Aya gani katika quran imefuta hiyo ndoa?
Quran si imeshushwa na mwenyezi Mungu ama kuna baadhi ya mambo katika quran yanaruhusiwa kufutwa?
Mkuu naomba kujua Kwanza
Aya gani katika quran imefuta hiyo ndoa?
Quran si imeshushwa na mwenyezi Mungu ama kuna baadhi ya mambo katika quran yanaruhusiwa kufutwa?
Wakati najibu hoja yako ya msingi nilikwambia hiyo Aya 4:24 bado wanazuoni wako kwenye mijadala mizito juu ya uhalali wake kuhusiana na Nikah Al Muttah,,,kuna ambao wanasema inazungumzia Aina ya ndoa hiyo na wengine wanasema inazungumzia Ile ndoa halisi au ya Mda mrefu....
Sikutaka kukupa details nyingi kwakuwa najua zitakuchanganya,,,,ndio maana nilikujibu Kwa uchache.
Mfano kuna mkanganyiko mkubwa Sana juu ya kudhibitika kwake au masharti yake,mfano katika ndoa ya kawaida tuliyo izoea ni lazima wawepo mashahidi na vile vile ndugu WA mke lazima watoe idhini Kwa ndoa hiyo kufungwa,Kwa Jina lingine awepo walii wake lkn ndoa hii haina mashahidi wala idhini toka Kwa ndugu WA mke,yaani mnakutana Tu wewe na mwanamke mnatamkiana kuwa mmefunga ndoa na tayar ndoa imepita.
Kwahiyo kuna wanazuoni/wasomi wa kiislamu wanasema hiyo ni Sawa na zinaa Tu!
Na kumbuka pia wanazuoni wote hawajakubaliana kama hiyo Aya tajwa kuwa je kweli inazungumzia Muttah au ndoa Ile ya Mda mrefu? Utata unakuja kwenye maneno ambayo yametumika katika hiyo Aya kuwa na maana zaidi ya moja.
Lau kuwa ingekuwa wazi kuwa ayah hiyo ni kweli inazungumzia Muttah na baadae kufutwa basi lazima ingekuja Aya nyingine ambayo ingekuwa wazi kufuta swala Hilo.
Nami nilikujibu kutokana na mitazamo na maoni ya wanazuoni.
Kwa kifupi uhalali WA hiyo ndoa ina UTATA!
Shukrani.