Demokrasia na Maendeleo ndani ya CHADEMA

Demokrasia na Maendeleo ndani ya CHADEMA

Amegilizia makala ya johnson mbwambo ya raia mwema toleo liliopita, hana hoja zaidi ya unafiki, je lipumba alishandana vipi kuupata uenyekiti wa CUF , majungu yatawamaliza baadhi ya vijana wa kitanzania ambao wamenyimwa fursa za kuwa wezi na mafisadi.

Hata wao CCM juzi wamemchagua mwenyekiti wao "mpya" wa taifa bila kuwa na mpinzani. Kwa nini watu wengine hawakuruhusiwa kama kweli kuna demokrasia?
Halafu lazima
TUNTEMEKE ujuwe kuwa ugomvi wa BESIGYE na M7 ni zaidi ya siasa na hivyo usifananishe ya kule na huku kwetu.
 
Hata wewe Matola DINI ya mtu inakusumbua! Nape nilimwona kule kwa Gwajima siku moja; AshaRose Migiro mumewe MKRISTO; Mwiguluuu....., wengine hawa akina JK, Kinana, Zakhia ni DINI majina tu!
Acha unafki wewe, JK kwenda kanisa la Lutheran na Lowasa ndio amekuwa Mkristo? Asha Rose Migiro kuolewa na Mkristo hii ndio inakuonesha kwamba ni Mkristo? au hujui kwamba yule DC Fatuma Kimario Mume wake ni Mkristo? ndio maana nakuita mnafki Mkubwa.

JK, Kinana, Zakhia ni Dini majina tu je hawa ni dini gani? wewe hapa unaonesha ni jinsi gani ulivyo mtu wa hovyo mwenye Hidden Agenda. hivi uchaguzi uliokwisha wa CCM ngazi ya Taifa kuna hata nafasi moja iliyogombewa kwa maana halisi ya uchaguzi?
 
Acha unafki wewe, JK kwenda kanisa la Lutheran na Lowasa ndio amekuwa Mkristo? Asha Rose Migiro kuolewa na Mkristo hii ndio inakuonesha kwamba ni Mkristo? au hujui kwamba yule DC Fatuma Kimario Mume wake ni Mkristo? ndio maana nakuita mnafki Mkubwa.

JK, Kinana, Zakhia ni Dini majina tu je hawa ni dini gani? wewe hapa unaonesha ni jinsi gani ulivyo mtu wa hovyo mwenye Hidden Agenda. hivi uchaguzi uliokwisha wa CCM ngazi ya Taifa kuna hata nafasi moja iliyogombewa kwa maana halisi ya uchaguzi?
Ukiacha JAZBA na MUNKHAR ukanisoma taratiiibu utanielewa tu. Acha pia kuhukumu ujadili hoja zilizo mbele yako. Wala usiniandikie ambacho sikuandika na hakimo akilini mwangu. Matola tumekuwa nawe humu muda sasa. Hauko hivi.
 
Habib Mchange kwanini kwenye kila andiko lako lazima umhusishe Zito Zuberi kabwe? Kwa nini kila unapotaka kupumua unataka kumfarakanisha ZZK na Chadema kwa kisingizio cha kumtetea. Sidhani wala siamini kama ZZK anakutuma.

Kwa nini usijitetee wewe mwenye au usiwe huru kuandika bila mtu mwingine kumwingiza kwenye vita vyako??

maandishi na tuhuma zako zinaonyesha hasira ya wazi dhidi ya wafuasi na wanachama pamoja na viongozi wa Chadema. Ila lazima ujue wazi dhambi ya rushwa na makundi uliyoitenda ndiyo inakusakama na kukuumiza roho. ungekuwa mwanasiasa mahiri ungeliona kosa na kutubu dhambi na kuanza kutenda mema.

Sidhani hata huyo ZZK anakuhitaji kwa sasa. Siasa huwezi ukawa na permanent adui wala permanent rafiki. Ndiyo siasa kaka. Uongozi huwezi kuongoza unaowataka tu au kuwapenda,huwezi kufanya kazi na marafiki zako kama ni hivyo ingekuwa rahisi.

Kwa jinsi unavyoutafsiri uongozi huwezi kuwa hata kiongozi kwenye kikundi cha watu kumi na ikiwa hivyo itakuwa Tsunami.

Uongozi ni art, kipaji, hekima, busara, utulivu, ushauri, akili, weledi, uvumilivu , uwezo nk ambavyo vyote huna. Kwanza nataka uje hapa JF na real ID ili watu wenye weledi wakujue sio unatuvurugia chama ukifikiri unamsaidia mtu.

Farakani alipojua kila akiongea wazungu wanampunguzia kura obama alisema maneno yenye busara sana; kwa manufaa mapana ya ushindi wa Obama kwenye historia ya marekani nitakaa kimya ili kijana wetu ashinde.

Kama kweli wewe ni mpiga debe wa ZZK unamharibia vibaya sana kuliko kumsaidia kwenye gwaride la ushindi wa kisiasa kaa kimya. Kwa sasa wewe ni mchafuzi

Hivi kundi lako likishinda uenyekiti wa CDM mnafikiri mtafanya kazi na nani? Mnawanachama kutoka mwezini ambao mtaona ndio wanaofaa??
Kwanini mchukie uongozi wa sasa wakati upo kikatiba?

Mnafikiri mkiingia madarakani huku mmejenga makundi sijui ya hawa wazee wale vijana mnafikiri ninyi mnakuwa kwa kwenda chini au umri unaongezeka? je unajua kwa umri wako wako madogo wanakuita mzee au kwa umri wa huyo unayempenda wako madogo tayari wanamwita mzee au mnafikiri uzee lazima uwe na miaka 60??

Na je akipendwa kijana mwingine mdogo na mwenye hekima kuliko kundi unalosarandia si utakuwa sakala??

Sio wote wanaouwezo wa kuwa viongozi hasa vyeo vya juu, wengi wanaweza kuwa watendaji, watu wa kutumwa na wachache viongozi kwani kiongozi anahitaji ngozi ngumu sio laini kama hizi ninazoziona.

Chadema itaendelea kuwepo kwa umakini wake na uchambuzi wake mahiri hasa kwenye kupata uongozi wake.
 
Tunachosema sis1 ndio mtizamo wa watu wengi huku mitaani kasoro zenu nyie ni mbaya sana machoni mwa watu kuliko za ccm kwa kuwa ccm wana mambo lukuki mazuri yanayoonekana kwa macho mwa watu.
Ambayo yanaweza kufunika yale maovu.mnachotakiwa ni kujisahihisha,wala sio kujifananisha na ccm.kama kweli nyie ni chama makini mnatakiwa maidentify kasoro zenu.kasoro yenu kubwa inayozungumzwa huku ni kwamba cdm mwonekano wake sio chama cha kitaifa na kama kikishika hatamu kitapendelea watu wa sehemu fulani.wekeni akilini hili na pia msijibu kwa matusi .nawakilisha.
 
Wanabodi.

Watanzania wamekuwa na uhuru wa kufanya na kushiriki katika shughuli za kisiasa, kufanya maandamano na kuitisha mikutano ya hadhara ya kisiasa, kijamii na mingineyo.

Watanzania wana haki ya kujivunia mafanikio hayo ya kupanuka kwa demokrasia kupitia vyama vyao vya siasa Watanzania wamekuwa na uhuru mkubwa wa kutoa maoni yao kupitia vyombo vya habari mitandao ya kijamii.

Changamoto hizo zimepelekea baadhi ya viongozi wa Chadema wanautumia vibaya uhuru huo na kusababisha sintofahamu kila siku. Chadema wanataka kuhatarisha maisha ya Wananchi. Tukiangalia matukio mengi yakifanywa na Chadema dhumuni lao kubwa nchi ingie kwenye machafuko ya umwagaji damu mapigano ya sisi kwa sisi kitu ambacho Watanzania wameapa kuwa hawatakubali.

Tumeshuhudia viongozi wa Chadema wakiomba kufanya maandamano bila vibali wanapozuiwa na polisi baada ya kubaini kutatokea uvinjifu wa amani, Chadema wanalazimisha kufanya maandano kwa nguvu. Leo Chadema ni chama cha upinzani sasa kama kitaendelea kutotii mamlaka nyingine zilizopo kisheria siku wakishika dola shughuli za kisiasa zitafanyika katika mazingira ya vurugu tupu.

Watanzania wengi wapenda amani na baadhi ya Watanzania ambao si wanachama wa Chadema huogopa kwenda katika mikutano yao ya hadhara na maandamano yao kwa kuhofia kutokea vurugu na hatimaye mauaji.

Ubabe wa viongozi wa Chadema wa kupenda vurugu limekuwa jambo la kawaida kwao kama ni utamaduni wa kuendesha shughuli za siasa nchini Watanzania tuwe makini sana na siasa za Chadema.

Watanzania tunapaswa kufahamu kuwa ni wajibu wetu kulinda amani iliyopo sasa na hii itawezekana tu kama wanasiasa watakubali kuheshimu misingi ya katiba ya nchi na kuzingatia sheria zilizowekwa.
 
unaposema dhumuni kubwa ni nchi iingie kwenye machafuko ni nyinyi magamba huwa mnasema hivyo kama mtaji wa kuwarubuni watanzania lkn si nia ya chadema kufanya hivyo.
 
Wanabodi.

Watanzania wamekuwa na uhuru wa kufanya na kushiriki katika shughuli za kisiasa, kufanya maandamano na kuitisha mikutano ya hadhara ya kisiasa, kijamii na mingineyo.

Watanzania wana haki ya kujivunia mafanikio hayo ya kupanuka kwa demokrasia kupitia vyama vyao vya siasa Watanzania wamekuwa na uhuru mkubwa wa kutoa maoni yao kupitia vyombo vya habari mitandao ya kijamii.

Changamoto hizo zimepelekea baadhi ya viongozi wa Chadema(1) wanautumia vibaya uhuru huo na kusababisha sintofahamu kila siku. Chadema(2) wanataka kuhatarisha maisha ya Wananchi. Tukiangalia matukio mengi yakifanywa na Chadema(3) dhumuni lao kubwa nchi ingie kwenye machafuko ya umwagaji damu mapigano ya sisi kwa sisi kitu ambacho Watanzania wameapa kuwa hawatakubali.

Tumeshuhudia viongozi wa Chadema(4) wakiomba kufanya maandamano bila vibali wanapozuiwa na polisi baada ya kubaini kutatokea uvinjifu wa amani, Chadema(5) wanalazimisha kufanya maandano kwa nguvu. Leo Chadema(6) ni chama cha upinzani sasa kama kitaendelea kutotii mamlaka nyingine zilizopo kisheria siku wakishika dola shughuli za kisiasa zitafanyika katika mazingira ya vurugu tupu.

Watanzania wengi wapenda amani na baadhi ya Watanzania ambao si wanachama wa Chadema(7) huogopa kwenda katika mikutano yao ya hadhara na maandamano yao kwa kuhofia kutokea vurugu na hatimaye mauaji.

Ubabe wa viongozi wa Chadema(8) wa kupenda vurugu limekuwa jambo la kawaida kwao kama ni utamaduni wa kuendesha shughuli za siasa nchini Watanzania tuwe makini sana na siasa za Chadema(9).

Total Mention = 9
Fee per Mention = 200
Total Amount Paid On this Thread = 9 X 200 = 1800

Ajira Nzuri sana Hii
 
unaposema dhumuni kubwa ni nchi iingie kwenye machafuko ni nyinyi magamba huwa mnasema hivyo kama mtaji wa kuwarubuni watanzania lkn si nia ya chadema kufanya hivyo.

Mkuu ni jukumu letu sote kulinda amani iliyopo.
 
unaposema dhumuni kubwa ni nchi iingie kwenye machafuko ni nyinyi magamba huwa mnasema hivyo kama mtaji wa kuwarubuni watanzania lkn si nia ya chadema kufanya hivyo.
nia ya chadema ni kupata madaraka ya kuidhibiti nchi kwa namna na gharama yeyote ile.
 
Chadema pamoja na wafuasi wenu mnatakiwa kufahamu kuwa mamlaka waliyonayo polisi wetu hapa nchini hata nchi nyingine duniani yako hivyo. Hakuna kikundi au taasisi inayoweza kufanya mikutano au maandamano bila ya ridhaa ya polisi.
 
Mnadhani watanzania ni wajinga tena, hizo propaganda zenu za kuichafua CHADEMA walishazishtukia mapema.

Watanzania kwa sasa wanaipenda sana CHADEMA na wameshawaamini CHADEMA, wakati wowote CCM itakuwa chama cha upinzani.
 
Chadema (10) pamoja na wafuasi wenu mnatakiwa kufahamu kuwa mamlaka waliyonayo polisi wetu hapa nchini hata nchi nyingine duniani yako hivyo. Hakuna kikundi au taasisi inayoweza kufanya mikutano au maandamano bila ya ridhaa ya polisi.

Fee paid 1800 + 200 = 2000
 
......jamani hali ya kijiwe(LUMUMBA) ni mbaya baada ya misele wadau wameleta fitina eti tulieenda kutalii......bora key board INALIPA!!!
 
Chadema pamoja na wafuasi wenu mnatakiwa kufahamu kuwa mamlaka waliyonayo polisi wetu hapa nchini hata nchi nyingine duniani yako hivyo. Hakuna kikundi au taasisi inayoweza kufanya mikutano au maandamano bila ya ridhaa ya polisi.
JK alisema CCM iache kutegemea polisi.
 
Back
Top Bottom