Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Alah, kumbe TANESCO wana uwezo wa kumiliki na kuendesha mitambo hiyo hiyo ya Dowans/Richmond ambayo walienda kuwa contract Dowans/Richmond ?

Hivi kumbe hizi contract - hata zile zilizokuwa halali - basi mi miradi ya watu!!!

I mean, unaweza kuingia mkataba wa kukodisha gari kulitumia mwaka mzima wakati una hela za kununua likawa lako ?

Somebody ask Ngeleja this question.


Kuhani, hiyo ndiyo Tanzania.

Miradi ya serikali inaagizwa magari mapya yenye thamani ya mamia ya mamilioni ya shilingi. Gari inatumika miaka miwili mitatu then inauzwa milioni tano (5m)..guess nani anayelinunua.

Hiyo yote ni miradi ya watu baba, halafu mwisho wa siku wanaenda kushangilia kuwashinda mafisadi, what the heck!
 
I smell another EPA! Kwani tukismea hatuitaki hiyo mitambo tutapoteza nini?
 
Hapa kinachotakiwa ni serikali kutaifisha hiyo mitambo. Baada tya kuitaifisha na wakaona hawaihitaji waiuze kwa anayeihitaji, sio wao kununua!
 
hahahha hapa kuna kamchezo ka kujificha na kubutua.....kombolelaa..hawatuambiii lolote twajua kamchezo kao....utasikia kuna kampuni moja toka sehemu.....wanaitaka watatangaza bei kubwa...ili Tanesco wapande dau zaidi wakati kutakuwa hakuna kampuni yeyote.....inayoitaka...stay tuned
 
Duh, kaaz kweli kweli hapa mahali..... Mitambo ilikodishwa na TANESCO kutoka Richmond... Richmond imefutwa kisheria miezi kadhaa baada ya kuuzwa/kununuliwa na Dowans... Then miezi michache baadaye Dowans wanaiuza mitambo ile!!!

Duh, hii inaitwa usanii daraja la kwanza sababu:
1. Serikali ilisaidia kupatikana kwa mitambo ile!
2. Mchakato wa kuipata na upatikanaji wake ulileta sokomoko nchi ikatikisika (PM kuresign etc etc etc)
3. Mapendekezo ya Kamati ya Mwakyembe hayajatimizwa

nadhani ni mimi nipo slow lakini hii kitu haileti maana ndani ya hii kichwa ya kiMasai kabisa!!!
 
Mzee wa wizara na yeye anataka apate kidogo kitu, wenzie si walikula bwana....sasa kwa nini yeye atoke patupu.
 
Hapa kinachitakiwa ni serikali kutaifisha hiyo mitambo. Baada tya kuifaifisha na wakaona hawaihitaji iiuze kwa anayeihitaji, sio wao kununua!

Hapo umenena Mama. Tukumbuke kwanza kuwa kwa kushirikiana na MAFISADI wa hapa nchini RICHMOND/DOWANS walisafirisha hii kutoka huko ilikonunuliwa kuja hapa kwa gharama yetu Watanzania. Pili, kwamba fedha za capacity charge wamelipwa kwa miezi mingi kuliko muda waliozalisha umeme. Tatu, wametuingiza hasara ya pili kugharamia tume kufanya kazi ili kugundua ukweli wa utapeli wote.

Sikutegemea Ngeleja aanze kutoa kauri za kuonyesha kuwa na nia ya kununua mitambo hii, ambayo ndani yetu bado hatujakomboa baadhi ya hela zetu. Mitambo hii ni ya kutaifisha, kuwabana DOWANS waseme ni FISADi gani aliwaunganisha na RICHMOND na kuwaleta hapa kwetu.

Kwa tamko hili la Ngeleja mimi nahisi hapa tayari mtu kesha ahidiwa dau na zinaanza jitihada za kuzugazuga ili jambo la ununuzi lianze kuzoeleka masikioni halafu wanunue!!! Tuzidisheni kelele za kuwapinga!!!
 
Tutaona bei ya kununua hiyo mitambo itakavyokuwa mara mbili ya mitambo mipya-

Swali ni kwa nini tununue mitumba tusinunue mipya ambayo ni more efficient?????

Ngeleja huyo huyo si alisema kwamba serikali haijawa na wala haina mipango ya kununua????
 
Duh, kaaz kweli kweli hapa mahali..... Mitambo ilikodishwa na TANESCO kutoka Richmond... Richmond imefutwa kisheria miezi kadhaa baada ya kuuzwa/kununuliwa na Dowans... Then miezi michache baadaye Dowans wanaiuza mitambo ile!!!

Duh, hii inaitwa usanii daraja la kwanza sababu:
1. Serikali ilisaidia kupatikana kwa mitambo ile!
2. Mchakato wa kuipata na upatikanaji wake ulileta sokomoko nchi ikatikisika (PM kuresign etc etc etc)
3. Mapendekezo ya Kamati ya Mwakyembe hayajatimizwa

nadhani ni mimi nipo slow lakini hii kitu haileti maana ndani ya hii kichwa ya kiMasai kabisa!!!


Government of the people by the people for the people hakuna. Hawana zaidi ya kuangalia maslahi yao binafsi. Usishangae kule Brella kuna kampuni inasajiliwa mahsusi kwa ajili ya ununuzi wa mitambo hii.
 
Hapa kinachitakiwa ni serikali kutaifisha hiyo mitambo. Baada tya kuifaifisha na wakaona hawaihitaji iiuze kwa anayeihitaji, sio wao kununua!

Kampuni iliyopata mkataba toka serikalini kwa kudanganya kwamba ni kampuni ya Marekani. Baada ya kupewa mkataba huo wakaonyesha hawana uwezo wowote wa kuzalisha umeme maana nchi iliendelea kugubikwa na giza nene, bahati nzuri Mungu akasikia vilio vya Watanzania na hatimaye mvua zikanyesha na mabwaya ya maji ya Kidatu na Mtera kujaa na hivyo kuweza kuzalisha umeme.

Inashangaza kuona kwamba serikali bado inataka kujihusisha na hii Kampuni ambayo imesababisha Waziri Mkuu na mawaziri wengine wawili Karamagi na Msabaha kupoteza kazi zao. Mitambo kama hiyo inaweza kununuliwa mipya kabisa ili kuachana na hao mafisadi wa Richmond/Dowans lakini inaelekea kuna watu labda wameshahakikishiwa mshiko mkubwa ikiwa serikali itanunua mitambo hiyo ambayo sasa imekaa idle. Ndiyo Tanzania yetu hiyo itajengwa na wenye moyo na kuliwa na mafisadi
 
Mwenyekiti wa kamati ya Bunge inayoshughulikia masuala ya Nishati na Madini Bw. William Shelukindo (CCM) anatarajia kutoa statement inayohusu Richmond na Dowans muda si mrefu.
 
Last edited by a moderator:
Kuna press conference au? Hayo mambo ya kuwaweka wawekezaji kwenye "tension and suspense" kunadhoofisha uwekezaji nchini!

Utafiti unaonyesha kwamba wawekezaji kwenye sekta ya madini hapa Tanzania ume-stagnate kwa karibu miaka miwili kutokana na hiyo kamati ya kuchunguza mikataba ya madini. Maana hawaelewi mwelekeo utaofuata baada ya hapo!

Ukichanganya na financial meltdown ndio kabisa, vijikampuni vidog vidogo vya exploaration vyote vimesimamisha shughuli zao na kupunguza wafanyakazi!
 
Mwenyekiti wa kamati ya Bunge inayoshughulikia masuala ya Nishati na Madini Bw. William Shelukindo (CCM) anatarajia kutoa statement inayohusu Richmond na Dowans muda si mrefu.

heshima mbele mkuu,
kwakuwa kinachotarajiwa kwa mujibu wa maelezo ya ko ni statement, inawezekana pia ikawa sio bomu!!!anaweza akatoa statement ya kuwanusuru wanaccm wenzake au CCM yenyewe.Pamoja na msukumo wa kamati anayoiongoza iliyopelekea kuundwa kwa kamati ya ya bunge iliyoongozwa na Dr.Mwakyembe, bado ukweli ni kuwa shelukindo ni mwangalifu sana.
Lakini pamoja na hayo yote tusubiri tuone........
 
Mzee Shelukindo ndio wale wale mtoto wa nyoka ni nyoka, Miaka yote walikuwepo kwenye bodi hizo kazi kujiweka wao safi tuu. Tunamshukuru mungu mabadiliko yanafika bila wao kutegemea kwani jamii ya mika ya 1975 sio ya hivi leo tunaona Wathailand wanaitoa serikali, Greece wanachachamaa hivyo viongozi wetu ni lazima wawajibike. Kwani kwa maisha ya sasa uongozi ni sawa na kukalia bomu la cluster likilipuka haliishi maisha
 
Wakuu, mmenishtua ikabidi heading iwe na "Question mark" maana wengi wanaonekana kutokuwa na imani na kitakachoongeleka.

Reporter wetu aliyekuwa Kisutu anafanya kufuatilia issues mbili kwa wakati mmoja (Chenge & Shelukindo) nasi tutawafahamisha kinachoendelea pindi tukikipata.
 
Mzee Shelukindo ndio wale wale mtoto wa nyoka ni nyoka, Miaka yote walikuwepo kwenye bodi hizo kazi kujiweka wao safi tuu. Tunamshukuru mungu mabadiliko yanafika bila wao kutegemea kwani jamii ya mika ya 1975 sio ya hivi leo tunaona Wathailand wanaitoa serikali, Greece wanachachamaa hivyo viongozi wetu ni lazima wawajibike. Kwani kwa maisha ya sasa uongozi ni sawa na kukalia bomu la cluster likilipuka haliishi maisha


What do you suggest brother !? I thought we preach chages ,if the guy has repent and start doing good things isn't good though!
 
Kweli Shelukindo ana ability na potentials za kufanya siginificant confrontation...?

Totaly independent and objective?

Asimame mwenye na "mzigo" wake huo kabisa... na ulete maana kiutedendaji na kimatokeo?

In that way Tutaanza kuamka kama waTz... But

Mhh...

Lt's wait and see!!!
 
Kuna press conference au? Hayo mambo ya kuwaweka wawekezaji kwenye "tension and suspense" kunadhoofisha uwekezaji nchini!

Utafiti unaonyesha kwamba wawekezaji kwenye sekta ya madini hapa Tanzania ume-stagnate kwa karibu miaka miwili kutokana na hiyo kamati ya kuchunguza mikataba ya madini. Maana hawaelewi mwelekeo utaofuata baada ya hapo!

Ukichanganya na financial meltdown ndio kabisa, vijikampuni vidog vidogo vya exploaration vyote vimesimamisha shughuli zao na kupunguza wafanyakazi!

Ebu rekebisha hapo sema wizi, bora wasimamishe ili kikieleweka kila moja afaidike sio tunaibiwa ibiwa tu alafu tunadanganywa eti uchumi umekua, umekuaje wakati rasilimali zinaibiwa??????
 
Kuna press conference au? Hayo mambo ya kuwaweka wawekezaji kwenye "tension and suspense" kunadhoofisha uwekezaji nchini!

Utafiti unaonyesha kwamba wawekezaji kwenye sekta ya madini hapa Tanzania ume-stagnate kwa karibu miaka miwili kutokana na hiyo kamati ya kuchunguza mikataba ya madini. Maana hawaelewi mwelekeo utaofuata baada ya hapo!

Ukichanganya na financial meltdown ndio kabisa, vijikampuni vidog vidogo vya exploaration vyote vimesimamisha shughuli zao na kupunguza wafanyakazi!

Mkuu Masaki are you for them or for us? Mwananchi Mtanzania maisha yake yana tofauti gani kwa hiyo miaka miwili unayoizungumzia wewe? Utafiti aliofanya nani kwa manufaa ya nani? By the way mwalimu wako alikufundisha madini yakikaa ardhini kwa muda mrefu bila kuchimbwa yanaoza? Please try to rethink your statement, hizo ngojera nadhani tunazijua
 
Back
Top Bottom