DC Hapi aagiza baa maarufu Jijini Dar, Corner bar ifungwe!

DC Hapi aagiza baa maarufu Jijini Dar, Corner bar ifungwe!

DC Hapi sidhani kama ni haki kwa amri hiyo kama ni kweli umeitoa wewe.

Bar ina leseni ya biashara ya vinywaji na inalipa Kodi na mishahara ya wafanyakazi kwa biashara.

Bar inahudumia Wateja ambao ni wanadamu wakike na wakiume.

Bar haianzi kufanya kazi ambayo haimuhusu eti kuuliza wateja kama ni wauza miili ama laa hayo ni majukumu ya mamlaka zingine zinazosimamia Kudhibiti wanawake kujiuza.
 
Nchi ya matamko,

Hatuna vipaumbele kila anayeibuka ana lake,

Watafuta sifa kwa vyombo vya habari.

Sas kuifungia baa ndio suluhisho.

Hivi ule msako wa bwana DAUDI ALBERT BASHITE uliishia wapi?

Nchi hii ili kuielewa unahitaji kujitoa akili kidogo.
Yani nchi imekuwa km IPO kwenye kipindi cha Mpito imetoka kupiNdULiwA ...BloodBasket [HASHTAG]#FvckGoverment[/HASHTAG]
 
Wakafunge na coco beach basi au bar zote zenye machangu,mbona zipo nyingi?utamjuaje kama ni changu wakati anakuja na kuomba huduma kama wateja wengine?
Na wakumbuke pia vijana wengi wamejiajiri pale,ukianzia kwenye bajaj,bodaboda,jikoni etc,wataenda wapi?.sidhani kama kutakuwa na matokeo chanya kwenye maamuzi haya.
 
DC elewa Pombe sio chai unalewa madaraka,sidhani una nguvu ya kisheria kuua mitaji na biashara halali za mtu,kwa kuwa wanaouza papuchi sio wenye baa.
Kuanzia Madukani mpaka Container wauzaji wamejaa tele barabarani
 
Aiseee... hivi hawa viongozi walichaguliwa kwa kutumia vigezo gani, khaaaa... ufunge biashara ya mwenzio kisa dada poa... hapana huo ni uonezi, kama vipi bar zote zifungwe tujue moja...
 
Ntaponea wapi maana hapo ndo sebuleni kwangu nikitoka tu opoa mboga
 
Dah.....mambo mengine.ni ngumu kumeza....hizo mambo zipo miaka yote....kwa binadamu ngumu, ngumu kuzuia...cha msingi ni kutoa elimu, kuwataka hao wadada wajiunge kwenye vikundi..wawezeshwe kidogo....etc....kufungiana biashara ni kuuwana na presha aiseee.....
Hawawezi kuacha wakt wanapata ela nyingi tena isio na kodi
Chamuhimu ni kuwapa Leseni then walipie
 
Inayojiuza ni bar au watu? kwanini wasiwakamate wanaojiuza? kwanini na ile mitaa maarufu ya machangudoa isifungwe? mwenye bar akisema ni chuki binafsi DC atakataaje?

Kaka hawa viongozi wana mihemko na wala hawajui misingi ya Biashara, huwezi kisema mtu afunge Biashara yake bila kupata misingi na undani wa hiyo Biashara, Huyo mtu aliomba kibali cha kuuza pombe na akapewa, sasa habarimza hao Malaya yeye zinamuhusu nini?, yeye anauza Malaya?

Cha pili, huwezi kumwambia mtu afunge Biashara zake bila kujua status ya hiyo Biashara, Huyo mkuu wa Wilaya anajua capital ya hiyo Biashara imetoka wapi?, kama ni Bank je atalipaje deni huku kafungiwa biashara bila kufata sheria?

Je Mkuu wa Wilaya anajua hiyo Bar ina wafanyakazi wangapi na wanalipwa mshahara kiasi gani?, je wataendeshaje maisha yao ikiwa hakuna kazi?

Je TRA inapoteza kiasi gani cha mapato kwa hiyo Bar ikifungwa?

Vipi kuhusu viwanda vya Bia, Soda, Maji? Vipi watu wa tax, bodaboda, Bajaji?

Cha mwisho, je hao Malaya wakiamia Bar zingine nazo zitafungwa?
 
Kwa mfano Mimi ni mmliliki wa hiyo bar halafu hao machangu wanakuja kama wateja wengine wanaagiza vinywaji baadae wakipata wateja wanaondoka na ikumbukwe hawana alama kuwa wanajiuza na makubaliano yao uongoz wa bar haujui sasa hapo kosa la kufunga bar ni nini!?
 
Baada ya malalamiko kuzidi kutokana nakuwapo biashara zisizo rasmi katika baamaarufu ya Corner, sasa baa hiyo imeamriwakufungwa.

IMG_20170225_203946.JPG


Akiwa katika ziara ya kawaida leo (Jumamosi), mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amemuagiza Ofisa Biashara wa Kinondoni, Mohamed Nyasama kuifunga baa hiyo.

“Hatuwezi kuvumilia vitendo hivi vikaendelea kufanyika huku tukiwa kimya…natoa agizo kesho nendeni kaifungieni hiyo baa kwa kuwa inakiuka maadili, ”amesema Hapi.Hata hivyo Nyasama amesema walishaitoza baahiyo faini ya Sh 300,000 kwa kosa hilo.“Mkuu hii baa ni sugu, nimewahi hata kuipigafaini na bado imeendelea na utaratibu huo huowa kuruhusu kina dada kujiuza.Kwa amri yakomkuu naanza taratibu za kuifungia leo, hadikufikia kesho itakuwa tayari,” amesema.

Source: Mwananchi
 
Back
Top Bottom