Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Napenda uelewe kuwa, mitambo yote mikubwa ni bora zaidi iliyokwisha tumika kwa muda mfupi na kurekebishwa faults zote zilizojitokeza kuliko kuinunuwa brand new, ambayo hakuna company yoyote duniani itayoweza kukupa guarantee kuwa ni ''plug and play''. commissioning ya mitambo kama hii inachukuwa at least mwaka mmoja. Jee unafahamu hilo?

Nafahamu ila inategemea na mtazamo pamoja na mambo mengine.

Sheria inasemaje?
Na hiyo iliyokwishatumika ilitoka wapi? Ilishuka toka mbinguni au nayo ilinunuliwa brand new then ikarekebishwa hadi ikawa kwenye hali hii tunayoiona?
Mwenye mali ni nani? Mwizi au mtu muungwana ambaye nikipata tatizo na mali aliyoniuzia tutaonge tuelewane jinsi ya kufanya?
Je ni bora kununua kwa machinga kuliko kwa mwenye mali (dukani) hata kama utapoteza muda na gharama kidogo?
Je mke alieyezaa ni bora kuliko binti kwa sababu huna hakika kama atazaa?
Je makuwadi wako wanakusaidia kumpata huyo ni akina na nani na wana sifa zipi kuhusiana na dili yenyewe? Ni watu wa kuwaamini na wana aminika?

Samahani mkuu, mimi siko tayari kununua kanyaboya kwa ajili ya kukwepa gharama!
 
Upuuzi huu, hizi data na figures mnazitowa wapi? Process yetu ya manunuzi ilivyo na bureaucracy it takes 2 years to process, au hulijuwi hilo? unless kuwe na emergency, na ndio hizo wanazopigania zikiukwe ili muda usipotezwe.

Mitambo kama anayoongelea ndg Kokolo na hii ya DOWANS inaweza ikawa inalingana, ni kipi kingeharakisha ununuzi wa mitambo ya DOWANS, na isiwe vinginevyo?

Usikurupuke mzee...
 
Hayo matatizo ya Tanesco yalianza 2006?, Kikwete ndie aliyepiga kifuwa kuyatatuwa, au umesahau? Na alipobaini kuwa watu aliowaachia majukumu ya kutatuwa matatizo ya umeme wamefanya madudu (Lowassa, Karamagi, Msabaha), hakuwasamehe wala kumtetea hata mmoja, akawacha sheria ichukuwe mkondo. Au yote hayo huyajui. Besides, akatimuwa uongozi wa juu karibu wote wa Tanesco, akmuweka trouble shooter (Dr. Rashid), ambae ana track record nzuri, katika taasisi zote alizoongoza kwa wakati wake, hakuna scandals na madudu anayo yakuta anayanyoosha. Kaanza kuiweka sawa Tanesco, watui wanalalamika, Jee hamuujuwi uozo uliokuwa Tanesco kwa miaka ne miaka rudi? mnafikiri JK au trouble shooter wake wanaweza kuya tatuwa matizo hayo kwa mwaka mmoja? No way, Tanesco ni shirika kubwa lililooza kila sehemu, lina hitaji total overhaul, na ndio Dr, Rashid yupo mbioni kuliweka sawa na at the same time anataka watu wasitaabike kwa umeme, simple solution: Mitambo tayari ipo Ubungo, madudu yamefanyika, yanashughulikiwa. Kesi ipo Paris, Jee hamkumbuki ya IPTL, kwa kujidai kuvunja nao mkataba sasa tunalipa kutoke puani na vinywani mwetu, IPTL kesi wameshinda, ikabidi tulipe gharama za kesi zao na zetu, fidia, na faida na pia kulipa muda wote ambao wallikuwa idle na mkataba bado uendelee.

Ukifikiria hayo machache tuu, Dowans hali kadhalika, kesi watashinda, kwani ipo Paris, hakuna longo longo huko. Mkataba ni wa kimataifa, mitambo itumike isitumike tutailipia, gharama za kesi, zao na zetu tutazilipia. Na ikiwa IPTL imetutokea puwani basi hii itatutokea (sijui wapi?).

Simpo solushen, negotiate na hawa jamaa, nunua mitambo ya mambo yao kwa bei nafuu, kila mtu alipe gharama zake za kesi (ambayo hatushindi kabisa), watu wapate umeme. Other than that ni kuwatesa wa Tanzania.

Tatizo hili ni pure commercial na watu walichukulie hivyo, mambo ya kuchanganya politics na commerce ndio yanatuweka pabaya. Jee hatuoni yaliyokwisha tukuta tukajifunza?


nakubaliana na wewe faida ni kuokoa jahazi kwa kutumia mitambo ambayo tayari ipo nchini...someni mwananchi ya leo mahojiano na warioba..pia naye ametaka taifa liache mijadala mirefu .....na kuangalia namna ya kufanya tusikose umeme ..huo ndio uwe mjadala.zaidi amesifu role ya bunge ila akawataka wakumbuke wajibu wao ni kusimamia na sio kuagiza.Amesema kiutaratibu wala serikali haikutakiwa kupeleka suala hili bungeni..na akauita huo ni woga kwa serikali na kuogopa majukumu kwa woga wa impact za kisiasa,amesema sheria zinajitosheleza na utaratibu wa sheria wa kununua vitu wakati wa dharura au maafa upo kwenye sheria....[dhana ni kuwa serikali inaogopa bunge???]..ametabiri hali ya uchumi kuwa ngumu zaidi ...hasa kutokana na bei za maza kushuka...na njaa inayokuja..kakini akishangaa waandishi wa habari kutoipa mijadala hiyo nafasi...

kuhusu kikwete ...zaidi ya kubadili chimwaga na kujenga chuo kikuu dodoma kwa kuunganisha nguvu za mashirika ya hifadhi jamii...hakuna kitu kingine anachoweza kusimama na kusema amefanya kwa dhati.....
 
Nafahamu ila inategemea na mtazamo pamoja na mambo mengine.

Sheria inasemaje?
Na hiyo iliyokwishatumika ilitoka wapi? Ilishuka toka mbinguni au nayo ilinunuliwa brand new then ikarekebishwa hadi ikawa kwenye hali hii tunayoiona?
Mwenye mali ni nani? Mwizi au mtu muungwana ambaye nikipata tatizo na mali aliyoniuzia tutaonge tuelewane jinsi ya kufanya?
Je ni bora kununua kwa machinga kuliko kwa mwenye mali (dukani) hata kama utapoteza muda na gharama kidogo?
Je mke alieyezaa ni bora kuliko binti kwa sababu huna hakika kama atazaa?
Je makuwadi wako wanakusaidia kumpata huyo ni akina na nani na wana sifa zipi kuhusiana na dili yenyewe? Ni watu wa kuwaamini na wana aminika?

Samahani mkuu, mimi siko tayari kununua kanyaboya kwa ajili ya kukwepa gharama!

Tatizo lako unatazama upande mmoja wa shillingi, Jee, unajuwa ni hasara ngapi tunayoipata kila siku (sisi watumiaji umeme) kwa kesi tuliyoshindwa ya IPTL? na mwisho wake ni nini? inabidi tulipe, tulipe, tulipe. Na kama haya ndio yatatukuta kwa Dowans, tutalipa, tutalipa, tutalipa. tukiinunuwa tusiinunuwe tutailipia, hatuna uwezo wa kushinda kesi ya mkataba tuliosaini wenyewe, wenye makosa ni hao waliosaini hii mikataba mibovu mwanzoni kwa tamaa ya kujipatia vi-ten percent. Na si Dowans wala Dr. Idriss Rashid. Jee, unatatuwa tatizo kwa kujiongezea matatizo? hii ni kama, mtoto akikunyea wewe unakata mkono badala ya kwenda kuuosha.
 
Hakuna ubishi katika hili.

Si kweli.

Hamna kitu kama hicho. Mitambo iliyotumika inabakia kuwa mitambo iliyotumika, na hakuna guarantee kuwa itafanya kazi vyema kuliko mitambo mipya, na kinyume chake ni kweli vilevile. Hivyo hamna sababu ya msingi ya kununua kitu kilichotumika ilhali kuna uwezekano wa kupata kipya, chenye warranty na makaratasi yote yaliyokamilika.
 
Mitambo kama anayoongelea ndg Kokolo na hii ya DOWANS inaweza ikawa inalingana, ni kipi kingeharakisha ununuzi wa mitambo ya DOWANS, na isiwe vinginevyo?

Usikurupuke mzee...

Mitambo ya Dowans, already installed, tested and commissioned na tayari ipo Ubungo. Na Dowans wako tayari kuiuza its a matter ya serikali kukubali tu. It wont take a month, once ikikubaliwa. Simpo.
 
Nafahamu ila inategemea na mtazamo pamoja na mambo mengine.

Je mke alieyezaa ni bora kuliko binti kwa sababu huna hakika kama atazaa?

daaaa kaka dhana yako kiboko ..so tukienda kununua generator tusilipe hadi iwake na kudhibitika....hiyo safi...

kwani hata siku hizi ukiona kijana amekuja kulipa mahari aoe binti yako ujuwe kabisa ameshajaribu na akaona ..dalili ya mtoto ipo...

sasa ajali ni pale anapokimbia na kukuachia mjukuu.....binti atajitetea kwa mama yake kuwa alikuwa anajaribu mitambo..ya kuzalisha...

dhana yetu ya watanzania ...tunataka kujaribu ....au kuonja kama tunanunua karanga ..tungeitumia vema tusingenunua madege mabovu,mapantoni na mitambo mingine.....!!!!
 
Si kweli.

Hamna kitu kama hicho. Mitambo iliyotumika inabakia kuwa mitambo iliyotumika, na hakuna guarantee kuwa itafanya kazi vyema kuliko mitambo mipya, na kinyume chake ni kweli vilevile. Hivyo hamna sababu ya msingi ya kununua kitu kilichotumika ilhali kuna uwezekano wa kupata kipya, chenye warranty na makaratasi yote yaliyokamilika.

Hahahaha, mengine inabidi kuyaacha kama yalivyo. Sababu ya msingi ni kuwa wengi wetu hatujuwi somo la hesabati na hili lina matter sana.
 
Mitambo ya Dowans, already installed, tested and commissioned na tayari ipo Ubungo. Na Dowans wako tayari kuiuza its a matter ya serikali kukubali tu. It wont take a month, once ikikubaliwa. Simpo.

Hii sio sababu tosha ..

Ratiba ya mchakato wa manunuzi ni ileile, hivyo hapa hamna jipya, iwe mitambo kutoka nje au hii ya DOWANS.
 
Dar Es Salaam;391442]Tatizo lako unatazama upande mmoja wa shillingi, Jee, unajuwa ni hasara ngapi tunayoipata kila siku (sisi watumiaji umeme) kwa kesi tuliyoshinwa ya IPTL? na mwish wake ni nini
.
Mkuu, siangalii upande mmoja ila naomba utumia busara za kawaida tu. Unaweza kukaa meza moja kudiliana na mwizi aliyekuibia? Mbona hatufanyi hivyo kwa mambo binafsi, kujadili jinsi ya kurekebisha mambo na mgoni wako?

inabidi tulipe, tulipe tulipe. Na kama haya ndio tayatukuta kwa Dowans, tutalipa, tutalipa tutalipa.tukiinunuwa tusiinunuwe tutailipia, hatuna uwezo wa kushinda kesi ya mkataba tuliosaini wenyewe, wenye makos ni hao waliosaini hii mikataba mibovu mwanzoni kwa tamaa ya kujipatia vi-ten percent. Na si Dowans.
Kama tutalipa sasa tunasumbuliwa na nini? Kwa nini tusiachane naye ili angalau tupunzuze hasara. Kama tutalipa na sasa tunanunua mitambo yake maana yake tunampa jamaa mafuta na moto ili atukaange?

Jee, unatatuwa tatizo kwa kujiongezea matatizo? hii ni kama, mtoto akikunyea wewe unakata mkono badala ya kwenda kuuosha.
Mkuu unachanganya mambo. Mtoto hafanyi vitu makusudi. Ndiyo maana akikunyea unafuta na kucheka. Ila njema ikikurushia mavi naamini utapambana nayo ili angalau kieleweke. Ndiyo maana jamaa waliotaka kuturushia huo uozo wao tumepambana nao hadi wakatimua mbio. Kama si hivyo kwa nini Daktari mzima anapandisha mori na kususa kazi aliyoikubali mwenyewe?
 
Hahahaha, mengine inabidi kuyaacha kama yalivyo. Sababu ya msingi ni kuwa wengi wetu hatujuwi somo la hesabati na hili lina matter sana.

Hesabati ndio nini, au ndo version mpya ya uwizi na ufisadi? Usipime intelligence ya watu na fani zao, kwa makisio, lete hoja zenye mashiko.
 
Hesabati ndio nini, au ndo version mpya ya uwizi na ufisadi? Usipime intelligence ya watu na fani zao, kwa makisio, lete hoja zenye mashiko.

Kwa mwendo huu naona itabidi tuweke vyetu hapa kabla ya kujadili issues. Kwa hiyo mafisadi watatutesa kwa sababu kila utakachokiongea utaulizwa kama ulipata A au F kwenye hilo somo. Itabidi tunyamaze kama Mzee Kawawa! 🙄
 
.
Mkuu, siangalii upande mmoja ila naomba utumia busara za kawaida tu. Unaweza kukaa meza moja kudiliana na mwizi aliyekuibia? Mbona hatufanyi hivyo kwa mambo binafsi, kujadili jinsi ya kurekebisha mambo na mgoni wako?


Kama tutalipa sasa tunasumbuliwa na nini? Kwa nini tusiachane naye ili angalau tupunzuze hasara. Kama tutalipa na sasa tunanunua mitambo yake maana yake tunampa jamaa mafuta na moto ili atukaange?


Mkuu unachanganya mambo. Mtoto hafanyi vitu makusudi. Ndiyo maana akikunyea unafuta na kucheka. Ila njema ikikurushia mavi naamini utapambana nayo ili angalau kieleweke. Ndiyo maana jamaa waliotaka kuturushia huo uozo wao tumepambana nao hadi wakatimua mbio. Kama si hivyo kwa nini Daktari mzima anapandisha mori na kususa kazi aliyoikubali mwenyewe?


1) Dowans hakuiba na wala huwezi kumshika kwa wizi aina yoyote na ndio maana hakuweza kushitakiwa. Na ndio maana yeye ndio kashitaki huko Paris, na sisi ndio tunajitetea. Walioiba wanajulikana.

2) Hilo ndio liwe msingi wa ku-negotiate, tunajadiliana kununuwa, tukikubalina, kesi zote za madai zifutwe na mikataba yote zamani ifutwe, kulipia. Mfanya biashara yeyote mzuri ambae atapata mkwanja na kafaida kake haraka haraka badili ya kungoja, atakubali. Na nadhani hii offer kisha itowa yeye mwenyewe na ndio maana ikafikia watu kuongelea hili la kuinunuwa. Simpo.

3) Njemba zilizoharisha si unazijuwa? Dowans hayumo katika hao na ndio maana anadunda mpaka wa leo.

Daktari anaona upuuzi huu, ameshatowa ushauri wake na wa kuamuwa manunuzi si si yeye, kwani Tanesco hawana kitu, mifedha yote wanayoingiza wanalipa madeni ya kina IPTL na wengine, ambayo daktari kaikuta. Hataki yajirudie, kama wanasiasa hamtakai haya fanyeni nyinyi maamuzi. Mgao waja, msimlaum.
 
Kwa mwendo huu naona itabidi tuweke vyetu hapa kabla ya kujadili issues. Kwa hiyo mafisadi watatutesa kwa sababu kila utakachokiongea utaulizwa kama ulipata A au F kwenye hilo somo. Itabidi tunyamaze kama Mzee Kawawa! 🙄

Hawa jamaa wanaopigia upatu hii ishu siwaelewi kwa kweli. Wanazungukazunguka tu kama kuku aliyepigwa jiwe la utosini.


Unajua Dr. Mwakyembe amewaeleza vizuri kabisa hawa watu, amewaambia TANESCO wanunue hiyo mitambo, kama wanajua wanafanya kitu sahihi, kwani jambo la manunuzi mbona ni jambo la kila siku ndani ya Serikali na TANESCO? Iweje hili walilete bungeni? Wanataka ku-achive nini? Au wanataka huo ufisadi uanze kupata baraka za bunge ?
 
Hesabati ndio nini, au ndo version mpya ya uwizi na ufisadi? Usipime intelligence ya watu na fani zao, kwa makisio, lete hoja zenye mashiko.

Haswa, kwa kujuwa mambo wewe, nakusifu. Uliyajuwaje yote haya?
 
Tatizo kubwa ni kwamba TANESCO walilitupa suala hili barazani kabla hawajamaliza assignment yao. Matokeo yake, wanasiasa wakalidaka na kuwa ajenda muhimu kuelekea 2010.

Zitto sio mjinga, ameamua kuwapambanisha wabunge wa CCM kwa manufaa anayoyajua mwenyewe.

Kabla ya kung'ang'ania kwamba mitambo ya Dowans ndio mkombozi, TANESCO walitakiwa kuwa na quotations angalau tatu za mitambo mipya ya aina hiyo zikionyesha gharama na delivery time. Kwa kufanya hivyo wangeepusha uwezekano wa kuonekana wana agenda binafsi na Dowans. Kwa bahati mbaya mpaka leo sijasikia lolote juu ya hilo, zaidi ya kauli za wanasiasa.
 
1) Dowans hakuiba na wala huwezi kumshika kwa wizi aina yoyote na ndio maana hakuweza kushitakiwa. Na ndio maana yeye ndio kashitaki huko Paris, na sisi ndio tunajitetea. Walioiba wanajulikana.

2) Hilo ndio liwe msingi wa ku-negotiate, tunajadiliana kununuwa, tukikubalina, kesi zote za madai zifutwe na mikataba yote zamani ifutwe, kulipia. Mfanya biashara yeyote mzuri ambae atapata mkwanja na kafaida kake haraka haraka badili ya kungoja, atakubali. Na nadhani hii offer kisha itowa yeye mwenyewe na ndio maana ikafikia watu kuongelea hili la kuinunuwa. Simpo.

3) Njemba zilizoharisha si unazijuwa? Dowans hayumo katika hao na ndio maana anadunda mpaka wa leo.

Daktari anaona upuuzi huu, ameshatowa ushauri wake na wa kuamuwa manunuzi si si yeye, kwani Tanesco hawana kitu, mifedha yote wanayoingiza wanalipa madeni ya kina IPTL na wengine, ambayo daktari kaikuta. Hataki yajirudie, kama wanasiasa hamtakai haya fanyeni nyinyi maamuzi. Mgao waja, msimlaum.

Labda mimi ndiye sielewi na nahitaji kukimbizwa Mzambaluni. Gere anafanya nini lupango? Dowans na Richmond wana uhusiano gani (Richmond = or ≠ Dowans? Kwa nini Bunge liliagiza mkataba uvunjwe? Kama ni hivyo inabidi nikajaribu kufuta F ya Hisabati kwanza!
 
Hawa jamaa wanaopigia upatu hii ishu siwaelewi kwa kweli. Wanazungukazunguka tu kama kuku aliyepigwa jiwe la utosini.


Unajua Dr. Mwakyembe amewaeleza vizuri kabisa hawa watu, amewaambia TANESCO wanunue hiyo mitambo, kama wanajua wanafanya kitu sahihi, kwani jambo la manunuzi mbona ni jambo la kila siku ndani ya Serikali na TANESCO? Iweje hili walilete bungeni? Wanataka ku-achive nini? Au wanataka huo ufisadi uanze kupata baraka za bunge ?

Okay, tuseme Dr kafanya makosa kusema aliyoyasema ambayo wengine wam,ebatiza maneno yake kama kuwa ni kitisho... !!
Je ni kweli tutakua na tatizo la umeme kama Tanesco wasemavyo?
Je zoezi la kutengeneza mchakato wa manunuzi ya mitambo kwa maana ya kutengeneza tenda linaweza kufanyika kwa muda mfupi kabla tatizo hili halijaanza kama lipo?
Je kama mitambo ya Dowans inawezekana kutatua tatizo hili na kama bei zinazo tajwa ni anuai... ni kitu gani kinachotufanya tusite..

KUna mwanabodi mmoja amekuja na ile theory ya Arusha na Vodacom connection ambayo hata mimi ninaifahamu pia.Lakini je ni kweli kwamba kwa kuwa tu Dowans ina tokea katika mizizi ya Richmonduli basi ndio kila kitu kihusishwe na ufisadi?
 
Duh mbunge wetu kijana kachemka kupita kiasi.Ukisikilza kwa makini bila ushabiki utagundua Zitto bado ni mchanga mno katika siasa anahitaji msaada wa wakongwe wa siasa kama Dr Slaa.

Mheshimiwa Zitto anaweza kufanya jambo moja kubwa na zuri kwa watanzania.Aombe radhi watanzania.Hii inaweza kumsaidia siku za usoni kwasababu mpaka sasa naona anajaribu kujivua dhambi aliyojitwika mwenyewe ya kuwa mpiga debe wa Dowans.
 
Lakini je ni kweli kwamba kwa kuwa tu Dowans ina tokea katika mizizi ya Richmonduli basi ndio kila kitu kihusishwe na ufisadi?

Nadhani kuna ishu za msingi ambazo zimekwisha wekwa bayana. Nazo ni kama hivi;

1. Kuna suala la kesi huko Paris.

2. Ununuzi wa mitambo iliyotumika, ingali sheria za manunuzi zinakataza. (Sheria ya matangazo ya serikali, kama nipo sahihi)

3. Suala la warranty, na mengineyo kuhusiana na mitambo yenyewe.

4. Suala la ugeugeu wa TANESCO, mara wanataka mara hawataki kuinunua mitambo hii.

5. Kutaka kuzihusisha kamati za bunge ktk hili, wakti wakijua wao na Wizara ndio wenye maamuzi. Bunge kazi yake ni kushauri tu.


Haya ni baadhi ya mambo yaliyojitokeza kwa upande mmoja.
 
Back
Top Bottom