DK. Bilali Chaguo la JK Kumrithi 2015?

download+%2834%29.jpg
 
Watanganyika hatuwezi kukubali Kamwe kukabidhi Nchi hii kwa Wazanzibar, Lile ni Koloni letu hata Jussa anajua
 
Hakuna kiongozi bora anayeweza kutoka CCM sasa. Aje Bilal, Halal na Hilal yote ni magamba. Heri tuwape wapinzani nao wajaribu vitu vyao. Otherwise we are doomed. Tuna kaugonjwa kaitwako Ammaglobulinemia kisiasa.
 
Inaonekana Jk anawakosesha usingizi kabisaa!! Mara eti anamuandaa migiro,mara membe,mara bilal.achen kuweweseka,jk anae mgombea wake na ndio ataeshinda,jk alimpeleka zenj karume akiwa hana mvuto kupitia mtandao wake akiwa waziri wa mambo ya nje,akampeleka shein akiwa hana mvuto,kawasaidia wabunge wengi wa ccm kuingia bungen na pia kawasaidia wapinzan wengi tu kuingia bungeni,mkitaka kujua nguvu zake muulizeni yule padri muasi asiewahi kuvaa pete ya ndoa!
 
Watanganyika hatuwezi kukubali Kamwe kukabidhi Nchi hii kwa Wazanzibar, Lile ni Koloni letu hata Jussa anajua

Mkuu katika Siasa chochote kinawezekana kwa mujibu wa katiba tuliyonayo.

tatizo ni kuwa hamuwezi kukubali kivipi? Mtafanya maandamano kupinga? Wangapi watayaunga mkono?

Au mtapiga kura za kumkataa? wangapi watapiga?

Kwa baadhi ya Watanzania imedhihirika ni wepesi kuongea kuliko kutenda.
 
Hakuna kiongozi bora anayeweza kutoka CCM sasa. Aje Bilal, Halal na Hilal yote ni magamba. Heri tuwape wapinzani nao wajaribu vitu vyao. Otherwise we are doomed. Tuna kaugonjwa kaitwako Ammaglobulinemia kisiasa.

Mkuuu issue ni kuwa nani atawapa wapinzani? Ni Watanzania hawa hawa kweli? Assume kura hazitaibiwa, watawapa kweli wapinzani?

Na huu ugonjwa wa Ammaglobulinemia ni ugonjwa gani?
 
Inaonekana Jk anawakosesha usingizi kabisaa!! Mara eti anamuandaa migiro,mara membe,mara bilal.achen kuweweseka,jk anae mgombea wake na ndio ataeshinda,jk alimpeleka zenj karume akiwa hana mvuto kupitia mtandao wake akiwa waziri wa mambo ya nje,akampeleka shein akiwa hana mvuto,kawasaidia wabunge wengi wa ccm kuingia bungen na pia kawasaidia wapinzan wengi tu kuingia bungeni,mkitaka kujua nguvu zake muulizeni yule padri muasi asiewahi kuvaa pete ya ndoa!

FYI: Sheini hata siku moja halikuwa chaguo za JK.

Source zako zikujulishe vema.

La Karume ni kweli ingawa sasa Karume kamgeuka.

Migiro: Si kwa Tanzania ya leo, labda huko CCM, wapiga kura watamtoa knock out. She is not a popular figure TZ. labda apewe U-PM sasa hivi au huko mbeleni.

Membe: Siasa za makundi.

Wabunge wengi wa CCM: mmh, kuna issue tata ya wizi wa kura

Padri (assuming ni Dr. Slaa) kaingiza Wabunge wengi Chadema. Pia alipata asilimia kubwa ya kura za Urais. Pamoja na utata wa kuiba kura lakini siyo siri kuwa anakubalika.

By the way: Hoja ya katiba Mpya ni ya nani? Jibu litakujulisha ni nani wanakubalika.
 
Wanajamii;

Kwa wafuatiliaji wa habari bila ya shaka watakua wamegundua kuwa Makamu Wa Rais Mh. Dk Bilali kwa kipindi kirefu sasa amekuwa katika ziara za kikazi mikoani na wilayani na kupewa kipau mbele katika media za Tanzania. Ziara hizi kwa mtazamo wa haraka japokuwa ni za kikazi lakini zimekuwa ni nyingi sana zaidi ya kiongozi mwingine yoyote wa Kisiasa.

Ikumbukwe kuwa Dr. Bilali ni Makamu wa Rais na anafanya zile kazi ambazo Rais amemwagiza au yuko aware nazo.

Yawezekana kabisa kuwa Rais Kikwete ameamua kuchukua uamuzi huo wa kumuandaa na kumtangaza Bilali awe mgombea Urais wa CCM 2015 ili kukinusuru chama chake CCM kutokana na makundi ambayo itake isitake 2015 yatakimega CCM kabisa kwa asilia 100%. Huenda akawa na sababu nyingi lakini chache ni zifuatazo:


  • Safari hii ni zamu ya Wazanzibar kutoa Rais. Kumbuka hii ni hoja rahisi kama walivyoamua kuwa safari hii Spika ni Mwanamke na hivyo kumweka Sita pembeni. K
​
  • Dk. Bilali hana Makundi na amekuwepo katika siasa za Bara na Visiwani na anakubalika (Of course ziara za sasa zimam-promote)
​
  • Dk. Bilali amekuwa Makamu wa Rais na anakubalika kama Presidential Material
​

  • Ili kuzima chokochoko za Wazanzibari kuua Muungano dawa ni kumweka Mzanzibar. JK hawezi kuruhusu Zanzibar iwe Nchi au Dola (Historically na Kikatiba).
​

  • JK hataki aonekane kaivuruga Nchi ndo maana kwa mambo yote makubwa nchi hii kaamua bora tu akae kimya kuliko kusema. La kuhusu katiba ameona bora atofautiane na Chama chake ili kuacha Lergacy na kuleta utengamao katika Nchi.

Ni nini maoni yako binafsi kuhusu Dk. Bilali na harakati zake za kuzunguka mikoani na wilayani in connection na mbio za Urais 2015? Je yawezekana akawa ni Chaguo la JK?

Nawasilisha.


Ni maneno ya Ukweli Ndugu Yangu Superman.Nami nimesikia kutoka vyanzo vya Uhakika kuwa Dr Bilal anatayarishwa kuwa Mgombea wa Urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.Dr.Bilal ni mzoefu wa siasa za Tanzania Bara kuliko Visiwani ukichukulia kuwa amewahi kufanya kazi kwa karibu na marais wote toka Mwalimu mpaka sasa Kikwete pia ana ushawishi wa kutosha Zanzibar,Wale wafuatiliaji wa siasa za huko kumbukeni kinyanga'nyiro cha Urais kati ya Rais mstaafu wa Zanzibar Mzee Aman karume na Dr Bilal mpaka kumuondoa Dr Bilal kugombea nafasi hiyo kwa kupitia vikao vya Chama,kumbukeni pia Uchaguzi wa Rais wa sasa wa Zanzibar,Dr Bilal alikuwa na ushawishi mkubwa,na pengine kapewa nafasi hii ya Umakamu wa Bara ili kutuliza lile vurugu lililokuwepo alipoenguliwa na kumpisha Rais wa sasa Ali Mohamed Shein.

Dr Bilal ni msomi na mzoefu wa Utendaji kuliko siasa za Majukwaani,kinachoniogopesha Mimi ni Afya yake na umri ambao unaonekana hautoweza kuhimili mikikimikiki ya Kampeni na baadaye Uongozi katika Taifa hili ambalo linahitaji Kiongozi Makini na mwenye Afya isiyo na migogoro.CCM wanatumia nafasi hii kumtembeza Dr kila pande ya Nchi ili apate popularity,kwa lolote litakalokuwa kutakuwa na mgawanyiko mkubwa ndani ya Chama Tawala.Kwa sababu jinsi hali ilivyo sasa,kila mwanasiasa anajiona anaweza kuikwaa kazi hiyo......"Kama kaweza Kikwete,kwa hakika hakuna atakayeshindwa!".Katika list ndefu kuna akina Membe,Lowassa,Nchimbi,Magufuri na hata Mama Migiro.

Vyama vya Upinzani viangalie kwa makini nyendo za huyu Mzee,kwani siasa ya kweli inaanza katika ushindani wa kujadili Hoja za kumjenga Mtanzania.......Wapambane nae kihoja nao wapite mikoani na kila pande anayopita huyu Mzee kuzima Hoja zake na kuwapa wananchi nafasi ya kuona upande wa pili wa serikali hii dhalimu!
 
Dr. Bilal umri nao unaelekea machweo, sidhani kama hata yeye mwenyewe ana wazo la kugombea. Kwa jinsi watu walivyoichoka ccm, bila kupatikana mgombea kijana basi tutegemee uchakachuaji wa kura kwa mara nyingine.

Unaweza kuwa sahihi kwa manufaa ya taifa na kwa fikra nje ya Boksi. Bilal si chaguo sahihi kwa CCMau Nchi

Lakini "Ki CCM"( Makundi) na kujaribu kuunga unga muungano amabao siku zinavyozid kwenda nyufa zinazidi Huyo mzee ndiyo anaweza kuwa best option ya CCM kutusogeza tu . Sio kwamba ni option ya kutatu matatizo ya UCHUMI UFISADI, Mungano etc

Hata fanya chochete kuhusu Muungano lakini uwepo wake ni sawa na Vidonge ARV kwa mgonjwa wa ukimwi. Kuchelewesha madhara ya tatizo....

Zaidi ya muungano Bilal inaweza kuwa option nzuri kwa ksingizo cha zamu "yao" lakini lengo kuu ni kumpiga chini EL ambaye wameshindwa na hawana nguvu za kumkatalia kavu kavu.

So mpaka hapo nadhani bilal ni chaguo bora kufunika/kufukia matatizo halisi na muda uende lakini sio chaguo bor kutatua na kushghulikia matatzio. iwe ni ya muungano au mengineyo.

Sana sana atachofanya kama akiwa rais atachemsha zaidi ya Kikwete. Hiyo itatufanya tumkumkbuke JK kwa sifa kama tulivyosahau mabaya ya Mkapa sababu ya underpefromnce ya ya JK..... ....

Huo ni mtazamo wangu.
 
Ni maneno ya Ukweli Ndugu Yangu Superman.Nami nimesikia kutoka vyanzo vya Uhakika kuwa Dr Bilal anatayarishwa kuwa Mgombea wa Urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.Dr.Bilal ni mzoefu wa siasa za Tanzania Bara kuliko Visiwani ukichukulia kuwa amewahi kufanya kazi kwa karibu na marais wote toka Mwalimu mpaka sasa Kikwete pia ana ushawishi wa kutosha Zanzibar,Wale wafuatiliaji wa siasa za huko kumbukeni kinyanga'nyiro cha Urais kati ya Rais mstaafu wa Zanzibar Mzee Aman karume na Dr Bilal mpaka kumuondoa Dr Bilal kugombea nafasi hiyo kwa kupitia vikao vya Chama,kumbukeni pia Uchaguzi wa Rais wa sasa wa Zanzibar,Dr Bilal alikuwa na ushawishi mkubwa,na pengine kapewa nafasi hii ya Umakamu wa Bara ili kutuliza lile vurugu lililokuwepo alipoenguliwa na kumpisha Dr Omar.

Dr Bilal ni msomi na mzoefu wa Utendaji kuliko siasa za Majukwaani,kinachoniogopesha Mimi ni Afya yake na umri ambao unaonekana hautoweza kuhimili mikikimikiki ya Kampeni na baadaye Uongozi katika Taifa hili ambalo linahitaji Kiongozi Makini na mwenye Afya isiyo na migogoro.CCM wanatumia nafasi hii kumtembeza Dr kila pande ya Nchi ili apate popularity,kwa lolote litakalokuwa kutakuwa na mgawanyiko mkubwa ndani ya Chama Tawala.Kwa sababu jinsi hali ilivyo sasa,kila mwanasiasa anajiona anaweza kuikwaa kazi hiyo......"Kama kaweza Kikwete,kwa hakika hakuna atakayeshindwa!".Katika list ndefu kuna akina Membe,Lowassa,Nchimbi,Magufuri na hata Mama Migiro.

Vyama vya Upinzani viangalie kwa makini nyendo za huyu Mzee,kwani siasa ya kweli inaanza katika ushindani wa kujadili Hoja za kumjenga Mtanzania.......Wapambane nae kihoja nao wapite mikoani na kila pande anayopita huyu Mzee kuzima Hoja zake na kuwapa wananchi nafasi ya kuona upande wa pili wa serikali hii dhalimu!

Mkuu, kama kuna ukweli katika hili basi inafaa opposition Waanze kujipanga mapema maana ukiondoa Uzee jama yuko vizuri.

Kila siku hupata nafasi ya kupitia magazeti na blogs kwa almost 6 months, kwa kiasi kikubwa kumekuwa na habari za Bilali more than any politician kumpita Pinda au hata JK mwenyewe. Why?

Katika hatua hii, ningependa tujikumbushe historia yake:

Mohammed Gharib Bilal ,mwanasayansi wa nuklia alizaliwa Unguja mwaka 1945 na kufanikiwa kumaliza elimu yake ya msingi katika skuli ya Makunduchi, wilaya ya Unguja mwaka 1958.

Elimu yake ya sekondari alipatia katika ya shule Beit-el-ras mwaka 1962 na kufanikiwa kuingia kidato cha tano mwaka 1963 katika skuli ya sekondari ya Lumumba, Zanzibar.

Kabla ya kumaliza kidato cha tano alipata scholarship ya kwenda Marekani,ambapo alisomea masomo ya fizikia katika Chuo Kikuu cha Howard na kuhitimu shahada yake ya kwanza katika fizikia na hesabati mwaka 1967.

Baada ya shahada ya kwanza alijiunga na Chuo kikuu cha Carlifonia kwa shahada ya juu kwenye Chuo cha Berkely na kupata shahada ya M.A Physics mwaka 1969. Baada ya kuhitimu alianza kazi kama msadizi wa elimu yaani, Teaching assistant

Mohammed Gharib Bilal alikuwa mkufunzi wa utafiti (research assistant) hadi mwaka 1976 alipofanikiwa kupata Phd ya fizikia kutoka Chuo Kikuu cha Carlifonia.

Baadae mwaka huohuo alijiiunga na Chuo kikuu cha Dar-es-salaam kama mhadhiri wa fizika katika kitengo cha fizikia.

Mwaka 1983 alichaguliwa kuwa mkuu wa Idara na kuongoza kitengo cha Fizikia ya Nyuklia.Katika kipindi hicho aliwafundisha zaidi ya wanafunzi 10 kwenye masomo ya shahada ya uzamili.

Mwaka 1983 alishiriki kuanzisha shirika la mionzi la Taifa kwa kuchangia kitaalamu maandalizi ya mswada ambao ulitupatia sheria ya udhibiti wa matumizi ya mionzi ya nyuklia nchini.

Mwaka 1988 aliteuliwa kuwa mkuu wa Kitivo cha Sayansi cha Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam na kuendelea katika wadhifa huo hadi mwaka 1990 alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu katika Wizara mpya ya wakati huo ya Sayansi Teknolojia na Elimu ya Juu mwaka 1990-1995.

Akiwa Katibu mkuu alishiriki katika kuanzisha utaratibu wa kuchangia gharama za elimu ya juu na kuanzisha utaratibu wa mikopo. Pia wizara hiyo ilianzisha Chuo Kikuu Huria , pamoja na kuanzisha udhibiti wa vyuo vya elimu ya juu ( accreditation council).

Mnamo mwaka 1988 Dr Bilal alianzisha mradi wa science camp mjini Zanzibar iliyolenga kuwahamasisha vijana kusoma sayansi na kuzisaidia shule za sekondari zote za Zanzibar(Unguja na Pemba) Kupata vifaa vya kuwezesha kufanya majaribio ya wanafunzi ili waelewe zaidi sayansi kwa vitendo.

Mradi huo hatimaye ulirithiwa na Wizara ya Elimu Zanzibar. Mradi huo uliwasisimua vijana wengi katika sayansi na kuwapa changamoto nyingi za kujifunza mada mbali mbali zilizogusa mazingira ya Zanzibar.

Akiwa mwalimu wa Chuo Kikuu Dr Bilal aliweza kushiriki katika bodi mbali mbali, kama vile Tume ya Sayansi na Teknolojia(COSTECH), Tume ya mionzi (NRC), Mwenyekiti wa science panel ya Inter university council of East Africa na pia alishiriki kuasisi masomo ya juu ya mazingira katika sayansi(1990).

Mohammed Gharib Bilal alipata fursa ya kuhudhuria semina na kozi fupi katika fani mbali mbali kwa mfano, semina za shirika la Atomiki (IAEA) 1980 Kwabena, Ghana. 1984/85. Fellowship chuo kikuu cha Singapore. Vilivile huudhuria vikao vya kila mwaka vya shirika la Atomic.

Mwaka 1995 Dr Mohammed Gharib Bilal aliteuliwa kuwa Waziri kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar hadi 2000.

Na katika siasa Dr Bilali amekuwa akikitumikia Chama Cha Mapinduzi katika nafasi mbali mbali kama vile kuwa Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa na Kamati Kuu tangu mwaka 1995 na pia amekuwa Mlezi wa Mkoa wa Mjini Magharibi na Mkoa wa Pwani.

Dr Bilal alikuwa Mwenyekiti wa kutafuta utaratibu bora wa kura za maoni wa kuwapata wagombea katika chaguzi za Dola kwa tiketi ya CCM.

Mwaka 2004, aliteuliwa na Chama kuwa Mwenyekiti wa Shirika la Magazeti ya Chama.

Mnamo mwaka 2007, Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe Jakaya Kikwete alimteua Dr Bilal kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Cha Dodoma.
 
Mkuu Logically, ukishakuwa VP unafanya kazi zote za Urais unazopewa. Rais asipokuwepo wewe unakaimu. So with time say 5 years kama kichwa chako kizuri, unakuwa na nafasi nzuri ya kurithi hicho kiti. Ni nini maoni yako?
Mkuu, maoni yangu ni kwamba kweli Bilal analo jukwaa lakini hatimaye atashindwa kung'ara. Kwa nini nasema hivyo? Bilal hawezi kujiuza kwa Watanzania bila kufarakana na CCM. Idadi kubwa ya Watanzania hata vijijini hivi leo wanaelewa kuwa ufisadi ndilo tatizo kubwa lililotufikisha hapa tulipo. Bilal atawashawishije hawa Watanzania kama kweli atapambana na ufisadi? Kumbuka Mwalimu Nyerere alituasa kuwa kiongozi akisema anapinga ufisadi hata ukimwangalia usoni lazima ionekane kweli kwamba huyu anapinga ufisadi. Bilal ataanzia wapi? Hiyo ndiyo changamoto ya Bilal na yeyote yule atakayesimama ndani ya CCM kutaka ridhaa ya Watanzania kuwaongoza kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
 


Yawezekana kabisa kuwa Rais Kikwete ameamua kuchukua uamuzi huo wa kumuandaa na kumtangaza Bilali awe mgombea Urais wa CCM 2015 ili kukinusuru chama chake CCM kutokana na makundi ambayo itake isitake 2015 yatakimega CCM kabisa kwa asilia 100%. Huenda akawa na sababu nyingi lakini chache ni zifuatazo:


  • Safari hii ni zamu ya Wazanzibar kutoa Rais. Kumbuka hii ni hoja rahisi kama walivyoamua kuwa safari hii Spika ni Mwanamke na hivyo kumweka Sita pembeni. K
​

Suala la kurithishana urais kati ya bara na visiwani sio la kikatiba, ni utamaduni unaozingatia zaidi ustaarabu. Moja ya matatizo makubwa katika kuhalalisha hoja hii - kwamba sasa ni zamu ya upande wa pili wa muungano, inaweza kuzua hoja ya kuhalalisha kwamba sasa ni zamu ya upande mwingine wa imani ya kidini. Inabidi wahusika wawe makini sana katika kulijengea hoja suala hili. Lakini suala la zamu ya mwanamke kwa kweli ni vigumu sana kulikwepa, na ndio maana hata katika uspika halikukwepeka. Iwapo CCM wanataka kushinda urais 2015, moja ya gimmicks wanazoweza fanikiwa nazo ni suala la kumsimamisha mwanamke Urais. Asilimia karibia 70% ya wapiga kura ni wanawake, kwahiyo hili watavutiwa nalo sana, bila ya kujali kama kweli mgombea huyo ana uwezo au zero.

  • Dk. Bilali hana Makundi na amekuwepo katika siasa za Bara na Visiwani na anakubalika (Of course ziara za sasa zimam-promote)
​
Hii sio sahihi. Mheshimiwa huyu amewekwa pale kwa manufaa ya kundi husika, ingawa ilikuja gundulika hivyo baadae sana.


​
  • Dk. Bilali amekuwa Makamu wa Rais na anakubalika kama Presidential Material
​

Kama alivyohoji Jasusi, hii inatokana na utafiti gani? Mimi binafsi simwoni kama ana uwezo huo, ingawa kabla ya kuwa makamo wa Rais nilimwona kama ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa uongozi. Huu ni mtazamo wangu binafsi, na nasimama kupingwa kwa hili.

  • Ili kuzima chokochoko za Wazanzibari kuua Muungano dawa ni kumweka Mzanzibar. JK hawezi kuruhusu Zanzibar iwe Nchi au Dola (Historically na Kikatiba).
​

Kama assumption ni kwamba wenye kuweza kuua muungano ni wazanzibari pekee, na uwezo huo watanganyika hawana, hoja hii inasimama.


  • JK hataki aonekane kaivuruga Nchi ndo maana kwa mambo yote makubwa nchi hii kaamua bora tu akae kimya kuliko kusema. La kuhusu katiba ameona bora atofautiane na Chama chake ili kuacha Lergacy na kuleta utengamao katika Nchi.

Inawezekana una hoja nzuri lakini ingeboreshwa zaidi na experiences nyingine ndani na nje ya Tanzania kwamba 'ukimya' is a strategy that can work.

Ni nini maoni yako binafsi kuhusu Dk. Bilali na harakati zake za kuzunguka mikoani na wilayani in connection na mbio za Urais 2015? Je yawezekana akawa ni Chaguo la JK?
Inawezekana kuna connection,lakini binafsi sioni zaidi ya kuwa ni matokeo ya kukosa kazi kwani cheo cha makamu wa rais huko nyuma kilikuwa kinabebwa na uwaziri mkuu and/or urais wa zanzibar. Bilal ni makamo wa kwanza wa rais per se, ambae anatokana na tume ya Bomani kupendekeza Tanzania kuiga mfano wa Marekani wa running mate, ambae hata nchi marekani anaonekana anapwaya na kuna baadhi ya watu wanajenga hoja kwamba ni ubadhirifu tu wa kodi wa wananchi kuwa na nafasi kama hiyo.

Naomba nikurudishie swali mleta mada - ikizingatiwa sasa kwamba kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar 2010, Zanzibar ni moja ya nchi inayounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na sio tena kama zamani ilipokuwa inatambulika kwamba zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Je, uhusiano wa kikazi baina ya Hawa makamo watatu wa Urais yani - Maalim Seif, Balozi Seif Iddi na Dr. Bilal ni wa namna gani?
 
Unaweza kuwa sahihi kwa manufaa ya taifa na kwa fikra nje ya Boksi. Bilal si chaguo sahihi kwa CCMau Nchi

Lakini "Ki CCM"( Makundi) na kujaribu kuunga unga muungano amabao siku zinavyozid kwenda nyufa zinazidi Huyo mzee ndiyo anaweza kuwa best option ya CCM kutusogeza tu . Sio kwamba ni option ya kutatu matatizo ya UCHUMI UFISADI, Mungano etc

Hata fanya chochete kuhusu Muungano lakini uwepo wake ni sawa na Vidonge ARV kwa mgonjwa wa ukimwi. Kuchelewesha madhara ya tatizo....

Zaidi ya muungano Bilal inaweza kuwa option nzuri kwa ksingizo cha zamu "yao" lakini lengo kuu ni kumpiga chini EL ambaye wameshindwa na hawana nguvu za kumkatalia kavu kavu.

So mpaka hapo nadhani bilal ni chaguo bora kufunika/kufukia matatizo halisi na muda uende lakini sio chaguo bor kutatua na kushghulikia matatzio. iwe ni ya muungano au mengineyo.


Sana sana atachofanya kama akiwa rais atachemsha zaidi ya Kikwete. Hiyo itatufanyat umukbuke JK kwa sifa kama tulivyosahau mabaya ya Mkapa sababu ya underpefromnce ya ya JK..... ....

Huo ni mtazamo wangu.

Mkuu hapo penye Red hasa pana mantiki.

Lakini pia EL & RA kama kweli inadaiwa kuwa walimweka Bilali, then ina maana wanaweza "Wakamkubali" kiushikaji. may be EL anaweza kuwa VP. Then Bilali baada ya Mwaka akaachia ngazi sababu ya Uzee au Afya. hapo RL akashika Nchi.

Ndo hapo tutajua EL ni noma na unstoppable. kama si hivyo may be Bilali anweza kudumu kipindi kimoja.

Alternatively Bilali akiwa Rais anaweza akampa power kubwa EL za kiutendaji yeye "akajipa likizo". EL ataonyesha cheche zitakazomfanya Watanzania wamkubali kabla hajawa Rais.

Sisemi kuwa itakuwa hivyo bali hizi ni possible Scenarios.
 
Mkuu, maoni yangu ni kwamba kweli Bilal analo jukwaa lakini hatimaye atashindwa kung'ara. Kwa nini nasema hivyo? Bilal hawezi kujiuza kwa Watanzania bila kufarakana na CCM. Idadi kubwa ya Watanzania hata vijijini hivi leo wanaelewa kuwa ufisadi ndilo tatizo kubwa lililotufikisha hapa tulipo. Bilal atawashawishije hawa Watanzania kama kweli atapambana na ufisadi? Kumbuka Mwalimu Nyerere alituasa kuwa kiongozi akisema anapinga ufisadi hata ukimwangalia usoni lazima ionekane kweli kwamba huyu anapinga ufisadi. Bilal ataanzia wapi? Hiyo ndiyo changamoto ya Bilal na yeyote yule atakayesimama ndani ya CCM kutaka ridhaa ya Watanzania kuwaongoza kwa kipindi kingine cha miaka mitano.


Kiongizi Jasusi,

Kilichonifanya nilete hoja hii hapa ni kasi ya bilali huko vijijini, wilayani na mikoani ambapo feedback za media, picha nk zinaonyesha kuwa anagain umaarufu. Sasa akiendelea hivyo for next 3 years na hana record mbaya, basi bidhaa ya kichina si ajabu kuonekana ni bidhaa bora.
 
Ndo hapo tutajua EL ni noma na unstoppable. kama si hivyo may be Bilali anweza kudumu kipindi kimoja.

Hapa una maana noma na unstoppable from what point of view: umma wa watanzania au vikao vya maamuzi vya CCM? Ni muhimu kujadili wagombea mbalimbali na nguvu zao in a holistic way kwani nadhani hata wao wanajipima hivyo.
 
Mwawado,
Asante kwa ushauri mkuu. Ni kweli upinzani unapaswa kuwa makini wasimwachie jukwaa la bure makamu wetu wa rais akizunguka nchi na kujiuza. Lakini turufu ambayo upinzani ulio nayo hivi sasa, hasa Chadema, ni hii kensa ya ufisadi na jinsi inavyoendelea kuitafuna nchi na kutuacha maskini wakati tuna maliasili nyingi.
 
Kiongizi Jasusi,

Kilichonifanya nilete hoja hii hapa ni kasi ya bilali huko vijijini, wilayani na mikoani ambapo feedback za media, picha nk zinaonyesha kuwa anagain umaarufu. Sasa akiendelea hivyo for next 3 years na hana record mbaya, basi bidhaa ya kichina si ajabu kuonekana ni bidhaa bora.
Na mimi nimeshaona hivyo na kwa kweli mada yako imesaidia kunifungua zaidi macho na akili. Nilikuwa najiuliza hizi safari za mara kwa mara za Bilal mikoani zina tija gani? Mara leo anakagua miradi, mara anapokea kadi ya mwana Chadema aliyeamua kurudi nyumbani CCM. Nina hakika ujumbe kwa upinzani umeshafika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom