Dini si imani, Mimi mkristo nimekubali kuoa ndoa ya kiislamu, ndoa ya kikristo inampa kiburi mwanamke na ni ngumu kusuluhisha matatizo

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
Kwa kipindi kirefu nimekuwa nasita kuoa, kwa umri wangu wa miaka 28 nimeona ni wakati sasa niwe na ndoa official, Si mara ya kwanza kufikiria hili jambo, ni tangu nipo 25 nafikiria ila sheria za ndoa za kikristo zilikuwa zikinipa hofu kubwa mno hasa kwa tunayojionea kwa wahanga, Ni lazima tukubali wanawake wa sasa sio kama mama zetu wa enzi zile ambao tayari walikuwa wamefundwa kuishi maisha ya ndoa na mwanaume na ndio maana hakukuwa na vimbwanga vingi kama sasa. Ndoa za kikristo kwa sasa zimekuwa mtihani jamani.


Ndoa za kikristo ni ngumu kusuluhisha matatizo

Kwa mama zetu miaka hiyo ahsafundwa majukumu ya ndoa, kuishi na mwanaume, n.k. lakini siku hizi hali ni tofauti yani ukiongezea mambo ya usawa, wanawake walioelimika, ushauri wa mashosti watukutu, n.k. ndoa zimeingia kwenye matatizo mengi sana, Huko kanisani usuluhishi unaotumika ni ule wa kina mama zetu ambao angalau walikuwa waelewa ila kwa hawa wanawake wa sasa ni kama kumpigia mbuzi gitaa, na hapo ndipo watu wanakimbilia mahakamani wanaona kanisani ni kupoteza muda tu, kwa hili tu unaona ni wazi kabisa usuluhishi wa kikristo umefeli, Kwanini wakimbilie mahakamani na sio kwa wachungaji ?

Kuoa upya ni ngumu kwenye ukristo

Ndoa ya kikristo imejaa bureacracies nyingi sana, mnaweza kauchana hata miaka miwili hurusiwi kuoa upya mpaka kanisa litoe kibali chao, ukilazimisha kuoa upya shoka la sheria linakukata, what is ithis ?

Ndooa ya kikristo inampa mwanamke kiburi cha usawa

Mwanamke anajua ukishamvisha pete ashakubana hapo kuchomoka ngumu, Anajua fika kabisa hata afurukute mtaenda kanisani kwa wachungaji wataokuwa wanawabembeleza kila siku mkayamalize, anajua huna uhuru wa kuoa upya kirahisi, anajaua mkiachana ana mali zako pasu kwa pasu, n.k.

Ndoa za kikristo zinaleta tamaa ya mali

Pia katika suala la wale majambazi wanaoingia kwa nia ya kula timing muachane ili wapate mgao wa mali katika ndoa za kikristo ni rahisi sana, katika uislamu mwanaume hana wajibu huo, hapa pia adabu inaongezeka kwa mwanamke, hata mwanamke akikaza waweza kumpiga biti utaongeza wenzake watatu asiingilie mgao wao
.........................................................................

Binafsi nimekata shauri kwamba tamaduni za ndoa za kiisalamu ndio zitanipa ahueni zaidi ya kuishi maisha ya ndoa, mwanzoni nilikuwa nikisita kwa kuunganisha imani na dini kuwa kitu kimoja lakini kwa sasa nimeweza kukubali imani na dini ni vitu viwili tofauti nimeona ni sawa tu kuoa kwa misingi ya dini ya kiislamu, lakini kwa imani bado mimi ni mfuasi ya Yesu / Mkristo,
 
Kwa mentality hiyo hata hiyo ndoa ya kiislamu haikufai, utamnyanyasa huyo mwanamke.

Inshort ndoa haikufai kwa sasa, subiri ukue kue kidogo upate busara.
Inaelekea jamaa kapitia experience mbaya kwenye mahusiano. Hata mimi ningeelezea niliyopitia kwenye ndoa nadhani ungekubali kukua na kuwa na busara wakati mwingine havimaanishi ndoa stable.
 
Inaelekea jamaa kapitia experience mbaya kwenye mahusiano. Hata mimi ningeelezea niliyopitia kwenye ndoa nadhani ungekubali kukua na kuwa na busara wakati mwingine havimaanishi ndoa stable.
Bado uko kwenye ndoa? Au umeshajitoa?

Sasa huyo kabla tu hajaingia kashaanza kujitabiria mambo ya ugomvi sijui mwanamke anapata kiburi.
Anaona kuoa ni kama kumfanyia favour mwanamke, hiyo sio dhana ya ndoa.
 
Bado uko kwenye ndoa? Au umeshajitoa?

Sasa huyo kabla tu hajaingia kashaanza kujitabiria mambo ya ugomvi sijui mwanamke anapata kiburi.
Anaona kuoa ni kama kumfanyia favour mwanamke, hiyo sio dhana ya ndoa.
Ndoa za misukosuko mara nyingi kuachana nako kunakuwa na makandokando mengi. Bado hujaweka tena na muda na plan za maisha zilizovurugika. Nafanya bidii nijitoe.
 
Ukiona kwenye imani unaanza kuamua vile unavyofikiri na bongo yako kukubali ujue sasa mungu ni wewe mwenyewe!

Kama unamtaka Mungu fuata maelekezo ya Dini, kama Mkristo omba Roho Mtakatifu na tumia akili yako kutafiti kwa kina ujue dini ya kweli ( IPO!). Kama sio Mkristo mf. Muislamu fata taratibu za dini yako usijiongoze!

Sasa ukianza kuona kwenye Ukristo unakubali hivi na unakataa vile na unachagua hivi vya kiislamu na kukataa vile ujue umeamua kuwa mungu mwenyewe bila kujua!
 
Ukiona kwenye imani unaanza kuamua vile unavyofikiri na bongo yako kukubali ujue sasa mungu ni wewe mwenyewe!

Kama unamtaka Mungu fuata maelekezo ya Dini, kama Mkristo omba Roho Mtakatifu na tumia akili yako kutafiti kwa kina ujue dini ya kweli ( IPO!). Kama sio Mkristo mf. Muislamu fata taratibu za dini yako usijiongoze!

Sasa ukianza kuona kwenye Ukristo unakubali hivi na unakataa vile na unachagua hivi vya kiislamu na kukataa vile ujue umeamua kuwa mungu mwenyewe bila kujua!
Ina maana hao wakristo wenye changamoto kwenye ndoa hawakuomba Roho mtakatifu!!?

Muwe mnaacha kuwadanganya watu!

Sheria za ndoa KWA wakristo ni zile za roman nazo ni za SERIKALI!!

Ndoa KWA wakristo changamoto zake ni kuzikimbia au mbaki muuane!maana hata mahakama hayo imeegemea upande mmoja!!
 
Back
Top Bottom