Ni kweli malaika kama malaika au ROHO yeyote hawezi kuzalisha sababu haikuumbwa kwa sababu hiyo ila mwili unaweza kuzalisha sababu uliumbwa kwa kazi hiyo na ndipo mjadala unapoaanza.
kutokana na ushahidi wa kibiblia (sijui imani yako utaniradhi) tunaweza kuona mwandishi wa kitabu cha Yuda ambaye alikuwa kaka yake Yesu anaongelea kisa hiki cha malaika kuwaingilia wanadamu,twende pamoja
Waraka wa YUDA
6
Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.
7 Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
Hapa tukisoma tunaona wazi mwandishi anafananisha dhambi waliofanya watu wa sodom ya uzinzi kma walivyofanya wale malaika.... Neno
JINSI MOJA NA HAWA.... Linaweza kusummarise kuwa iliwezekana malaika kuwaingilia wanadamu na kuwazalisha viumbe na watafiti wengine wanadai ndio moja ya sababu Mungu aliamua kufuta uzao huo kwa gharika ila Yuda hapa anaelezea kuwa malaika hao kwa sasa wamefungwa kuzimu hivyo kuna uwezekano kwa sasa hawana uwezo huo wa kuhamisha asili yao kwa mwili kama walivyofanya kwa WANEFILI
2. Nadharia ya pili malaika kuvaa mwili wa binadamu ili aweze kuzalisha however swali lako linahoji kivpi anaweza hamisha genes zake
Kwa maoni yangu binafsi nachoona kuna uwezekani mtoto asiwe na gene yoyote ya kimapepo/kimalaika sababu mwili umezaa na mwili ila MAKUZI yanaweza kumbadilisha huyo mtoto kuwa wa mazingara..... Mfano mtoto aliyezaliwa kibinadamu akachukuliwa na wachawi lazima atakua tofauti na mtoto wa kawaida maana atapandikizwa matambiko ya ajabu yanayomuwezesha kupaa...kuyeyuka....kuua....nguvu za ajabu n.k
Hivyo kwa nadharia hii ya pili hao wanefili wanaweza kuwa walizaliwa kwa malaika kuvaa miili ya binadamu wengine na watoto walizaliwa kma wanadamu tu ila makuzi mfano waliwafanyia matambiko.... Walihamishia mapepo yao mengine humo..... Waliwapa nguvu zao n.k mwisho wa siku miili yao ikabadilika ikawa ya kimazingara maana mfano kma leo hii mchawi anaweza akakuotesha busha...tumbo n.k kwa nni tusiamini hao MALAIKA walikuwa na uwezo wa kuwapa urefu wa ajabu... Nguvu za ajabu nyingine kma leo hii tu wachawi wakawaida wanavyoweza kuotesha viungo flani vya mwili
Sijui it makes sense now ila all in all nakubaliana na ww malaika HAWEZI kumzalisha mwanadamu ila inawezekana kwa exception nlizotaja hapo juu
Ni hayo tu labda tuwaite na wajuvi wengine watusaidie
Cc :
SALA NA KAZI @Malcom Lumumba [USER=113939]Palantir hearly Eiyer Kudo900 Mshana Jr[/USER]