Tunaomba maelezo kuhusu Nikah Muttah quran inasemaje?
Naam mkuu....
Je Nikah Muttah ni nini?
Hii ni ndoa ya mkataba wa Muda maalum,ambapo mwanaume na mwanamke wanakubaliana kuwa katika ndoa Kwa kipindi Fulani,mfano labda miezi sita (6) hlf ikitimia na ndoa inakuwa imekwisha na hakuna talaka,na muoaji anatoa mahari kama kawaida.
Baada ya muda wa mkataba kuisha basi mwanamke ataangalia kipindi kimoja cha mzunguko wa hedhi kama ana mimba au laa!
Kama ulivyotaka kujua je Qur'an inasemaje kuhusu Muttah, Aya ifuatayo 4:24 Kwa mujibu wa wanazuoni wengi wanasema inazungumzia Muttah:
"NA WANAWAKE wenye waume, isipo kuwa walio milikiwa na mikono yenu ya kulia. Ndiyo Sharia ya Mwenyezi Mungu juu yenu. Na mmehalilishiwa wasio kuwa hao, mtafute kwa mali yenu kwa kuowa pasina kuzini. Kama mnavyo starehe nao, basi wapeni mahari yao kwa kuwa ni waajibu. Wala hapana lawama juu yenu kwa mtakacho kubaliana baada ya kutimiza waajibu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua na Mwenye hikima."
Katika Aya hii mistari mitatu ya mwanzo ni muendelezo wa Aya ya 23 ambayo inazungumzia wanawake ambao ni haramu kuwaoa na ikamalizia hapo na wanawake wenye waume zao tayar,nimeamua kulisema hili ili msomaji asipate taabu kuelewa.
Aina ya ndoa hii inasemwa ilitumika mwanzo kabisa kipindi kile Uislamu unaenezwa,lakini baadae ndoa hii ilikuja kuharamishwa na Sheria au ilikuja kufutwa kabisa,,,,lakini kuna mijadala mbali mbali ya wanazuoni juu ya uhalali WA kuwepo Kwa ndoa au laa! Wengine wanasema ndoa hii hazikuwepo kabisa na wengine wanasema ndoa ilikuwepo awali na ikaja kufutwa na Sheria,kwahiyo kuna malumbano ya namna hiyo,,,na wengine wanasema Aya hiyo hapo juu haikuzungumzia kuhusiana na Nikah Al Muttah.
Lakini Kwa vyovyote itakavyokuwa lengo kubwa lilikuwa ni kuzuia Zinaa,kama unavyojua Mwenyezi Mungu hapendi kabisa zinaa,kwahiyo inasemwa ndio maana ndoa hizo zilikuwepo kipindi ambapo waislamu walienda hapa na Kule katika Vita na kutangaza Dini,kwahiyo walioa Kwa Mda Fulani ili kuepuka kufanya zinaa.
Nadhani maelezo hayo Kwa uchache yanatosha kuhusiana na Nikah Al Muttah
Shukrani.