ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,597
- 21,642
Naam mkuu,,,,mwanaume akimkosea mwanamke Napo kuna namna ya kutoa suluhisho Kwa mujibu wa Qur'an.Na mwanaume akimkosea mwanamke Qur'an inasemaje?
Katika 4:128 Aya inasema hivi:
"Na mwanamke akichelea kutupwa au kutojaliwa na mumewe, basi si vibaya kwao wakisikizana kwa suluhu. Na suluhu ni bora. Na nafsi zimewekewa machoni mwake tamaa na choyo. Na mkifanya wema na mkamchamngu basi hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za yote mnayo yatenda."
kwahiyo kama Aya ilivyojieleza hapo juu mwanamke akiwa hatendewi haki na mumewe basi hawana budi kutafuta suluhisho na kuyaweka mambo Sawa,,,lakini Lau suluhisho limeshindikana sasa itakuja hatua ya huyo mwanamke kwenda Kwa Kadhi au Kiongozi wa kidini ambaye Kwa mujibu wa Sheria ana uwezo wa kusikiliza Hilo shauri na kutoa maamuzi,,,,hiyo ndio Hali halisi.
Huenda ungekuwa na swali lingine,,,Kwa mfano je vipi sasa mwanaume na mwanamke wote wamekoseana je Qur'an inasemaje?
Qur'an haikuacha kitu hapa Napo imetoa mwongoz ufuatao ktk 4:35
"Na mkichelea kutakuwapo mfarakano baina ya mke na mume basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke. Wakitaka mapatano Mwenyezi Mungu atawawezesha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye khabari."
Hapa ktk ugomvi WA mwanaume na mwanamke basi inatakiwa katika kikao cha usuluhishi kila upande kuwepo na mwakilishi ili usawa upatikane na kila mtu awe na haki Sawa.
Huo ndio Uislamu unatoa majibu Kwa kila maswali.
Bwana Mokiti ,,,,nasikitika kukwambia kwamba sitajibu hoja zako kwakuwa wewe ni mpuuzi Sana,,,,huwa unapika data za kupaka Uislamu matope Hali ya kuwa unajua sio sahihi,,,,,unachukua hadith ambazo sio sahihi na Stori ambazo unajisikia wewe mwenyewe kuzipika na kuleta upuuzi wako humu.
Kuna posti ulinikoti nikakupuuza na sikukujibu Kwa makusudi kwakuwa nakujua vizur,,,,na ndugu zangu waislamu huyu mpuuzi msishughulike nae mumdharau Tu namwacheni kama alivyo coz anapenda ligi Sana zisizo na kichwa wala miguu.