Dkt. Samizi ashuhudia Serikali ya Rais Samia ikimwaga vyeti vya kuzaliwa bure kwa watoto

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
328
414
Mbunge wa Jimbo la Muhambwe mkoani Kigoma, Dkt. Florence George Samizi akiambatana na mkuu wa wilaya ya Kibondo Agrey John Magwaza, leo tarehe 03/10/2023 amekuwa Mgeni rasmi katika zoezi la kampeni ya usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5(0-5) ambao umefanyika katika Viwanja vya ofisi ya Kata - Kitahana.

Katika Uzinduzi huo amehudhuria Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Kibondo, Hamis Salum Tahilo na viongozi mbalimbali wa chama na serikali. Viongozi wote wamempongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Saluhu Hassan kwa namna anavyoendelea kuwahudumia Watanzania na kuwasogezea wananchi huduma hii muhimu tena kwenye ngazi ya chini kabisa ya zahanati na kijiji.
 

Attachments

  • IMG-20231004-WA0008.jpg
    IMG-20231004-WA0008.jpg
    85.4 KB · Views: 2
  • IMG-20231004-WA0007.jpg
    IMG-20231004-WA0007.jpg
    72.1 KB · Views: 1
  • IMG-20231004-WA0006.jpg
    IMG-20231004-WA0006.jpg
    67 KB · Views: 1
Mbunge wa Jimbo la Muhambwe mkoani Kigoma, Dkt. Florence George Samizi akiambatana na mkuu wa wilaya ya Kibondo Agrey John Magwaza, leo tarehe 03/10/2023 amekuwa Mgeni rasmi katika zoezi la kampeni ya usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5(0-5) ambao umefanyika katika Viwanja vya ofisi ya Kata - Kitahana.

Katika Uzinduzi huo amehudhuria Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Kibondo, Hamis Salum Tahilo na viongozi mbalimbali wa chama na serikali. Viongozi wote wamempongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Saluhu Hassan kwa namna anavyoendelea kuwahudumia Watanzania na kuwasogezea wananchi huduma hii muhimu tena kwenye ngazi ya chini kabisa ya zahanati na kijiji.
Mnaboa sana washenzi nyie
 
Machawa mna kazi sana,ukitoka hapa unapiga pesa kwa kumwonyesha umemfungulia thread JF mbunge wako
 
Acheni upumbavu wenu hakuna serikali ya mtu kuna serikali ya Jamhuri ya Tanzania, pumbavu
 
Cheti cha kuzaliwa ni kumbukumbu ambayo inatakiwa itunzwe kuanzia hospitali au sehemu alipozaliwa mtu.
Haya maigizo ya kuvitoa ukubwani kutoka RITA au kuvigawa kwa watoto mtaani ni upuuzi tu.
Ni uzembe wa serikali na taasisi zake kushindwa kuweka kumbukumbu pale tu binadamu anapozaliwa au kufa.
Lazima tukubaliane kuwa kuanzia sasa kila mtoto anapozaliwa anapewa cheti na wale watu wazima wabaki bila kusumbuliwa hadi wafe kwa kuwa utaratibu huo haukuwepo huko nyuma.
 
Vyeti vya kuzaliwa navyo vinatumika kisiasa wakat ni haki ya kla mzazi pale anapojifungua

Kwel Tz wajinga ni weng na CCM itatutawala ad sku ikichoka yenyewe yan kijiji kizima na viongozi wake wote wanaenda kupokea vyeti vya kuzaliwa

Yan mtu unaanzisha uzi kupongeza utoaji wa vyeti vyakuzaliwa

Wazo la bure sabu sko apa kuomba msaada JF wabadilike waache kutumika kisiasa wanaboa na watapoteza iman kwa watumiaji wake
Sku izi mada za maana wanakwambia fungua browser ila mada za kijinga ndo wanaziacha
Moderator wanatumika vibaya habar mbaya au zle za kuponda serikal ad tufungue browse na wakat mwingne znapigwa pin kbsa hazifunguki af mada za kijinga ndo mnapromote
 
Mbunge wa Jimbo la Muhambwe mkoani Kigoma, Dkt. Florence George Samizi akiambatana na mkuu wa wilaya ya Kibondo Agrey John Magwaza, leo tarehe 03/10/2023 amekuwa Mgeni rasmi katika zoezi la kampeni ya usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5(0-5) ambao umefanyika katika Viwanja vya ofisi ya Kata - Kitahana.

Katika Uzinduzi huo amehudhuria Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Kibondo, Hamis Salum Tahilo na viongozi mbalimbali wa chama na serikali. Viongozi wote wamempongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Saluhu Hassan kwa namna anavyoendelea kuwahudumia Watanzania na kuwasogezea wananchi huduma hii muhimu tena kwenye ngazi ya chini kabisa ya zahanati na kijiji.
Serikali zipo mbili? Serikali ya Samia inayotajwa kumwaga vyeti na pesa wakati ile ya Jamhuri ya Muungano ikiwa kimya huku rushwa ikishamiri, ubadhirifu ukiendelea kwa kasi
 
Yaani haya yalitakiwa kuwa utekelezaji wa msingi toka wakati wa Uhuru sasa mnakuja kuyafanya kwa sasa mnawa brtain wash wasiofahamu|? Halafu mnaita maendeleo, Ujunga Mtupu
 
Back
Top Bottom