Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Siku hizi internate inafanya kazi ,kujua bei ya kifaa ni jambo la kung'oli tu ,sasa huku kutaka kuibiana mchana ,sasa hawa akina zitti na kundi lake si wataumbuka ,halafu inashangaza jamaa wana mitandao kabakaba lakini wanashindwa kufahamu bei ya kifaa kipya ,kama hakuna wizi hapo kuna nini ?
 
wenyewe wanaita utaifa sisi tunaita uzalendo.
Ni rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kufika sir god.
Wakati Zito analeta utetezi wake lazima afanye cost anlysis na comparison and contrastya hayo waliyoyaona atueleze mradi mzima wa richmunduli uliwagharimu wamatumbi kiasi gani na huo wake na mwizi dr idrisa utatugharimu kiasi gani vile vile atueleze dowans ni akina nani kwani lazima tuwalipe.kwani muda wote wanajifanya hawajulikani.

Tanzania ya leo hakuna wa kumuamini ni lazima kujenga utawala wa sheria na wala rushwa wapewe adhabu za kunyongwa hadharani saa sita mchana .
Nchi inanuka rushwa hakuna utaifa wazalendo wote hawajaingia bungeni.
 
Wakuu kuna habari mbaya sana zimenifikia sasa hivi (according to TBC Taifa),

Dr Idrisa Rashidi ametangaza kuwa TANESCO wamefutilia mbali mpango wa kununua mitambo ya DOWANs eti kwa sababu watu wengine wameshindwa kuuelewa kwa hiyo wameptosha umma! Tumekosa huo utamu wa 10% toka kwa RA. Sina hamu kabisa, umeme umekatika wakati sinema imefikia patamu!
 
Last edited by a moderator:
Dr Idrissa nadhani ni Doctor wa ubabaishaji. Ubabaishaji BOT, Ubabaishaji VODA, Ubabaishaji Akiba cormmercial bank....malizieni!
 
Dr Idrissa nadhani ni Doctor wa ubabaishaji. Ubabaishaji BOT, Ubabaishaji VODA, Ubabaishaji Akiba cormmercial bank....malizieni!

Hivi Watanzania ni wajinga sana (mabwege au mazezeta) kiasi kwamba wababaishaji ndio wanatunukiwa nishani?? Kama mtu ameboronga huko kote kwa nini aendelee kuongoza shirika nyeti linalosimamia uhai wa Taifa kama TANESCO?

Kwa wajuvi wa sheria; ni kitu gani kama raia tunaweza kumfanya mtu huyu? Kwa hali ilivyo inaonekana aliyemteua au ambaye ana mamlaka na kitumbua chake hana shaka naye (he is very happy with his performance)!!

Kazi tunayo, tena siyo ndogo!!🙄
 
Sasa nadhani kuna kitu kitalipuka, si kwa dowans tu bali ni akribuni tu tutawajua wale wote wanaodhani sisi hatuelewi wao ni kina nani na wapo kwa maslahi ya nani. Mwakyembe kasema vizuri ni bora kukaa giza(ambalo tumelizoea na wengine umemem wanausikia tu) kuliko kununua kitu chakavu.

Zitto amechemka



BENDERA YA NCI KUKOSA RANGI NYEKUNDU NI TATIZO, DAMU NI MUHIMU
 
Wakuu kuna habari mbaya sana zimenifikia sasa hivi (according to TBC Taifa),

Dr Idrisa Rashidi ametangaza kuwa TANESCO wamefutilia mbali mpango wa kununua mitambo ya DOWANs eti kwa sababu watu wengine wameshindwa kuuelewa kwa hiyo wameptosha umma! Tumekosa huo utamu wa 10% toka kwa RA. Sina hamu kabisa, umeme umekatika wakati sinema imefikia patamu!

Ndio hilo 'jipu' lililosemakana litapasuliwa jana!? Angalau wamesikiliza maoni yetu ingawa kwa shingo upande.


Tanesco kupasua jipu
Mwandishi Wetu
Daily News; Thursday,March 05, 2009 @19:40

Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) leo linatarajiwa kupasua jipu juu ya mjadala ulioibuka hivi karibuni, ukihusu ununuzi wa mitambo ya umeme ya Kampuni ya Dowans.

Ingawa shirika hilo halikueleza wazi kuwa lengo ni kuzungumzia suala hilo, lakini waandishi wa habari waliokuwa wameitwa leo ofisini hapo kwa ajili ya mkutano, waliambiwa kuwa leo ndipo Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco atazungumzia kile kilichoelezwa kuwa ni taarifa nyeti ambazo wananchi inafaa ziwafikie kwa usahihi.
 
Kutokana na Mwakiyembe Zitto amepokea posho kubwa ,hapa anatoboa yaliofanywa nyuma ya pazia na ndio yanayomfanya Zitto awe mstari wa mbele katika kuipendekeza hoja ya kuinunua mitumba.

Dk. Mwakyembe aliwashangaa wanaotaka kupindisha sheria ya manunuzi kwa kigezo cha utaifa ili nchi isikae gizani na kuishutumu Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma kuwa walifanya ukaguzi katika shirika ambalo hakulitaja na kuishia kupewa posho kubwa.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Seriklai, Zitto Kabwe alisema kuwa, sheria za manunuzi inaweza isikiukwe lakini kinachotakiwa ni kuwepo mjadala wa kuangalia manufaa ya kununua mitambo hiyo kwa maslahi ya umma.

Kumekuwa na malumbano yanayoendelea kati ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, inayoongozwa na mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ambayo inaunga mkono kununuliwa kwa mitambo hiyo ya Dowans hata kama kufanya hivyo itakuwa ni kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma, inayoizuia serikali kununua vitu vilivyokwishatumika.
 
Summary:

Kwenye hii issue pande zote husika zina hoja ambazo ziko sahihi kabisa; ambacho hakiko sawa mpaka sasa hivi ni pande zinazobishana kutoelewa mwingine anabisha kwa sababu gani? Na kwa masilahi gani? Bila pande husika kusikilizana na kuelewa... kitakachotokea ni upuuzi mtupu.

Mimi nizungumzie tu upande mmoja ambao hautendewi haki kwa kuwa tu sio upande wa siasa (TANESCO)!

Interest ya TANESCO kutaka kununua mitambo iko kwenye upungufu wa uzalishaji wa umeme uliopo, hivyo wao wanaona kununua mitambo ambayo iko tested kwamba inafanya kazi kunaifanya TANESCO kuweza kupunguza tatizo ya upungufu wa umeme Haraka.

Kwa nini TANESCO wasitangaze tenda kununua mtambo mwingine?
1. Hawana Hela, lakini wanaamini wakiiambia serikali tununue mtambo ulioko site itakuwa rahisi kwa kupata support.
2. Taratibu za kununua mtambo mpya ni kwamba umeme utakaozalishwa na huo mtambo utapatikana baada ya miaka miwili.

Napingana vikali kabisa na wanaosema Dr. Idra... bla bla bla... ninavyoijua TANESCO hiyo report na recommendation zinatoka kwa wahusika wahandisi... kumbukeni pia jamaa walisha engage consultant ambaye aliangalia hali ya mtambo...
In short... TANESCO wanaongea reality, wakati WANASIASA wanaongelea HISIA. na si hivyo tu, wanasiasa bado wanaongozwa na mzimu RICHMOND... and this is very WRONG.
Kibaya zaidi umeme ukikosekana na athari zake ni kubwa kuliko hizo difference ya bil. 10 na hao wanasiasa wanaopiga mdomo sasa watakuwa wamelala usingizi mnono wakati TANESCO wakihangaika.....
 
NO NO NOOOO, Zito is not to blame he is acting in gudfaith for the nation kutokana na tarifa ya threat kutoka KWA IDRISA RASHID MD TANESCO,HUYUUU NI FISADI NA MWIZI AMEZOEA HELA KUBWA KAMA ZA RADA NA SASA BILIONI 90 ZA DOWANS
 
Fairpalyer,
Mkuu samahani, lakini maelezo yako ni biashara za kitindiga kwa sababu kila ulozungumza halipo pande zote mbili kimahesabu..Ni rahisi kukisia matumizi makubwa na muda mrefu ktk kuagiza mitambo mipya toka nje wakati jibu lako ni kuwepo kwa mtambo kama huo nchini na hutataka kutazama undani wa mtambo uliopo nchini gharama zake pia..

Nitarudia kusema magari yote yanayotoka nje yaliyoibiwa, huwa yana gharama ndogo sana kulinganisha na jipya linalotoka nje kihalali kwa sababu moja kubwa huwa yameibiwa na risk yake ndiyo hupunguza gharama zote!..Sasa hata hapa tunaweza kusema mwizi na mkosa ni binadamu, sio magari haya (ndio maana hayapelekwi mahakanai) na siku zote yanapouzwa mitaani mwenye kucheza kamari ni mnunuzi..gharama ya ununuzi kama huu ni kubwa kuliko unavyofikiria mkuu wangu..anything can happen!

Tofauti na magari, mitambo hii haikuibiwa, as afact hatufahamu lolote zaidi ya kwamba iopo nchini na inauzwa na Dowans ambaye anaweza kuwa dalali (mtu wa kati) au mwenye mali (Dowans=Richmond) au kweli wali waliinunua toka Richmond..

Hakuna mtu anayefahamu ukweli ama Tanesco wanafahamu isipokuwa wanaficha.. why? ni moja ya maswali tunayoshindwa kuelewa..

Na ndipo maswali mengi yanapofuatia..Ikiwa hatufahamu Dowans ni kina nani kesho mitambo hiyo ikiharibika tutamfuata nani? hawa jamaa hawana biashara Bongo hivyo wakiuza mitambo wataingia mitini na hatuna forwarding address yao..

Pili, mkataba kati ya Richmond na Dowans hatuufahamu zaidi ya kwamba Lowassa alishauri ubadilishaji wa mkataba mzima kutoka Richmond kwenda Dowans wakati jipu hili likianza kuiva..How! wananchi bado tupo kizani hatufahamu iliwezekana vipi shirika ambalo limejulikana kuwa ni feki limeweza kuuza mkataba kwa shirika jingine lililopendekezwa na waziri mkuu baada ya kutambua kuhusika kwa waziri huyo..

Haya baada ya yote haya..

Dowans pia wamekumbwa na matatizo hapa katikati kiasi kwamba Tanesco wenyewe walipendekeza kuvunja mkataba, na siku zote mkataba huvunjwa sio kwa sababu ya mtambo ila hutokana na hitilafu za kiutendaji kulingana na mkataba hivyo wahusika ni shirika moaj kwa moja na sio mitambo yao..again, sisi tunaweza pia jiuliza hao Tanesco walifahamu kuwa tunachohitaji ni UMEME toka mitambo yao kwa nini uvunje mkataba na Dowans wakati umeme unapatikana!..

Je walipovunja mkataba hawakufahamu kwamba nchi itaweza kuingia kizani ikiwa hawana option B au ndio walivunja mkataba wakifahamu kwamba tutainunua mitambo hiyo!..Why tyhis case haikuanzia siku ambayo Tanesco walivunja mkataba na Dowans tukaanza kufikiria Kiza na mengineyo yote yanayozungumzwa leo..Hawa wanasiasa walikuwa wapi?..

Kwa hiyo hasira za wananchi hazikuanza hivi hivi tu, toka Richmond hadi Dowans ni matatizo matupu..Na kama kuna watu wa kucharazwa bakora basi ni hawa viongozi wetu kwani ni wao toka Mkapa tumekuwa na tatizo la Umeme.. kumbuka Kikwete alipoingia miaka MITATU iliyopita tulikuwa kizani, hakuna solution iliyokwisha patikana pamoja na hesabu zako zote za upatikanaji wa mitambo mipya iwe kwa GHARAMA au MUDA tatizo la Umeme lipo palepale leo tunaingia mwaka wa NNE..Ni miaka mingapi inatakiwa ili hesabu zenu za cost analysis!.. ikiwa htaha huko GE kwenyewe hakuna aliyekwisha piga simu zaidi ya fikra za kunadi Tender tena kwa wababaishaji!..why tuuze Tender ikiwa wanufacturer wanauza moja kwa moja kwa mtumiaji?..

Kwa hiyo sababu sio ukosekanaji wa mitambo mkuu wangu tatizo lipo ktk uongozi toka ngazi za wanasiasa hadi viongozi ktk mashirika yetu..
 


Wadau, kuna taarifa zimenifikia kuwa Tanesco imesema sasa mitambo ya Dowans basi, imebatilisha uamuzi wa kuinunua, je kuna mwenye uwezo wa kutafuta taarifa zaidi afanye hivyo?

Kama ni kweli, kulikuwa na sababu gani za kufanya jaribio hilo? nani alitoa hoja hiyo kwa shirika ambalo, mwezi October tu mwaka jana lilikanusha tetesi kuwa lilikuwa mbioni kununua mitambo hiyo?

Je nini sababu za kubatilisha uamuzi wake wa sasa, hasa baada ya kututisha kuwa nchi itaenda gizani, kama vile hatujawahi kuliona giza, na kwamba Dowans ilikuwa ni suluhisho pekee?

Wakati Dr Rashid anachukua shirika, alielezwa kuwa ni mtu mwenye hekima na uwezo wa juu. Muda mfupi baadaye, alijaribu kujiuzuru kwa madai ya kuingiliwa kiutendaji, na sasa katika zogo la Dowans, ana nafasi gani ya kuaminika?

Watu wanasiasa kama Zitto, wana nafasi gani sasa katika kutetea utawala bora unaofuata sheria? Zitto alikuwa mkweli alipokuwa akitetea uwezekano wa kununua mitambo ile au alikuwa anataka kuiingiza serikali "king?"

Je, nani hasa alikuwa nyuma ya plani za kuhakikisha mitambo inanunuliwa, na mwekezaji hapati hasara, ni mmiliki wa awali wa Richmond, binamu yake Dowans, au maswahiba wake waliomsaidia kupata tenda iliyosababisha wanene wajiuzulu mwaka jana?

mambo yote haya yana kishindo gani uchaguzi ujao, 2010?

Tujadili tafadhali.
 
Last edited by a moderator:
FairPlayer,

Nimefuatilia kwa makini sana hoja zako. Sidhani kama wana JF wanashindwa kukuelewa, bali tatizo ni kwamba inawezekana maswali yako yamejikita kwenye utalaam zaidi na uhalisia ambao kwa wana JF inaweza kuwa vigumu kuupata. Kupata bei ya hiyo mitambo [c.i.f, Dar] ni jukumu la Tanesco, sisi tunaweza kupata bei ya kiwandani na ni rahisi kuipata kupitia kwenye mitandao.

TANESCO kosa lao ni kwamba walienda na pendekezo moja tu la kununua mitambo ya Dowans na sababu kubwa ni kwamba kwa kuwa iko Tanzania tayari, inafanya kazi na imeishaunganishwa na grid ya taifa. Hawakutoa alternative nyingine ambayo wangeitumia na ndiyo maana kuna watu wameuliza why mitambo ya Dowans tu?

Idea ya kununua mitambo ya Dowans ipo tangu Oktoba mwaka jana, ni zaidi ya miezi 6 sasa tangu wapate hiyo idea. Walitakiwa wakati wanajenga hoja ya kununua mitambo ya Dowans waje na pia alternative ya kununua mitambo mipya. Kama wali-take trouble ya kumtafuta consultant wa kufanya evalutiona ya mitambo ya Dowans, kwanini hawakufanya effort ya kupata bei za mitambo mipya pamoja na muda unaweza kutumika kusafirisha, kufunga, na kuanza kazi.

Tanesco walipogundua ununuzi wa mitambo ya Dowans una walakini ndipo wakaona wapitie njia ya kulishirikisha Bunge kwa kupitia Kamati ya Bunge. Kwa kufanya hivyo inawapa Tanesco kinga ya kutokuwajibika in case "dili" likiwa chafu. Uliona Mama Shamsha Mwangunga alivyokwepesha shingo yake kwenye kitanzi cha Mzee wa Kwela? Alisema alipata baraka za kamati ya Bunge na hivyo Bunge likashindwa kumshughulikia na issue ikawa imekwisha kwa kuombana msamaha, na hapa kwenye Dowans ndicho kilichokuwa kinatafutwa ili huko mbele ya safari mtu asije akawekwa kwenye kitanzi cha Dowans.

Nije kwenye swala la Bei, Bodi ya Tanesco iligoma kununua mitambo Dowans na walipendekeza kwamba timu ya wataalam wa Tanesco waende US kufanya window shopping ya mitambo hiyo na hivyo kwa kupitia timu hiyo tungejua bei ya mitambo mpaka ikiwa Bandari ya Dar na ingetumia muda gani. Hapo tungejua kufunga mitambo ingechukua muda gani, mpaka ku-commission na finally mitambo ingeanza kufanya kazi baada ya muda gani.

Kwenye huu ushauri kosa la Bodi ya Tanesco ilikuwa ni kuomba wajumbe 2 wa kamati ya Bunge ya Nishati na Madini iungane na hao watalaam wa Tanesco kwenye hiyo wondow shopping. Kiutendaji ni kosa kulishirikisha Bunge kufanya window shopping ama manunuzi ya vitu mbali mbali, kwa kuwa hiyo siyo kazi ya Bunge. Nadhani Bodi haikutaka kuingizwa mjini na ndiyo maana ikapendekeza wabunge waungane na hiyo timu. Lakini bado Bodi ilikuwa na nafasi ya kuteua wajumbe 2 waungane na timu ya watalaam ili kuepuka kuingizwa mjini, maana mambo yakija kuharibika watawajibika.

Sasa tujiulize, tangu mwaka jana December mpaka leo hii tunapojadili ununuzi wa mitambo ya Dowans, Je, Tanesco wameishafanya hiyo kazi ya window shopping? Kama hawajafanya wanangoja nini na wakati Bodi iliagiza wafanye hivyo ili Tanesco inunue mitambo mipya? Je, hawa jamaa hawana hila ya kutuingiza gizani? Mwezi June/July tukiingia gizani watasema kwamba hawakuwa na muda wa kununua mitambo mipya?

Kama walikuwa na nia njema na kutaka kuweka mbele maslahi ya taifa, nina amini kabisa watu wengi wenye mwelekeo wa kutaka kufanya CBA ya mitambo ya Dowans na mitambo mipya wangeweza kuwaunga mkono, lakini inakuwa ngumu kuwaunga mkono kwa kuwa wao wenyewe Tanesco wana info za mitambo ya Dowans.

Ngeleja alipoulizwa swali kuhusu bei ya mitambo mipya alisema ni around $ 90 million [Dowans wanauza kwa $ 69 million]. Hapa jamvini kuna watu wanasema bei ya mitambo mipya ni $ 39 million, Spika wa Bunge anasema ni $ 34 million. Hizo ni bei za mitambo ikiwa US kwa manufacturer. Waziri alipata wapi hiyo bei? Kwanini kuna tofauti kubwa sana kati ya bei ya Ngeleja na bei ya Spika na bei nyingine zilizo hapa Jamvini? Sijaona bei hapa jamvini iliyo zaidi ya $ 50 million kwa mitambo ya MW 100.

Tanesco wangetutendea haki na ningeona wamefanya kazi iwapo wangekuja na info full kwamba gharama za kununua Dowans ni hizi hapa, na gharama za kuagiza mitambo mipya ni hizi hapa na kwamba ununuzi mpaka ufungaji na kuanza kazi kungechukua miezi kiasi kadhaa.

Kama waliweza kuleta mtalaam kutoka Ujerumani kuja kufanya tathimini ya mitambo na wakajua thamani yake, kwanini wasifanye homework ya kujua gharama halisi na muda wa kupata mitambo mipya. Wanaishia kusema ni bei ghali ni kiasi gani hawasemi, kununua mitambo mipya itachukua muda mrefu, miezi mingapi hawasemi. Kwanini watu wasi-doubt kwamba wanataka kulishwa kasa huku wakiwa wanaona?

Dowans walirithi mkataba wa Richmond mwanzoni mwa 2007, na within 6 months waliweza kuagiza mitambo na kuifunga na kuanza kuzalisha umeme, na mojawapo ya hiyo mitambo ni ule ambao Tanesco wamekuwa wakidai kwamba ni kama mpya, sasa kama wao walitumia miezi 6 kwanini sisi tutumie miaka miaka 2????
 
Kama ni kweli itakuwa wamefanya U-turn. Kelele na kuambiwa ukweli zimesaidia. Taifa likienda hivyo ambapo mawazo ya Wananchi yanasikilizwa tunaanza piga hatua njema.
 
Kama ni kweli itakuwa wamefanya U-turn. Kelele na kuambiwa ukweli zimesaidia. Taifa likienda hivyo ambapo mawazo ya Wananchi yanasikilizwa tunaanza piga hatua njema.

Thanks Mkuu;

Idris ana matatizo yake lakini sometimes ana maamuzi ya kiume... kama hili la u-turn ni kweli, basi ni dume haswaa (PS: hapa simuhusishi chochote kuhusu EPA/BOT etc.]

Alkaloids ni chungu sana lakini zina medicinal properties
 
Wakuu Mkandara, Keil na Companero

nimefurahi kwa hoja zenu. mimi pia nimekuwa nikijiuliza maswali hayo, na kuona viongozi kama Marmo wanasema sema spika asitoe hukumu kwa kuwa si kazi yake (wakati hata hivyo alitoa maoni tu jana) inazidi kunishangaza sana. Ni nguvu gani inayosukuma hii hoja? sasa nasikia leo Tanesco imesema haitanunua tena hiyo mitambo, nimepost thread hiyo kule Business thread mtaiona.
 


Wadau, kuna taarifa zimenifikia kuwa Tanesco imesema sasa mitambo ya Dowans basi, je kuna mwenye uwezo wa kutafuta taarifa zaidi afanye hivyo?

Kama ni kweli, kulikuwa na sababu gani za kufanya jaribio hilo? nani alitoa hoja hiyo kwa shirika ambalo, mwezi October tu mwaka jana lilikanusha tetesi kuwa lilikuwa mbioni kununua mitambo hiyo?

Je nini sababu za kubatilisha uamuzi wake wa sasa, hasa baada ya kututisha kuwa nchi itaenda gizani, kama vile hatujawahi kuliona giza, na kwamba Dowans ilikuwa ni suluhisho pekee?

Wakati Dr Rashid anachukua shirika, alielezwa kuwa ni mtu mwenye hekima na uwezo wa juu. Muda mfupi baadaye, alijaribu kujiuzuru kwa madai ya kuingiliwa kiutendaji, na sasa katika zogo la Dowans, ana nafasi gani ya kuaminika?

Watu wanasiasa kama Zitto, wana nafasi gani sasa katika kutetea utawala bora unaofuata sheria? Zitto alikuwa mkweli alipokuwa akitetea uwezekano wa kununua mitambo ile au alikuwa anataka kuiingiza serikali "king?"

Je, nani hasa alikuwa nyuma ya plani za kuhakikisha mitambo inanunuliwa, na mwekezaji hapati hasara, ni mmiliki wa awali wa Richmond, binamu yake Dowans, au maswahiba wake waliomsaidia kupata tenda iliyosababisha wanene wajiuzulu mwaka jana?

mambo yote haya yana kishindo gani uchaguzi ujao, 2010?

Tujadili tafadhali.

Mkuu Mbalamwezi,
Kama ni kweli Idrisa amegeuka na kusema hawatanunua mitambo ya binamu wa Richmond a.k.a Dowans basi tunajua kuwa sasa kelele za wananchi kupitia viongozi wazalendo bila kusahau vyombo vya habari basi vimesikika. Na tukifanikiwa hili, basi na tuongeze kelele nyingi hadi mafisadi wote katika kila nyanza (EPA, ubadhirifu wa madaraka, mikataba mibovu, tender mbovu, etc) watupwe gerezani. Ila mimi na wewe hatujui Rais wetu yuko upande upi?????
 
Back
Top Bottom