Mada zako hazina mshiko unaangalia penye makosa ila huangaliii faida ya jumla ivi nikuulize swali mkeo ametoka zake ndani kapiga kimini au suruali kasuka kajiremba na manukato ya kutosha akaenda uko akatongozwa wakamzini utamlaum nani na si kwamba naongea hayatokei ni mengi tuuu ila nikuulz kati ya hao wanawak yan alievaa kimini na alievaa ninja au baibui ni nani atakuwa na mvuto zaidi na atatongozwa zaid kwa watu bila shaka jibu unalo ivoivo ndo maana dini ya uislam ikakataza mwanamke kwenda uchi kwasbb ya madhara kama hyo na mengine meengi sasa basi si tu katik mavazi kila kitu dini ya uislam imefundisha sasa niambie huo ukrist umefundisha kila kitu? ,et unaenda kumuomba mungu umemvalia uchi Kwani Mungu ana shida na uchi wako kwamb ukimvalia ivo ndo atakujibia maomb yako haraka?? Kwanza hiyo biblie yenyew imesema mwanamke afunike kichwa chake sjui kama unaijua!!!!
#Jitambue#
Nimekuambia, hakuna dini hata moja ambayo nimewahi kusikia kuwa inahamasisha waumini wake wavae mavazi yasiyo ya heshima. Kama ipo, niambie ni ipi.
Awe mkeo au dadako au binti yako, sidhani utapenda avae mavazi yanayoonesha sehemu ambazo kila mmoja anajua kuwa zinatakiwa kusitiriwa, na hilo siyo kwa sababu ya kuogopa kuwa atatongozwa, bali ni kulinda maadili ya jumla. Hata wewe hapo ukawa na dadako, amevaa hovyo, ni dhahiri kuvaa kwake hovyo hakuwezi kukufanya wewe umtongoze, lakini itakukera kwa vile dadako inaonekana haheshimu utu wake.
Kuna kosa linafanyika, tendo la mtu binafsi iwe huyo mtu ni mkristo au muislam au wa dini nyingine yoyote, lisichukuliwe kuwa ndiyo mafundisho au maagizo ya dini yake. Mimi mwenyewe, miaka ya huko nyuma nilienda beach hotel ilikuwa inaitwa Silversands Hotel muda wa jioni, mita chache kabla ya kufika hotelini tumawaona mabinti wanavua hijabu, wanabakia na vimini, zile hijabu wanawapa vijana wawatunzie. Nilishtuka, nilipowauliza wazoevu wa.mazingira yale, nilishangaa. Lakini ujumbe wa wazi nilioupata ni kwamba wale mabinti ni lazima wanatoka kwenye familia zisizoruhusu uvaaji wa namna ile, lakini ambaye hakumwona wakati anatoa hizo hijab, kama akimwona vile alivyokuwa na vimini, na akijua ni muislam, unataka aamini kuwa uislam ndiyo umemwelekeza avae vile. Nilienda Zanzibar, nako ni vile vile, tena naona kule imekuwa rasmi. Kwenye mahoteli makubwa yale ya kitalii, mabinti wa kiislam wanatoka majumbani na hijabu, wakifika pale kuna chuma maalum cha kwenda kubadilishia nguo, wanatoka na vimini.
Ndiyo maana tunasema kuwa kwenye imani, mfundishe muumini anachotakiwa kufanya, uamuzi wa mwisho ni wa kwake. Huwezi kulazimisha imani, la sivyo utadanganywa. Mimi sinywi pombe, siyo kwa sababu ya imani, bali mwenyewe siamini kaa ni kinywaji chema. Kwa sababu hicho ndicho ninachokiamimi, siyo rahisi mtu kunibadilisha. Lakini wapo waislam ambao wanaambiwa wasinywe pombe, wanakubali, lakini wakitoka hapo, wanaitafuta hata kwa gharama kubwa, lazima wapate. Nenda Saud Arabia, ukishuka tu uwanja wa ndege wa Riadhi, unaanza kufuatwa na waarabu wa pale, kwa siri wanaanza kukuuliza kama unataka pombe au mwanamke, uwaambie utakuwa hoteli gani ili wakuletee. Lakini Saud Arabia, biashara ya pombe na ukahaba imezuiwa. Ukienda kwenye takwimu za ununuzi wa mitambo ya kutengenezea pombe majumbani toka Marekani, Saudi Arabia ndiyo nchi inayoongoza kununua. Kwa hiyo ina maana pombe haitengenezwi kwenye viwanda rasmi, inatengenezwa majumbani