Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Mkuu Mfamaji, nilifikiri Badra masoud kasema huo mtambo wa watsila unamilikiwa na TANESCO,sasa unaufananishaje mtambo wa TANESCO wenyewe (kwa maana ya umiliki) na mtambo wa kukodisha wa richmond/dowans? tafadhali naomba nisaidie ufafanuzi nipate kuelewa vizuri mkuu.
 
Kungurumweupe, ni suala la makubaliano ya kibiashara tu, mbona wasafirishaji hutumia barabara ambazo ni public goods na wanalipa ada ya barabara kupitia ushuru wa mafuta kama sikosei tanroad wanalipwa shs 90/= kwa kila lita ya diesel.

Nalishauri tanesco iwe holdings company ndani yake yaundwe mashirika matatu wazalishaji, wasafirishaji na wauzaji. Hivyo Dowans wanaweza kuzalisha umeme wakausafirisha kwa mtandao wa tanesco kwenda kwa wateja wao, pia Dowans wanaweza kununua umeme wa ziada toka tanesco na kuuza kwa wateja wao.
 
Kuvunjka kwa mkataba wa Dowans na Tanesco unatokana na utata wa kisheria kwa sababu kwanza mwenye mkataba imedhihirika kisheria is not there. Yaani Tanesco waliweka mkataba na mzimu au kivuli kwa jina lingine.
Hata hivyo hiyo haiwazuii Dowans kama ni legal company kufanya biashara na kampuni nyingine kama watakuwa na mikataba mizuri isiyo ya kinyonyaji.
Kuhusu kuwa na mitambo ndani ya eneo la Tanesco hiyo ni juu yao kukubaliana na hata kuhusu usambazaji pia kunaitaji maelewano ya kibiashara. Hapa Tanesco kama haikujiingiza tena katika mikataba ya kifisadi watanufaika sana. Shida ni kwamba mikataba mingi whether ni ya mashirika au sirikali yote wanatuambia ni siri na mwisho inadhihirika ni ubabaishaji tupu.
 
Siku hizi hii Dowans ni kampuni ya Manji, sio ya Rostam tena kweli wajinga ndio wali wetu!

Hivi Manji na mipesa yote hiyo, kwanini sasa asiamue kufanya biashara ambazo sio controversial sana?

Watu wanatake risk mwanzoni lakini baada ya muda ndio wanakuwa wa kwanza kuingia kwenye miradi ambayo inakuwa na aina fulani ya kusaidia jamii badala ya kuibia jamii.

Yeye kila mradi ni ufisadi tu hata sasa ambapo tayari ana pesa za kutosha?
 
nafikiri kama dowans ni kampuni halali na wanataka kufanya biashara ya umeme, wangepewa nafasi ya kupeleka umeme kule ambako tanesco haijafikisha huduma zake.
 
Wakifanya biashara ya wazi ambayo haina hata chembe ya kuibia wananchi ilo si tatizo wanakaribishwa tanzania waendelee kufanya biashara lakini kama nia yao ni kuendeleza wizi tutakufa nao.
 
Dowans : Hatuondoki
Faraja Mgwabati
Daily News; Friday,July 25, 2008 @00:02

Hata hivyo, alisema wananchi wasiwe na wasiwasi kwa kuwa umeme wa megawati 100 ambao ulikuwa ukitolewa na Dowans, sasa utapatikana kupitia mitambo ya Watsila ya megawati 100 ambayo inamilikiwa na shirika hilo

If you want to hide something from africans/black people put it in the book, Watu hamtaki kusoma kabisa, mkisoma hamuelewi wala hamtaki kufanya uchunguzi japo kidogo. Watsila Power Plant belongs to TANESCO.

MY TAKE:-

Mimi sioni ubaya wa DOWANS kuuza umeme wao Tanzania, kama mitambo yao ni mizuri na tuwaache wasambaze na kuuza umeme wao nchini, kiasi cha umeme wanachozalisha ni kikubwa na kinahitajika sana Tanzania, kuna maeneo mengi ambayo hatuna umeme, na hii itakuwa vizuri kuwaweka Tanesco kwenye ushindani ili waweze kuongeza ufanisi,wachape kazi wakishindwa wafuate nyayo za ndugu zao TTCL na UDA. Tunahitaji makampuni binafsi waje na kuwekeza kwenye umeme, gharama za Tanesco zimekuwa kubwa sana, labda kwa kuleta makampuni mengine binafsi kusambaza na kuuza umeme inchi kunaweza shusha gharama za umeme.

Ni hayo tu.
 
Nani atawapatia tena kibali cha kuuza huo umeme huko machimboni,Huyo mchawi akamatwe na asulubiwe mchana kweupe.

FYI kuna sheria mpya ya nishati na umeme iliyopigiwa kelele na wabunge ishapitishwa na makampuni binafsi yemeruhusiwa kuzalisha umeme - mafisadi waliona mbali mitambo yao pindi tukisitisha mkataba watayapeleka wapi bora wabadili sheria na mambo ndio hayo Single
 
Miaka kadhaa iliyopita mawasiliano na watu waishio maeneo kama, Misozwe-Muheza, Nanjilinji, tandahimba, kibakwe, mgololo hawakuwa na mawasiano ya simu, lakini hivi sasa wanatesa masaa 24, unaweza kuwajulia hali bibi na babu zako hata usiku wa manane, shukrani ziwaendee mashirika ya simu za mikononi hawa jamaa wanafanya kazi kweli kweli minara yao inapanda kila kukicha, kama hadi sasa tungekuwa na TTCL pekee mambo kama haya yasingetokea ingebaki kuwa hadithi tuu, wacha yaje makampuni binafsi yaifundishe TANESCO jinsi yakusambaza umeme mpaka Misozwe-Muheza, Nanjilinji, tandahimba, kibakwe hadi mgololo..na kama DOWANS wanazosifa zinazohitajika basi nao wapewe nafasi hiyo.

Ni hayo tu.
 
Kwa wale mnaoifahamu bongo yaani Dsm,pale ubungo baada ya jengo la makao ya Tanesco kama unakwenda Kimara kuna mtambo mkubwa kabisa umejengwa na kampuni ya Watsila ni wa kisasa(according to them).

Lakini Watsila ndo kampuni iliyojenga mitambo ya IPTL pia. Nijuavyo mimi ni kwamba watsila ni mjenzi na mmiliki ni serikali. Sasa kama nimekosea mnisamehe na mwenye ukweli atusaidie.
 
Kungurumweupe, ni suala la makubaliano ya kibiashara tu, mbona wasafirishaji hutumia barabara ambazo ni public goods na wanalipa ada ya barabara kupitia ushuru wa mafuta kama sikosei tanroad wanalipwa shs 90/= kwa kila lita ya diesel.

Nalishauri tanesco iwe holdings company ndani yake yaundwe mashirika matatu wazalishaji, wasafirishaji na wauzaji. Hivyo Dowans wanaweza kuzalisha umeme wakausafirisha kwa mtandao wa tanesco kwenda kwa wateja wao, pia Dowans wanaweza kununua umeme wa ziada toka tanesco na kuuza kwa wateja wao.


Mkuu Eddy,

I concur with you with regard to dividing tanesco into three separate companies, because it will enhance her profitability. But do you think is a fair game for the government to still allow dowans to operate in tz after all what they did to the tanzanians??!!

I think dowanass should be fully and completely banned from exercising any business operation in tz! They are thugs!
 
Miaka kadhaa iliyopita mawasiliano na watu waishio maeneo kama, Misozwe-Muheza, Nanjilinji, tandahimba, kibakwe, mgololo hawakuwa na mawasiano ya simu, lakini hivi sasa wanatesa masaa 24, unaweza kuwajulia hali bibi na babu zako hata usiku wa manane, shukrani ziwaendee mashirika ya simu za mikononi hawa jamaa wanafanya kazi kweli kweli minara yao inapanda kila kukicha, kama hadi sasa tungekuwa na TTCL pekee mambo kama haya yasingetokea ingebaki kuwa hadithi tuu, wacha yaje makampuni binafsi yaifundishe TANESCO jinsi yakusambaza umeme mpaka Misozwe-Muheza, Nanjilinji, tandahimba, kibakwe hadi mgololo..na kama DOWANS wanazosifa zinazohitajika basi nao wapewe nafasi hiyo.

Ni hayo tu.

Mkuu MJ,

Dowans hawana hizo sifa.
 
Kwa wale mnaoifahamu bongo yaani Dsm,pale ubungo baada ya jengo la makao ya Tanesco kama unakwenda Kimara kuna mtambo mkubwa kabisa umejengwa na kampuni ya Watsila ni wa kisasa(according to them).

Lakini Watsila ndo kampuni iliyojenga mitambo ya IPTL pia. Nijuavyo mimi ni kwamba watsila ni mjenzi na mmiliki ni serikali. Sasa kama nimekosea mnisamehe na mwenye ukweli atusaidie.


Hata mimi nimewahi kuuona huo mtambo, lakini je 'who is the owner'??
 
Hata mimi nimewahi kuuona huo mtambo, lakini je 'who is the owner'??
Ndugu Kungurumweupe kama alivyosema ndugu malila, Watsila ni wajenzi wa mitambo ya umeme na wanawajengea TANESCO. kuna kazi moja tulifanya nao hawa jamaa. wanajenga tu na baadaye watakabidhi TANESCO itakayoiendesha mitambo hivyo.
 
Dowans wasanii wanapitisha muda ili watege maana mambo yaweza badilika siku moja....hakuna nini wala nini...labda wafikiriwe...ili waachiwe kuuza umeme wao kupitia GRid ya Taifa....la msingi kama vipi heri watangaze kuuza mitambo yao kwa bei poa........kama hawataki watoe mitambo yao......
 
Hawa wezi hakuna mwenye shida nao walivyoiba inatosha, ni swala la Tanzania kuweka mikakati na kuondokana na hawa MAFIA. Na tusije kusikia kuna tapeli lingine linataka mikataba mibovu kama hii iendelee.
 
Dowans yafungasha virago leo

2008-08-01 10:57:40
Na Dunstan Bahai

Mkataba kati ya kampuni ya Dowans Tanzania Ltd na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), unasitishwa rasmi leo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dk. Idris Rashidi, uamuzi wa kusitisha mkataba wa kuuziwa umeme na kampuni hiyo umekuja baada ya kikao cha Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo.

Dowans ambayo ilichukuwa mikoba ya kampuni ya kufufua umeme ya Richmond Development LLC, ilipewa muda wa mwezi mmoja na bodi hiyo ya Wakurugenzi ya Tanesco kufungasha mikoba yake ikiwa ni pamoja na kuandaa utaratibu wa malipo kwa wafanyakazi wake.

Alipoulizwa juu ya utekelezaji wa maagizo hayo ya Bodi ya Wakurugenzi kwa Dowans, Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Badra Masoud, alisema mwisho wa kampuni hiyo ni leo, lakini alimshauri mwandishi kuvuta subira hadi leo ili apate taarifa zaidi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Dk. Rashid, mchakato wa utaratibu mzima kuhusu Richmond na TANESCO ulitiwa saini Juni 23, 2006 na Bodi ya Wakurugenzi iliamua kupata ushauri wa kitalaamu ili kujua uhalali wa mkataba husika.

Dk. Rashidi alisema ili kufanikisha azma hiyo, kampuni ya sheria iliajiriwa ili kutoa ushauri wa kitaalamu ili kujua uhalali wa mkataba husika.

Alisema ushauri huo wa kisheria ulibaini pamoja na mambo mengine kwamba utaratibu mzima wa manunuzi ya huduma hiyo ya umeme na kuingia mkataba na Richmond ulikiuka sheria ya manunuzi namba 21 ya mwaka 2004.

Jitihada za kuwapata maofisa wa kampuni ya Dowans jana zilishindikana, ingawa zinaendelea.

* SOURCE: Nipashe
 
Lets wait and see kama wataondoka kweli leo ama utasikia wamefungua shauri mahakamani na blabla kibao.
 
sijui kama kweli wataondoka, sana watapewa "mradi" mwingine kama kawaida yetu!!
 
Back
Top Bottom