Mkuu Mhe.Professor... Kiukweli nimetumia biblia tu pamoja na mythology nyingine kwa kiasi kikubwa kwa sababu moja kuu kwamba makabila mengi duniani kila mmojawapo lina story ya uwepo wa mtu mwenye futi zaidi ya 40??
Ahsante
Kama ulitumia Biblia kama chanzo (Persuasive Source) basi hapa lazima umuweke mwanahistoria Flavius Josephus,
Huyu ndiye anayetumiwa mwanahistoria nguli wa Karne ya kwanza ambaye wanahistoria wengi na wasomi wengi wa taalimungu wanamtumia kama chanzo chao. Kwenye kitabu chake cha The Antiquities of the Jews amezingumzia uwepo wa majitu na jinsi yalivyopigana vita na Mfalme Daudi. Humu amewataja ndugu zake Goliati waliokuwa na vidole sita mikononi na miguuni, moja wapo ni Ishbibenob ambaye mkuki wake ulikuwa na kama kilo tatu na gramu kadhaa.
Kwanini umtuie Flavius Josephus ???
Huyu alikuwa ni msomi wa Kiyahudi ambaye alipewa Uraia wa Rumi na Kaisari Vespasian. Baada ya Jemedari Titus kuhusuru Israel mwaka 70 B.K huyu jamaa alichukuliwa mateka baada ya Masada kuanguka. Huko Rumi alionekana ni moja ya wasomi wenye akili sana basi mfalme akampa kazi ya kuandika kuhusu vita dhidi ya Wayahudi na Warumi ili kwamba huenda Wayahudi wengine wasifikirie kuleta uasi dhidi ya Rumi. Kitabu chake cha kwanza kiliitwa The Wars of the Jews. Hivyo kutokana na nafasi yake ya kitaifa aliyokuwa nayo mbele ya kaisari Vespasian na Titus wasomi wengi wa dini huwa wanamtumia huyu mwanahistoria kwasababu alikuwa msomi anayeaminika sana kwa kipindi hicho.
Kuhusu majitu ya kale,
Kweli yalikuwepo kwasababu ushahidi wa kihistoria bado tunao na kila siku unaendelea kupatikana.
Japo hapo katikati kuna mianya mingi sana ambayo sisi hutuwezi kuijaza kwa ushahidi mkubwa zaidi ya kutafuta nadharia mbali mbali (Theories). Wengine wanasema Majitu ni wana wa malaika (Bi'nai elohim), wengine wanasema wanadamu wa kale walikuwa majitu na kadiri siku ziendavyo tukapungua maumbile na wengine wanasema kabisa kulikuwa na kizazi cha majitu ambayo yalikuwa ni binadamu kama wengine lakini kikapotea tu. Hii ya mwisho inawezekan vizuri tu maana kuna viumbe kama dinosauri viliwahi kuwepo lakini leo vikapotea na kilichobaki kwetu ni mifupa ambayo wanasayansi wanaisoma.
Lakini kama umetumia Biblia kama chanzo chako mimi nakuachia maswali haya ya utafiti:
Kwanini Wahebrania walifanikiwa kupiga sehemu zote za Israeli kasoro Yerusalemu ??
Au kwanini Yerusalemu ulikuwa ndiyo mji wa mwisho kukamwatwa na Waisraeli baada ya Daudi kuwa mfalme ??
Kwanini mfalme Daudi aliwachukia sana wale vipofu na viwete waliokuwa wanakaa Yerusalemu ??
Kwanini Wakina Sauli hawakufikiria kuukamata Yerusalemu wakati ulikuwa ndani ya nchi yao ??
NB 1 : Kitu cha kukumbushana ni kwamba, kitu kuaminiwa au kutajwa na watu wengi haithibitishi uhalisia wake.
Hivyo kuwepo kwa hadithi nyingi na nadharia kunasiaidia tu kukuza uelewa wetu ili tuweze kuamua nini cha kuamini.
Hivyo kuna sehemu inasema Farao aliwahi kuwalaani kishirikina watu wa Kaanani (Majitu ) kwasababu walikuwa na ugomvi naye. Lakini pia usisahau kwamba haya majitu ya kwenye Biblia yalikuwa ni wana wa Kanani ambaye alikuwa ni mtoto wa Nuhu. Hivyo basi tuchambue taratibu na kusoma sana vitu vya kutosha halafu tuchague nini cha kuamini kuhusu asili ya haya majitu.
NB 2: Lakini muhimu kuliko yote, MAJITU YALIKUWEPO.
Ushahidi wa kihistoria unathibitisha uwepo wa majitu japo historia inashindwa kututhibitishia asili yao.
Mpaka sasa hatujui haya majitu yalikuwa ni Uzao wa binadamu (Adam) au Ilikuwa ni jamii nyingine tofauti kabisa na jamii ya Binadamu. Hivyo kwenye huu mjadala tungesema:
GIANTS DID EXIST, BUT WHERE DID THEY COME FROM AND WHERE ARE THEY NOW ???? Hapa sasa ndipo tungeanza kuja na nadharia za kidini ambazo zinatoka kwenye Biblia, Kurani na hadithi za kidini (Mythologies) au Utafiti wa kisayansi ambao unazungumzua mabadiliko kutokana na muda na mzaingira (Evolution)