Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Sasa Mwakyembe ameacha kuwa msemaji wa kamati yake ya Madini na Nishati na karukia kuwa msemaji wa kamati ya Hesabu za Mashirika ya umma. Unaona sasa tatizo la ku poke his nose kila mahala? Kama uwaziri umempitia mbali basi asubiri awamu ya tano. Njia anayotumia sasa haimsaidii sana hasa kwa huyu Rais aliyopo madarakani.

Mkuu acha kauli za kikuda, swala sio mtu kupitiwa mbali na uwaziri? hapa tunaangalia hoja yake ya msingi kwani uwaziri hautusaidii sisi bari mawazo yenye kujenga taifa letu. Usionyeshe uvivu wako wa kufikiri. Lengo mahususi la kuwa mbunge si kuwa waziri!
 
Je kama mitambo ya Dowans inawezekana kutatua tatizo hili na kama bei zinazo tajwa ni anuai... ni kitu gani kinachotufanya tusite..

Suala jingine nyeti, ni kuhusu bei yenyewe. Gharama iliyotajwa ya sh. 60 bilioni, inatiliwa shaka kuwa ni kubwa kuliko hata gharama ya mitambo mipya.

Hivyo basi, hapa kuna kuingizana kingi tu. Watu hawana huruma na jinsi mwananchi wa kawaida anavyopigika, wanataka kuwanyonya hadi damu ya mwisho.
 
Wakuu, kuna hoja mbili hapa tusiweke nguvu kubwa kujadili hoja moja. Kuna hoja ya Zitto, na maoni au ushauri wa Jaji Warioba.

1. Kwanza tukubaliane Zitto hapo alichemka sana: maelezo mengi yashatolewa juu yake.

2. Jaji Warioba nae pia kachemsha sanaaa, tena kama jaji na msomi ameonyesha uvivu wa kufikiri, kibaya zaidi fikra zake zimekuwa kama za samaki (Samaki anamtizamo mmoja tofauti na chura). Huwezi sema uchumi wa nchi utaporomoka bunge likiingilia utendaje hivyo liache umeme upatikane kwa mitambo ya Dowans, bila kujiuliza kuwa utendaji mbaya ndio uliotufikisha hapo tulipo. Inflation rate with financial engineering sasa inaweza kuwa 16% (13.5% December, 2008).

Binafsi sijamuelewa Warioba anamanisha nini kuponda jitihada za bunge kupambana na ubadhirifu wa mali za umma. kawashambulia wanahabari kuwa wameshikilia ufisadi tu na kusahau habari nyingine. Sasa kama habari za kifisadi zinamkera siwahusika waache ufisadi na hizi news zitakoma?. Kukemea bunge kuingilia mabo ya kisheria pia kachemka sana, kwani kama angekuwa anafanya kazi yake vizuri ya taruma yake kama mwanasheria basi angeweza shauri bunge juu ya mambo ya kisheria yanayovunjwa na serikali mfano swala la mgombea binafsi mahakama ilisha rule kuwa is unconstitution kumzuia mtu kugombea kama mgombea binafsi na bado hakushauri bunge kutunga sheria kueffect shauri la mahakama. Pia, swala la umeme, si bidhaa ya kuharibika (perishable good) kama nyanya. Nasema hivi nikimaanisha kunaishara ya muda mrefu inayoweza kukupa muda wa kujiandaa kutafuta suruhu nini kifanyike kupata umeme wa kutosha wakati wa upungufu. Kinachonshangaza inaonekana Dr. Idris hana njia mbadala isipokuwa kununua mitambo chakavu na kupiga mkwala kuwa hospitali zikikosa umeme asilaumiwe. Ukweli hastaili kuwa kiongozi kwani hana uwezo wa kuchambua mambo na hii ni pamoja na Walioba, kimsingi hawa nao ni wale wale tu.
 
Ikiwa kidogo ni ufisadi ikiwa kikuni ufisadi ,mitambo hiyo ni haramu kutumika na kununuliwa ukizingatia ina kesi na lawama kibao ,ili kuepuka kuoneana imani mitambo hiyo kununuliwa ni batili mpaka hapo kesi na malalamiko yatakapokwisha ndio trutajua kama wanaimani ya kweli ya kutuuzia.
Bonde la mto rufiji lina uwezo wa kutoa megawati zaidi ya 3000 ,sasa inakuwaje Mtz analala kiza baada ya uhuru miaka 50 iliyopita ,hivi gharama za kulivaa bonde la mto huo linagharimu kiasi gani ambacho Tz kama Tz kinashindwa kumiliki ? au kuna akina Anaconda kwenye bonde la mto Rufiji ambao ndio wakwamishaji wakubwa wa maendeleo hapa Tanzania ,hakuna maendeleo kama hawajakatiwa fungu ?
 
mkuu umesikia mahojiano waliofanya Zitto na Mwakyembe na ITV? Mwakyembe kasema live msimamo wa Zitto si wa kamati yake.....ni wake binafsi na anamshangaa kama ndio Zitto anaemfahamu.....Zitto hakubisha....

Mimi nimuuliza Zitto mwenyewe hilo swali hapa JF kwenye thread yenye heading " Dowans watupiga bao...", jibu alilotoa ni kwamba anao msimamo wake ila hawezi kuutoa kwa sasa kwa sababu wadau watashindwa kutofautisha msimamo wake binafsi na ule wa kamati. Alichokisema several times ni kwamba kwa sasa anasimamia maamuzi ya kamati.
Hata hivyo nilicholearn ni kwamba msimamo wake hautofautiani na huo anaouita wa "kamati yake" ndio maana nimekuwa nikimshauri aweke bayana msimamo wake juu ya hili la sivyo kila mtu atajitafutia jibu lake mwenyewe.
 
LAITI ZITTO ANGEUJUA UZITO

Wahenga walinena nasi tukatega sikio
Hoja walitoa waasisi tena nzito nzito
Ziumiazo ndizo nyasi wapiganapo tembo
Laiti Zitto angemdisi Idrisa wa Tanesko

Laiti Zitto angemdisi Idrisa wa Tanesko
Mbunge Kijana angehisi Dowani imedisko
Wala singedadisi uazizi wake mitambo
Angechukua bisi bisi aifungue wozo

Angechukua bisi bisi aifungue wozo
Kwa yake kasi angeunyofoa huo utumbo
Wanainchi ndio sisi tungelimuunga mkono
Laiti Zitto Mfanisi angejua tu wazito

Laiti Zitto Mfanisi angejua tu wazito
Asingelikuwa mwepesi wa kulitoa tamko
Sasa lafanya aonwe muasi wa wazalendo
Uwi mwokoeni na majasusi kijana Zitto


I like it kwa kuwa wengi humu ni watu wenye upeo tumemwelewa ni ajali ya mbinu za mafisadi
Ni kama kilichomkuta MR Pinda kuhusu mauaji ya maalbino pinda alilia tukamwelewa sasa yeye akiendelea kulumbana atazidi kulikoroga
Bora akubali tuu kosa ili awe amejifunza bado tutamuona ni mpiganaji
Vinginevyo atakuwa amevaa ngozi ya upiganaji na sio mwenzetu
 
Mimi sualalangu hapa sio Zitto kwenye hii habari....namshangaa Warioba, na niseme kuwa sijamwelewa kabisa ana maanisha nini? Kwa nini anadhani vyombo vya habari vinapotoka kuandika habari za ufisadi kwa kirefu? Hayo marobota ya pamba aliyoyatolea mfano anajua ni kwa nini hayanunuliwi? ukichunguza si utakuta noi mwendelezo wa ufisadi huo huo?

Simwelewi!
 
rushwa rushwa rushwa ni ugonjwa mbaya kuliko ukimwi, unaua unatoa akili unazabaza unatoa ushindani, na wazuri wanapataubutu.

Nimeandika sana nimelia sana kuhusu Zitto . badala ya kutoa ufafanuzi anasema tunamchukia tunamsema tunamsimanga . simwelewe amelishwa damu ya dhambi hajijui. kwa hili lazima ajieleze la sivyo kala sumu ya rostom hawezi kuitapika.

Chonde chonde tuwe wazalendo wa kweli na utaifa usiwe wimbo wa mafisadi.
 
Mimi nilimsifia Zitto na hotuba yake mbadala ya nafikiri Mawasiliano na Uchukuzi, kwa sababu ulikuwa ina stimulate economy na kuleta ufanisi, lakini hili suala la Umeme ukitilia maanani fani yake ya Uchumi na matatizo tuliokuwa nayo Tanzania baada ya kuangalia hayo mahesabu, na kuona hayo mapungufu ya mapato vs matumizi, soulution ni nini? si ni kuinvest kwenye njia mbadala amazo ni nafuu, kuliko kupiga kiswahili eti yeye kama mchumi anahofia nchi kwenda Gizani? oh na tax exemption hivyo taifa litakosa mapato, wakati hiyo nchi yenyewe inapatia only 23% ya population yake umeme. Ikiwa kama kweli ni mchumi mwenye kufikiria mbali angezungumzia Moja Stigler Gorge na miradi mingine, pili angezungumzia Sera ya uzalishaji umeme wa tanzania amapo hawa wawekezaji wanatuweka mateka katika ku-supply hiyo nishati, eg hiyo kiwira haijatoa umeme , wakati tulikuwa tunautegemea na Miradi mingine ambayo haijakamilika, kwanini kama nchi tujiweke kwenye hali kama hiyo?
 
Nashauri tu,tukitaka kuwa na consistent Debate,we must avoid childish speculation.

Kwanini tutangulize hisia za mtu kununuliwa? kwa mtindo huu,hatuwezi kuwa na mjadala wenye tija.Let us just dwell katika debate
Ubalikiwe mkuu,hapa naona kuna mashujaa wa CCM wanataka kupotosha mawazo ya watu dhidi ya Zitto na wao kujijenga kisiasa.Suala lililo mbele yetu ni namna ya kupata nishati ya uhakika kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.Sasa hapa watu wanataka kuaminisha watu kuwa Zitto ndie mwenye ukiritimba wa mawazo na ni wazo lake tu ndio lichukuliwe uzito.
 
Bunge linaweza kuingilia ununuzi hata kama jukumu ni la serikali..Kama mnakumbuka serikali ya Bush ilitaka kuipa contract shirika la Arabuni UAE kuendesha shughuli za bandari zake, bunge wakaingilia kati na mkataba huo ukafutwa.. Serikali ya Canada ilikuwa na mpango wa kununua Helikopta za kijeshi, bunge likaingilia kati kutokana na hitilafu za mkataba uliokuwepo..Na ktk mlolongo wa mijadala iliyopitishwa ktk nchi hizo hatukuona mgogoro wa kisiasa kati ya vyama, watu, serikali au mtu mmoja kunyooshewa kidole kwa sababu amepinga au amependekeza..Lengo ni kufikia maamuzi ya busara kwa kuzingatia maoni ya pande zote mbili kuhakikisha taratibu za jukumu linalokabidhiwa hazitoki nje ya sheria au malengo yaliyokusudiwa..

Kwa hiyo sii swala la ununuzi maadam serikali imekabidhiwa jukumu hilo, kabla ya hapo kuna kupitisha taratibu za matumizi hayo kama vile serikali (wizara ya Nishati) inavyoweza kupitisha matumizi ya mtambo huo na kuikabidhi Tanesco jukumu ununua..taratibu zikikiukwa serikali inaweza kabisa kusitisha ununuzi. Hatuwezi kusema sio jukumu la bunge, serikali kusitisha ununuzi huo hata kama Tanesco wamefikia makubaliano na shirika au bidhaa yenye utata..

Na sii kweli ununuzi wa kitu ambacho kinahitajika basi kinunuliwe hata kama ununuzi huo umekiuka sheria na taratibu za mwongozo wa nchi husika..Haya ndio yalke ya Karamagi kwenda UK kuweka mkataba wa Buzwagi kisha serikali ikadai sio kazi ya Bunge na kumshutumu Zitto kwa kuingilia majukumu yasiyokuwa yake.. wakati Zitto kaliokoa Taifa letu kuingizwa mkenge.
Kweli mh. Zitto kachemsha lakini ndivyo inavyotakiwa kisiasa, kuwa na mitazamo tofauti ktk kutafuta maamuzi ya maana kwa Taifa letu..lakini pia tukumbuke kuwa Zitto ni msemaji wa kamati yake hivyo yawezekana kura yake ilikuwa against ununuzi isipokuwa wengi wape ndicho kilichoondoa upinzani wake kuwa msimamo wa kamati ya mahesabu - who knows!
Ni through mijadala ya vikao hivi ndipo hoja huzuka, busara na taaluma zikatumika kulingana na vipimo tofauti.. hapo ndipo maamuzi ya maana hufikiwa na pengine kulinusuru Taifa gharama kubwa au mgawanyiko ndani ya serikali..
Matokeo ya ununuzi wa mitambo ya Umeme umetufunua wengi, hii ikiwa ni pamoja na viongozi, wabunge na wananchi wenyewe kuweza kuelewa hoja toka pande zote mbili za ununuzi. Sio swala la nani kasema nini isipokuwa ni swala la mjadala unaolenga manunuzi ya kifaa chenye utata....
 
Ningekuwa Zitto ningejitokeza na kusema nilishawishiwa vibaya na wajumbe wenzangu wa kamati ya bunge ya mahesabu ya mashirika ya umma. Hapo angeweka msimamo wake ambao tulikuwa tumawamini tungeweza mwamini tena ingawa wanasiasa huwa hawaaminiki!
 
Ahaaa, ni muongo,alipata kidogo dogo fulani !! Ana price zito asituzuge hapa,tena akitaka usalama wa chama chao ajiuzulu tu,hapo hamna short cut ya kujiosha kwa wana jamii forum.
 
Zitto,
Hapana sijaandika barua kwa Waziri ili asupport kununua mitambo ya Dowans. Sina mamlaka ya kuingilia manunuzi ya Shirika. Shirika linapokuja kwenye Kamati yetu huwa linakuja na Bodi, ikiwakilishwa na Mwenyekiti wao wa Bodi.

Nilizungumza na Shelukindo. Nilizungumza na Mwambalaswa. Sikumpata Mwakyembe kwani huwa hapatikani kwa urahisi kwa simu na alikuwa Kahama na Mengi. Seleli sikumtafuta maana asuingeweza kusaidia. Stella Manyanya nilimtafuta.

I am always like that napokutana na suala tete. Ndio maana hata Kamati nilipoona ina sway kwa TANESCO nikasema hapana, hatuwezi kupingana na Kamati ya Nishati na Madini. Nikaatoa hoja ndani ya Kamati kwamba Kamati 2 zikutane. Wenzangu hawakutaka kukutana na kuanza kulobby kwa spika asikubali kukutana. Wakaanza kujibu kupitia press. Sikuwa na cha kufanya bali kundika barua kwa Waziri kutoa maoni ya kamati kwa majibu wa kanuni za Bunge.

I tried my level best and all documented. JF ninavyoijua itapata tu hizo documents. Walionihukumu wataona aibu tu! I am genuine, i am honest and as always i sub-ordinate my interests to those of the nation. Sijakurupuka. Wazee wanaogopa kuwa challenged na vijana.
Mkuu wangu nadhani nimekusoma... nashukuru sana kwa maelezo haya na hakika ungeyaweka mwanzoni hapa JF tungekuwa ukurasa mmoja..Huko ktk magazeti ungesema kama kamati ilivyotaka lakini hapa nyumbani ungetushtua kinachoendelea laa sivyo mkuu wangu ilionyesha wazi sio Zitto tunayemfahamu..Kumbuka mengi yaliyopita siku zote umekuwa ukitushtua kwanza hata kama sio kwa habari kamili lakini tulifahamu umesimama wapi..Lakini ktk hili mkuu wangu ulipoanza kuwa mkali na kutoa maneno mazito ya kuhoji uzalendo wa wananchi kwa sababu tunaishi nje nilishtuka sana..Nikasema huyu kweli Zitto ama mtu mwingine maanake hao wanaishi ndani ya nchi kina Yona, Mramba, Rostam, Lowassa, Karamagi, yaani baraza zima la Mawaziri waliotangulia toka Mkapa hadi Kikwete wana uzalendo gani!.Ni kitu gani kinachompa ushujaa Zitto kama sio kupambana na mafisadi walioko ndani ya nchi na sio sisi tunaoishi nje!..mkuu sikukuelewa kabisa!
Hata hivyo, mkuu wangu sisi binadamu tunachokiomba kwako ni kusimamia maslahi yetu iwe hata kwa gharama kubwa..
 
Mkandara
Umeeleza vizuri sana juu ,lakini umefika sehemu ya Zito umempa nyepesi.Kila siku wewe na wote humu ndani tunalia na utawala wa sheria , kama unaamini utawala wa sheria basi kubali Zito anaunga Violation of laws

Na ndio maana mimi nafikiri tuambiwe ktk kifungu fulani cha sheria kinachosema ktk sakamstancesi fulani violation ya sheria inakubarika.

Harafu kingine kama kweli unakuwa na msimamo tofauti ktk masilahi ya Taifa si lazima uunge msimamo ambao huuamini eti kuisemea kamati mambo ambayo unaamini ni upekenyevu wa Taifa,Unajitoa ktk kamati .
 
Ahaaa, ni muongo,alipata kidogo dogo fulani !! Ana price zito asituzuge hapa,tena akitaka usalama wa chama chao ajiuzulu tu,hapo hamna short cut ya kujiosha kwa wana jamii forum.

By the way naona chama chake kipo kimya tu kuhusu hili nadhani wanaogopa kumcompromise kisiasa...ila wanajua ukweli ni upi...
 
Zitto,

Mkuu wangu nadhani nimekusoma... nashukuru sana kwa maelezo haya na hakika ungeyaweka mwanzoni hapa JF tungekuwa ukurasa mmoja..Huko ktk magazeti ungesema kama kamati ilivyotaka lakini hapa nyumbani ungetushtua kinachoendelea laa sivyo mkuu wangu ilionyesha wazi sio Zitto tunayemfahamu..Kumbuka mengi yaliyopita siku zote umekuwa ukitushtua kwanza hata kama sio kwa habari kamili lakini tulifahamu umesimama wapi..Lakini ktk hili mkuu wangu ulipoanza kuwa mkali na kutoa maneno mazito ya kuhoji uzalendo wa wananchi kwa sababu tunaishi nje nilishtuka sana..Nikasema huyu kweli Zitto ama mtu mwingine maanake hao wanaishi ndani ya nchi kina Yona, Mramba, Rostam, Lowassa, Karamagi, yaani baraza zima la Mawaziri waliotangulia toka Mkapa hadi Kikwete wana uzalendo gani!.Ni kitu gani kinachompa ushujaa Zitto kama sio kupambana na mafisadi walioko ndani ya nchi na sio sisi tunaoishi nje!..mkuu sikukuelewa kabisa!
Hata hivyo, mkuu wangu sisi binadamu tunachokiomba kwako ni kusimamia maslahi yetu iwe hata kwa gharama kubwa..

Na yule aliyesikika ktk radio Kenedy sio Zitto?
 
Wakuu, hizo sababu za Paris hazina mpango kabisa... Dowans hadi sasa hivi hawana address zaidi ya ile ya Rostam.. hawana makao makuu mara utasikia South Afrika, Arabuni, Costa Rica lakini kote hakuna shirika lililosajiliwa kwa jina hilo na linashughulika na uzalishaji umeme, manufacturer wa mitambo hiyo au supplier..Ni shirika BOMU hivyo kesi ya Paris itakuwa tamu ajabu kuisikiliza..Mengi yatafumka wakuu zangu na nina hakikka serikali ikidai uhalali wa chombo hicho tutafikia pale viongozi wengi hawakutaka tufike..ndipo tutyafahamu Who is Who..
Hizi habari zote za ununuzi sasa hivi ni kuepuka yanayokuja Paris, sasa hivi viongozi wanahaha wanajua wazi kwamba swala hili sio dogo kama walivyotegemea na walifikiria wakitumia neno Paris wananchi tutavua chupi zetu..HATUVUI.. na halali mtu mpaka kieleweke!
Nina hakika kesi ya Richmond itafunguliwa Paris kwa sababu mkataba wa Dowans ni wa kurithi, ilikuwaje hapo ndipo ngoma itakapo fikia mnenguo!...Ushahidi unaweza kwenda kwa mapana yoyote yake!..
 
Serikali ya Tanzania inaongozwa Kisiasa zaidi na isitoshe hata hiyo siasa yenyewe hatuijui vyema yaani ni wababaishaji tuuu .....sasa hakuna watendaji serikalini ila kuna wababaishaji ndiyo wamejaa .....badala ya kushughulikia vitu kitaalamu zaidi wao wanapiga makelele kutafuta UMAARUFU kisiasa waonekane wasemaji .............Ukiangalia mbali zaidi hakuna hata shirika moja la serikali limeendelea au linaongozwa kitaalamu waliojaa ni wababaishai tu serikalini.......hebu angalia mahakamani...wale wahusika wakuu wa ufisadi EPA na wengineo mahakama ilisema udhamini upo wazi ila lazima walete mali isiyohamishika na kama ni nyumba basi tathmini ifanywe na wathamini waliopo serikalini ............sasa nenda kaangalie valuation report nyingi zimefanywa mitaani .......ushahidi unaonekana hapo mahakamani sasa hapo utasema kuna watendaji?????
 
MkamaP,
Mkuu kwanza samahani, nilikujibu lakini naona maelezo yangu yamepotea sijui kilichotokea zaidi ya kuona kuwa mada zimeunganishwa, hivyo ktk process yao maelezo yangu yamepotelea somewhere..
Nitarudia kusema nakubali sana kuwa Zitto alichemsha na kweli alitoka nje ya sheria, ila hakuvunja sheria isipokuwa alipotoka (mtoto mpotevu) kwani hakuna kitu kilichofanyika.. yalikuwa ni maoni yake tu..Haramu kitendo mkuu wangu.
Turudi kwenye issue, mimi nadhani Zitto kilichomponza ni SIASA na ndio maana nilimwonya toka mapema.. na pengine swala zima limeanzia pale alipojiunga na kamati hizi na nakumbuka kina J.J Mnyika walikuwa wakipinga sana Zitto kujihusisha na mipango ya CCM..Hilo kwanza, Pili kilichotokea ktk kamati hii ni moja ya process za kawaida ambazo kwa nchi kama Tanzania mara nyingi sheria na taratibu zinaweza vunjwa kutokana na mazingira tuliyokabiriwa nayo!.. Kama sisi Waislaam nguruwe ni haramu lakini yawezekana kabisa ikatokea udhui ukamtafuna nguruwe, tena kwa kulamba vidole!..Haa haa haa!..Kesho yake baada ya matatizo ya njaa unatia udhu maneno yanarudi palepale..
Kilichotokea hapa ni Zitto kuwaambia waislaam wanaweza kula nguruwe katika mazingira ambayo hayakubaliki.. Uharamu wa guruwe Dowans bado upo palepale na Zitto kachuma dhambi lakini dhambi hizo hazimuondoi ktk Uislaam kwa sababu hakuna aliyekula nguruwe!..
Sasa kama imani yenu imeondoka kutokana na maoni yake ambayo aidha yalitokana na msukumo wa kisiasa bila yeye kufahamu kwamba anatumika kama chambo hilo ni maamuzi yenu.. binafsi siwezi kumhukumu hata kidogo..
 
Back
Top Bottom