Siasa zinaipeleka nchi bapaya!!!!
Niko upande wa TANESCO 110% shabikieni siasa lakini nchi iko kwenye hati hati... siku yoyote kukiwa na mtambo wa MW hata 45 unatatizo tunaenda kwenye mgao...
It takes time kununua, kuagiza, kufunga na ku-komisheni mtambo... tutakuwa pamoja kwenye vibari au sio...
Heri yenu mlioko US... mtatucheka tu.
TANESCO wana facts,,, ninyi mnaongelea HISIA.
Kasheshe, niruhusu nizungumze kama kwa niaba ya watanzania walioko nje ya nchi na ambao wamechukua msimamo wa kuipinga Dowans!
1. Ninakuelewa unachosema na usifikiri ya kwamba tunapopinga hivi sisi familia zetu zote ziko marekani au ulaya. Tuna mama, kaka, dada, watoto na wengine tumeacha wenzi wetu huko. Tunapopinga miradi hii ya kifisadi siyo kwamba hatujui gharama yake. Kwa hiyo kutufikiria kwamba tunaandika kwa sababu hatuguswi na tatizo la umeme moja kwa moja ni kutokututendea haki. Hali ya umeme inagusa vimiradi vyetu, inagusa mipango yetu, na inagusa maisha ya ndugu zetu na wale tunaowapenda. Hivyo hatupingi kama watu tusio na maslahi katika matokeo ya upingaji wetu.
2. Kusema kuwa uko upande wa Tanesco unataka tuonekane kuwa sisi tunaipinga Tanesco. Hii ni kutubebesha mzigo ambao wenyewe hatukuchutama kuubeba. Tulichokipinga ni Tanesco kununua mitambo toka kampuni ya kifisadi ya Dowans. Period. Hakuna mtu aliyeipinga Tanesco kama miezi sita iliyopita ingeanza mchakato wa kununua majenereta toka GE au watengenezaji wengine. Kama Tanesco wangetangaza tenda mwezi ule ule wa nane walipovunja mkataba na Dowans nina uhakika makampuni mbalimbali yangejitokeza kushindania na hasa katika hali hii mbaya ya kiuchumi.
Hadi hivi sasa ninajua for a fact kuna majenereta ambayo yako tayari GE (gas turbines ya uwezo mbalimbali) ambayo waliotaka kuyanunua wameahirisha kutokana na hali mbaya ya kiuchumi. Taarifa hizi tayari zimefikishwa nyumbani na kinachohitajika ni uongozi makini tu. Kama kweli tunataka majenereta hayo yatakuwa nchini ndani ya miezi mitatu na yakaanza kazi. Watanzania wanaweza kuvumilia kwa miezi mitatu!
Hivyo hatuko kinyume na Tanesco bali tunaungana na bodi ya tanesco, wanasheria, na wadau mbalimbali ambao katika suala la Dowans waliona mwelekeo wa kifisadi wa Watanzania kulishwa kwa nguvu chakula kilichooza ati kwa vile nyama imeisha jikoni. Wakati kuna kuku wako bandani, na msitu umejaa paa na visungura!
3. Katika hili hakuna cha kuchekesha. Hili ni suala nyeti na zito. Ni suala ambalo maamuzi yake ni lazima yaume. Hata hivyo katika kuumiza huko tusikubali hata kidogo kuvunja sheria zetu au kuwanufaisha watu wachache ati kwa kuwa!
Tuungane tulilie utawala bora, uwajibikaji, uwazi, na matumizi bora ya madaraka. Inashangaza kuona kuwa wewe hutatizwi na tishio/mkwara wa Dr. Idris kwa vile unajua kuwa ni kweli anachosema kwamba kwa vile hatujanunua mitambo ya Dowans basi nchi itakuwa gizani, wagonjwa watakufa mahospitalini, wanafunzi hawatasoma vizuri na viwanda vitafungwa! Yote haya nii kwa sababu ya Dowans!