ikulu ??

Ili kusudi DPP awe beholden to statehouse crooks???? Rais ndio aamue nani ashitakiwe nani apeteshwe nani afutiwe kesi?

Eti kwa sababu rushwa ni suala muhimu, basi wekeni na KILIMO, MADINI, UTALII chini ya Ikulu kwa sababu hayo ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi hii.

Professional rubbish za Tundu Lissu ndio hizi alizosisema. Incompetent dumbbells ndio wanapewa kuendesha nchi, hatuwezi kupiga hatua.
Umenena vyema sana mkuu
 
Hivi mtu ukiandika uharifu badala ya uhalifu unakuwa unajisikiaje? Basi andika kikwenu kabisa. Kiswahili nacho Cha kukosea kweli?
Sio cha kukosea, hata wewe umenisikitisha yaani hujui wapi uandike herufi kubwa na wapi uandike herufi ndogo. Acheni kujifanya mnajua kila kitu.
 
Sio cha kukosea, hata wewe umenisikitisha yaani hujui wapi uandike herufi kubwa na wapi uandike herufi ndogo. Acheni kujifanya mnajua kila kitu.
Sawa hii ni clerical error inayotokana na simu Ila hizi R zenu zinaboa
 
Katika watu serious na wasioyumba misimamo ni Wanyakyusa si wanawake si wanaume

DPP Mnyakyusa hatanii nawajua.Take care
Siyo kwa katiba hii ambapo mzizi wa muhimili mmoja umejichimbia zaidi kuliko mingine.
 
Huyu DPP urefu wa kamba yake haumruhusu yeye kula kwenye hayo maeneo.
 
TOTAL NONSENSE

Eti watumishi wa serikali na wapiga hela kubwa wao kushitakiwa itakuwa lazima DPP yeye binafsi apitie faili au atoe kibali maalum. Lakini vidagaa na wezi wadogo wadogo wanaweza kushitakiwa ovyo ovyo kwenye ma wilaya kata vijiji huko huko!

Yani mpiga dili kubwa ndio anapata more robust due process! Kuhakikisha kwamba haonewi, habambikwi kesi, hakai rumande bila sababu. Mmesoma sheria wapi nyinyi vilaza wakubwa ?

Na kwa nini mapambano ya rushwa yaratibiwe na Ikulu ??

Ili kusudi DPP awe beholden to statehouse crooks???? Rais ndio aamue nani ashitakiwe nani apeteshwe nani afutiwe kesi?

Eti kwa sababu rushwa ni suala muhimu, basi wekeni na KILIMO, MADINI, UTALII chini ya Ikulu kwa sababu hayo ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi hii.

Professional rubbish za Tundu Lissu ndio hizi alizosisema. Incompetent dumbbells ndio wanapewa kuendesha nchi, hatuwezi kupiga hatua.
Daah mkuu umechafukwa kweli kweli
 
Aache story, amshughulikie kwanza DPP aliyekuwepo enzi za Magu ambaye ni Jaji kwa sasa Biswalo Kwa mali nyingi alizozulumu vikiwemo viwanja na majumba kwa kigezo cha Plea bargain kisha anajimilimisha kwa kutumia majina ya nduguze.
Hili swala limeumiza wengi na kuliacha kimya ni uhalifu mkubwa sana
Hapa na kuunga mkono. Na hiyo plea bargain dhuluma iliyotendeka pale sio biswalo mganga peke yake. Kumbuka ccm ni ukoo was panya.
 
Back
Top Bottom