Elewa mada mjomba
Unavosema hakufua dafu mda haujafika mzee
Pia mimi nmekuja hapa kukutadharisheni kwakuw mnapinga ushahid wa maneno yote na yapo wazi kweny kitabu kitukufu (Quran) na bado mmeyapinga basi tulieni subirini hukumu ila sio kuleta mada za kijinga kuhusu uislam kwasbb hata mlete mada kias gan uislam ulikuja mpya na utaondoka ukiwa mpya na bado hata mjiteteee kivipi ukwel mnaujua ndani ya nafsi zenu kwaiyo kama unajua kabisa wewe umeshindwa kuamini uislam kaa tulia subiri hukum yako ila sio kuongeza chuki juu ya uislam kwani hutoongeza zaid bali utakuwa ni kama unautangaza zaidi
Kuna kitu kimoja tu cha muhimu ulichokiongea, nacho ni kuwaacha wanaoamini katika mafunfisho ya uislam waendelee na wanachokiamini bila ya kukejeliwa, kutukanwa au kudharauliwa. Na kwenye hili ungetumia muda wako mwingi kuwaonya waislam wenzako hasa wale mawakala wa shetani wenye misimamo mikali.
Kuna shida kubwa kwenye uislam na waislam, japo siyo wote. Jiulize kwenye mambo yafuatayo:
1. Hivi umewahi kusikia kuna wakristo wamewahi kuvamia msikiti na kuwaua waumini wa kiislam wakati wakiendesha ibada zao?
2. Na vipi hao waislam wa misimamo mikali huko Nigeria, DRC, n.k. wanaowavamia na kuwaua Wakristo wakati wanafanya ibada zao?
3. Je, umewahi kusikia kuna nchi yoyote Duniani, yenye waumini wengi wa Kikristo, ambayo waislam wanazuiwa kuabudu, kujenga misikiti au hata kubeba Quran?
4. Lakini nadhani unafahamu kuwa kwenye mataifa mengi ambayo waislam ni majority, hasa Mashariki ya kati, baadhi ya nchi haziruhusu wakristo kuendesha ibada kwa uhuru, hawaruhusiwi kuonekana wamebeba biblia, na nyingi zinazuia hata kujenga Kanisa.
5. Uliwahi kuwasikia wakristo wamemwua mtu aliyekuwa mkristo kwa sababu ameslimu? Lakini nina hakika umewahi kusikia mara nyingi, kuna nchi ambazo muislam akibatizwa na kuwa mkristo, anauawa.
Jiulize:
1. Dini zote zinaamini kuwa Mungu hashindwi chochote, kama ndivyo, kwa nini wewe ukamwue binadamu mwenzako kwa madai hajafuata maagizo ya Mungu wako? Ina maana huyu Mungu kama anataka mtu aliyefanya dhambi afe, anashindwa kumwua?
2. Kila dini, wakiamini kuwa wasiofuata dini yao, wanatakiwa kuuawa, kama yanavyofanya makundi ya kishetani ya waislam, unadhani Ulimwengu utakuwaje? Nasema ni makundi ya kishetani kwa sababu hata waislam wanasema kuwa Uislam ni dini ya haki, hayo haki ni ipi, kama unamwua mwanadamu mwenzako?
NB: Nakubaliana sana na Mahubiri ya Papa, wakati fulani akiwahubiria waumini wa Kanisa Katoliki kule Brazili, yeye alisema:
'Ni nani mimi hata nimhukumu mwanadamu mwenzangu? Kazi niliyopewa na Kristo ni kuwafundisha na kuwaelekeza wanadamu wenzangu wanatakiwa kufanya nini kadiri ya mpango na mapenzi ya Mungu. Kazi ya kuhukumu si ya yangu, bali ni ya Mungu mwenyewe". Mafundisho haya nayaona ni sahihi sana maana hata tukisoma kwenye Biblia, Yesu Kristo aliyepewa mamlaka yote, na ambaye hata waislam wanaamini atarudi kuutawala Ulimwengu, hakuna mahali alitoa amri au aliwahamadisha waliomwamini na kumfuata wawaue wale waliomkataa.
Falsafa kama hiyo inakosekana kwa baadhi ya makundi ya kiislam. Yaani uhubiri, ufundishe, umwachie yeye uliyemhubiria aamue. Maana wewe siyo wa kwanza wala siyo pekee uliyewahi kumhubiria, na kila aliyemhubiria amemwambia kuwa mahubiri na mafundindisho yake ndiyo sahihi. Kwa nini ulazimishe kuwa ya kwako ni lazima yafuatwe, na asipoguata umwue? Vitendo vya kikatili vya makundi kama hayo ya kiislam, ndivyo vinavyofanya uislam ubagazwe na kuonekana ni imani iliyopoyoka, maana inaxungumzia haki na amani, halafu watu wake wanaharibu haki na amani ya watu wengine.
NB: Ufahamu kuwa wewe unapoamini kuwa watu wasioufuata uislam wamepotea na watahukumiwa, ndivyo na wale wasioufuata uislam wanaamini kuwa wanaoufuata uislam wamepotea. Jambo jema ni kuhubiri na kufundisha imani yako, uhuru wa kuamua umwachie anayehubiriwa. Atakayehukumu ni Mungu mwenyewe. Dini zote zikizingatia hilo, Dunia itakuwa ni mahali pa amani.
Kwa sasa, dini zote Duniani, hakuna inayolazimisha watu, na kuwashambulia waumini wa imani nyingine, isipokuwa baadhi ya makundi ya kiislam. Leo kwa baadhi ya mataifa, makundi hayo ya kiislam yamekuwa laana kwa mataifa yao. Cha kushagazaha, makundi hayo yanapofanya mauaji kwa kutumia jina la uislam, husikii taasisi wala viongozi wa dini ya kiislam wakitoa kauli ya kukemea, kulaani au kujitenga nayo. Kukaa kimya, maovu yanapofanya kwa jina la imani yako, inatafsiriwa kuwa unakubaliana na uovu huo.
Waumini na viongozi wa dini ya Kiislam, wanapotaka wasibagazwe, nao wajue wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha hawaharibu wala kutishia uhuru na haki ya watu wengine ya kuabudu na kufuata kile wanachokiamini kwa kadiri ya mafundisho ya imani zao.