Dear Mama! Usipoweka sheria nzuri za chaguzi utaishia kwenye stress sana mwisho wake!

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,609
8,753
Napenda kupendekeza kwa Mama. Hayo maendeleo pekee haita kuwa sababu ya watu kukusamehe kwenye sheria mbovu za chaguzi hasa kama vyama vikuu vya upinzani vitagomea uchaguzi. Ukweli ni kwamba huko ndiko tunaelekea. Hao wanao kudanganya mambo yatakuwa powa sio kwako ni kwao. Mambo hayatakuwa powa.
1. Kwanza wakigomea uchaguzi washiriki watapungua
2. Heshima yako itashuka kwa wananchi na kimataifa
3. Utaacha historia kama mwizi wa kura. Hata kama wengine hawatafikiri ni fair lakini huo ndiyo ukweli
4.Itakuwa vigumu hata kufanya katiba baada ya chaguzi maana nani atakuamini?
5. Mashindano ya mridhi wako yataanza baada ya chaguzi na kama chaguzi zimegomewa dharau kwako itakuwa kubwa hata ndani ya CCM.

Hii step ya tume huru ni ndogo sana na kama hili limekushinda kukubaliana na wadau wengine utapata shida sana mwaka huu Mama. Nashauri rekebisha sheria zote za chaguzi, tume na wape wadau wa demokrasia wanauotaka ili kama kushinda ushinde kihalali na kuweza kupeleka nchi mbele. Mnayofanya kwa sasa hayasaidiii nchi yetu. Hutaweza kuendeleza nchi na chama kimoja pekee huo ndiyo ukweli.
 
Mama kaambiwa BILA KUPORA UCHAFUZI hashindi Ng'o.

Haya MAIGIZO yaliyopelekwa Bungeni wanawadandanganya WAFADHILI wa NCHI ZA MAGHARIBI.

WANAOGOPA KUKATIWA MISAADA.😂
 
Sishauri wapinzani wa kweli kushiriki kwenye chaguzi ambazo tume ya uchaguzi itaendelea kudhibitiwa na mwenyekiti wa ccm. Ni ujinga kwenda kusimamisha watu kwenye mistari ya kura huku tayari nyuma ya pazia watu wamepanga matokeo yaweje.

Ni vizuri kususia hizo chaguzi, vile vitisho vya sijui Chama kitakosa ruzuku ni vitisho kwa vyama vyenye mtazamo wa muda mfupi. Kinachotakiwa ni kushusha uhalali wa umma. Acha washinde kisheria, lakini sio kuwapa uhalali wa umma wasiokuwa nao.
 
CCM inalazimisha kutawala Nchi kwa nguvu bila RIDHAA ya WATANZANIA.
 
Huyu Kizimkazi ili arejee ikulu ni lazima uchaguzi uendeshwe kwa sheria mbovu. Ndiyo maana miswada ya sheria mbovu imepelekwa bungeni
 
Kwamba eti bashite ndiyo ana suluhu za shida za watanzania??? Hii ni dhihKa kwakweli
Hawa Watawala WAMESHAFELI wameingiza SIASA zao BUNGENI na kwenye MAHAKAMA wameua TAASISI sasa wamebaki na MAIGIZO.

Kila Kitu kimewashinda kwanini sasa WANG'ANG'ANIE?
 
Napenda kupendekeza kwa Mama. Hayo maendeleo pekee haita kuwa sababu ya watu kukusamehe kwenye sheria mbovu za chaguzi hasa kama vyama vikuu vya upinzani vitagomea uchaguzi. Ukweli ni kwamba huko ndiko tunaelekea. Hao wanao kudanganya mambo yatakuwa powa sio kwako ni kwao. Mambo hayatakuwa powa.
1. Kwanza wakigomea uchaguzi washiriki watapungua
2. Heshima yako itashuka kwa wananchi na kimataifa
3. Utaacha historia kama mwezi wa kura. Hata kama wengine hawatagikiri ni fair
4.Itakuwa vigumu hata kufanya katiba baada ya chaguzi maana nani atakuamini?
5. Mashindano ya mridhi wako yataanza baada ya chaguzi na kama chaguzi zimegomewa dharau kwako itakuwa kubwa hata ndani ya CCM.

Hii step ya tume huru ni ndogo sana na kama hili limekushinda kukubaliana na wadau wengine utapata shida sana mwaka huu Mama. Nashauri rekebisha sheria zote za chaguzi, tume na wape wadau wa demokrasia wanauotaka ili kama kushinda ushinde kihalali na kuweza kupeleka nchi mbele. Mnayofanya kwa sasa hayasaidiii nchi yetu. Hutaweza kuendeleza nchi na chama kimoja pekee huo ndiyo ukweli.
Naunga mkono hoja.
P
 
Back
Top Bottom