DC Hapi aagiza baa maarufu Jijini Dar, Corner bar ifungwe!

MAHOJIANO MAHAKAMANI YATAKUWA HIVI:

WAKILI: Unaweza kuiambia mahakama umri na elimu yako?
DC: Nina umri wa miaka 29. Nimesoma hadi darasa la saba na kisha nikajiendeleza hadi ngazi ya cheti katika chuo cha chama Kivukoni.

WAKILI: Je, kuna sheria yoyote inayoharamisha biashara ya kuuza uchi katika nchi hii?
DC: Hapana

WAKILI: Kama ndivyo, je wauza uchi wakikamatwa na polisi hufunguliwa kesi gani?
DC: Hufunguliwa kesi ya uzururaji.

WAKILI: Je, mliwahi kumkamata mmiliki wa bar hii ndugu (anamtaja jina) akizurura na mlimchukulia hatua gani?
DC: Hapana. Hatujawahi kumkamata akizurura, hivyo hatuwezi kumfungulia mashtaka.

WAKILI: Unaweza kuiambia mahakama huyu mteja wangu mmefikisha hapa kwa kosa gani la jinai alilotenda?
DC: Tumemfikisha mahakamani kwa kuwa tulikuta watu wakizurura kwenye bar yake.

WAKILI: Kwanini hamkuwakamata wao badala ya kumkamata mmiliki wa bar?
DC: (huku akikuna kichwa) KIMYA!!!!!!!!!!

WAKILI: Je, ni nani mwenye jukumu la kuwakamata na kuwafungulia mashtaka wazururaji?
DC: Ni polisi na kisha kuwafikisha mahakamani.

WAKILI: Nikikuambia kwamba elimu yako ni ya kutiliwa mashaka sawa na ya ndugu Bashite nitakuwa nimekosea?
DC: Utakuwa sahihi kabisa mheshimiwa. Unachosema ni........

....INTERUPTION....wakili wa serikali anasimama na kumzuia DC asiendelee kujibu swali hilo lakini wakili wa utetezi anapinga na mahojiano yanaendelea.....

WAKILI: Je, kuna kifungu chochote kinachotamka kwamba mtu anaweza kushtakiwa na kufungwa kwa kosa au makosa yaliyotenwa na mtu au watu wengine?
DC: Hapana.

Maswali kutoka upande wa utetezi yanafungwa na baada ya siku tano hakimu anasoma hukumu.

*********************************************
HAKIMU: Baada ya kupitia hoja za pande zote mbili nimejiridhisha kwamba mtuhumiwa hana kosa lolote kisheria hivyo upande wa mashtaka (DC na wapambe wake) wanaamriwa kulipa gharama za kesi, pamoja na fidia ya Tsh 1.2 bilioni kwa kuvuruga biashara ya ndugu (anamtaja jina).

Koooooooooooooooooti!!!!!!!!!!!!!!!!
Hahahahahahahah..., koooooooooot.!
 
Basi na NIGHT CLUBS zote zifungwe kwa maana ya bidhaa ngono ipo nje nje kwenye clubs kama tafsiri ndiyo ipo hivyo, mburula kabisa
 
Sheria zetu hazisapoti biashara ya kuuza mwili... Ndo maana wanakamata wafanya biashara hiyo.
Sheria zimekaa kimya, that means haitahesabika kuwa ni kosa kumkumbatia mtu kwa makubaliano, tena faraghani (katiba inaelekeza kuwa kila mtu anastahili kuheshimiwa akiwa faragha)

HII AKILI YA KUKIMBIZANA NA MAKAHABA NI YA KIOVU.
 
Hii sio amri halali. Unawafungiaje kisa kuna machangu? Hawa vijana sijui Dr. JPM aliwaokota wapi?
Maamuzi ya kukurupuka! ..tulisema vijana vijana, wengi naona hata uwezo wa kutafakari mambo bado kabisa, wanakurupuka!
Kusema kweli hivi vyeo vya DCs na RCs, vinatumiwa vibaya na baadhi ya wahusika! ..ndiyo maana baadhi yetu tumediriki kusema vyeo hivi havihitaji hata checti cha shule, sasa kazi ya namna gani hii serekalini, ...dunia hii ya leo?
 
M
Na wewe ukifungua ya kwako wembe utakuwa ni ule ule tu, tutaipiga pini
Kuuza mwili usiku kuna mwaffect vipi MTU asiyekuwepo? Haya mambo huwa hayana mtendewa. Mwenye mwili wake ana Uhuru nao ili mradi hajamdhuru MTU. Halafu hii siyo nchi ya kidini.
 
Back
Top Bottom