Labda bwana Tuntemeke hajui anachokiongea ama anamlenga Lipumba. Kiiza Besigye ameshagombea urais wa Uganda zaidi ya mara mbili, CDM hakuna kiongozi aliyewahi kugombea urais zaidi ya mara moja. Besigye kakiongoza chama hicho toka kuundwa kwake, chadema kimeshakuwa na wenyeviti watatu, makatibu wakuu watatu katika miaka yake 20 tangu kuanzishwa kwake. Sijui unapozungumzia kuachiana madaraka una maanisha nini. Kwa kumbukumbu sahihi wale wanaopiga chapuo la ukabila na kutokuwa na demokrasia kumbuka, Mwenyekiti wa kwanza wa CDM ni Edwin Mtei (Mchaga), Katibu wake Marehemu Bob Makani (Msukuma), Bob Makani (Mwenyekiti wa pili), Dr. Amani Waridi Kabourou (Katibu mkuu) - Kigoma.
Freeman Aikaeli Mbowe (Mwenyekiti 3 - Mchaga), Dr. Wilbrod Peter Slaa (sahaa) Katibu wa sasa Muiraqwi. Katika umri huo wa miaka 20, baadhi ya vyama vya siasa Tanzania na wenyeviti wao CCM - 3 A. H. Mwinyi, B. W. Mkapa, J. M. Kikwete. Makatibu wakuu kama 7 hivi, Marehemu Horace Kolimba, ................. nimewasahau, Philip Mangula, Lt. Makamba, Mukama, Kinana. CUF James Mapalala, Prof. Lipumba katibu (wenyeviti), Maalim Seif (katibu .... wa maisha?), UDP John Momose Cheyo (Mwenyekiti), Marehemu Amani Nzugile Jidulamabambasi (Mwenyekiti kwa mapinduzi ya muda mfupi). NCCR, Mabere Nyaucho Marandu, Augustin Lyatonga Mrema, James Mbatia (wenyeviti). TLP Mwenyekiti wa kwanza alimuachia chama Augustino Lyatonga Mrema, akamtimua ktk chama, vingine kama DP mwenyekiti ni Mchungaji Christopher Mtikila (His personal property?).
Tuntemeke kati ya hivi vyote, ni kipi chenye kufanya chaguzi za kidemokrasia kwelikweli? Mtafute Profesa Safari muulize akupe uzoefu wake. Vipi Hamad Rashid wa Wawi? Kafulila ......., Na vipi kura za maruhani za Kizota unajua kilichotokea? CHADEMA walipobaini ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi wa BAVICHA na tuhuma za rushwa kwa BAWACHA, walionesha njia walifuta chaguzi hizo 2010. Chama kipi kingine kilichoweza? (Reference CCM 2012, rtushwa mpaka mwenyekiti katoa machozi, je walithubutu kufuta chaguzi za ndani zilizogubikwa kwa rushwa?). Besigye amerun out of time na kaliona hilo ndiyo maana ameamua kung'atuka.NINA IMANI NA CHADEMA OYA OYA OYA!!!! NINA IMANI NAYE MBOWE OYA OYA OYA!! NINA IMANI NA SLAA OYA OYA OYA!!! CHADEMA KWELI KWELI, KWELI KWELI KWELI KWELI CHADEMA, KWELI, KWELIII, KWELI KWELI KWELI KWELI CHADEMA!!!!!!!!!!!!!