Duh nashkuru kwa darasa ila kwa upande wangu story ya huyu Unju Bin Unuq nliwahi kusimuliwa kidogo na mtu wa pwani alidai huyu jamaa alikuwa anaishi pwani ya afrika mashariki na ndio aliyemsaidia Nuhu kujenga safina kwa kumletea mbao ngumu kutoka afrika ya kati (DRC ya sasa) maana mashariki ya kati ilikuwa na asili ya jangwa hivyo jamaa alichukua miti huku na kuifanya mbao na kuwapelekea nuhu wajengee safina
Pia wanadai kwakuwa wanadamu walimuona Nuhu kma "mzinguaji" sababu alikuwa anawaambia habari za waache madhambi n.k kila wakitaka kumvamia kumpiga au kumsonga songa basi huyu Unju bin unuq alikuwa anajitokeza kumkingia kifua wengine wote wanakuwa wapole
Simulizi hiyo inaishia pale wakati wa gharika wanadai kwamba kwakuwa yeye alikuwa sio uzao wa asili wa kibinadamu(huenda uzao wa malaika/majini) hivyo asingekuwa msafi kuwepo baada ya gharika hivyo baada ya KUFUNGA mlango wa Safina basi alijua wakati wake wa kufa umefika
Ila advantage aliyopewa ni kwamba hatokufa wakati wa gharika ila alikufa mwanzoni kabisa kabla ya gharika lile kushika kasi.....inadaiwa wakati mvua inaanza yeye aliteleza kwenye ardhi yenye matope tope ukanda huu wa afrika mashariki(wakazi wanadai mtwara) na mwili wake kupigizwa kwenye bahari hivyo mwili wake upo baharini kuendana na simulizi hii na wengine wanadai unyayo wake ambao ulitengeneza kma bonde upo huko mtwara
Naweza kubaliana na kisa hiki kuliko hicho cha wayahudi kinachosema alipona gharika sababu haiingii akilini gharika na maji kujaa siku zaidi ya 120 huyo mtu apone kumbuka kulikuwa na upepo.... Mawimbi.... Radi..... Mavolcano n.k sioni kivp angepona hayo mapito!!! Kingine angekosa chakula lazima sababu bahari ilichafuka angekula wapi?? Mizoga ya wanadamu??
Kuhusu mfalme ogu ni kweli alikuwepo ila sidhani kma ndie huyo huyo mmoja na Uj sababu mfalme ogu alikuwa ni muamori mtoto wa canaan mjukuu wa ham na kitukuu cha Nuhu ila hyu UJ alikuwepo kabla ya gharika hivyo sidhani kma angehusishwa na kabila moja tu
Wajuvi zaidi mtupe story ya LIJIMTU hili la ajabu kuwahi kutokea
Cc
Mitha