Nimebahatika kuzungumza na wajumbe wengi wa kamati ya Zitto, nimebahatika pia kuzungumza na wajumbe wengi wa kamati ya kina Mwakyembe, nimebahatika pia kuzungumza na watu wa ofisi ya Bunge, nimebahatika pia kusoma nyaraka za kamati ya Zitto na ile ya Mwakyembe, nimebahatika pia kusoma nyaraka za Waziri Ngeleja na mawasiliano yake na....... (nitaweka wazi siku mwafaka)... Nimebahatika pia kupata nyaraka zote muhimu na ambazo nadhani zitaanikwa JF soon.
Kwa maelezo hayo hapo juu, hakuna ambaye haiungi mkono Tanesco (si Dk. Rashidi) kupata mitambo mipya, hiyo iko katika mipango yao ya muda mrefu na mfupi. Hata wewe utapenda Tanesco wapate mitambo. Zitto anakosea kutosema asichosema na hivyo kutoa nafasi ya kuwachanganya watu, na kuna mahali alisema anafanya makusudi. Sijui anateka kutuambia nini. Pengine huu mjadala umesaidia sana kuwabana Tanesco mpaka wamekwama. Zitto amefanikiwa lakini amekuwa KAFARA wetu. Kama si Zitto suala hili lisingekuwa HOT kama ilivyo sasa na ndio maana limekuwa na wasemaji wengi na limesaidia mjadala kupaaa na kuwatisha kina Dk Rashidi am baya akageuka kuwatisha Watanzania.
Soma maandiko yake. Sikiliza matamshi yake ya SAUTI si ya kunukuliwa, utaona hakusema anaunga mkono kwamba lazima kunuliwa kwa DOwans. Kuna mahala amesema (narudia) kwamba kaama kuna ulazima wa kununua Dowans basi sheria zizingatiwe. na Kuwepo mjadala ili uamuzi ufanyike kwa HOJA si kwa JAZBA. Hapo sioni kosa la kimantiki ila kuna kosa la KISIASA kwam ba Dowans/Richmond ni alama ya mafanikio ya vita ya UFISADI kwa hiyo hatuwezi kukubali kwa gharama yoyote mtu yeyote (hata Zitto) kuuvunja huu MNARA wa vita ya UFISADI
Halisi,
Zitto nimemsoma kw amakini sana kauli zake hapa JF
1. Zitto alizungumza kwa niaba ya Kamati
2. Ni kweli Zitto alisema kama kuna ulazima wa kununua Mitambo ya Dowans basi sheria zifuatwe..............wat wakamuwekea sheria.........yeye akasema sheria mama haisemi hivyo....watu wakamwambia unaposoma sheria mama unatakiwa usome na regulations zake.....sikumsikia akijibu......Zitto anasahau kuwa sheria mama haiwezi kuainisha kila kitu
sasa basi narudia
1. Msimamo wa TANESCO ulikuwa nikununua mitambo ya Dowans....eti wakidai ni "Opportunity" iliyojitokeza
2.Zitto akaja boldly kuweka msimamo wake hapa JF kuwa he stands with TANESCO......nafikrir hili kosa la KIMANTIKI na wala si kisiasa au
3.Kosa lake kisiasa ni kukubali kuburuzwa na msimamo wa kamati yake.......kama alivyotuonyesha awali kuwa anasimama na kamati yake
4.Nia yake ya kukutana na Kamati ya Shelukindo...naweza kuelewa ilikuwa ni opportunity nzuri kwake kupata support kama yeye KWELI alikuwa anapinga ununuzi wa Mitambo ambayo TANESCO wanaitaka i.e. DOWANS....unfortunately hiyo nafasi haikutokea......na akaja akaharibu zaidi kuja kuweka msimamo wake hapa JF........
Well Halisi.....Mkuu wewe nakuaminia sana tu........labda hapo baadaye utakapokuja na facts zingine pengine nitakuelewa..........