R-K-O
JF-Expert Member
- Jun 27, 2023
- 482
- 2,138
Vitendo vya unyanyasaji kwa wanaume wa kikristo kupigwa na wake zao vimeshamiri kiasi kwamba wanaume wameamua kuweka aibu pembeni na kuililia serikali ifungue dawati la unyanyasaji kwa wanaume, licha ya hivi bado msaada unakuwa mdogo maana wakikimbilia polisi ama ustawi wa jamii wanachekwa.
Si vipigo tu, pia kuna unyanyasaji kwa wanaume wa kikristo kufanyiwa visa vya kunyimwa unyumba na wake zao, mtu unakuta hadi yamemfika shingoni inabidi aweke wazi kwamba kanyimwa unyumba mwaka mzima.
Nachoona ni kwamba ndoa za kikristo mwanamke akiolewa tu anaridhika anajua ndio mwisho wa safari hapo, mwanaume hawezi kuongeza mke na anaogopa kuvunja ndoa ili kuzilinda mali zake zisipigwe pasu kwa pasu, hapa ndio kiburi kinaanza sasa inafikia kipindi mwanamke anaanza kumdunda hata mme wake ama kumnyima unyumba maksudi, anajua tayari huyo mwanaume hana ujanja.
upande wa ndoa za kiislam na za kitamaduni ni nadra sana maana mwanamke anajua kabisa talaka inaweza kuwa muda wowote na kuhusu mali hakuna pasu kwa pasu, atapewa tu mgao wa mali alizochangia lasivyo mwanaume atampa chochote cha kuanzia maisha kadiri ya uwezo wake, pia mwanamke anajua wazi kabisa kwamba hata kama yupo peke yake miaka 20 bado mme wake anaweza kuongeza mke.