Usafirishaji ni sekta muhimu kwa biashara yoyote duniani, ili biashara endelevu iwepo ni lazima kwanza kuwepo na MAHITAJI pili kuwepo UZALISHAJI tatu kuwepo USAFIRISHAJI au USAMBAZAJI hapo biashara hufanyika ni kanuni mojawapo ya biashara baina ya wauzaji na wanunuzi kimoja wapo kikikosekana biashara huwa ni ngumu kufanyika kwa muelekeo huo wakulima wetu watapata wakati mgumu kuuza bidhaa zao kama vile choroko, dengu, mbaazi, giligilani ambazo zote hizo hutumika kidogo sana nchini , kiasi kikubwa husafirishwa nchi zs mashariki ya kati ambao ndio walaji wakubwa wa bidhaa hizo mamia ya matani kama sio maelfu ya matani , na zote hizo husafirishwa kwa meli kubwa kubwa ambazo huja nchini kushusha bidhaa kutoka China India ,Japan na kwingineko na kawaida za meli hufanya biashara zake kama dala dala yaani hushusha na kupakia na huzunguka duniani kote kwa stail hiyo hiyo isipokuwa baadhi chache sana zile ndogo ndogo hupata mizigo ya kwenda mahali pamoja
Sasa ikiwa meli zinakuwa chache bandarini kuna maanisha shusha pakia itakuwa kwa kiasi kidogo sana hiyo itasababisha gharama za usafirishaji huenda zikawa ghali kwa maana hiyo atakaye fidia ughali wa usafirishaji akawa mkulima kwa kununuliwa bidhaa zake kwa bei pungufu kuliko miaka iliyopita , huu ni mtizamo tu