Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Zitto, Dk. Mwakyembe watofautiana Dowans

2009-02-27 10:07:44
Na Muhibu Said


Dhamira ya Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) ya kutaka kununua mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura yenye uwezo wa kutoa megawati 100 inayomilikiwa na Kampuni ya Dowans, imezua mambo.

Hiyo imetokana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Dk. Harrison Mwakyembe, kutofautiana kuhusu suala hilo.

Tofauti kati ya Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) na Dk. Mwakyembe Mbunge wa Kyela (CCM), imeibuka siku sita baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, William Shellukindo kutamka hadharani kuwa kamati yake haikubaliani na dhamira hiyo ya Tanesco inayoonekana kuungwa mkono na Kamati ya Zitto.

Shellukindo, ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), alitangaza msimamo huo wa kamati yake, siku moja baada ya Tanesco kuripotiwa na vyombo vya habari ikiendeleza dhamira yake mbele ya Kamati ya Zitto ya kutaka kununua mitambo hiyo.

Tofauti kati ya wabunge hao, ambao katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, wametokea kuwa kivutio kikubwa kwa Watanzania kwa ujasiri wao wa kupambana na ufisadi na mafisadi nchini, imedhihirika baada ya Dk. Mwakyembe, ambaye kueleza hisia zake kwamba, ameshangazwa na hatua ya Kamati ya Zitto kuzungumzia suala la Dowans wakati si kazi yake.

``Kazi ya Kamati ya Zitto ni kuangalia mahesabu na siyo sera. Nadhani Zitto anapaswa kusoma kanuni za Bunge aelewe,`` alisema Dk. Mwakyembe katika mahojiano maalum na Nipashe juzi.

Dk. Mwakyembe alisisitiza kuwa maamuzi yaliyofikiwa na Kamati ya Madini na Nishati kuhusu suala hilo, hayawezi kamwe kupingwa na kamati yoyote hivyo, akamshauri Zitto kusoma kanuni za Bunge.

Naye Zitto, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, alisisitiza kuhusu uamuzi wa kamati yake wa kumuomba Spika wa Bunge kibali ili aruhusu kuitisha kikao cha kamati zote mbili (ya Hesabu za Mashirika ya Umma na Nishati na Madini), serikali, Tanesco na Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA) ili wajadili na kufikia muafaka wa pamoja kuhusu suala la kununua mitambo ya Dowans ili kuepuka kamati kupingana.

Alisema wazo la Dowans lilikuja baada ya kamati yake kukagua matumizi ya Tanesco na kugundua kuwa katika kila Sh. 100 inazopata shirika hilo, Sh. 84 zinakwenda kwa makampuni yanayoiuzia umeme.

``Hivyo, ndio tukaamua kuomba kukutana na Kamati ya Nishati na Madini tujadili hiyo hali kwa pamoja ili nchi isije kukumbwa na giza,`` alisema Zitto.

Alisema kazi ya Bunge si kuingilia utendaji wa serikali bali kusimamia.

``Hata hivyo, inaonekana Bunge linataka kuingilia utendaji wa serikali, linatakiwa lisimamie tu,`` alisema Zitto na kuongeza: ``Kamati ya kina Mwekyembe haikusikiliza Tanesco, hivyo tunaiomba ifanye hivyo``.

Zitto alisema suala lolote lenye maslahi ya umma yuko tayari kukosolewa, hawezi kamwe kuingiza siasa.

``Hivi kweli Watanzania wako tayari kukaa katika giza? Kamati yangu ina nia njema kwamba kamati zote mbili ziwasikilize ndio tutoe uamuzi ambao utakuwa na maslahi kwa taifa kuliko kulumbana,`` alisema

Alisema kwa hali ilivyo sasa taifa linakabiliwa na upungufu wa megawati za umeme zaidi ya 100, hivyo haoni sababu gani nchi iingie katika gharama kubwa za kuweza kuangiza mitambo wakati tayari ipo ya Dowans.

``Kwanza tukianza kuagiza mitambo kutakuwa na gharama kubwa ambazo tutalipa, mawazo yangu ni kwamba tuangalie uwezekano wa kununua mitambo ya Dowans ili nchi isije kuingia katika giza kama Tanesco walivyotuambia. Tukiingia katika giza uzalishaji utakupungua na uchumi utatetereka,`` alisema Zitto
Mimi Jumatatu wiki hii, Nipashe ilimkariri Shellukindo akisisitiza msimamo wa kamati yake wa kupinga dhamira hiyo ya Tanesco kwa vile inakiuka taratibu na haina maamuzi ya kununua mitambo hiyo.

Shellukindo, alisema mwenye maamuzi ya kununua mitambo hiyo ni serikali kama imeona kuna dharura ya kufanya hivyo.

Hata hivyo, alisema taratibu zilizopo zinataka suala hilo lifikishwe kwanza bungeni ili likajadiliwe na kupata baraka za Bunge.

Alisema ipo pia, sheria ya manunuzi inayozuia kununua mitambo chakavu kwa vile hatua hiyo ni ya hatari.

Kutokana na hali hiyo, alisema haoni kuwa ni busara kung'ang'ania kutaka kununua mitambo ya Dowans kabla taratibu zinazohusika hazijafuatwa na kwa kuzingatia pia, kwamba, mitambo ya kampuni hiyo haijulikani ilitumika kwa muda gani.

``Tanesco wanadai kuwa Dowans wanalo jenereta jipya. Lakini mitambo yao (Dowans) iliingizwa nchini mwaka 2006 na utekelezaji ulianza Desemba 2007. Sasa hilo jenereta linaweza kuwa jipya? Na hata yale (majenereta) mengine hatujui kama ni mapya,`` alisema Shellukindo.

Alisema inashangaza kuona Tanesco iking`ang`ania kutaka kununua, huku mkononi mwake ikiwa na amri ya mahakama iliyoomba kuzuia kuuzwa kwa mitambo ya Dowans kwa vile inaidai kampuni hiyo.

``Hatuna uhakika Tanesco wanaidai nini Dowans, hilo haliko wazi, tunataka tujue kwanza hilo. Hata hivyo, kama hilo lipo basi si wangekubaliana wabadilishane badala ya kununua,`` alisema Shellukindo.

Tanesco iliifikisha dhamira yake hiyo kwenye Kamati ya Zitto miezi miwili baada ya Kamati ya Nishati na Madini inayoongozwa na Shellukindo, kupinga suala hilo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja Desemba, mwaka jana.

Awali, Zitto alikaririwa na Nipashe Jumatatu wiki hii akisema kuwa katika kikao kati ya kamati yake na Tanesco kilichofanyika jijini Dar es Salaam Jumamosi wiki iliyopita, uongozi wa shirika hilo walitoa hoja za msingi kuhusu dhamira ya shirika ya kutaka kununua mitambo ya Dowans.

Zitto alitaja sababu nyingine ya kamati yake ya kuomba kibali hicho kwa Spika, ni kwa vile Kamati ya Nishati na Madini, haikutoa nafasi ya kukutana na Tanesco ili waeleze kwanini wanataka kununua mitambo hiyo ya Dowans.

``Walikutana tu na Waziri Ngeleja wakapinga Tanesco kununua mtambo huo wa Dowans,`` alisema Zitto, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Alisema pia, watatumia fursa ya ruhusa hiyo Spika kujadili kuhusu hatma ya umeme wenye megawati 300 wa Mtwara baada kampuni ya Barick kujitoa na umeme wa upepo wa Singida.

SOURCE: Nipashe
 
Kubalini yaishe, nunueni hayo majenereta, mwachilieni Gire.. tusonge mbele! what is the problem?
 
Mtazungushana hadi miguu iote sugu! Nunueni mitambo ya Dowans, walipeni kina Rostam, mwachilieni Gire, yaishe tusonge mbele.. hii kambi ni lazima tuanze kutoka sasa. Viongozi tumewachagua wenyewe, na tuwe tayari kuishi na kuona matokeo yake. Mkitaka kitu tofauti tuchague viongozi wengine!!!
 
wait on a minute........hapo unamzungumzia Zitto as Zitto...au unaizungumzia kamati ambayo Zitto yumo............

.........kama sikosei kauli ya Zitto kwenye hii issue alikuwa against kununua mitambo michakavu.......kutokana na sheria za manunuzi...........ndani ya kamati kuna wajumbe waliokuwa wanakubali maneno ya Dr Idris........au mimi ndio sielewi

Zitto anataka TANESCO wanunue mitambo hiyo chakavu kwa shilingi bilioni sitini.
 
Nini kinamsukuma Zitto leo kutetea ununuzi wa mitambo ambayo Kamati ya Bunge ilishasema kuwa ni chakavu?

Amefanya wapi utafiti wake na kuona kuwa walichosema kamati ya Shelukindo ni uongo?

Nani mkweli kati ya hawa wawili? Zitto anapaswa kutoa majibu ya uhakika kwa watanzania ili kuondoa maneno ambayo yamezagaa sana mitaani kuwa amemezeshwa kitu????
 
Hivi Zitto ana utaalamu gani katika ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme? Je, TANESCO walikuwa hawajui kama kutakuwa na matatizo ya umeme miezi michache baadaye? Kama walijua kwa nini walisubiri mpaka dakika ya mwisho ili kuishinikiza nchi kununua mitambo ya Dowans? Sasa hivi wanapoteza muda chungu nzima kwa malumbano ya mitambo ya Dowans muda ambao ungetumika kuanza procedures za kununua mitambo mipya kabisa ambayo naamini inaweza kuwa na bei nafuu kuliko hiyo mitambo ya Richmond/Dowans.
 
Why not DOWANS: legal opinion
Among the factors which vitiate under The Law of Contract Act (LCA)is FRAUD and MISREPRESENTATIO. Effects of these two will render the contract to be voidable. The contract will be void ab initio once you discover there was a fraud or misrepresentation Ss. 17 and 18 LCA.

For anyone to enter into a contract there is something which we call capacity. S. 11 of LCA provides for who is competent to enter into a contract. Sub-section 2 says;

"an agreement by a person who is not hereby declared to be competent to contract is void."

In the contract between RICHMOND and TANESCO there was a fraud and misrepresentations on then part of the Richmond. Second since Richmond was not in existence it had no capacity to enter into any form of contract. Since DOWANS inherited the Richmond's contract, and since there was no legal contract, Dowans inherited un-existed contract which is not enforceable anywhere.

My stand; since the government incurred very big loss because all deeds which involved Richmond, and since Richmond has no legal existence, government has to confiscate the so called DOWANS turbines. Dowans has to sue Richmond and Richmond has to sue government. Since Richmond can't sue or be sued there is no case.

Kwa hiyo hili la kununua mitambo halipo bali ni kuitaifisha. Maana ililetwa hapa kwa garama zetu na insurance tulilipia sisi na umeme hatukupata tukaingia hasara kubwa. Hii case serikali inipe niisimamie nitashinda tu



Ochu, heshima mbele mkuu

Asante kwa analysis yako but with due respect I have to differ with your opinion.

Kama sheria ya Tanzania ndio imeanishwa kutumika katika huo mkataba basi uchambuzi wa sheria hapo juu waweza kuchukua mkondo wake.

Lakini, as i can feel it, this was a kind of International Business Transaction na inanifanya nichelee kukubaliana na wewe kuhusu hizo principles ulizoweka hapo juu unless umeona mkataba unasimamiwa na sheria ya nchi gani au kanuni zipi; yote yanawezekana, unaweza kuta Tanzania courts do not have jurisdiction on the matter na kwamba ikitokea kukiwa na msuguano wa mkataba, labda Iternational Arbitration will take over mfano mzuri ni Kesi ya IPTL na TANESCO ambayo ilifanyika hapa marekani.

Deal kubwa kama hiyo, I am sure jamaa watakuwa wameweka kifungu kinachoonyesha sheria ya nchi gani itatumika au vitu kama Incoterms au UCP.

Kwa hiyo tukiupata huo mkataba itakuwa vema na rahisi kuuchambua otherwise we are just dealing with some kind of speculation.

Shadow.
 
Last edited:
Zitto anapaswa kutoa majibu ya uhakika kwa watanzania ili kuondoa maneno ambayo yamezagaa sana mitaani kuwa amemezeshwa kitu????

Maneno yaliyozagaa ama maneno mnayotaka/penda yazagae?

Tatizo watanzania tunaamini sana katika nguvu ya rushwa kiasi ya kwamba tunaashindwa kuamini kuwa kuna watu wanaweza kuchukua maamuzi magumu bila ya kuwa wamepewa rushwa ama kufaidika na maslahi binafsi.

Anyway, kuna uwezekano mkubwa sana kuwa KIRANJA anajua ukweli lakini nkwake ni wakati muafaka wa kupunguza udhia wa imani ya watanzania kwa Zitto na kuinua uhalali wa POLITICAL MERCINARIES wa mfumo fisadi kama kina MWAKYEMBE......

Omarilyas
 
Mkataba wa Richmond/Dowans uliingiwa kwenye mazingira kama haya , kwani walisubiri mpaka dakika za mwisho kisha wakasema kulikuwa na dharura.

Zitto naye ameamua kutoa kauli za kuwa kuna dharura na kama tukiamua kuagiza mitambo eti itachelewa sana , na hivyo nchi kuwa gizani , ni lazima tujifunze kujenga taifa ambalo linafanya mambo yake kwa mipango kamilifu na sio kuamua kwa misingi ya dharura ile hali Taifa haliko vitani.
 
Hivi Zitto ana utaalamu gani katika ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme?...

Kaka nakuhakishia kuwa Zitto kamwe haingili jambo bila ya kufanay utafiti wa kina. Kama kuna mbunge anayefanya utafiti wa kazi yake kwa kusoma na kukusanya taarifa kwa juhudi kubwa basi huyo ni Zitto. Nasema haya nikiwa na authority ya kutosha kuhusu utendaji kazi wa Zitto tangia enzi za MLIMANI.

omarilyas
 
Zitto anataka TANESCO wanunue mitambo hiyo chakavu kwa shilingi bilioni sitini.
Hapo ndipo Rostum alipotupiga changa la macho. Dowans walishachukua billioni 30 na sasa wanataka tuwalipe tena nyingine billioni 60. Kwa kweli Tanzania ni nchi ya kusadikika.
 
Zitto anapaswa kujua kuwa ni miongoni mwa wawakilishi wa wananchi ambao watanzania wengi wana imani naye sasa anapokua anajiingiza kwenye kutetea kununuliwa kwa Mitambo ya Dowans , ajue kuwa ni yeye mwenyewe anawatengenezea mazingira watanzania ya kutaka wakose imani naye ama wapunguze imani kwake.

Zitto should be smart than this.
 
Waungwana nadhani itakuwa jambo la busara kama tukiwekewa majukumu ya kamati hizo hapa ili tuweze kujuwa kama nani alisema nini na kwanini. Kabla hatujaspeculate sana tujuwe kwanza majukumu yao.

Zito yuko kamati ya mahesabu,yeye nadhani kamati yao inaangalia kama pesa hizo zimetumika ipasavyo, halafu lazima kuna kamati itakayokuwa na majukumu ya kuhakikisha ufanisi wa mitambo hiyo, ie hiyo ya kina Mwakyembe na kamati hizo lazima zishirikiane ili kufikia maamuzi constructive yasiyoliletea Taifa hasara....Hivyo kwa wenye kuweza kutuwekea responsibilities za kamati hizo mbili yaani ya Mwakyembe vs ile ya Zitto then tuendelee na mjadala ya kwamba tuweigh pande zote mbili yanai kununuliwa ama kutokununuliwa na sababu za maamuzi ya either or.

Ila Zitto kukubali mitambo chakavu kwa kigezo cha kutokutaka watanzania wasikae gizani ni kama political opportunity,well inaweza kuwa Zitto ana nia nzuri lakini si ni kinyume cha sheria kunua mitambo chakavu? Hii issue ni ya muda muda mrefu na hivyo walikuwa na nafasi ya kuja na altenative solution,ila inawezekana amekubali yaishe. Kwamba penye udhia? Hiyo ni juu ya wananchi...Ila tuwekewe majukumu yao hapa ili mjadala usiegemee upande mmoja.
 
Zitto anapaswa kujua kuwa ni miongoni mwa wawakilishi wa wananchi ambao watanzania wengi wana imani naye sasa anapokua anajiingiza kwenye kutetea kununuliwa kwa Mitambo ya Dowans , ajue kuwa ni yeye mwenyewe anawatengenezea mazingira watanzania ya kutaka wakose imani naye ama wapunguze imani kwake.

Zitto should be smart than this.

That is called true leadership. Kuwa tayari kusimamia kile unachoamini kuwa kinalinda ama kina maslahi kwa Taifa hata kama kitaathiri umaarufu wako....

omarilyas
 
Zitto inaonyesha ameanza kulewa na ukamati alioingizwa ,na sasa inaonekana wazi si mwenzetu ni mwenzao , ila kitu kimoja tu ambacho ni cha kuzingatia nacho ni gharama za mitambo hiyo na mitambo mipya..
Jambo jingine ikiwa kampuni yenye mitambo hiyo bado ipo kwenye mgogoro na serikali naona itakuwa si jambo la busara kuinunua labda serikali watumie mbinu za kuitaifisha mara moja. Ili kurahisisha kazi.
 
Kwa hiyo tunaweza sema ile misimamao yake ya awali ni kwasababu alikuwa hajajua system inavyofanya kazi.
 
Maneno yaliyozagaa ama maneno mnayotaka/penda yazagae?

Tatizo watanzania tunaamini sana katika nguvu ya rushwa kiasi ya kwamba tunaashindwa kuamini kuwa kuna watu wanaweza kuchukua maamuzi magumu bila ya kuwa wamepewa rushwa ama kufaidika na maslahi binafsi.

Anyway, kuna uwezekano mkubwa sana kuwa KIRANJA anajua ukweli lakini nkwake ni wakati muafaka wa kupunguza udhia wa imani ya watanzania kwa Zitto na kuinua uhalali wa POLITICAL MERCINARIES wa mfumo fisadi kama kina MWAKYEMBE......

Omarilyas

Kwa mtindo huu nawaambia kuwa tutakua hatumjengi Zitto , kama tukiendeleza kuamini kuwa hawezi kuteleza ama kila analofanya basi ni sahihi.

Kama tukiendelea kuamini kuwa kila anayesema jambo kuhusu Zitto basi huyo ana niambaya naye , na kuonekana kuwa yeye ni adui ama anataka kumbomoa Zitto.

Zitto anapaswa kusaidiwa kwa kuambiwa pale atakapokuwa anateleza ama wengine tunaamini kuwa hakupaswa kwenda njia hiyo.

Lazima tufike mahali tuwe tayari kuukabili ukweli hata kama gharama zake ni kubwa.

Ninavyomjua Zitto sio kiongozi wa kupenda kusifiwa sifiwa ila ni mtu ambaye yupo tayari kukosolewa na huwa anajisahihisha.
 
Maneno yaliyozagaa ama maneno mnayotaka/penda yazagae?

Tatizo watanzania tunaamini sana katika nguvu ya rushwa kiasi ya kwamba tunaashindwa kuamini kuwa kuna watu wanaweza kuchukua maamuzi magumu bila ya kuwa wamepewa rushwa ama kufaidika na maslahi binafsi.

Anyway, kuna uwezekano mkubwa sana kuwa KIRANJA anajua ukweli lakini nkwake ni wakati muafaka wa kupunguza udhia wa imani ya watanzania kwa Zitto na kuinua uhalali wa POLITICAL MERCINARIES wa mfumo fisadi kama kina MWAKYEMBE......

Omarilyas

Hapo naanza kuogopa! Hivi maamuzi magumu ni kununua vyuma chakavu (scrapers)? Ingekuwa pesa yako ya mfukoni ungenunua scraper badala ya gari na wakati huo ukiwa na uwezo wa kwenda kuchukua brand new pale Toyota Motors? Shida kubwa kwa watanzania ni kuiona pesa ya serikali kama mtoto wa kambo!

Hapo juu.... kama Mwakyembe ni fisadi RA nani? Malaika Gabriel au Mjukuu wa Mtume Mohamad?
 
Back
Top Bottom