Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amemtabiria mtoto wa kwanza kuzaliwa katika kituo cha afya Ketumbeine kuja kuwa Makamu wa Rais miaka ijayo.
Dkt. Mpango ametoa utabiri huo leo Februari 10, 2024 kwa mtoto aliyezaliwa na kupewa jina la Philipo baada ya msichana, Nengai Nairowa (17) kutembelewa na makamu huyo wa Rais katika wodi ya wajawazito wakati wa uzinduzi wa kituo cha afya Kitumbaine kilichoko wilaya ya Longido mkoani Arusha.
“Mtoto huyu ni bahati yangu na amepewa jina langu kwa sababu amezaliwa baada tu ya kumtembelea wodini na sasa Mtanzania huyu mpya aliyekuja na kilo 2.8 atakuja kuwa Makamu wa Rais wa nchi hii, yaani mrithi wangu nimempata mapema,” amesema Dk Mpango.
“Na nitaenda kumtembelea kumsalimia ili kumjua mrithi wangu baada ya hotuba hapa,” amesema.
Mpango ameyasema hayo baada ya kupokea taarifa za kuzaliwa mtoto huyo, akiwa jukwaani akihutubia wananchi wa Longido baada ya uzinduzi wa kituo hicho cha afya Kitumbaine.
Katika hatua nyingine, Dk Mpango amewapongeza wananchi wa Longido kwa kutoa mifugo yao kuchangia zaidi ya Sh300 milioni katika kituo hicho kilichogharimu zaidi ya Sh1.32 bilioni, huku Serikali kuu ikitoka Sh800 milioni na Shirika la World Vision wakichangia Sh215 milioni.
Source - Mwananchi
Dkt. Mpango ametoa utabiri huo leo Februari 10, 2024 kwa mtoto aliyezaliwa na kupewa jina la Philipo baada ya msichana, Nengai Nairowa (17) kutembelewa na makamu huyo wa Rais katika wodi ya wajawazito wakati wa uzinduzi wa kituo cha afya Kitumbaine kilichoko wilaya ya Longido mkoani Arusha.
“Mtoto huyu ni bahati yangu na amepewa jina langu kwa sababu amezaliwa baada tu ya kumtembelea wodini na sasa Mtanzania huyu mpya aliyekuja na kilo 2.8 atakuja kuwa Makamu wa Rais wa nchi hii, yaani mrithi wangu nimempata mapema,” amesema Dk Mpango.
“Na nitaenda kumtembelea kumsalimia ili kumjua mrithi wangu baada ya hotuba hapa,” amesema.
Mpango ameyasema hayo baada ya kupokea taarifa za kuzaliwa mtoto huyo, akiwa jukwaani akihutubia wananchi wa Longido baada ya uzinduzi wa kituo hicho cha afya Kitumbaine.
Katika hatua nyingine, Dk Mpango amewapongeza wananchi wa Longido kwa kutoa mifugo yao kuchangia zaidi ya Sh300 milioni katika kituo hicho kilichogharimu zaidi ya Sh1.32 bilioni, huku Serikali kuu ikitoka Sh800 milioni na Shirika la World Vision wakichangia Sh215 milioni.
Source - Mwananchi