Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Wakisha pata detils hizo wafanye nazo nini? Mbona walipata details za ndege ya Rais (Gulfsteam) na bado ndege ikanununliwa kwa bei ile ile ya serikali..

Hizo zilikuwa enzi nyingine.....Tanzania ya 2009 sio ile ya kabla ya 2006...

Omarilyas
 
Waheshimiwa ZITTO KABWE, Dr. SLAA::::

Tafadhali wabunge wetu na viongozi wa kamati mbalimbali, DOWANS ni Kanyaboya, Rashid ni fisadi na yuko kwenye mikono ya hao kina Chenge, Lowassa, Rostam.

Let us start from this premise:: Dowans generators are defective and/or are not available.

What next?? Kama kweli mitambo ya Dowans ni mizima mbona karibu mwaka sasa hakuna wanunuzi wengine popote duniani?? Si wakaiuze kwingine au logic hapa ni kuwa kama sio Tanesco (Wadanganyika) mitambo hiyo aina pengine pa kupelekwa??

Yaani Tanesco iwasiliane na Wartsila au GE wakati huu ambao mashirika haya hayana wanunuzi sababu ya credit crunch, tuone kama hatutapata mitambo ya 100mW within 3 months and at a better price or maybe slightly more with warranty for at least the next 10yrs.

So, Zitto itakuwa aibu mno tena mno kama ukishindwa mkuu kutumia ujanja wetu watoto wa mjini kuleta makampuni haya makubwa ili iwe mfano kwa mafisadi kuwa sasa TZ tumezinduka.

Zitto pse pse For the sake ya sisi vijana mkuu usituangushe kwenye hili sababu kutavunja hata maana ya kuwa na JF kama hata wewe utashindwa kuonyesha vitu vilivyo wazi kabisa, Yaani Mh. Shelukindo aweze kupiga full stop huu wazimu wa Dowans, halafu wewe Zitto kama mwenyekiti wa kamati unapiga danadana tena as a member wa JF, hapana MKUU, ukishindwa omba JF ifanye contact moja kwa moja na Wartsila au GE, ili kieleweke.

Najua hapo juu I'm rambling sababu nimeamka na mshangao kamati iliyo chini ya Zitto inashindwa ili suala straight forward au ndio Rostam kafika mpaka kwako mkuu???
 
Inaelekea mkurugenzi wa TANESCO alishakuwa na mpango wa kufanya biashara na DOWANS siku nyingi. Badala ya kupanga jinsi ya kununua mitambo yake, husubiri tu mpaka sababu ya uharaka itokee ili aushinikize umma. Soma ilivyokuwa mwaka jana.


Govt: No Dowans-Tanesco deal

2008-10-18 11:07:19
By Rose Mwalongo


The Government and the Tanzania Electric Supply Company (Tanesco) have categorically refuted claims of a move to buy power generators from Dowans Tanzania Ltd.

The measure was allegedly intended to offset the critical power shortage in the country.

A state-run Sunday newspaper, quoting an impeccable source, said in its latest edition that the country`s giant utility firm had written a letter to the government urging the authorities to approve the sale.

According to the report, in its application, Tanesco had sought permission to take part in the procurement process of the 35 mw gas turbines lying idle at Ubungo in Dar es Salaam.

However, Energy and Minerals minister William Ngeleja yesterday told The Guardian that he was completely unaware of such a move.

``What is wrong? Where did you get this information from?`` said the minister. He said he had just arrived from abroad and therefore knew nothing about it.

Later during the day, this reporter eventually met Minister Ngeleja in his office. The minister categorically stated that the government had no plan to buy or hire any of Dowans turbines.

``The government is keen to abide to regulations. Tanzanians should not worry when it comes to utilization of natural resources. We (the government) are keen about doing things properly and are taking charge of everything appropriately,`` said Ngeleja.

An impeccable source within Dowans told The Guardian that the Dowans management had on Thursday night visited the plants and tested them.

The source said the Dowans boss who had inspected the machines had informed the staff that they were only waiting for the minister to come back from a trip to strike the deal.

``The boss is just waiting for the minister to sign the documents. This (Friday) morning, we expected the deputy minister to visit Dowans plants, then later today or tomorrow, the machines would be put to use,`` informed the source.

Tanesco board chairman, Ambassador Fulgence Kazaura when contacted for comments, appeared to be shocked: ``Tanesco wants to buy power from Dowans! Ask that question to the Managing Director,`` he said.

However,
the Tanesco MD was apparently not available for comments.

The Tanesco-Dowans ill-fated wedding ended in August this year with Tanesco claiming that the contract between the two parties was unbearable and could not just continue because the company ``is now generating adequate power`` from its own sources.

Tanesco communication manager Badra Masoud told The Guardian in an exclusive interview on Thursday in Dar es Salaam that she was completely unaware of the said deal
When reached for comments, Energy and Minerals deputy minister Adam Malima said he was not aware of anything in regard to the issue.

``The minister is out of the country at the moment (Thursday) and no one can make decisions regarding the issue in his absence. Whatever speculations you heard about the matter are mere fabrications. I am not aware of anything like that,`` said Malima.

However, a close source to Tanesco confirmed that the government had actually attempted to buy the Dowans' generators.

``Dowans owners wanted the government to sign a contract with them before they could switch on their machines. This happened during the recent power rationing crisis,`` said a source, who preferred anonymity.

The source further stated that Dowans had never attempted to switch on its plants since the plant`s closure at midnight on July 30, this year.

A source close to Dowans confirmed that Tanesco had had an encounter with the Dowans entrepreneurs over the same issue, but said ``the boss refused and said he can only do so with the signing of legally binding documents.``

Dowans and Tanesco entered into the contract after Richmond Development Company LLC failed to generate 100mw as stipulated in the June 23, 2006 agreement, which was signed after power-generation dams ran dry following prolonged drought.

Revoking the contract some few months ago, Tanesco said its contract with Richmond had no legal mandate and its transfer from Redvo to Richmond, later on to Dowans Holding SA Limited and eventually to Dowans Tanzania Ltd., did not conform to the original terms and was therefore illegal.

Last month, Tanesco customers connected to the national grid experienced five days of power rationing when Songas switched off three gas turbines for technical reasons.

Another power shedding stint followed some few days later when a Tanesco transformer and one of the Aggreko turbines developed technical hitches.

SOURCE: Guardian
 
Wako wapi akina Shelukindo waliopinga kukata deal na DOWANS mwaka jana, je misimamo yao imebadilika?

Richmond ghost haunts Dowans

2008-12-18 11:37:56
By Angel Navuri

The government has directed Tanesco to abandon negotiations on purchase of Dowans power generators, which are located at Ubungo in Dar es Salaam. Minister of Energy and Minerals William Ngeleja told a fully-packed press conference yesterday in Dar es Salaam that the Dowans` turbines were too old to be purchased.

His announcement came barely two days after the House Committee on Energy and Minerals, chaired by MP William Shelukindo, rejected the proposed deal.

The committee`s reaction came in the heels of reports from a cross section of the media, which quoted Tanesco Communications Manager Badra Masoud as saying that the issue was still at the stage of internal discussion between Tanesco and Dowans.

Minister Ngeleja said the government had sought the views of the House Committee on Energy and Minerals and concluded that Tanesco would leave the negotiation table.

``We have directed Tanesco to opt out of the deal as we shall be violating both the National Assembly recommendations and the Public Procurement Act. The turbines are too old for use by Tanesco,`` said Ngeleja.

``Dowans produces electricity that can be generated by other power plants like Mtera Dam, Hale, and Nyumba ya Mungu.``

He said the Dowans' generators were able to operate continuously for 12 to 13 years but thereafter, the refurbishing would be quite expensive and take a long time.

The minister said the government would purchase similar plants directly from manufacturers, although the process could take time.

On Tuesday, MP Shelukindo said that he was surprised to hear that the government wanted to get involved with people who had once conned it.``We call upon the government to find an alternative solution to the problem, rather than rushing for fire brigade solutions,`` said Shelukindo.

He said the government had had a whole year to find alternative means, and experience had proved that fire brigade decisions had caused the nation to suffer giant losses.

Shelukindo said what was left was for the government to implement the recommendations of the Mwakyembe Committee, one of which was to terminate the Dowans contract.

``For us, going back to discuss an issue that the House had already resolved amounts to breach of Parliamentary regulations. Should the government decide to buy the machines, let them do so on their own but not involve us,`` he said.

He said the Mwakyembe Committee had proposed legal action against those implicated in the scam, but the culprits were yet to be taken to court.

``The culprits could be the very same people who are now advising the country to buy the machines,`` said Shelukindo.

For his part, Simanjiro legislator Christopher Ole Sendeka said buying second hand machines went against the Public Procurement Act.

``It is crystal clear that the Procurement Act does not allow the government to purchase used machines,`` the MP said.

Dowans and Tanesco entered into the contract after Richmond Development Company LLC failed to generate 100MW of electricity as stipulated in the June 23, 2006 agreement, which was signed after power-generation dams ran dry following prolonged drought.

Revoking the contract some few months ago, Tanesco said its contract with Richmond had no legal mandate and its transfer from Redvo to Richmond, later on to Dowans Holding SA Limited and eventually to Dowans Tanzania Ltd., did not conform to the original terms and was therefore illegal.


SOURCE: Guardian
 
CCM sasa tishio
• Sasa yatishia kulisambaratisha taifa
na Mwandishi Wetu

SIASA za makundi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimeanza kuchukua sura mbaya na ya hatari inayoonyesha kila dalili za kutishia mustakabali wa taifa katika kipindi kifupi kijacho.

Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili uliofanyika wiki hii umebaini kwamba, iwapo hatua za makusudi na madhubuti hazitachukuliwa na uongozi wa juu wa CCM na serikali yake, upo uwezekano wa hali kuendelea kuwa ya wasiwasi mkubwa muda si mrefu.

Matukio ya hivi karibuni kabisa, yanayojumuisha aina ya uandishi wa habari unaochafua na kuwatukana watu uliodumu, ni matokeo ya kustawi kwa makundi yenye uhasama mkubwa ndani ya CCM ambayo yamejipenyeza kwa siri na wakati mwingine kwa uwazi ndani ya vyama vya upinzani na kwa watu walio nje ya ulingo wa kisiasa.

Ufuatiliaji wa muda mrefu wa mwenendo huo wa mambo umeonyesha kwamba, kushamiri na kustawi kwa makundi hayo kwa kiwango kikubwa kumechochewa na hulka ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa CCM kuamua kukaa kimya na kuonyesha msimamo wa kutofungamana na upande wowote.

Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili unaonyesha kwamba uamuzi wa baadhi ya vyombo vya habari kuandika habari zinazolenga maisha binafsi ya watu maarufu kisiasa na wakati mwingine kugusia maisha yao binafsi, ni matokeo ya kuibuka kwa mgawanyiko na uhasama mkubwa uliojidhihirisha ndani ya CCM, tangu Februari mwaka jana mara tu baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na mawaziri wengine wawili kulazimika kujiuzulu, baada ya majina yao kutajwa kwa namna moja au nyingine katika kashfa ya Richmond.

Uhasama huo unaoendelea kukua na kuchukua sura tofauti kila wakati, ndio ambao hivi karibuni umesababisha kubadilika kwa mara kwa mara kwa upepo katika suala nyeti linalohusu zabuni ya kutengenezwa kwa vitambulisho vya taifa.

Matukio ya karibuni yanaonyesha kuwa, hoja hiyo ya vitambulisho vya taifa, iliyoibuliwa bungeni na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA) sasa imegeuka na kuchukua mwelekeo unaoonyesha kuwapo kwa makundi mawili ambayo ama yanajaribu kumwangamiza Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha au kumnusuru kutoka katika sakata hilo ambalo linaweza likawa kashfa nyingine serikalini.

Wakati taifa likisubiri kuona hatima ya matukio hayo mawili ya kuchafuana kwa watu maarufu na lile la vitambulisho vya taifa, umeibuka mjadala mwingine mkali wa chini kwa chini na mwingine wa wazi, unaohusu uamuzi wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kuendelea na dhamira yake ya kutaka kununua mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura ya Dowans, yenye uwezo wa kutoa megawati 100.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumapili unaonyesha kwamba, tayari makundi yale yale yenye uhasama mkubwa ndani ya CCM, tayari yameligeuza suala hilo nyeti, linalogusa hatima ya taifa katika kutafuta suluhu ya tatizo la miaka mingi la upungufu wa nishati ya umeme kuwa ajenda za kupingana na kuhujumiana kisiasa.

Uchambuzi uliofanywa na gazeti hili kutokana na mahojiano ya wazi na mengine yasiyo ya wazi (off records) na wanasiasa na wataalamu wa masuala ya nishati, unaonyesha kwamba, makundi yaliyoibuka wakati wa sakata la Richmond Februari mwaka jana, ndiyo ambayo ama yatafanikisha au kukwamisha mpango huo wa TANESCO kununua mitambo hiyo.

Habari za uhakika zinaonyesha kwamba, baadhi ya wabunge wengi wanaopinga mpango huo wa TANESCO ni wale ambao wameendelea kuwa na mawazo kwamba, kukubali hoja ya kununua mitambo hiyo, itakuwa ni kumnufaisha hasimu wao mkubwa wa kisiasa, Rostam Aziz ambaye wanaamini kwa njia moja au nyingine ana uhusiano na kampuni ya Dowans.

Kwa mujibu wa habari hizo, wabunge hao wameendelea kushikilia msimamo wao huo, pamoja na Rostam mwenyewe mara kadhaa kukanusha hadharani na katika vikao vya ndani anavyofanya na watu walio karibu naye kuwa hamiliki mitambo hiyo ambayo ililetwa nchini baada ya Kampuni ya Richmond kushindwa kutimiza malengo ya mkataba wake.

Taarifa nyingine zinaonyesha kwamba, uamuzi uliofikiwa mwaka jana na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini ya Bunge inayoongozwa na Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo (CCM), wa kuikatalia na kuizuia TANESCO kuendelea na mpango wake wa kuinunua mitambo ya Dowans, ulichagizwa kwa kiwango kikubwa na matakwa hayo hayo ya kimakundi ndani ya CCM na kwa kiwango kikubwa ‘Kivuli cha Rostam’, kuliko ukweli wa kimahitaji wa nishati muhimu ya umeme nchini.

Habari zinaeleza kwamba, uamuzi wa serikali na hususan wa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kusalimu amri mbele ya kamati hiyo ya Bunge Desemba mwaka jana, haikutokana na kutambua kwake nguvu ya hoja waliyokuwa nayo wabunge, bali ilisababishwa na kuhofia kwake kufikwa na dhoruba ya kisiasa ambayo ingeweza kumlazimisha kujiuzulu uwaziri akiingizwa katika kashfa ya Richmond.

Vyanzo vya kuaminika vya habari kutoka ndani ya Bunge na TANESCO vimeieleza Tanzania Daima Jumapili kwamba, uamuzi wa wiki hii wa shirika hilo, kuamua kulifikisha upya suala lao katika Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma inayoongozwa na Mbunge kijana na machachari wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), umejengwa katika misingi ya kuwa na imani na kamati hiyo ambayo wajumbe wake wengi hawatokani kwa namna moja au nyingine na mzozo wa Februari mwaka jana wa Richmond.

Katika kuthibitisha ukweli wa uchunguzi huo wa Tanzania Daima Jumapili, taarifa za uhakika kutoka ndani ya kikao kati ya kamati hiyo na TANESCO kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam zinaeleza kwamba, kilimalizika kwa wabunge takriban wote kuunga mkono ajenda ya kununua mtambo wa Dowans, tofauti na ilivyofanyika Desemba mwaka jana wakati wa kikao cha Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.

Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili katika viwanja vya Ofisi Ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam, muda mfupi kabla hajaingia katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dk. Idris Rashidi, alisema wakati umefika kwa Watanzania kuweka pembeni matakwa ya kisiasa katika mambo yanayoweza kugusa moja kwa moja mustakabali wa kiuchumi wa taifa.

“Ifikie wakati tuache kuingiza siasa katika masuala ya kitaalamu, kwani hazitatufikisha popote. Kama watu wana matatizo na watu fulani, basi wasiyaingize katika mitambo. Nchi hii inaelekea kubaya,” alionya Dk. Rashidi, mmoja wa wachumi wanaoheshimika nchini.

Akiendelea, alisema kuna uwezekano mkubwa kwa taifa kuingia katika mgawo wenye madhara makubwa iwapo serikali na Bunge vitaendelea kushikilia msimamo wa kutonunua mitambo ya Dowans au mingine kutoka nje ya nchi haraka.

Alisema ni vyema penye ukweli watu wauseme ili taifa liweze kuendelea kuliko kuendelea kushikilia msimamo ambao kwa siku za usoni zinazoweza kuwa na ukame, kutakuwa na madhara makubwa.

Mchumi huyo alisema tatizo la kukwama kununuliwa kwa mitambo ya Dowans limekuwa ni watu fulani kuhusishwa kuwa ni wamiliki wake na wala si mitambo yenyewe, hivyo ni vema viongozi wakatenganisha mambo hayo ili kulinusuru taifa na kuanguka kiuchumi kunakolinyemelea.

Alisema mahitaji ya nchi kwa sasa ni makubwa kuliko uwezo wa kuzalisha umeme, ambapo kwa siku zinahitajika megawati 700 huku uwezo wa TANESCO kuzalisha umeme ukiwa hauzidi megawati 600, hivyo ni dhahiri wanahitaji mitambo ya ziada kuzalisha umeme.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili, ilizipata baadaye kutoka ndani ya kikao hicho cha Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma zilieleza wajumbe wake walikubaliana kwa kauli moja kuwasiliana na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ili awaruhusu kukutana na wajumbe wenzao wa Kamati ya Nishati na Madini, TANESCO na Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA) ili kuangalia kwa kina suala hili la kununua mitambo ya Dowans.

Kwa mujibu wa habari hizo, kamati hiyo ilifikia uamuzi huo baada ya kubaini kwamba, katika maazimio 21 ya Bunge ya Februari mwaka jana, hakukuwa na azimio ambalo liliizuia TANESCO au serikali kununua mitambo ya Dowans ambayo mkataba wake wa kuiuzia TANESCO umeme ulivunjwa Agosti mwaka jana.

Tanzania Daima Jumapili, ilipowasiliana na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Kabwe, alilielezea suala hilo zima kuwa ni jaribio la kiuongozi, ambalo kamati yake imekutana nalo na bila ya kufafanua akasema, kuna kipindi ambacho kiongozi hulazimika kachukua maamuzi yanayoudhi watu ili kuokoa taifa.

“Ni kweli tumeomba Spika Sitta kukutana na Kamati ya Nishati na Madini kuzungumzia suala hili na nina imani tutakubaliana kwa misingi ya kuliokoa taifa katika hatari ya kuingia katika mgawo wa umeme,” alisema Zitto katika kauli ambayo ilionyesha dhahiri kujitoa mhanga kukabiliana na siasa za kimakundi ndani ya CCM.

Habari zaidi kutoka ndani ya kamati hiyo ambayo Mbunge wa Moshi mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), ni mjumbe wake zinasema, mzee huyo naye alisema gharama za kununua mitambo mipya ni kubwa na itachukua si chini ya miaka miwili kukamilika, hivyo ni vyema chuki za kisiasa zikawekwa kando katika masuala muhimu ya kuinua uchumi wa taifa.

“Hatuna sababu ya kuendekeza chuki za kisiasa katika masuala muhimu kwa maendeleo ya uchumi wa nchi hii, lazima tufike mahali tukubaliane kuwa masilahi ya taifa kwanza na mambo mengine yafuatie,” alikaririwa akisema Ndesamburo ndani ya kikao hicho.
 
Tuachane na .....................Ahh. Huko majuu watu..........Ahh wanaendesha nchi na shughuli zao kwa ufanisi na bila kubaguliwa.

Katika hili, mawazo yake huyo huyo ......Ahh ni ya busara sana kuliko hao straights.

1. Mitambo yote iliyo nchini kwa sasa inafanya kazi. Mitambo hiyo ilinunuliwa ikiwa mipya na imezeekea humu humu nchini ikitumiwa na Tanesco. Kwa hiyo hiyo sheria ya kununu mitambo ya zamani hai apply hapa. Ingekuwa ilikuwa ikitumiwa na mtu mwingine nje ya nchi, hapo ingekuwa issue.

2. Tunajua milolongo iliyopo ya ku order mitambo mipya. Mpaka ifike hapa si chini ya miaka miwili. Kwanza ufanyike upembuzi yakinifu, ziitwe tenda, kamati ya zabuni ikae, majadala wa waziri mhusika kuingilia tenda process ufuate, mwishowe oda ifanywe, kampuni iliyopata tenda ichelewe utekelezaji, etc. By the time mradi unaanza kazi si chin ya miaka miwili. Wakati huo wote Tanesco inalipa capacity charges. Sasa badala ya kutumia hizo pesa za capacity charges kununulia mitambo zinakuwa zinapotea bure. Kama si ujuha ni nini?

3. Jamaa wakikatalia mitambo yao, nyie hao hao ndio mtakao anza kulalamikia mgao.

4. Tuache siasa jamani. Tuwaachie wataalam akina Dr. Rashid, wafanye kazi yao.

Kwanza naomba ukanushe kauli yako kuwa tuwaachie wataalam akina Dr. Rashid. Sijaona mtaalam asiye kuwa na dira wala Plan B. Kinachoonekana hapa Management ya Tanesco na supporters wake washakubaliana kununua hiyo mitambo hivyo hawahitaji kuwa na mipango mingine ambayo ni endelevu kwa taifa juu ya upatikanaji wa umeme. Mbaya zaidi hapa jamvini kuna taaluma kulikounavyotegemea wewe hivyo watu wanaongea wakiwa informed sio kwa sababu ya kisiasa inayo potosha mambo.

Tatizo la umeme Tanzania halija anza jana wala juzi. Huyo mtaalamu wako Rashid sijaona mpango wake wa maana kuhakikisha umeme unapatikana nchi nzima. Namaanisha hana plani hata ya muda mrefu at hand. Bali analazimisha tununue mitambo chakavu unayoitetea kuwa ni mipya na imechaka ikiwa nchini. Mkuu hata ukitetea mwathilika namba moja ni sisi wenyewe.
 
Baadhi ya wabunge wa kamati hiyo iliyokuwa chini ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe waliwabana maafisa wa Tanesco waliokuwa wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Dk Idrisa Rashid ili waeleze sababu iliyowafanya waamue kununua mitambo chakavu ya Dowans badala ya mipya.

Wabunge hao walionyesha wasiwasi wao kufuatia nia ya Tanesco kutaka kununua mitambo hiyo huku wakijua kuwa sheria ya manunuzi inazuia ununuzi wa mitambo chakavu.

Mbunge wa Bukombe, Emmanuel Luhahula, alihoji iwapo Tanesco na serikali hawana wazo mbadala zaidi ya kununua mitambo ya Dowans.

Zitto alimtaka Mkurugenzi wa Tanesco aieleze kamati mitambo ile inayotaka kununuliwa na shirika hilo ina ubora wa kiasi gani.

Akijibu baadhi ya hoja za wabunge, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk Idriss Rashid kwa kushirikiana na timu ya wataalam wake, alisema mtambo mmoja ni mpya na mingine imetumika kwa takribani saa 800 kila mmoja.

Alisema mitambo hiyo inao uwezo wa kufanya kazi kwa miaka 10 bila kufanyiwa ukarabati na kwamba ikifanyiwa ukarabati inaweza kufanya kazi kwa miaka mingine 10 na kufikisha miaka 20.

Dk Rashid aliongeza kuwa shirika lake lilipata mkaguzi kutoka Ujerumani ambaye aliikagua mitambo na kutoa taarifa kuwa mitambo hiyo ni mizima na inao uwezo wa kuzalisha umeme.

Alisema jambo kubwa linaloisukuma Tanesco kushinikiza ununuzi wa mitambo hiyo ni hali ya ukame inayotarajia kuikumba nchi katika kipindi cha miezi kadhaa ijayo.

Zitto alipomtaka Mkurugenzi huyo aeleze mbadala endapo bunge halitaridhia ununuzi wa mitambo hiyo, Dk Rashid alisema hakuna chaguo jingine ni ama kununua mitambo hiyo au nchi kuingia katika giza.

"Nafikiri suala hili ni la kitaifa, tunapaswa kuliangalia kwa uzito wake, au tuendelee hivi tulivyo na kuwa na shortage (upungufu) ya umeme au kununua mitambo iwe ya Dowans au mingine yoyote, lakini tukumbuke kuwa tukiamua kukodi itabidi kuendelea kulipia capacity charges (gharama ya mitambo)," alieleza Dk Rashid.

Kwanza, huyu Idris Rashidi ni fisadi, ushahidi wa wazi upo kule kwenye dili la Rada. Sasa mtu huyu atadai vipi anafanya kazi kwa ajili ya kuliokoa Taifa?

Pili, hawa Dowans wananuka Rushwa, kupitia Richmond. Hizo Capacity Charges zinatokea wapi iwapo kulikuwa na ukiukwaji wa sheria.

Tatu, hivi visingio vyakusema eti mitambo haiwezi kupatikana haraka ni mkusanyiko wa uongo, uvivu wa kufikiri na kiburi. Kiburi hiki anakipata wapi?

Waache kutufanya wa-Tanzania mabwege.
 
........Ndiyo maana BRAZAMENI kajichukulia GANDA/MKOBA.........wake.....aaghh
 
Dowans = Kikwete + lowassa + Rostam... ndio maana nguvu yake kubwa kushinda chochote Tanzania

Dowans is Rostum Aziz and Rostum Aziz is Dowans. Doesn't make sense? At the end of the day mitambo itanunuliwa, Rostam ataweka hela yake mfukoni, mambo kwisha.

To kill a snake you strike its head and since we are far from doing that, the snake is coiled safe with its ugly head tucked in comfort in the realms of our sacred house.
 
CCM sasa tishio
• Sasa yatishia kulisambaratisha taifa
na Mwandishi Wetu


Dk. Idris Rashidi, alisema wakati umefika kwa Watanzania kuweka pembeni matakwa ya kisiasa katika mambo yanayoweza kugusa moja kwa moja mustakabali wa kiuchumi wa taifa.

“Ifikie wakati tuache kuingiza siasa katika masuala ya kitaalamu, kwani hazitatufikisha popote. Kama watu wana matatizo na watu fulani, basi wasiyaingize katika mitambo. Nchi hii inaelekea kubaya,” alionya Dk. Rashidi, mmoja wa wachumi wanaoheshimika nchini.

Dk Idrisa anang`ang`aniza Kununua mitambo iliyotumika kinyume na sheria ya manunuzi ambayo hairuhusu kununua mitumba.Bunge lenyewe limeshupalia kutetea kuwa isinunuliwe maana ni kupingana na sheria.Hapo mtaalamu ni yupi bunge au Dk.IDRISA? Kwangu mimi bunge ndio wataalamu maana wanazingatia Sheria ya manunuzi lakini Idrisa ndiye mwanasiasa katika suala hili la Mitambo ya Dowans kwani anataka sheria ivunjwe ili inunuliwe.

hAYO MANENO ALIYOWASEMA VIBAYA WANASIASA AWAOMBE RADHI YEYE NDIYE ANALETA SIASA KWENYE UNUNUZI WA MITAMBO ILIYOTUMIKA YA DOWANS.Akome na awaombe radhi kwa statement hiyo aliyotoa.

Pia kitendo cha Idrisa Kukosa plan B mbadala badala ya Dowans ni kukiabisha chuo alikopatia hiyo PHD.Na Kwa mamlaka ninayojipa mwenyewe bila ruksa ya jamii forums namtangaza Idrisa kuwa si DOKTA tena kuanzia sasa na hana PHD kuanzia leo. Anayejua chuo alikosoma awapelekee nakala.

Ieleweke kuwa vita na Dowans haina macho hatutajali ni Lowasa,Idrisa,Rostam,Kikwete,Slaa au zitto kabwe,GAZETI LA MTANZANIA n.k kama wakiunga mkono wakakiuka sheria ya manunuzi tutapambana bila kulala kupinga.Kama ni kukaa gizani tukisubiri mitambo mipya wacha tukae.Kuna eneo tumekaa gizani miaka 47 toka uhuru upatikane hakuna umeme tunaendelea kusubiri sembuse kusubiri mwaka mmoja au miwili mitambo mipya.Tuko tayari kusubiri lakini mitambo mitumba ya Dowans Noooooooooo!

Hata aje mtaalamu toka wapi wa kuthibitisha mitumba ya DOWANS ni safi ni safi tunasema noooooooo! Hatutaki mitumba ya Dowans.
 
Kwanza, huyu Idris Rashidi ni fisadi, ushahidi wa wazi upo kule kwenye dili la Rada. Sasa mtu huyu atadai vipi anafanya kazi kwa ajili ya kuliokoa Taifa?

Pili, hawa Dowans wananuka Rushwa, kupitia Richmond. Hizo Capacity Charges zinatokea wapi iwapo kulikuwa na ukiukwaji wa sheria.

Tatu, hivi visingio vyakusema eti mitambo haiwezi kupatikana haraka ni mkusanyiko wa uongo, uvivu wa kufikiri na kiburi. Kiburi hiki anakipata wapi?

Waache kutufanya wa-Tanzania mabwege.

Kinacho zidi nishangaza idris ndo mkuu, Haja shuka toka sayari ya Jupiter leo.., yupo sayari hihi ya dunia, tena ndani ya TANESCo hii hii, yupo siku zote akiona hali ya TANESCO kwanini emergency? Anaweza kutueleza sababu zilizo mfanya asichukue tahadhari hadi asubiri muda wote huo dakika za majeruhi na kutuijia na hadithi za kununua mitambo iliyo choka toka kwa taperi wetu? Yaani mtu alitutaperi halafu tunaishia kununua makabrasha aliyo tumia
kututaperia? Hainiingii akilini hata!

Ikumbukwe kwamba ni kisingizio cha emergency, na hadithi za kulinusuru taifa kilicho tuingiza kwenye mkenge huu huu, haitashangaza kwamba hiyo mitambo tunayo taka nunua baada ya myezi sita itakuwa juu ya mawe!

Please stop wizi huu immediately!
 
Wakati Richmond ikiletwa tuliambiwa kwamba hilo lilikuwa ni suluhisho la muda mfupi wakati serikali ikiangalia namna ya kupata ufumbuzi wa muda mrefu. Je, TANESCO na serikali walifanya nini kwa kipindi cha miaka 3 ili kuwa na ufumbuzi wa muda mrefu?

Hivi kuna sababu gani ya kununua mitambo ambayo ilishatumika? Kusema kwamba imetumika kwa masaa 800, hatuna uhakika kama kweli imetumika kwa masaa hayo tu. Kwanini serikali isitangaze tenda ya kununua mitambo mipya? Dr. Rashid anaposema kwamba mchakato wa kununua mitambo mipya kwamba itachukua muda mrefu, tunarudi kule kule kwenye mkenge wa Richmond, kwamba mambo yalifanyika kwa dharura na hivyo hakukuwa na umakini wa kutosha, je bado tunarudia kutumia same excuses kwamba hali ni mbaya sana na hatuwezi kusubiri?

Ni vyema TANESCO na serikali wakaanza mchakato wa kununua mitambo mipya, maana naona yanatengenezwa mazingira ya kutuingiza kwenye mkenge mwingine.

Ni kweli kuwa wala uhakika kuwa Richmond/Dowans walinunua mitambo mipya haupo vile vile, ni mipango ile ile ya kutuingiza mjini. Kama watu tunaowaita watalaam wetu wana uwezo wa kuchezea vipimo vinavyohusu maisha ya watu (suala ya vipimo vya ukimwi na wizara ya afya), hili la kutuzuga kwenye mitambo ya umeme mbona ni dogo. Hawa watu tunaowaita wataalam wengi ni baada ya matumbo yao na kufanikisha tamaa za mabosi wao tu.
 
Please Dr. Idriss tell us how a middle man (DOWANS) can sell to us 'NEW' Generators for 30% less ($60million) than the manufacturer ($90million)?

What is the explanation for these huge discrepancies?


Why should we believe a person linked to RADAR-Gate, that $90million is the Real Price for the Generators?
 
Huyu Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO Idrisa Rashid tayari ana tuhuma nzito za kukutwa $600,000 zilizowekwa na Mzee wa Vijisenti Chenge kwenye bank account yake ya nje. Alitakiwa awe ameshafukuzwa kazi siku nyingi huku uchunguzi dhidi yake ukiendelea lakini bado anapeta tu na kutaka kuingiza serikali kwenye mkenge mwingine.

Nguvu za Dowans zaibuka upya

2009-02-23 10:01:37
Na Muhibu Said

Kuna kila dalili kwamba nguvu za kampuni ya Dowans iliyorithi mkataba wa Richmond bado zinasumbua na sasa kamati mbili za Bunge ya Nishati na Madini na ile ya Hesabu za Mashirika ya Umma zinagongana kutokana suala la mitambo ya kampuni hiyo.

Kutokana na uzuri, uimara au upya wa mitambo hiyo, Shirika la Umeme nchini (Tanesco) bado inaililia na inataka kuinunua licha ya maamuzi ya kuachana nayo kutolewa na serikali zaidi ya miezi mitatu sasa.

Hali hii imejitokeza siku mbili tu baada yaTanesco kuibua tena nia yake ya kutaka kuinunua mitambo hiyo yenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 mbele ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma.

Wakati Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma ikitaka mwafaka utafutwe kwa kukutanisha wadau wote kwenye suala la ama kununua au la, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, imesisitiza msimamo wake wa kupinga ununuzi huo kwa kuwa ni kinyume cha taratibu.

Akizungumza na Nipashe jana, Mwenyekiti wa Kamati Nishati na Madini, William Shellukindo, ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), alisema mwenye maamuzi ya kununua mitambo hiyo ni serikali kama imeona kuna dharura ya kufanya hivyo.

Hata hivyo, alisema taratibu zilizopo zinataka suala hilo lifikishwe kwanza bungeni ili likajadiliwe na kupata baraka za Bunge.

``Kuna taratibu za kufuata. Anayetakiwa kununua ni serikali kama imeona kuna dharura. Lakini ilete kwanza hoja hiyo bungeni ili ijadiliwe na Bunge,`` alisema Shellukindo.

Alisema ipo pia sheria ya manunuzi inayozuia kununua mitambo chakavu kwa vile hatua hiyo ni ya hatari.


Kutokana na hali hiyo, alisema haoni kuwa ni busara kung'ang'ania kutaka kununua mitambo ya Dowans kabla taratibu zinazohusika hazijafuatwa na kwa kuzingatia pia kwamba, mitambo ya kampuni hiyo haijulikani ilitumika kwa muda gani.

``Tanesco wanadai kuwa Dowans wanalo jenereta jipya. Lakini mitambo yao iliingizwa nchini mwaka 2006 na utekelezaji ulianza Desemba 2007. Sasa hilo jenereta linaweza kuwa jipya? Na hata yale (majenereta) mengine hatujui kama ni mapya,`` alisema.

Alisema inashangaza kuona Tanesco iking`ang`ania kutaka kununua, huku mkononi mwake ikiwa na amri ya mahakama iliyoomba kuzuia kuuzwa kwa mitambo ya Dowans kwa vile inaidai kampuni hiyo.

``Hatuna uhakika Tanesco wanaidai nini Dowans, hilo haliko wazi, tunataka tujue kwanza hilo. Hata hivyo, kama hilo lipo basi si wangekubaliana wabadilishane badala ya kununua,`` alisema Shellukindo.


Kauli hiyo ya Shellukindo imetolewa siku moja baada ya vyombo vya habari jana kuripoti kwamba juzi Tanesco ilifikisha upya dhamira yao katika Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema).

Tanesco iliifikisha dhamira yake hiyo kwenye kamati hiyo miezi miwili baada ya Kamati ya Nishati na Madini inayoongozwa na Shellukindo, kupinga suala hilo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Desemba mwaka jana.

Akizungumza na Nipashe jana, Zitto alisema katika kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam Jumamosi iliyopita, Tanesco walitoa hoja za msingi kuhusu dhamira yake ya kutaka kununua mitambo ya Dowans.

Hata hivyo, alisema waliafikiana wamuombe Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kuruhusu kuitisha kikao cha kamati zote mbili (ya Hesabu za Mashirika ya Umma na Nishati na Madini), serikali, Tanesco na Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA) ili wajadili na kufikia mwafaka wa pamoja kuhusu suala la kununua mitambo hiyo ili kuepuka kamati kupingana.

Zitto alisema sababu nyingine ya kamati yake kuomba kibali hicho kwa Spika ni kwa vile Kamati ya Nishati na Madini, haikutoa nafasi ya kukutana na Tanesco ili waeleze kwanini wanataka kununua mitambo hiyo.

``Walikutana tu na Waziri Ngeleja wakapinga Tanesco kununua mtambo huo wa Dowans,`` alisema Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Alisema pia, watatumia fursa ya ruhusu hiyo Spika kujadili kuhusu hatma ya umeme wenye megawati 300 wa Mtwara baada Kampuni ya Barrick kujitoa na hatma ya umeme wa upepo wa Singida.

Alisema kamati yake ilikutana na Tanesco juzi kwa lengo la kukagua hesabu za shirika hilo baada ya kuonekana wanatumia gharama kubwa kulipia umeme na hoja ya kutaka kununua mtambo wa Dowans iliibuka katika kikao hicho.

Hata hivyo, Zitto alisisitiza kwa kusema kuwa: ``Kazi ya Kamati ya Bunge ni ku-oversight (kusimamia) na siyo utendaji wa serikali wa kila siku, kwamba serikali inunue au isinunue.``

Dowans ni mrithi wa kampuni ya Richmond Development Corporation, Kampuni iliyopewa mkataba na serikali wa kuzalisha umeme wa dharura wa megawati 100, lakini ilishindwa na baadaye iligundulika ilikuwa kampuni feki.

Sakata la mkataba wa Richmond ndio ulisababisha kujiuzuku kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, mawaziri Dk Ibrahim Msabaha na Naziri Karamagi. Kutokana na kujiuzulu kwa Lowassa, Baraza lote la Mawaziri lilivunjika Februari mwaka jana.

Tangu wakati huo, kutokana na ripoti ya kamati teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa makataba wa Richmond na maazimio ya Bunge, matukio kadhaa yametokea ikiwa ni pamoja na kumfikisha mmiliki wa Richmond mahakamani.

Aidha viongozi wengine wanachunguzwa na vyombo vya dola juu ya ushiriki wao kwenye mkataba huo.

SOURCE: Nipashe
 
Siri ya wizi mkubwa Richmond

  • Watimka na mabilioni ya walipa kodi
  • Walichotewa kabla hata ya kazi
Mwandishi Wetu Januari 28, 2009
Raia Mwema~Sauti ya Watu

WAKATI Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akisubiriwa na wabunge kuwasilisha taarifa ya Serikali kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya Bunge kuhusu kampuni ya Richmond Development, kampuni hiyo iliyorithiwa na kampuni ya Dowans, ilitokomea na zaidi ya Sh. bilioni 23, Raia Mwema imebaini.

Kinyume cha maelezo yaliyowahi kutolewa na baadhi ya viongozi wakuu serikalini katika Bunge, kwamba Richmond haikuwahi kupewa fedha za Serikali, ukweli ni kwamba kampuni hiyo ilichotewa zaidi ya Sh. bilioni 30 (Dola 30,696,598 za Marekani).


Kiasi hicho ni sawa na asilimia 35 ya gharama ya kodi ambayo msingi wake ulikuwa kufanikisha mchakato wa ufunguaji wa hati ya muamana (letter of credit) kati ya kampuni hiyo na Benki ya Biashara.

Malipo hayo ya asilimia 35 ni utekelezaji wa makubalino yaliyofikiwa awali, kati ya Serikali na wawakilishi wa kampuni ya Richmond Development.

Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwa baada ya kupewa kitita hicho cha zaidi ya Sh bilioni 30, Richmond ilipewa masharti ya kurejesha fedha hizo serikalini katika malipo ambayo yangefanyika kwa awamu tatu.

Hesabu zilizofanywa ni kwamba Richmond ilitakiwa kurejesha serikalini dola 1,279,044 za Marekani (zaidi ya Sh bilioni 1.3), kila mwezi, lakini katika mikupuo (awamu) mitatu
.

Hesabu hizo zinabainisha kuwa kama makubaliano hayo yangefanyika bila ukorofi au kasoro yoyote, Richmond ingefanikiwa kurejesha serikalini fedha ilizopewa katika miaka miwili. Kwa tafsiri nyingine ni kwamba, Richmond ingelipa deni hilo serikalini ndani ya muda wa uhai wa mkataba wake na Serikali, ambao ni miaka miwili.

Lakini uchunguzi zaidi wa Raia Mwema umebaini kuwa malipo ya awali yalipaswa kuanza kufanyika Novemba, mwaka 2007. Hata hivyo, kutokana na utata wa kampuni ya Richmond hasa kwa upande wa uwezo wake kiteknolojia na utendaji, kampuni hiyo iliuza shughuli zake kwa kampuni nyingine binafsi ya Dowans.

Imebainika kuwa wakati mchakato wa uuzaji wa shughuli za kampuni hiyo kwa Dowans unafanyika, Richmond ilikuwa haijarejesha fedha ilizopewa na Serikali na kwa kuwa Dowans ndiyo iliyobeba mikoba, ilipaswa kuendeleza urejeshaji huo wa fedha.

Kutokana na hali hiyo ya fedha za Serikali kubaki kwa 'wawekezaji' hao waliopasiana mpira wa uwajibikaji, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kupitia timu ya watalaamu wa sheria, ilichunguza mkataba kati yake na Richmond ambao ulirithiwa na Dowans.

Taarifa ya timu ya wanasheria wa TANESCO ilibaini kuwa mkataba huo hauna nguvu za kisheria na kuamuru uvunjwe. Mkataba ukavunjwa rasmi Agosti mosi, mwaka 2008.

Hata hivyo, wakati mkataba huo unavunjwa uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwa fedha zilizopaswa kurejeshwa Serikali hazikuwa zimerejeshwa zote.

Imebainika kuwa fedha zilizorejeshwa hadi mkataba unavunjwa ni jumla ya dola 7,674,186 za Marekani (zaidi ya Sh bilioni 7.7), huku dola za Marekani 23,022,412 (zaidi ya Sh. bilioni 23) zikibakia kwa Richmond na mrithi wake Dowans.


Taarifa zaidi za kiuchunguzi zinaeleza kuwa kutokana na hali hiyo Bodi ya TANESCO pamoja na uongozi wa shirika hilo umekwisha kuchukua hatua.

Hizo ni pamoja na maagizo ya Bodi ya TANESCO kwa uongozi wa shirika hilo kuchukua hatua zinazostahili kuhusu deni hilo na kutokana na maagizo hayo, uongozi wa TANESCO ulilazimika kutoa taarifa rasmi serikalini ili hatimaye ijulikane namna fedha hizo zitakavyorejeshwa.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwa ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imechunguza mchakato huo na kubaini kuwa Serikali ilitoa fedha hizo kwa Richmond.

Ofisi hiyo ya CAG, katika taarifa yake ya ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka ulioishia Desemba 31, mwaka 2007, imeweka bayana kuwa fedha hizo bado hazijarejeshwa serikalini.

"Tunafahamu kutokana na taarifa za uongozi kwamba mkataba kati ya TANESCO na Dowans ulivunjwa Agosti mosi, 2008. Matokeo yake ni kwamba kiasi cha fedha kilichotolewa na kutakiwa kurejeshwa kinaweza kuwa hasara kwa TANESCO au Serikali," inaeleza sehemu ya waraka rasmi wa ofisi ya CAG kwa serikali ambao Raia Mwema imeuona.

Kampuni ya Richmond Development ilipewa zabuni tata na Serikali kuagiza mitambo ili kuzalisha umeme wa dharura nchini.


Kutokana na utata wa zabuni hiyo, Bunge lililazimika kuunda Kamati Teule kuchunguza na kubaini upungufu ambao hatimaye ulimgharimu aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na mawaziri Nazir Karamagi na Dk. Ibharim Msabaha waliojiuzulu Februari 2008.

Mbali na viongozi hao kujiuzulu, Kamati ya Bunge iliwasilisha mapendekezo 23 yanayohitaji kufanyiwa kazi na Serikali. Mapendekezo hayo ni pamoja na kuwawajibisha baadhi ya watendaji wa Serikali na baadhi ya vyombo nyeti, akiwamo Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika.

Katika mkutano wa Bunge ulioanza wiki hii, Serikali inatarajiwa kuwasilisha taarifa yake kuhusu utekelezaji wa mapendekezo hayo. Taarifa hiyo inatarajiwa kuwasilishwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.


 

Imebainika kuwa fedha zilizorejeshwa hadi mkataba unavunjwa ni jumla ya dola 7,674,186 za Marekani (zaidi ya Sh bilioni 7.7), huku dola za Marekani 23,022,412 (zaidi ya Sh. bilioni 23) zikibakia kwa Richmond na mrithi wake Dowans.

Kama bado wana pesa yetu, ni kwanini hadi hivi sasa hatujaichukua hiyo mitambo yao na kuinadi tuone kama inaweza kutoa angalau hata nusu ya deni letu?
 
Kama bado wana pesa yetu, ni kwanini hadi hivi sasa hatujaichukua hiyo mitambo yao na kuinadi tuone kama inaweza kutoa angalau hata nusu ya deni letu?

Unachosema ni sawa kabisa. Kama Richmond/Dowans walitakiwa warudishe shilingi 23 billioni na wameshindwa kufanya hivyo basi mitambo yao ilitakiwa ikimatwe na kupigwa mnada ili kurudisha pesa hiyo, lakini hakuna anayejali huko serikalini wala TANESCO kufuatilia hiyo 23 billioni bali wanataka mshiko wao haraka sana na ndiyo maana wameshupalia kuinunua mitambo hiyo michakavu kwa 60 billioni.
 
Unachosema ni sawa kabisa. Kama Richmond/Dowans walitakiwa warudishe shilingi 23 billioni na wameshindwa kufanya hivyo basi mitambo yao ilitakiwa ikimatwe na kupigwa mnada ili kurudisha pesa hiyo, lakini hakuna anayejali huko serikalini wala TANESCO kufuatilia hiyo 23 billioni bali wanataka mshiko wao haraka sana na ndiyo maana wameshupalia kuinunua mitambo hiyo michakavu kwa 60 billioni.


....Let Me Get This Straight.
Hawa Wakalamba wa Dowans Bado tunawadai Bilioni 23 ambazo tungeweza kuichukua mitambo tunayotaka kuuziwa bure na ikaanza kufanya kazi kama fidia ya hela tunayowadai. Badala yake tunataka kuingizwa mkenge wa kuuziwa mitambo hiyo hiyo kwa shilingi Bilioni 60, mitambo ambayo kama tungekuwa na biongozi wazalendo ingekuwa ni yetu!! How mazumbukuku can we get????
 
Who is the power behind Dowans calling shots in govt?

CHARLES RUMISHA
THIS DAY
Dar es Salaam


TANZANIANS sighed with relief when Energy and Minerals Minister William Ngeleja announced that the government has directed TANESCO to ditch the talks with the infamous Dowans Holding over the procurement of its derelict power generating plant.

The past few weeks have been a testing moment, or simply put, a test of wits between the government and the parliamentary select committee on energy and minerals over the buying of the Dowans generator.

In the view of the select committee, the plant could not be purchased because it was second-hand, and therefore contradicting the Public Procurement Act.

Also, the committee stood put on its rejection because the parliament had censored the entire Richmond-Dowans-government deal and demanded the perpetrators to be fired and taken before a court of law.

As good citizens of this land, we were all in shock and had a lot of unanswered questions hovering over our sober minds.

How could the government pay 70bn/- to Dowans for its used power plant? Had Dowans, whose proprietors the government said had not been identified now emerged from Mars, earned credence and are seriously negotiating with the very government it had swindled and embarrassed?

To many Tanzanians there was no way Dowans Holding could be separated from Richmond. There are many unanswered questions on their association.

Taxpayers were still bitter on the 153m/- daily capacity charges that Dowans collected. We are not sure if the tax-man remembered to collect the revenues from the disbursement! But, most importantly, it has never been clarified on who paid the letter of credit that was guaranteed to Richmond by the government


It is undeniable that Dowans, which inherited the power generating assignment from the briefcase company, accomplished the task in default; thus perfecting a typical hoodwinking that in all essence was illegal and undesirable.

Richmond and Dowans, the former a brief-case company, and the latter a registered firm that inherited an illegal contract from Richmond in bizarre circumstances, raised eyebrows to the extent that the parliament formed a probe team to straighten out the entire tangle.

After the parliamentary probe team, led by Harrison Mwakyembe (Kyela MP), tabled its findings, the House affirmed inter alia that the deal was dirty, the government had been conned by the brief case company and that the entire deal was floppy and corrupt.

Parliament passed 23 resolutions on Richmond, demanding the government to take stern action including abrogating the contract with Richmond-Dowans and putting to task all those who collaborated in the scam.

The Prime Minister of the time, Edward Lowassa and two ministers resigned and a few months later the government cancelled the controversial Richmond-Dowans contract.

After the dust that the scam had raised settled, Tanzanians felt relieved and the parliament regained its position in society. The JK government received new baptism and people kept waiting for the culprits to be either sacked or taken to court.

As if opening up an old wound, reports emerged that TANESCO was negotiating with a censored company to purchase the Dowans plant.

The news was like a bolt from the blue because the House was waiting to know what the government had done on its recommendations.

We began wondering if the minerals and energy ministry had suffered a curse, or was it led by big headed people who no longer respected the rule of law and the wish of the people.

Indications were that the lackluster and laissez faire tradition in the ministry had recaptured its seat.

Thank God sanity has reigned and the whole shabby deal dropped. Albeit we want to insist that it is time the government skirted around silly and embarrassing actions.

The TANESCO Board of Directors, the government negotiation team and the ministry lawyer cannot be absolved of the heinous crime of treachery.

We assert that it was shameful for the ministry to open new avenues with a firm that had been censored by parliament and declared illegal.

We want to state categorically that the Public Procurement Act prevents government from buying second-hand items. Who are those powers behind government forcing public institutions to break the law?

But, most importantly, since TANESCO and the government negotiation team have talked face to face with representatives of Dowans over the purchase of the latter’s plant, it’s the right time Tanzanians were told the powers behind Dowans.

Tanzanians want to know the power behind Dowans that calls shots in government; earns favours and cash, tramples the law and just walk off scot-free.

We want to emphasize that public servants have obligations to the public and not to any other forces. It is indeed a bizarre situation to see the ministry of energy collaborating with Dowans, a firm that has much to account to the taxpayers for the millions it has pocketed before the abrogation of the contract.

While many Tanzanians are anxiously waiting for the suspects of the Richmond scam to get a sack while others are sent to court, we believe it was inappropriate, totally shameful and illegal for a public institution like TANESCO to sit face to face with Dowans holding to negotiate over the purchase of its used plant.

Where has the civil service lost its morals and respectability Can’t people draw a lesson from the stunning events witnessed in the last four weeks at Kisutu Resident Magistrate’s Court?


NEW UNIT OF 100 MW SIMPLE CYCLE=$25-30 MILLION

Please call this company and ask for the quotation you will suprise yourself: The have in stock, 20MW 50MW 100MW NEW UNIT: BAADA YA FINANCIAL CRISIS KAMPUNI NYINGI ZIMECANCEL ORDER, HIVYO WANASTOCK KUBWA YA HII MITAMBO NA NI MIPYA KABISA BEI NDO HIYO $25-30MILLION FOR 100MW

PRICE RANGE FROM $250,000. -$300,000.00 PER MW FOR 100MW=$25-30 MILLION

GE Energy
GE Energy - Contact Us
 
Who is the power behind Dowans calling shots in govt?

CHARLES RUMISHA
THIS DAY
Dar es Salaam


TANZANIANS sighed with relief when Energy and Minerals Minister William Ngeleja announced that the government has directed TANESCO to ditch the talks with the infamous Dowans Holding over the procurement of its derelict power generating plant.

The past few weeks have been a testing moment, or simply put, a test of wits between the government and the parliamentary select committee on energy and minerals over the buying of the Dowans generator.

In the view of the select committee, the plant could not be purchased because it was second-hand, and therefore contradicting the Public Procurement Act.

Also, the committee stood put on its rejection because the parliament had censored the entire Richmond-Dowans-government deal and demanded the perpetrators to be fired and taken before a court of law.

As good citizens of this land, we were all in shock and had a lot of unanswered questions hovering over our sober minds.

How could the government pay 70bn/- to Dowans for its used power plant? Had Dowans, whose proprietors the government said had not been identified now emerged from Mars, earned credence and are seriously negotiating with the very government it had swindled and embarrassed?

To many Tanzanians there was no way Dowans Holding could be separated from Richmond. There are many unanswered questions on their association.

Taxpayers were still bitter on the 153m/- daily capacity charges that Dowans collected. We are not sure if the tax-man remembered to collect the revenues from the disbursement! But, most importantly, it has never been clarified on who paid the letter of credit that was guaranteed to Richmond by the government


It is undeniable that Dowans, which inherited the power generating assignment from the briefcase company, accomplished the task in default; thus perfecting a typical hoodwinking that in all essence was illegal and undesirable.

Richmond and Dowans, the former a brief-case company, and the latter a registered firm that inherited an illegal contract from Richmond in bizarre circumstances, raised eyebrows to the extent that the parliament formed a probe team to straighten out the entire tangle.

After the parliamentary probe team, led by Harrison Mwakyembe (Kyela MP), tabled its findings, the House affirmed inter alia that the deal was dirty, the government had been conned by the brief case company and that the entire deal was floppy and corrupt.

Parliament passed 23 resolutions on Richmond, demanding the government to take stern action including abrogating the contract with Richmond-Dowans and putting to task all those who collaborated in the scam.

The Prime Minister of the time, Edward Lowassa and two ministers resigned and a few months later the government cancelled the controversial Richmond-Dowans contract.

After the dust that the scam had raised settled, Tanzanians felt relieved and the parliament regained its position in society. The JK government received new baptism and people kept waiting for the culprits to be either sacked or taken to court.

As if opening up an old wound, reports emerged that TANESCO was negotiating with a censored company to purchase the Dowans plant.

The news was like a bolt from the blue because the House was waiting to know what the government had done on its recommendations.

We began wondering if the minerals and energy ministry had suffered a curse, or was it led by big headed people who no longer respected the rule of law and the wish of the people.

Indications were that the lackluster and laissez faire tradition in the ministry had recaptured its seat.

Thank God sanity has reigned and the whole shabby deal dropped. Albeit we want to insist that it is time the government skirted around silly and embarrassing actions.

The TANESCO Board of Directors, the government negotiation team and the ministry lawyer cannot be absolved of the heinous crime of treachery.

We assert that it was shameful for the ministry to open new avenues with a firm that had been censored by parliament and declared illegal.

We want to state categorically that the Public Procurement Act prevents government from buying second-hand items. Who are those powers behind government forcing public institutions to break the law?

But, most importantly, since TANESCO and the government negotiation team have talked face to face with representatives of Dowans over the purchase of the latter’s plant, it’s the right time Tanzanians were told the powers behind Dowans.

Tanzanians want to know the power behind Dowans that calls shots in government; earns favours and cash, tramples the law and just walk off scot-free.

We want to emphasize that public servants have obligations to the public and not to any other forces. It is indeed a bizarre situation to see the ministry of energy collaborating with Dowans, a firm that has much to account to the taxpayers for the millions it has pocketed before the abrogation of the contract.

While many Tanzanians are anxiously waiting for the suspects of the Richmond scam to get a sack while others are sent to court, we believe it was inappropriate, totally shameful and illegal for a public institution like TANESCO to sit face to face with Dowans holding to negotiate over the purchase of its used plant.

Where has the civil service lost its morals and respectability Can’t people draw a lesson from the stunning events witnessed in the last four weeks at Kisutu Resident Magistrate’s Court?


NEW UNIT OF 100 MW SIMPLE CYCLE=$25-30 MILLION

Please call this company and ask for the quotation you will suprise yourself: The have in stock, 20MW 50MW 100MW NEW UNIT: BAADA YA FINANCIAL CRISIS KAMPUNI NYINGI ZIMECANCEL ORDER, HIVYO WANASTOCK KUBWA YA HII MITAMBO NA NI MIPYA KABISA BEI NDO HIYO $25-30MILLION FOR 100MW

PRICE RANGE FROM $250,000. -$300,000.00 PER MW FOR 100MW=$25-30 MILLION

GE Energy
GE Energy - Contact Us
 
Back
Top Bottom