DK. Bilali Chaguo la JK Kumrithi 2015?

Mwandosya wameshammaliza.

Professor Mwandosya alibainika kuwa na "Bone Marrow Cancer" kabla hata ya Dr. Mwakyembe lakini pengine ili kuepuka mifarakano isiyo na ulazima, familia hii imeamua kumwachia mungu kila kitu. Je suala la Mwakyembe na MWandosya ni coincidence? Sipo hapa kuzungumzia afya za watu au taarifa za familia za watu, lakini ipo siku ukweli utakuja kusimama.
 
Mkuu Mchambuzi, nimekusoma.

Ngoja nijaribu kutoa ufafanuzi:

Suala la kurithishana urais kati ya bara na visiwani sio la kikatiba, ni utamaduni unaozingatia zaidi ustaarabu. Moja ya matatizo makubwa katika kuhalalisha hoja hii - kwamba sasa ni zamu ya upande wa pili wa muungano, inaweza kuzua hoja ya kuhalalisha kwamba sasa ni zamu ya upande mwingine wa imani ya kidini. Inabidi wahusika wawe makini sana katika kulijengea hoja suala hili. Lakini suala la zamu ya mwanamke kwa kweli ni vigumu sana kulikwepa, na ndio maana hata katika uspika halikukwepeka. Iwapo CCM wanataka kushinda urais 2015, moja ya gimmicks wanazoweza fanikiwa nazo ni suala la kumsimamisha mwanamke Urais. Asilimia karibia 70% ya wapiga kura ni wanawake, kwahiyo hili watavutiwa nalo sana, bila ya kujali kama kweli mgombea huyo ana uwezo au zero.


Mkuu katika hili na kutokana na makundi Bilali anweza ku-prevail. Kushinda Bilali kuwa Rais bado inaweza kuwa strategy ya JK kumpa EL kijiti ila shida afanyaje watu wasigundue? Kama kuna argument kuwa Bilali aliwekwa na mafisadi ni rahisi pia kumtumia yeye ashinde Urais na baadaye aondolewe ili Mafisadi wachukue nafasi hiyo.

Kuhusu candidate Mwanamke, si kwa Tanzania ya sasa. Charity begins at home: wabunge wangapi wanashinda majimboni? Kwa nini hawachaguliwi?

Bi kiroboto hakupewa kwa sababu ni hoja ya zamu ya wanawake ila Mafisadi walitaka kumzima SS aka 6.

katika sisa za Watanzania no matter kama wapiga kura wengi ni Wanawake haina maana watawapigia kura jinsia yao, tungewaona majimboni. Unamkumbuka Anna Senkoro aligombea Urais 2005 kupitia TADEA? What happened?
​

Hii sio sahihi. Mheshimiwa huyu amewekwa pale kwa manufaa ya kundi husika, ingawa ilikuja gundulika hivyo baadae sana.

Nikifanya reference ya uzi wa "Hutaki Unaacha" wa hapa JF hili lina mshiko na nalikubali na ndo maana nasema bado mafisadi wanaweza kumtumia kama stepping stone maana ni mtu wao na hii itaondoa makundi.

​

Kama alivyohoji Jasusi, hii inatokana na utafiti gani? Mimi binafsi simwoni kama ana uwezo huo, ingawa kabla ya kuwa makamo wa Rais nilimwona kama ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa uongozi. Huu ni mtazamo wangu binafsi, na nasimama kupingwa kwa hili.

Mkuu, suala la siasa za Tanzania halina utafiti wala uzoefu. Zote ni kama Hekaya za Abunuasi. Ukiacha Mwalimu JK Nyerere marafiki wote waliofuata hawakutegemewa na Watanzania. Jk alitegemewa sana na alikuwa chaguo la wengi ila sasa amevurunda. katika hakli hii hakuna jipya juu ya Bilali kuwa Rais. jamaa anakata mbuga sasa hivi kila kona ya Nchi. In the next 3 years akifanya hivyo, bila ya shaka atakuwa amejiongezea umaarufu.


Kama assumption ni kwamba wenye kuweza kuua muungano ni wazanzibari pekee, na uwezo huo watanganyika hawana, hoja hii inasimama.


Mkuu, kwa hili la Muungano walioshika bango ni Wazanzibari. Kwa wa-TZ who cares? Ila kwa Mkazi wa Magogoni hii ni issue lazima ailinde kwa nguvu zote. Dont ask me why? LOL. Of course mienendo yote ya Wazanzibar ina mwelekeo wa kuvunja Muungano.

Inawezekana una hoja nzuri lakini ingeboreshwa zaidi na experiences nyingine ndani na nje ya Tanzania kwamba 'ukimya' is a strategy that can work.

Kamanda huko nyuma JK alikuwa Vocal kuyaongelea masuala ya Nchi. Sasa hivi hotuba zake nyingi zimejaa tende na harua. Mfano, uliona alivyomchachafya Mgaya wa TUCTA na Hotuba yake ya Mbayuwayu. Iweje issue nyeti ya Mgomo wa Daktari akawa Kimya? Kuna matukio mengine makubwa mengi yuko Kimya. Uzuri wa watanzania ukikaa kimya wanaona poa tu na JK analijua hilo kuliko ukisema kisha waanze kukuchambua. So, this is his own experience.

Inawezekana kuna connection,lakini binafsi sioni zaidi ya kuwa ni matokeo ya kukosa kazi kwani cheo cha makamu wa rais huko nyuma kilikuwa kinabebwa na uwaziri mkuu and/or urais wa zanzibar. Bilal ni makamo wa kwanza wa rais per se, ambae anatokana na tume ya Bomani kupendekeza Tanzania kuiga mfano wa Marekani wa running mate, ambae hata nchi marekani anaonekana anapwaya na kuna baadhi ya watu wanajenga hoja kwamba ni ubadhirifu tu wa kodi wa wananchi kuwa na nafasi kama hiyo.

Hoja hii ina mshiko ingawa haiondoi uwezekano wa mtu kutake advantage ya nafasi hiyo.

Naomba nikurudishie swali mleta mada - ikizingatiwa sasa kwamba kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar 2010, Zanzibar ni moja ya nchi inayounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na sio tena kama zamani ilipokuwa inatambulika kwamba zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Je, uhusiano wa kikazi baina ya Hawa makamo watatu wa Urais yani - Maalim Seif, Balozi Seif Iddi na Dr. Bilal ni wa namna gani?

Mkuu, katiba ya Zanzibari ni fake na wao wanajua. Sibiri mambo yatulie lije suala la katiba mpya au Mahakama kutoa uamuzi. Hili ni moja ya mambo makubwa ambayo JK ameyakalia kimya. Nchi ili iwe dola inatakiwa iwe na sovernity, jeshi na kutambuliwa kimataifa kama Nchi. So far Zanzibar Si Nchi ya Kimataifa. Ila ni Nchi ndani ya TZ. Kudadadeki nisije pigwa mawe.
 
Superman said:
Mwaka 1988 aliteuliwa kuwa mkuu wa Kitivo cha Sayansi cha Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam na kuendelea katika wadhifa huo hadi mwaka 1990 alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu katika Wizara mpya ya wakati huo ya Sayansi Teknolojia na Elimu ya Juu mwaka 1990-1995.
Superman said:
Akiwa Katibu mkuu alishiriki katika kuanzisha utaratibu wa kuchangia gharama za elimu ya juu na kuanzisha utaratibu wa mikopo. Pia wizara hiyo ilianzisha Chuo Kikuu Huria , pamoja na kuanzisha udhibiti wa vyuo vya elimu ya juu ( accreditation council).



Superman,

..wakati wake pale Sayansi na Teknolojia rushwa,udini,na ngono, vilitamalaki.

..pia aliunda genge lake la waZNZ kuminya nafasi za scholarship kwa wa-Tanganyika.

..I hope amebadilika, lakini huyu akipewa nafasi ya Uraisi na akaongoza kwa mentality aliyokuwa nayo pale Sayansi na Teknolojia, basi msije mkashangaa nchi ikisambaratika.
 
Hapa una maana noma na unstoppable from what point of view: umma wa watanzania au vikao vya maamuzi vya CCM? Ni muhimu kujadili wagombea mbalimbali na nguvu zao in a holistic way kwani nadhani hata wao wanajipima hivyo.

Mkuu what is Vikao vya CCM vya maauzi? Waliamua kujivua gamba wamejivua? why?

Uma wa Watanzania upi? Wenye dhiki ya maisha mabo unaweza kuwadanganya kwa vitu vidogo wakati wa Uchaguzi wakawapigia kura mafisadi? sina haja ya mifano maana ni mingi na iko wazi. hapa yunazungumzia nguvu za ufisadi ambazo CCM na serikali yake zimeshindwa kuzuia. unfortunately hii ni dalili ya Chama na Dola linaloanguka. Its a matter of time kabla kamba haijakatia pabovu.
 


Superman,

..wakati wake pale Sayansi na Teknolojia rushwa,udini,na ngono, vilitamalaki.

..pia aliunda genge lake la waZNZ kuminya nafasi za scholarship kwa wa-Tanganyika.

..I hope amebadilika, lakini huyu akipewa nafasi ya Uraisi na akaongoza kwa mentality aliyokuwa nayo pale Sayansi na Teknolojia, basi msije mkashangaa nchi ikisambaratika.
jokaKuu,'
Nahisi kusambaratika kwa nchi ni the least on Kikwete's priorities or cares. Nahisi hivi sasa anatafuta mtu atakayemlinda atakapotoka mamlakani kwa sababu amefanya madudu mengi kuliko aliyoyafanya Mkapa katika kipindi cha pili cha utawala wake. Priority ya hivi sasa ya CCM na viongozi wake ni kuendelea kushikilia dola kwa sababu wanatambua kwamba dola ikishaanguka mikononi mwa wapinzani basi their days of reckoning will be here. Kwa hiyo hizi tetesi za Migiro, na sasa Bilal kushika nafasi ya Kikwete zina fall under that category. Kama alivyosema Mwawado, it is up to the opposition, especially Chadema, to follow up these trips of the VP
 


Superman,

..wakati wake pale Sayansi na Teknolojia rushwa,udini,na ngono, vilitamalaki.

..pia aliunda genge lake la waZNZ kuminya nafasi za scholarship kwa wa-Tanganyika.

..I hope amebadilika, lakini huyu akipewa nafasi ya Uraisi na akaongoza kwa mentality aliyokuwa nayo pale Sayansi na Teknolojia, basi msije mkashangaa nchi ikisambaratika.

Mkuu kumbuka pale Sayansi waziri wake alikuwa Mr. Clean na alikuja kutuongoza kwa miaka 10.
 
uraisi wa hii nchi si wa kupeana kama pipi
kwa nini tuwape wanzanzibar?kwani huku tanganyika tumekosa watu wa kuongoza?
kwa nini watanganyika hawatawali zanzibar?
kuleta wanzanzibar huku bara wanafanya nafasi za kazi ziwe chache,hawa wote ni wa kuondoa hii nchi
 
Professor Mwandosya alibainika kuwa na "Bone Marrow Cancer" kabla hata ya Dr. Mwakyembe lakini pengine ili kuepuka mifarakano isiyo na ulazima, familia hii imeamua kumwachia mungu kila kitu. Je suala la Mwakyembe na MWandosya ni coincidence? Sipo hapa kuzungumzia afya za watu au taarifa za familia za watu, lakini ipo siku ukweli utakuja kusimama.

Mkuu,

Kuna mada moja hapa JF inazungumzia vifo vya baadhi ya Viongozi. najua hakuna proof zozote ila mazingira ya walivyoumwa au kufa vina maswali mengi kuliko majibu.

Mwandosya, Salim Ahmed Salim; JK; Sumaye na Kigoda (Kama sijakosea) were among top contstants within CCM 2005. Mwandosya alongside Salim walijkuwa the finalist. Definetely Mwandosya na Salim could have been the next possible candidates kama wangependa.

Lakini Salim siasa za maji taka haziwezi so kaamua kupumzika. Mwandosya ilikuwa ndo aanze kujijenda akisaidiana na home boy Harrison. lakini sasa atajijengaje na Wanyakyusa hawa wote wagonjwa?

Wote hao wawili walitajwa katika taarifa ya Mwakyembe Police kuwa wamekuwa targeted kuuwawa kabla hata Mwandosya hajaanza kuumwa. Ni nini kimetokea? Mimi na wewe hatujui. Ila time will tell. kam si hapa basi siku ya ile hukumu kuu.
 
Mkuu kumbuka pale Sayansi waziri wake alikuwa Mr. Clean na alikuja kutuongoza kwa miaka 10.

Kakalende,

..Mr.Clean alipata kwasababu ya ukaribu wake na Nyerere.

..Mr.Clean hakuchanguliwa kutokana na performance yake pale Sayansi na Teknolojia.

..pia naweza kwenda mbali na kusema kwamba wana CCM wa waliokuwa wakimpigia kampeni Mr.Clean walikuwa wamechoshwa na utendaji wa Mzee Mwinyi na upendeleo wake wa waziwazi kwa Wazanzibari.
 


Superman,

..wakati wake pale Sayansi na Teknolojia rushwa,udini,na ngono, vilitamalaki.

..pia aliunda genge lake la waZNZ kuminya nafasi za scholarship kwa wa-Tanganyika.

..I hope amebadilika, lakini huyu akipewa nafasi ya Uraisi na akaongoza kwa mentality aliyokuwa nayo pale Sayansi na Teknolojia, basi msije mkashangaa nchi ikisambaratika.

Mkuu maneno mazito sana hayo.

Unaweza ukamwaga data kidogo nasi tupate kujua?
 
Bilal awe Rais?!!! Labda kama tume ya taifa ya UCHAFUZI aahh namaanisha UCHAGUZI itaongozwa na Prof. Sheikh Basalleh
 


Kudadadeki nisije pigwa mawe.

Tangia lini superman akapigwa mawe? Au ndio jina lako halisi.

Nimekusoma. Kimsingi hoja yako kuhusu Bilal ina mashiko, hasa iwapo suala la kuachia Urais baada ya muhula wake mmoja pia itazingatiwa, hivyo makamo wa Rais kuchukua nchi.

Suala la Anna Senkoro kidogo lina utofauti na Dr. Migiro, huyu anatokea CCM lakini kubwa zaidi ni kwamba profile yake ni kubwa sana kiasi cha kuweza kufunika kampeni za upinzani, kwani kasi ya kumrushia madongo mgombea mwanamke itaweza kuwa counter productive. Kwa kifupi, Migiro atawachanganya sana wapinzani hata kama eventually hatoshinda.

Kuhusu suala la muungano kwamba wabara do not care, ni kweli, lakini sidhani kama suala la serikali tatu linakwepeka, do you think so? Katika makosa ya Mwalimu kimantiki, lilikuwa suala hili la serikali mbili vis-a-vis tatu. Serikali tatu haikwepeki, na hii haita-ua muungano ila itaupunguzia nguvu yake kwa kiasi kikubwa sana, hivyo kutoa mwanya kwa foreign capital to exploit kule watakavyo. Na kama unavyojua, sikuhizi hakuna political diplomacy, hiyo ilikuwa enzi za Nyerere. Sikuhizi ni economic diplomacy, na hata mabalozi wetu huko nje hiyo ndio shughuli yao ya msingi.
 
Mkuu,

Kuna mada moja hapa JF inazungumzia vifo vya baadhi ya Viongozi. najua hakuna proof zozote ila mazingira ya walivyoumwa au kufa vina maswali mengi kuliko majibu.

Mwandosya, Salim Ahmed Salim; JK; Sumaye na Kigoda (Kama sijakosea) were among top contstants within CCM 2005. Mwandosya alongside Salim walijkuwa the finalist. Definetely Mwandosya na Salim could have been the next possible candidates kama wangependa.

Lakini Salim siasa za maji taka haziwezi so kaamua kupumzika. Mwandosya ilikuwa ndo aanze kujijenda akisaidiana na home boy Harrison. lakini sasa atajijengaje na Wanyakyusa hawa wote wagonjwa?

Wote hao wawili walitajwa katika taarifa ya Mwakyembe Police kuwa wamekuwa targeted kuuwawa kabla hata Mwandosya hajaanza kuumwa. Ni nini kimetokea? Mimi na wewe hatujui. Ila time will tell. kam si hapa basi siku ya ile hukumu kuu.

Upo sahihi. Mwandosya aligundulika na Bone Marrow Cancer, lakini yeye inaelekea hataki kuingiza ugonjwa wake katika siasa. Lakini ripoti ya Madaktari mwaka jana India kuhusu Mwandosya ni kwamba amekutwa na Bone Marrow Cancer. Lakini kama unavyosema, time will tell, and until then, tuombe uzima.
 
Mkuu hapo penye Red hasa pana mantiki.

Lakini pia EL & RA kama kweli inadaiwa kuwa walimweka Bilali, then ina maana wanaweza "Wakamkubali" kiushikaji. may be EL anaweza kuwa VP. Then Bilali baada ya Mwaka akaachia ngazi sababu ya Uzee au Afya. hapo RL akashika Nchi.

Ndo hapo tutajua EL ni noma na unstoppable. kama si hivyo may be Bilali anweza kudumu kipindi kimoja.

Alternatively Bilali akiwa Rais anaweza akampa power kubwa EL za kiutendaji yeye "akajipa likizo". EL ataonyesha cheche zitakazomfanya Watanzania wamkubali kabla hajawa Rais.

Sisemi kuwa itakuwa hivyo bali hizi ni possible Scenarios.

Hapa kwenye red sasa naelewa zaidi hii scenario na probability yake naona inaongezeka maana mlango wa EL kuingia directly tena unaonekana kmewekewa kauzibe. So kumbe watu wamejipanaga inwezekana kuna Plan B mtu arudi kwa mlango wa nyuma .......
 
Tangia lini superman akapigwa mawe? Au ndio jina lako halisi.

Nimekusoma. Kimsingi hoja yako kuhusu Bilal ina mashiko, hasa iwapo suala la kuachia Urais baada ya muhula wake mmoja pia itazingatiwa, hivyo makamo wa Rais kuchukua nchi.

Suala la Anna Senkoro kidogo lina utofauti na Dr. Migiro, huyu anatokea CCM lakini kubwa zaidi ni kwamba profile yake ni kubwa sana kiasi cha kuweza kufunika kampeni za upinzani, kwani kasi ya kumrushia madongo mgombea mwanamke itaweza kuwa counter productive. Kwa kifupi, Migiro atawachanganya sana wapinzani hata kama eventually hatoshinda.

Kuhusu suala la muungano kwamba wabara do not care, ni kweli, lakini sidhani kama suala la serikali tatu linakwepeka, do you think so? Katika makosa ya Mwalimu kimantiki, lilikuwa suala hili la serikali mbili vis-a-vis tatu. Serikali tatu haikwepeki, na hii haita-ua muungano ila itaupunguzia nguvu yake kwa kiasi kikubwa sana, hivyo kutoa mwanya kwa foreign capital to exploit kule watakavyo. Na kama unavyojua, sikuhizi hakuna political diplomacy, hiyo ilikuwa enzi za Nyerere. Sikuhizi ni economic diplomacy, na hata mabalozi wetu huko nje hiyo ndio shughuli yao ya msingi.

Mchambuzi,

..loyalty ya waZNZ kwa Tanzania ni ya mashaka-mashaka sana. matatizo yetu ktk muungano yanaanzia hapo.

..pia hili suala la kuachiana ni tete kwelikweli. kumbukeni jinsi Mzee Mwinyi alivyompiga bao Salim Salim na kuchukua Uraisi wa muungano.

..sasa mnapozungumzia mafisadi wamuweke Bilali wakitegemea ataongoza na baadaye aachie ngazi kuwapisha hamuoni kwamba it is such a big leap of faith? what if Bilali atachukua uraisi na ku-consolidate his powerbase?
 
Ni maneno ya Ukweli Ndugu Yangu Superman.Nami nimesikia kutoka vyanzo vya Uhakika kuwa Dr Bilal anatayarishwa kuwa Mgombea wa Urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.Dr.Bilal ni mzoefu wa siasa za Tanzania Bara kuliko Visiwani ukichukulia kuwa amewahi kufanya kazi kwa karibu na marais wote toka Mwalimu mpaka sasa Kikwete pia ana ushawishi wa kutosha Zanzibar,Wale wafuatiliaji wa siasa za huko kumbukeni kinyanga'nyiro cha Urais kati ya Rais mstaafu wa Zanzibar Mzee Aman karume na Dr Bilal mpaka kumuondoa Dr Bilal kugombea nafasi hiyo kwa kupitia vikao vya Chama,kumbukeni pia Uchaguzi wa Rais wa sasa wa Zanzibar,Dr Bilal alikuwa na ushawishi mkubwa,na pengine kapewa nafasi hii ya Umakamu wa Bara ili kutuliza lile vurugu lililokuwepo alipoenguliwa na kumpisha Rais wa sasa Ali Mohamed Shein.

Dr Bilal ni msomi na mzoefu wa Utendaji kuliko siasa za Majukwaani,kinachoniogopesha Mimi ni Afya yake na umri ambao unaonekana hautoweza kuhimili mikikimikiki ya Kampeni na baadaye Uongozi katika Taifa hili ambalo linahitaji Kiongozi Makini na mwenye Afya isiyo na migogoro.CCM wanatumia nafasi hii kumtembeza Dr kila pande ya Nchi ili apate popularity,kwa lolote litakalokuwa kutakuwa na mgawanyiko mkubwa ndani ya Chama Tawala.Kwa sababu jinsi hali ilivyo sasa,kila mwanasiasa anajiona anaweza kuikwaa kazi hiyo......"Kama kaweza Kikwete,kwa hakika hakuna atakayeshindwa!".Katika list ndefu kuna akina Membe,Lowassa,Nchimbi,Magufuri na hata Mama Migiro.

Vyama vya Upinzani viangalie kwa makini nyendo za huyu Mzee,kwani siasa ya kweli inaanza katika ushindani wa kujadili Hoja za kumjenga Mtanzania.......Wapambane nae kihoja nao wapite mikoani na kila pande anayopita huyu Mzee kuzima Hoja zake na kuwapa wananchi nafasi ya kuona upande wa pili wa serikali hii dhalimu!

Mwawado

Naomba kukuuliza, huyu Bilali amefanya kazi gani na mwalimu? hebu fafanunua?
 
Huyu bilali si tuliwahi kuambiana na kuaminishana hapa kwamba amewekwa pale na lowassa na rostam ili ampishe shein awe rais kule ikiwa na maandalizi ya lowassa kumrithi jk kwa kuwa shein alikua tishio pekee kwa lowassa kutokana na uzoefu ambao angekuwa nao kama angeendelea kuwa makamu wa rais wa tanzania kwa muhura wa tatu?kweli humu ukiamini kila linalolopokwa unaweza kuchangikiwa sana.
 
Mchambuzi,

..sasa mnapozungumzia mafisadi wamuweke Bilali wakitegemea ataongoza na baadaye aachie ngazi kuwapisha hamuoni kwamba it is such a big leap of faith? what if Bilali atachukua uraisi na ku-consolidate his powerbase?

Ni sahihi, kwani Bilali ana nguvu sana katika siasa za CCM zanzibar na ni nguvu hiyo ndio iliwavutia wahusika na washirika wake wa sasa wa upande wa bara; Vinginevyo kama nguvu yake ingekuwa ni matokeo ya upishi wa washirika wake wa bara, hapo tungesema kwamba akiwa rais haitakuwa rahisi kwake kufurukuta.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom